Mahakama ya Rufani Tanzania ina Majaji 31 wakati Supreme court ya Marekani ina majaji 9 tu. Tutaendelea kukopa madeni kwa sana!

Mahakama ya Rufani Tanzania ina Majaji 31 wakati Supreme court ya Marekani ina majaji 9 tu. Tutaendelea kukopa madeni kwa sana!

Status
Not open for further replies.

Bush Dokta

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2023
Posts
24,831
Reaction score
45,154
Hahahahaa......Mambo mengine inabidi tucheke tu hata kama yanahuzunisha.

Utangulizi
Marekani ina Majimbo 50 na jumla ya Wananchi( raia) wapatao Milioni 330+ kwa mujibu wa Takwimu za 2022.

Tanzania ina wananchi wapatao Milioni 65+ kwa mujibu wa Takwimu za 2022.

Wakati Marekani ina idadi ya Raia inayozidi ya Tanzania zaidi ya mara tano sisi Tanzania tuna idadi ya Majaji takribani mara nne ya ile ya marekani.

Screenshot_2024-06-09-03-19-11-324_com.android.chrome.jpg
Screenshot_2024-06-09-03-16-30-064_com.android.chrome.jpg

Tafakuli:
Wakati Nchi yetu kwa sehemu kubwa inaongozwa na bajeti inayotegemea mikopo kuhudumia wananchi na sehemu kadhaa ya kodi zinazokusanywa itakushangaza kuwa Tuna idadi kubwa ya Wateule na vigogo wa serikali wanaohudumiwa kila kitu kwa pesa hizo hizo za Kasungura kadogo.

Ikumbukwe kwa mujibu wa Sheria inayosimamia maslahi ya Watumishi wa Umma majaji ni miongoni mwa wanaolipwa na kuhudumiwa kifahari kutokana na hadhi yao pamoja na kuwa na mishahara minono.

Sasa tujiulize kwanini sisi wenye maeneeleo kidogo tunaonekana kuwa na matumizi makubwa wakati Nchi zenye watu wengi na shuguuli nyingi zikiwa na matumizi yakawaida na kuacha sehemu ya mapato yao yahudumie wananchi? Sisi tunakwamba wapi?

Ikumbukwe hapa tumeangalia sehemu ndogo tu ktk sekta hii ya watumishi wa Umma

Fikiria matumizi yakoje ktk ofisi zifuatazo

1. Ikulu
2. Ofisi ya waziri Mkuu
3. Ofisi ya Spika wa bunge
4. Ofisi ya DGIS
5. Ofisi ya CDF
6. Ofisi ya Makamu wa Rais
7. Ofisi ya IGP
8. Ofisi ya Takukuru

Hata tungekopa kiasi gani, hata wananchi walipe kodi kiasi gani tunadhani zitatosha?

Mapendekezo:

Chama cha mapinduzi kiangalie upya namna bora ya kusuka na kuunda serikali ili kulinda na kuweka akiba kwa ajili ya kutoa huduma bora kwa Wananchi badala ya kuwa na matumizi makubwa kwa watu wachache tu Mwisho wa siku tuko mwaka wa 60 madarakani bado changamoto za maendeleo na ustawi wa raia ziko pale pale.

Na nyie viongozi na vigogo mnaokula Jasho letu basi kuweni na huruma hata kidogo basi.

Nawatakia utumishi mwema na uchapa kazi watumishi wote wa umma waadilifu kwa Ajili ya Mama Tanzania.


========

Ufafanuzi juu ya Mfumo wa Mahakama nchini

Mfumo wa Mahakama wa Tanzania una Mahakama ya Mwanzo (Primary Court), Mahakama ya Wilaya (District Court), Mahakama ya Hakimu Mkazi (Resident Magistrate's Court), Mahakam Kuu (High Court) na (Mahakama ya Rufani (Court of Appeal), hii inamaanisha kuna Mahakama za aina 5 na mahakama ya Rufani ndio ya daraja kubwa kabisa, kwamba ukifika mahakama hiyo maamuzi yao ndio ya mwisho kwa Tanzania

Mahakama ya Rufani Tanzania ina Majaji 31 na Marekani ina majaji 179 na kwenye upande wa Supreme Court ndio ina Majaji 9.

