Mahakama yaamuru kupigwa mnada nyumba ya mjane ili kumfidia aliyeumia mguu kwa ajali ya bodaboda

Mahakama yaamuru kupigwa mnada nyumba ya mjane ili kumfidia aliyeumia mguu kwa ajali ya bodaboda

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Mjane mmoja aliyejulikana kwa jina la Beatrice Lyimo, mkazi wa Mbezi Makabe, jijini Dar es Salaam, yupo kwenye maumivu makali baada ya mahakama kutoa uamuzi kuwa nyumba yake ipigwe mnada mnamo Machi 10, mwaka huu, ili alipwe fidia abiria aliyekuwa amebebwa na bodaboda kugongwa na gari lililokuwa likiendeshwa na marehemu mumewe, na kusababisha abiria huyo kuvunjika mguu.

Akizungumza na Global TV Online, mjane huyo alisema kuwa baada ya ajali hiyo kutokea maeneo ya Mbezi Magufuli, mumewe alijitolea kuwapeleka hospitali dereva wa bodaboda na abiria, lakini abiria huyo alikataa na kusema kuwa atapelekwa na ndugu zake.

Hata hivyo, mumewe aliendelea kumhudumia dereva wa bodaboda hadi akapona.

Baadaye, walipokea wito kutoka kwa abiria aliyekuwa kwenye bodaboda, na alipokwenda kumuona alimlaumu kwa kutomfuatilia tena.

Mumewe alimueleza kuwa alimwomba kumtibu lakini alikataa, hivyo alidhani kuwa hakuhitaji msaada wake.

Abiria huyo akaomba alipwe shilingi milioni tano, lakini mumewe alikataa na badala yake alipokea barua kutoka kwa mwanasheria wa abiria huyo, akimtaka kulipa fidia ya shilingi milioni 200.

Mumewe aliomba suala hilo liende mahakamani. Shauri lilipofikishwa mahakamani, washtaki hawakufika siku ya kwanza, lakini mumewe alienda.

Kwa bahati mbaya, alipokuwa akirudi nyumbani, alipata ajali mbaya maeneo ya Mbezi Kibanda cha Mkaa na kufariki dunia.

Hivyo, walimuomba mjane huyo kuendelea na kesi, na hatimaye ikaamuliwa kuwa nyumba yake iuzwe kwa thamani ya shilingi milioni 35 ili alipwe fidia ya shilingi milioni 24 kwa abiria aliyekuja kuvunjika mguu, pamoja na shilingi milioni 10 za usumbufu.

Jambo hili linamuumiza sana mjane huyo kwani hana kazi, mumewe amefariki, na pia ana watoto wadogo.

 
Kuna boda amegonga mtoto mtaani kwetu. Kamvunja mfupa wa kiungo flani muhimu.
Boda katoa 35,000 tu.
Kasusa kuchangia matibabu mengine, kabadili namba ya simu, alivyo kosa akili anaendelea kufanya kazi jirani na nyumbani kwa mgonjwa.
Angeona hii angekimbia mji.
Pikipiki haina bima, dereva hakuwa na leseni.
 
Sio mjuzi wa sheria kabisa, lakini, Pana hujuma hapo, malipo ya ajali hufanywa na bima ambayo huwepo kwenye chombo cha moto, kibaya nadhani huyo aliyegongwa ni mchawi mbaya Sana, hilo ni game!, inachezwa na mahakama, na wapuuzi katika kudhulumu.
Serekali izuie ujinga huu.
 
Mjane mmoja aliyejulikana kwa jina la Beatrice Lyimo, mkazi wa Mbezi Makabe, jijini Dar es Salaam, yupo kwenye maumivu makali baada ya mahakama kutoa uamuzi kuwa nyumba yake ipigwe mnada mnamo Machi 10, mwaka huu, ili alipwe fidia abiria aliyekuwa amebebwa na bodaboda kugongwa na gari lililokuwa likiendeshwa na marehemu mumewe, na kusababisha abiria huyo kuvunjika mguu.

Akizungumza na Global TV Online, mjane huyo alisema kuwa baada ya ajali hiyo kutokea maeneo ya Mbezi Magufuli, mumewe alijitolea kuwapeleka hospitali dereva wa bodaboda na abiria, lakini abiria huyo alikataa na kusema kuwa atapelekwa na ndugu zake.

Hata hivyo, mumewe aliendelea kumhudumia dereva wa bodaboda hadi akapona.

Baadaye, walipokea wito kutoka kwa abiria aliyekuwa kwenye bodaboda, na alipokwenda kumuona alimlaumu kwa kutomfuatilia tena.

Mumewe alimueleza kuwa alimwomba kumtibu lakini alikataa, hivyo alidhani kuwa hakuhitaji msaada wake.

Abiria huyo akaomba alipwe shilingi milioni tano, lakini mumewe alikataa na badala yake alipokea barua kutoka kwa mwanasheria wa abiria huyo, akimtaka kulipa fidia ya shilingi milioni 200.

Mumewe aliomba suala hilo liende mahakamani. Shauri lilipofikishwa mahakamani, washtaki hawakufika siku ya kwanza, lakini mumewe alienda.

Kwa bahati mbaya, alipokuwa akirudi nyumbani, alipata ajali mbaya maeneo ya Mbezi Kibanda cha Mkaa na kufariki dunia.

Hivyo, walimuomba mjane huyo kuendelea na kesi, na hatimaye ikaamuliwa kuwa nyumba yake iuzwe kwa thamani ya shilingi milioni 35 ili alipwe fidia ya shilingi milioni 24 kwa abiria aliyekuja kuvunjika mguu, pamoja na shilingi milioni 10 za usumbufu.

Jambo hili linamuumiza sana mjane huyo kwani hana kazi, mumewe amefariki, na pia ana watoto wadogo.

View attachment 3252053
Dah!.. Dunia hii Kuna mambo ya kuhuzunisha sana
 
Sio mjuzi wa sheria kabisa, lakini, Pana hujuma hapo, malipo ya ajali hufanywa na bima ambayo huwepo kwenye chombo cha moto, kibaya nadhani huyo aliyegongwa ni mchawi mbaya Sana, hilo ni game!, inachezwa na mahakama, na wapuuzi katika kudhulumu.
Serekali izuie ujinga huu.
Siku zote ukipata shida inayohusiana na sheria ,wewe tafuta mwana sheria akusaidie vinginevyo utapewa hukumu hata ya mtu mwingine, tatizo ni kutokujua sheria ,kazi ya bima ni kudeal na ajali sio mtu binafsi
 
Siku zote ukipata shida inayohusiana na sheria ,wewe tafuta mwana sheria akusaidie vinginevyo utapewa hukumu hata ya mtu mwingine, tatizo ni kutokujua sheria ,kazi ya bima ni kudeal na ajali sio mtu binafsi
Kama gari au bodaboda ya matehemu ilikuwa na bima hata third party inatakiwa iwalipe wahusika (third parties) fidia na si kuuza mali zake. Hapa inawezekana chombo cha marehemu hakikuwa na bima.
 
Hii kesi na maamuzi yake ni ya kimagumashi sana.

1. Gari haikuwa na bima ?
2. Deni la marehemu linakwendaje kufidiwa na mjane?
3. Kwanini huyo mhanga alikataa kusaidiwa na marehemu kwa gharama za marehemu akiwa hai then aje kumfungulia mashitaka baadae akidai fidia?
 
Back
Top Bottom