Mahakama ya Rufani: Maamuzi ya Rais kuhusu Wafanyakazi wa Umma ni ya mwisho

Mahakama ya Rufani: Maamuzi ya Rais kuhusu Wafanyakazi wa Umma ni ya mwisho

Lord Diplock MR

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2015
Posts
1,393
Reaction score
3,237
MAHAKAMA YA RUFANI: CMA HAINA MAMLAKA WAFANYAKAZI WA UMMA

Mahakama ya Rufani ya Tanzania imesema Tume ya Usuluhishi ya wafanyakazi (Commission for Mediation and Arbitration-CMA) haina mamlaka ya kusikiliza na kutolea maamuzi kesi zinazohusu migogoro ya wafanyakazi wa umma.

Kupitia kesi ya rufaa ya madai CIVIL APPEAL NO. 12 OF 2022 TANZANIA POSTS CORPORATION VERSUS DOMINIC A. KALANGI mahakama hiyo ya juu zaidi ya Tanzania imesema migogoro ya wafanyakazi wa umma inatakiwa kuishia ndani ya Serikali, pale mfanyakazi anapofukuzwa kazi na mkuu wa idara au shirika la Serikali anatakiwa kukata Rufaa kwenda Tume ya Utumishi wa Umma, na endapo mfanyakazi atakuwa hajaridhika na maamuzi ya Tume ya Utumishi wa Umma basi anatakiwa akate rufaa kwenda Kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maamuzi ya Rais yatakuwa ya mwisho, hii ni Kwa mujibu wa Kifungu Cha 25 Cha sheria ya utumishi wa umma Public Service Act (Cap 298 R.E. 2019)

Dominic A. Kalangi alikuwa mfanyakazi wa Shirika la Posta (Tanzania Posts Corporation), mwaka 2017 ajira yake ilisitishwa Kwa utovu wa nidhamu.

Dominic alipeleka malalamiko yake CMA ambapo alishindwa kesi akakata Rufaa Mahakama kuu Mtwara ambapo mahakama kuu ikaamuru Shirika la Posta limlipe fidia ya mishahara ya miezi sita Dominic A kalangi. Shirika la Posta likakata Rufaa Mahakama ya Rufani ya Tanzania

Kwa Mujibu wa sheria Shirika la Posta la Tanzania ni Mali ya umma linalomilikiwa na serikali hivyo wafanyakazi wake ni watumishi wa umma.

"Going by the wording of the above-quoted provision, it is unambiguously clear that all disciplinary matters or disputes involving public servants are exclusively within the domain of the Public Service Commission whose decision is appelable to the President. As correctly submitted by Ms. Kinyasi and as amply demonstrated above, the CMA has no jurisdiction to adjudicate upon such matters."

View attachment 2175700View attachment 2175702
 
Mahakama wametafsiri Sheria ya Utumishi wa Umma.
 
Mahakama ya Rufaa imejiongoza vibaya kutafsiri hivyo vifungu. Nina imani muda sio mrefu watafanya marejeo au watatoa hukumu nyingine itayorekebisha maamuzi waliyotoa katika Rufaa hii.

Discplinary Matters ni sahihi kupitia mchakato wa ndani kabla ya kwenda CMA au Mahakama Kuu kwa Judicial Review lakini sio sahihi kwa migogoro (disputes) isiyo ya kinidhamu, hii inatakiwa kwenda moja kwa moja CMA maana hakuna sheria inayoelekeza kuwa ishughulikiwe ndani ya taasisi husika au kwamba iende huko Tume ya utumishi wa umma nk. Tume ya utumishi wa umma uwezo wake ni kupokea Rufaa na sio kupokea migogoro iliyo fresh
 
Wataalamu watufafanulie tuelewe maana ya hii hukumu
Mahakama imepiga msumari kuhusu watumishi wa umma kuwa hawatakiwi kwenda CMA pale wanapokuwa na mgogoro wa kazi na waajiri wao.

Kimsingi hukumu hii imeondoa haki ya watumishi wa umma kupata utatuzi wa migogoro yao. Ikumbukwe kuwa katika Sheria ya utumishi wa umma, mwajiri hana kosa na wala hakosei isipokuwa mwajiriwa tu.
 
Rais ana madaraka makubwa mno..
Rais ni mwanasiasa. Kwahiyo mtumishi wa umma akifukuzwa kwa sababu za meengo wake wa kisiasa ndiyo hana pa kwenda kupata haki yake?

Kwa mfano, CHADEMA imeshinda uchaguzi na kushika dola, kisha wakaja na mkakati wa kuwafukuza makada wa chama kitakachokuwa cha upinzani, hawataweza kuipata popote duniani?

Wataalamu wazidi kutufumbua macho
 
Rais ni mwanasiasa. Kwahiyo mtumishi wa umma akifukuzwa kwa sababu za meengo wake wa kisiasa ndiyo hana pa kwenda kupata haki yake?

Wataalamu wazidi kutufumbua macho
Rais anaposikiliza rufaa ya mtumishi wa umma hafanyi kama Rais (mwanasiasa) bali kama mamlaka ya nidhamu kwa mwajiriwa.

Maamuzi yake yanaweza kupingwa mahakamani wakati akiwa Rais mwanasiasa, anachokisema hakiwezi kupingwa mahakamani isipokuwa tu kikiwa kinavunja Katiba ya nchi.
 
Hapa lazima iwepo conflict of interest. Inawezekanaje mwajiri wako ambaye unaweza kumshtaki, yeye awe na mamlaka ya mwisho ya kukuwajibisha?

Ina maana akikuonea kwa sababu yoyote ile (tiseme ni ya kisiasa au yoyote ile atakayoona, mfano mlihitilafiana mahali), hakuna mamlaka yoyote nyingine ya kupeleka mashtaka yako?

Tutakuja kusababisha uonevu mkubwa usiorekebishika. Hii hukumu inapaswa ipelekwe kwenye ile mahakama ya haki za binadamu za Afrika. Ninaamini Itatenguliwa haraka sana.

Tatizo la baadhi ya watanzania ni kasumba chafu ya kuabudu watawala badala ya kuamini katika mifumo ambayo kupitia hiyo mtu yeyote ataweza kupata haki.
 
Hapa lazima iwepo conflict of interest. Inawezekanaje mwajiri wako ambaye unaweza kumshtaki, yeye awe na mamlaka ya mwisho ya kukuwajibisha?

Ina maana akikuonea kwa sababu yoyote ile (tiseme ni ya kisiasa au yoyote ile atakayoona, mfano mlihitilafiana mahali), hakuna mamlaka yoyote nyingine ya kupeleka mashtaka yako?

Tutakuja kusababisha uonevu mkubwa usiorekebishika. Hii hukumu inapaswa ipelekwe kwenye ile mahakama ya haki za binadamu za Afrika. Ninaamini Itatenguliwa haraka sana.

Tatizo la watanzania wengu gftuna kasumba chafu ya kuabudu watawala badala ya kuamini katika mifumo ambayo kupitia hiyo mtu yeyote ataweza kupata haki.
Kwani katiba inayoliliwa inasemaje
 
MAHAKAMA YA RUFANI: CMA HAINA MAMLAKA WAFANYAKAZI WA UMMA

Mahakama ya Rufani ya Tanzania imesema Tume ya Usuluhishi ya wafanyakazi (Commission for Mediation and Arbitration-CMA) haina mamlaka ya kusikiliza na kutolea maamuzi kesi zinazohusu migogoro ya wafanyakazi wa umma.

Kupitia kesi ya rufaa ya madai CIVIL APPEAL NO. 12 OF 2022 TANZANIA POSTS CORPORATION VERSUS DOMINIC A. KALANGI mahakama hiyo ya juu zaidi ya Tanzania imesema migogoro ya wafanyakazi wa umma inatakiwa kuishia ndani ya Serikali, pale mfanyakazi anapofukuzwa kazi na mkuu wa idara au shirika la Serikali anatakiwa kukata Rufaa kwenda Tume ya Utumishi wa Umma, na endapo mfanyakazi atakuwa hajaridhika na maamuzi ya Tume ya Utumishi wa Umma basi anatakiwa akate rufaa kwenda Kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maamuzi ya Rais yatakuwa ya mwisho, hii ni Kwa mujibu wa Kifungu Cha 25 Cha sheria ya utumishi wa umma Public Service Act (Cap 298 R.E. 2019)

Dominic A. Kalangi alikuwa mfanyakazi wa Shirika la Posta (Tanzania Posts Corporation), mwaka 2017 ajira yake ilisitishwa Kwa utovu wa nidhamu.

Dominic alipeleka malalamiko yake CMA ambapo alishindwa kesi akakata Rufaa Mahakama kuu Mtwara ambapo mahakama kuu ikaamuru Shirika la Posta limlipe fidia ya mishahara ya miezi sita Dominic A kalangi. Shirika la Posta likakata Rufaa Mahakama ya Rufani ya Tanzania

Kwa Mujibu wa sheria Shirika la Posta la Tanzania ni Mali ya umma linalomilikiwa na serikali hivyo wafanyakazi wake ni watumishi wa umma.

"Going by the wording of the above-quoted provision, it is unambiguously clear that all disciplinary matters or disputes involving public servants are exclusively within the domain of the Public Service Commission whose decision is appelable to the President. As correctly submitted by Ms. Kinyasi and as amply demonstrated above, the CMA has no jurisdiction to adjudicate upon such matters."

View attachment 2175700View attachment 2175702
Team = Serikalini security🤣
 
Hiyo itapinduliwa muda sio mrefu..
Cooperative bodies (mashirika ya umma) yanayo miongozo yake..
Kuna watumishi wameajiriwa na mashirika moja kwa moja.. Na mikataba ya kazi ipo open sana.. Kwamba ikitokea mgogoro ruksa kwenda Mahakamani na ni chombo cha mwisho cha uamuzi..

Kuna waajiri ambao wameajiriwa na Serikali kuu moja kwa moja bila kupitia Mashirika ya Umma.. Hao wanaweza kwenda kwa Rais.. Pia sio mwisho wanaruhusa kwenda Mahakamani kama kuna uonevu
 
Rais anaposikiliza rufaa ya mtumishi wa umma hafanyi kama Rais (mwanasiasa) bali kama mamlaka ya nidhamu kwa mwajiriwa.

Maamuzi yake yanaweza kupingwa mahakamani wakati akiwa Rais mwanasiasa, anachokisema hakiwezi kupingwa mahakamani isipokuwa tu kikiwa kinavunja Katiba ya nchi.
Kwani nchi ina katiba?
 
Back
Top Bottom