Kenya wana mfumo wa Supreme Court ambayo ina Majaji 7, na hii ni baada ya kufanya mabadiliko kwenye katiba yao mwaka 2010 baada ya vurugu za uchaguzi. Mahakama hii Kenya kwa kiasi kikubwa ni kwaajili ya kusikiza kesi za Uchaguzi kwenye nafasi ya Urais.

Uganda pia wana Supreme Court, ambako wao wana Majaji 10, na kwao pia Mahakama hii kwa kiasi kikubwa inasikiliza kesi zinazohusu Uchaguzi wa Urais.

Ili kuwa na Supreme Court nchini Tanzania inabidi mabadiliko yafanyike kwenye Katiba kwasababu Mfumo wa Mahakama unatengenezwa kutokana na Katiba.
 
2018 February Hayati Dr Magufuli wakati akiwapisha majaji alisema kuna majaji wakati wa Likizo wanaenda kula bata nje ya nchi na familia zao.

Hayati aliongeza kwa kusema anawafatilia kwa ukaribu kuona hizo pesa wanazitoa wapi.

Bahati Mbaya Mwenyezi Mungu alimchukua kabla hajafanya ukarabati na muundo mpya wa taasisi hiyo nyeti ya utoaji haki.
 
Court of appeal - mahakama ya rufaa (rufani)

Supreme court - mahakama turufu (hazipo Tanzania).

Mahakama za rufaa Marekani zina majaji 179, ambapo Bongo ni kama idadi uliyosema ya 32.

Hata hivyo, una wazo muhimu licha ya taarifa batili.
Na bado hao 31 hawatoshi.

Kesi mahakama ya rufani huchukua wastani wa miaka 2 ndio Ije kusikilizwa huko kuna mrundikano wa kesi nyingi mno,

Inawabidi majaji hao kuzunguka kwa katika kanda maalum kuzisikiliza.
 
2018 February Hayati Dr Magufuli wakati akiwapisha majaji alisema kuna majaji wakati wa Likizo wanaenda kula bata nje ya nchi na familia zao.

Hayati aliongeza kwa kusema anawafatilia kwa ukaribu kuona hizo pesa wanazitoa wapi.

Bahati Mbaya Mwenyezi Mungu alimchukua kabla hajafanya ukarabati na muundo mpya wa taasisi hiyo nyeti ya utoaji haki.
Magufuli alikuwa kiongozi mzuri tukubali tukatae pamoja na mapungufu yake kama binaadamu
 
Na bado hao 31 hawatoshi.

Kesi mahakama ya rufani huchukua wastani wa miaka 2 ndio Ije kusikilizwa huko kuna mrundikano wa kesi nyingi mno,

Inawabidi majaji hao kuzunguka kwa katika kanda maalum kuzisikiliza.
Kazi ipo......basi tuongeze wawe 100
 
Court of appeal - mahakama ya rufaa (rufani)

Supreme court - mahakama turufu (hazipo Tanzania).

Mahakama za rufaa Marekani zina majaji 179, ambapo Bongo ni kama idadi uliyosema ya 32.

Hata hivyo, una wazo muhimu licha ya taarifa batili.
Unajichanganya Kwetu Supreme ndio hiyo ya Rufani......tunaongelea mahakama za juu bila kujali Grades za kila nchi. Lakini tuelewani kwa marekani ndio mahakama ya juu na tanzania ndio ya juu pia.
 
Na bado hao 31 hawatoshi.

Kesi mahakama ya rufani huchukua wastani wa miaka 2 ndio Ije kusikilizwa huko kuna mrundikano wa kesi nyingi mno,

Inawabidi majaji hao kuzunguka kwa katika kanda maalum kuzisikiliza.
Kwanini wasitumie TEHEMA? wanazunguka kutatuta posho pekee wala hawana nia njema, kuna kesi zingine ni za kijinga kwanini wasizitute?
 
2018 February Hayati Dr Magufuli wakati akiwapisha majaji alisema kuna majaji wakati wa Likizo wanaenda kula bata nje ya nchi na familia zao.

Hayati aliongeza kwa kusema anawafatilia kwa ukaribu kuona hizo pesa wanazitoa wapi.

Bahati Mbaya Mwenyezi Mungu alimchukua kabla hajafanya ukarabati na muundo mpya wa taasisi hiyo nyeti ya utoaji haki.
Yeye mwenyewe alikuwa ni mla rushwa mzuri sn
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom