Mahakama Kuu yatupilia mbali kesi ya kupinga Ndugai kujiuzulu Uspika. Yasema hakuna ukiukwaji wa Katiba uliofanywa

Vyovyote vile, kuna tija gani ya Ndugai kubaki spika? Tunataka katiba mpya na bora, siyo hii mbovu!
 
Ile haikuwa barua bali TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Sawa, lakini pia katibu wa Bunge alikiri kupokea nakala ya barua aliyoandikiwa katibu mkuu wa CCM na Ndugai. Aidha katibu mkuu wa CCM alimwandikia barua katibu wa Bunge kuhusu kujiuzulu kwa Ndugai!

Huoni kuwa kuna barua ya kificho iliyoandikwa na Ndugai kwenda kwa katibu wa Bunge baada ya kesi kufunguliwa.
 
Nafikiri barua halisi umeiona. Tujadili ishu zingine
 

Unaijua unaisikia?
 
Hiyo barua ilifichwa wapi? Tulioonyeshwa ni barua kutoka kwa Ndugai kwenda kwa katibu mkuu wa CCM nakala kwa katibu wa Bunge!

Kama kuna barua nyingine, iweke hapa na sisi tuione. Tuliyoona wengine (na pengine wewe pia) ni Press Release, sio barua!
 
Kama kuna barua nyingine, iweke hapa na sisi tuione. Tuliyoona wengine (na pengine wewe pia) ni Press Release, sio barua!
Sina sababu ya kuiweka hapa wakati katibu wa Bunge alikiri kupokea nakala ya barua aliyoandikiwa katibu mkuu wa CCM na pia barua kutoka kwa katibu mkuu wa CCM.
 
Bunge butu kabisa. Kilichotokea ni β€œcoup” Bungeni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…