Mahakama ya Jumuiya Afrika Mashariki imetupilia mbali madai ya kupinga uhalali wa Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mahakama ya Jumuiya Afrika Mashariki imetupilia mbali madai ya kupinga uhalali wa Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR UPO KIHALALI

Mahakama ya Jumuiya Afrika Mashariki imetupilia mbali madai ya kupinga uhalali wa Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yaliyofunguliwa na baadhi ya wanaharakati.

Mapema leo Wakili Mkuu wa Serikali Gabriel Malata ameeleza kuwa mahakama hiyo imetoa uamuzi huo baada ya kukubaliana na hoja zote za upande wa serikali ikiwa ni pamoja na madai kuletwa nje ya muda, pamoja na uhalali wa mahakama kuhoji uhalali wa muungano huo.

Amesema Mahakama ya Afrika Mashariki imezaliwa kupitia makubaliano (The East African Community Treaty) ya mwaka 1999 na kuanza kufanya kazi mwaka 200, hivyo mahakama hiyo haina mamlaka ya kuhoji Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964.

Jana kulitolewa maamuzi ktk Mahakama ya Afrika Mashariki, wananchi wapatao 40,000 wa Zanzibar walifungua kesi dhidi ya Serikali ya Zanzibar, katibu Mkuu Kiongozi SMZ, Mwanasheria Mkuu wa Tanzania kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar." Gabriel Malata

Madai yaliyoletwa kuhoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yako nje ya muda, kwa mujibu wa kanuni malalamiko yanatakiwa kuwasilishwa ndani ya siku 60 tangu tukio lilipotokea, sasa kuanzia Aprili 26, 1964 mpaka leo ni miaka 56."-Gabriel Malata

Mahakama ya Afrika Mashariki imesema haina mamlaka ya kuhoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa sababu aliyetakiwa kuhojiwa ni Serikali zote mbili zilizoungana wala si kuhoji Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania." - Gabriel Malata

Upande wa Serikali zote mbili (Bara na Zanzibar) ulipeleka hoja kuthibitisha Muungano huo na mapingamizi ya awali (preliminary objections) kuhusu Mamlaka ya Mahakama (ya Afrika Mashariki) kusikiliza shauri hilo." - Gabriel Malata

Shauri hilo lilidai kama hakuna hati ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, hata Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania halipo sababu hakuna Muungano, hata kutiwa saini kwa Muungano huo ni batili sababu hakuna ridhaa ya watu wa sehemu hizo mbili." - Gabriel Malata

Shauri hilo lilikuwa linahoji; hati ya makubaliano ya Muungano kati ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar siyo halali na haipo. Msingi wa hoja hizo wanadai Zerikali ya Zanzibar haijawahi kuridhia hiyo hati ya Muungano." - Gabriel Malata

1601458845393.png
 
... kwa hiyo Zanzibar ndio hivyo imemezwa rasmi? Au sijaelewa. Kwamba kuanzia sasa madai yoyote dhidi ya muungano ni batili? Kwamba, hata Maalim akitwaa nafasi ya urais Zanzibar watulie tuli ndani ya muungano kama mke kwa mumewe?
 
Jibu linakuja 28th October, watanzania kwa umoja wenu wake kwa waume, hima-himaaa; njia pekee ya kuweka mambo yote sawa juu ya Muungano wetu huu wa Bara na Visiwani ni kumtoa kidudu mtu anaitwa CCM.
 
Hapo SIO uhalali wa Muungano uliohikumiwa, Bali ni Taratibu za kuwasilisha na Jurisdiction ya Mahakama vimegoma usikilizawaji wake.

Kuwepo kwa uhalali au kutokuwepo havijasikilizwa.
 
Jibu linakuja 28th October, watanzania kwa umoja wenu wake kwa waume, hima-himaaa; njia pekee ya kuweka mambo yote sawa juu ya Muungano wetu huu wa Bara na Visiwani ni kumtoa kidudu mtu anaitwa CCM.
... halafu hiyo hukumu ni kama imelenga tarehe "maalumu" 28/10!
 
Hapo SIO uhalali wa Muungano uliohikumiwa, Bali ni Taratibu za kuwasilisha na Jurisdiction ya Mahakama vimegoma usikilizawaji wake.

Kuwepo kwa uhalali au kutokuwepo havijasikilizwa.
... thanks kwa ufafanuzi.
 
Wakati Muafaka waZanzibari kupiga kura yao ya "maoni" hapo Oktoba 2020

Baada ya hukumu ya kesi ya Muungano kuamuliwa kisheria Mahakamani , sasa ni wakati muafaka waZanzibari kuliamua suala hili kisiasa kwa kupiga kura nyingi kuonesha maoni yao kupitia sanduku la kura upande unaotaka serikali tatu wakati wa Uchaguzi mkuu Oktoba 2020

29 September 2020
Dar-es-Salaam

WAKILI MKUU wa SERIKALI Azungumzia WALIVYOSHINDA KESI DHIDI ya WAPINGA MUUNGANO


Hon. Gabriel Pascal Malata (government solicitor general), Wakili Mkuu wa Serikali ya Tanzania amezungumza na wanahabari kuhusiana na Serikali kushinda kesi dhidi ya wanaharakati (40,000) waZanzibari ambao walitia saini kisha walifungua kesi Mahakama ya Afrika Mashariki wakipinga MUUNGANO wa TANGANYIKA NA ZANIBAR. Kesi hii ilifunguliwa tangu mwaka 2016..... Serikali ya Muungano kupitia jopo lake la mawakili toka ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Tanzania na ile ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar imeshinda kesi kupitia mapingamizi iliyowasilisha ikionesha mapungufu ya kisheria (on technicalities) mfano :

  1. Waliofungua kesi walikuwa hawajazaliwa wakati Muungano unaasisiwa,
  2. Mahakama haina mamlaka ya kuhoji uwepo wa nchi inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuzingatia treaties (makubaliano) ya nchi za Afrika Mashariki iliyoanzishwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki .
  3. Serikali ya Mapinduzi ndiyo ina uwezo wa kuhoji
  4. Siku 60 zimepita toka tukio la Muungano lilipifanyika tarehe 26 April 1964 kwa maana nyingine ushauri limechelewa kwa muda wa miaka zaidi 56 kwani kupinga muungano ilitakiwa pingamizi liwasilishwe si zaidi ya siku 60 tangu tarehe 26 Aprili 1964
  5. Mahakama na Jumuiya ya Afrika Mashariki ilianzishwa mwaka 1999 hivyo haina mamlaka ya kusikiliza masuala yaliyotokea tarehe 26 April 1964

Pia ukitaka kujua majukumu ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali bofya linki hii : Muundo wa Taasisi |Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali
 
Tanzania ni nchi moja iliyoundwa na Tanganyika na Visiwa vya Zanzibar (Unguja na Pemba).
 
Mkimaliz hili mtaenda na muungano wa Pemba na unguja
 
Safi saana.

Watu wenye busara na nia njema huangalia suala kwa sura yake ya nje na anatomy yake kwa utulivu na umakini.

Kwa mtu mwenye mtazamo jenzi, alitakiwa azungumzie tatizo specific ili litafutiwe uvumbuzi na siyo songombingo za kutuvuruga kwa chokochoko zinazopewa msukumo na utashi hasi!.

Ahsante sana Mheshimiwa Malata. Mungu akuweke zaidi.
 
18 Apr 2014

Sikiliza VIMBWANGA Vifupi vya Kamanda Lissu Tanganyika na Zanzibar



Mjumbe wa Bunge la Katiba, Tundu Lissu amesema Tanganyika ilikufa kwa amri iliyotolewa na Mwalimu Julius Nyerere na siyo kwa makubaliano katika hati ya Muungano.

Huku akinukuu maneno yaliyopo katika vitabu vilivyoandikwa na Profesa Issa Shivji na Makamu Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Pius Msekwa, Lissu alisema Jamhuri ya Muungano ilizaliwa bila uhalali wa kisheria kwa kuwa hayakuwapo makubaliano ya kila upande wa Muungano.

Alisema Aprili 26, 1964 (Siku ya Muungano), Mwalimu Nyerere alitoa amri ya masharti ya mpito ya mwaka 1964 ambayo pamoja na mambo mengine iliifuta Tanganyika. Akichambua kitabu cha '50 Years of Independence: A Concise Political History of Tanzania' (Miaka 50 ya Uhuru: Historia fupi ya Tanzania), kilichoandikwa na Msekwa na kuchapishwa Januari mwaka huu, Lissu alisema: "Msekwa anasema katika kitabu hicho kuwa amri hiyo ilichapishwa katika Gazeti la Serikali la siku hiyo.

Kwanza, iliwabadilisha waliokuwa watumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika kuwa watumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano."
 
Kuna mahakama hapo au genge lile, yaani Burundi, Uganda, Tz, Rwanda na Sudan? tetetete hapo ni Kenya pekee
 
21 March 2018
Historia ya wanaharakati 40,000 Zanzibari walivyopeleka kesi Mahakamani. Mihuri ya Jamhuri ya Tanganyika. Mihuri ya serikali ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, na nchi iliyojulikana kwa jina moja la Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar

Kesi Ya Kuupinga Muungano wa Tanganyika Na Zanzibar Awamu Yapili Ipo Hivi- Rashid Adi"

 
Hakuna aliyeshinda kesi hapo, maana mahakama imesema haina uwezo wa kusilikiza shauri hilo! Sasa huyo Malata atasemaje wameshinda? Akili finyu!
 
Back
Top Bottom