Mahakama mnapaswa kujitathmini sana

Mahakama mnapaswa kujitathmini sana

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Leo imetoka taarifa juu ya Mahakama Kuu kubatilisha hukumu iliyotolewa dhidi ya mtu aliyekutwa na hatia ya kufanya vitendo vya uchawi dhidi ya mtoto wa ndugu yake huko Njombe!

Hukumu hii ilitolewa kipindi ambacho vitendo vya uchawi na ushirikina vikiwa vimeshika hatamu kwa kiwango cha kusikitisha hapa Tanzania, hadi jamii ikawa imekosa mahali pa kwenda ili kupata suluhu na tumaini.

Vitendo vya uchawi na ushirikina si tu vimekuwa vikirudisha maendeleo ya jamii zetu nyuma bali vimekuwa vikiongeza mzigo mkubwa sana kwa serikali kwa kuongezeka jamii tegemezi kila kikucha. Vitendo hivi vimeangamiza watu tegemezi kwenye familia mbalimbali na kusababisha umasikini kuzidi kukithiri kwenye jamii nyingi Afrika na hasa Tanzania.

Waliotunga sheria ya kupiga marufuku vitendo vya uchawi hawakuwa wajinga. Kuna kitu waliona na walitaka kizuiwe na sheria ili jamii ipate kukombolewa na kuokolewa. Na mara nyingi nimekuwa nafikiri kuwa Mahakama zetu zinapotafrisi sheria hazina budi kwenda kuangalia sera iliyosabisha sheria husika kutungwa na pia asili hasa ya sheria hiyo ni nini na ilitungwa ili kukabili changamoto zipi kwenye jamii.

Nimesikitishwa sana na uamuzi ulitolewa na Mahakama kuu Iringa na kusema kweli, uamuzi huu sio tu utachochea kuongezeka kwa hizi imani za kijinga hapa Tanzania bali utachochea pia kurudi nyuma kwa jamii za kitanzania ambapo watu wataona sasa kuwa hakuna haja ya kuacha vitendo hivi vya ajabu kwa sababu sheria pia inawafumbia macho.

Hukumu hii pia sio tu itasababisha kuendelea kwa vitendo hivi bali itachochea sana kuongezeka kwa visasi hasa mauaji maana wahanga wataona hakuna tena msaada wanaopata kwenye vyombo vya kisheria.

Nahitimisha kwa kusema Mahakama ijitathimini kwa hukumu zake inazotoa!

Screenshot_20220914-121223_Facebook.jpg
 
Ile hukumu ilileta sintofahamu kwa sababu serikali na sheria zetu hazitambui ushirikina ndio maana watu walihoji walithibitishaje mpaka yule mtuhumiwa kukutwa na hatia,bila shaka hakimu alilambishwa mlungula

Mchawi anaweza kutumia hata nzi kuleta madhara ya kwenye maisha yako mfano ajali,,sasa ukienda mahakamani kumshtaki mtu unayemhisi, kwanza Huyo nzi utampata wapi na hata ukimpata utathibitisha vipi kwamba ni fulani ndiye kamtuma.

Haya mambo tuyaache yaende kiroho tu.
 
Tanzakiza Hakuna mahakama wakuu kuna majengo chakavu yaliyo andikwa mahakama wale wavaa suti na manywele meupe kwa kichwa ni vilaza wa kiwango Cha rami
 
Hakuna kujitathmini, mahakama haifanyi kazi kwa hisia, au maelezo yasiyojitosheleza, inapofikia hatua ya ku "prove beyond reasonable doubt" hapo ndipo ugumu hutokea.

Pale unapoiambia mahakama fulani alikufa kwa kulogwa, halafu kulogwa huko kukamsababishia ugonjwa uliomfanya hali ya afya yake kuwa mbaya hatimae akafa.

Sasa utatakiwa uioneshe mahakama uhusiano uliopo kati ya kulogwa na ugonjwa husika, ili mahakama isiamini huo ugonjwa ulisababishwa kwa sababu nyingine zilizothibitishwa kisayansi, hapa ndipo hizi kesi za uchawi huwa ngumu kwa walalamikaji.
 
Ile hukumu ilileta sintofahamu kwa sababu serikali na sheria zetu hazitambui ushirikina ndio maana watu walihoji walithibitishaje mpaka yule mtuhumiwa kukutwa na hatia,bila shaka hakimu alilambishwa mlungula

Mchawi anaweza kutumia hata nzi kuleta madhara ya kwenye maisha yako mfano ajali,,sasa ukienda mahakamani kumshtaki mtu unayemhisi, kwanza Huyo nzi utampata wapi na hata ukimpata utathibitisha vipi kwamba ni fulani ndiye kamtuma.

Haya mambo tuyaache yaende kiroho tu.
Kama hujui kitu ni bora ukakaa kimya

Sheria za nchi zinatambua uchawi kama kosa na kuna Sheria kabisa inaitwa The Witchcraft Act
 
Hakuna kujitathmini, mahakama haifanyi kazi kwa hisia, au maelezo yasiyojitosheleza, inapofikia hatua ya ku "prove beyond reasonable doubt" hapo ndipo ugumu hutokea.

Pale unapoiambia mahakama fulani alikufa kwa kulogwa, halafu kulogwa huko kukamsababishia ugonjwa uliomfanya hali ya afya yake kuwa mbaya hatimae akafa.

Sasa utatakiwa uioneshe mahakama uhusiano uliopo kati ya kulogwa na ugonjwa husika, ili mahakama isiamini huo ugonjwa ulisababishwa kwa sababu nyingine zilizothibitishwa kisayansi, hapa ndipo hizi kesi za uchawi huwa ngumu kwa walalamikaji.
Mahakama haijatengua uamuzi kwa kukosekana kwa ushahidi. Wametengua hukumu kwa sababu yq tafsiri ya kifungu. Ushahidi ulikuwepo na ulijitosheleza
 
Tanzakiza Hakuna mahakama wakuu kuja majengo chakavu yaliyo andikwa mahakama wale wavaa suti na manywele meupe kwa kichwa ni vilaza wa kiwango Cha rami

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Na hii ndo inavyoenda kuonekana

Watuhumiwa wakiendelea kuachiwa hivi basing on technical grounds na sio merits watu wataendelea kujichukulia sheria mkononi tu
 
Mwanasheria anapotoa hoja kama asiyekwenda shule.
 
Leo imetoka taarifa juu ya Mahakama Kuu kubatilisha hukumu iliyotolewa dhidi ya mtu aliyekutwa na hatia ya kufanya vitendo vya uchawi dhidi ya mtoto wa ndugu yake huko Njombe!

Hukumu hii ilitolewa kipindi ambacho vitendo vya uchawi na ushirikina vikiwa vimeshika hatamu kwa kiwango cha kusikitisha hapa Tanzania, hadi jamii ikawa imekosa mahali pa kwenda ili kupata suluhu na tumaini.

Vitendo vya uchawi na ushirikina si tu vimekuwa vikirudisha maendeleo ya jamii zetu nyuma bali vimekuwa vikiongeza mzigo mkubwa sana kwa serikali kwa kuongezeka jamii tegemezi kila kikucha. Vitendo hivi vimeangamiza watu tegemezi kwenye familia mbalimbali na kusababisha umasikini kuzidi kukithiri kwenye jamii nyingi Afrika na hasa Tanzania.

Waliotunga sheria ya kupiga marufuku vitendo vya uchawi hawakuwa wajinga. Kuna kitu waliona na walitaka kizuiwe na sheria ili jamii ipate kukombolewa na kuokolewa. Na mara nyingi nimekuwa nafikiri kuwa Mahakama zetu zinapotafrisi sheria hazina budi kwenda kuangalia sera iliyosabisha sheria husika kutungwa na pia asili hasa ya sheria hiyo ni nini na ilitungwa ili kukabili changamoto zipi kwenye jamii.

Nimesikitishwa sana na uamuzi ulitolewa na Mahakama kuu Iringa na kusema kweli, uamuzi huu sio tu utachochea kuongezeka kwa hizi imani za kijinga hapa Tanzania bali utachochea pia kurudi nyuma kwa jamii za kitanzania ambapo watu wataona sasa kuwa hakuna haja ya kuacha vitendo hivi vya ajabu kwa sababu sheria pia inawafumbia macho.

Hukumu hii pia sio tu itasababisha kuendelea kwa vitendo hivi bali itachochea sana kuongezeka kwa visasi hasa mauaji maana wahanga wataona hakuna tena msaada wanaopata kwenye vyombo vya kisheria.

Nahitimisha kwa kusema Mahakama ijitathimini kwa hukumu zake inazotoa!

View attachment 2356443
Uchawi ni dhana hovyo ya kufikirika,huo ni upuuzi wa watu wajinga
 
Hakuna ushahidi wa uchawai kuwepo popote
 
Uchawi upo na ni kitu kibaya sana, ila kuthibitisha ki Mahakama au ki sayansi ni ngumu...haya ni mambo ya kiroho.
 
Wachawi wote huwa wanaachiwa, nadhani mahakimu wanawaogopa wachawi na waganga, chek yule binti aliyemuua mama yake kwa kushirikiana na waganga nae aliachiwa.
 
Hukumu ya mchawi ni kuuwa na sio kwenda jela. Ukiua mchawi au jambazi laana haiwezi kukupata maana hawa tayari walishahukumiwa.
 
Leo imetoka taarifa juu ya Mahakama Kuu kubatilisha hukumu iliyotolewa dhidi ya mtu aliyekutwa na hatia ya kufanya vitendo vya uchawi dhidi ya mtoto wa ndugu yake huko Njombe!

Hukumu hii ilitolewa kipindi ambacho vitendo vya uchawi na ushirikina vikiwa vimeshika hatamu kwa kiwango cha kusikitisha hapa Tanzania, hadi jamii ikawa imekosa mahali pa kwenda ili kupata suluhu na tumaini.

Vitendo vya uchawi na ushirikina si tu vimekuwa vikirudisha maendeleo ya jamii zetu nyuma bali vimekuwa vikiongeza mzigo mkubwa sana kwa serikali kwa kuongezeka jamii tegemezi kila kikucha. Vitendo hivi vimeangamiza watu tegemezi kwenye familia mbalimbali na kusababisha umasikini kuzidi kukithiri kwenye jamii nyingi Afrika na hasa Tanzania.

Waliotunga sheria ya kupiga marufuku vitendo vya uchawi hawakuwa wajinga. Kuna kitu waliona na walitaka kizuiwe na sheria ili jamii ipate kukombolewa na kuokolewa. Na mara nyingi nimekuwa nafikiri kuwa Mahakama zetu zinapotafrisi sheria hazina budi kwenda kuangalia sera iliyosabisha sheria husika kutungwa na pia asili hasa ya sheria hiyo ni nini na ilitungwa ili kukabili changamoto zipi kwenye jamii.

Nimesikitishwa sana na uamuzi ulitolewa na Mahakama kuu Iringa na kusema kweli, uamuzi huu sio tu utachochea kuongezeka kwa hizi imani za kijinga hapa Tanzania bali utachochea pia kurudi nyuma kwa jamii za kitanzania ambapo watu wataona sasa kuwa hakuna haja ya kuacha vitendo hivi vya ajabu kwa sababu sheria pia inawafumbia macho.

Hukumu hii pia sio tu itasababisha kuendelea kwa vitendo hivi bali itachochea sana kuongezeka kwa visasi hasa mauaji maana wahanga wataona hakuna tena msaada wanaopata kwenye vyombo vya kisheria.

Nahitimisha kwa kusema Mahakama ijitathimini kwa hukumu zake inazotoa!

View attachment 2356443
Weka hiyo hukumu ya high court hapa ili tuone kama una hoja au nawe unaendekeza ushirikina....

Huwezi kumfunga mtu kizembe zembe eti anadaiwa ni mshirikina, itakuwa ni sawa tu na wale wanaoua vikongwe kwa tuhuma za ushirikina....

Jinai inapaswa kuthibitishwa beyond reasonable doubt and not on balance of probabilities!
 
Weka hiyo hukumu ya high court hapa ili tuone kama una hoja au nawe unaendekeza ushirikina....

Huwezi kumfunga mtu kizembe zembe eti anadaiwa ni mshirikina, itakuwa ni sawa tu na wale wanaoua vikongwe kwa tuhuma za ushirikina....

Jinai inapaswa kuthibitishwa beyond reasonable doubt and not on balance of probabilities!
Hajaachiwa kwa kukosekana ushahidi! Ameachiwa kwa kifungu cha sheria kukosewa tafsiri
 
Hukumu ya mchawi ni kuuwa na sio kwenda jela. Ukiua mchawi au jambazi laana haiwezi kukupata maana hawa tayari walishahukumiwa.
Na hivi ndo wananchi wanavyoenda kufanya kwa mahakama zetu kuendekeza technicalities badala ya merits
 
Leo imetoka taarifa juu ya Mahakama Kuu kubatilisha hukumu iliyotolewa dhidi ya mtu aliyekutwa na hatia ya kufanya vitendo vya uchawi dhidi ya mtoto wa ndugu yake huko Njombe!

Hukumu hii ilitolewa kipindi ambacho vitendo vya uchawi na ushirikina vikiwa vimeshika hatamu kwa kiwango cha kusikitisha hapa Tanzania, hadi jamii ikawa imekosa mahali pa kwenda ili kupata suluhu na tumaini.

Vitendo vya uchawi na ushirikina si tu vimekuwa vikirudisha maendeleo ya jamii zetu nyuma bali vimekuwa vikiongeza mzigo mkubwa sana kwa serikali kwa kuongezeka jamii tegemezi kila kikucha. Vitendo hivi vimeangamiza watu tegemezi kwenye familia mbalimbali na kusababisha umasikini kuzidi kukithiri kwenye jamii nyingi Afrika na hasa Tanzania.

Waliotunga sheria ya kupiga marufuku vitendo vya uchawi hawakuwa wajinga. Kuna kitu waliona na walitaka kizuiwe na sheria ili jamii ipate kukombolewa na kuokolewa. Na mara nyingi nimekuwa nafikiri kuwa Mahakama zetu zinapotafrisi sheria hazina budi kwenda kuangalia sera iliyosabisha sheria husika kutungwa na pia asili hasa ya sheria hiyo ni nini na ilitungwa ili kukabili changamoto zipi kwenye jamii.

Nimesikitishwa sana na uamuzi ulitolewa na Mahakama kuu Iringa na kusema kweli, uamuzi huu sio tu utachochea kuongezeka kwa hizi imani za kijinga hapa Tanzania bali utachochea pia kurudi nyuma kwa jamii za kitanzania ambapo watu wataona sasa kuwa hakuna haja ya kuacha vitendo hivi vya ajabu kwa sababu sheria pia inawafumbia macho.

Hukumu hii pia sio tu itasababisha kuendelea kwa vitendo hivi bali itachochea sana kuongezeka kwa visasi hasa mauaji maana wahanga wataona hakuna tena msaada wanaopata kwenye vyombo vya kisheria.

Nahitimisha kwa kusema Mahakama ijitathimini kwa hukumu zake inazotoa!

View attachment 2356443
Achana na mila potofu, huo uchawi unaosema,ukiaambiwa uthibitishe utaweza!!??
 
Back
Top Bottom