Maharage Chande: Tuache kupeana maneno tamutamu; bei ya Tsh 27,000/= haitoshi kuunganisha umeme

Maharage Chande: Tuache kupeana maneno tamutamu; bei ya Tsh 27,000/= haitoshi kuunganisha umeme

Nimesikiliza huyu mkurugenzi nikabaki nimeduwaa. Hivi concept ya serikali kusambaza umeme ikoje? Nilidhani kwamba gharama za kuunganisha zingekuwa as minimum as possible ili waunganishe wateja wengi halafu fedha zirudi kwa kuuza units za umeme. Ndiyo maana makampuni ya simu yanatafuta yenyewe fedha kwa ajili ya infrastructure installation (kuweka minara na vituo kadhaa then returns zao wanazipata kutoka kwa wateja kupitia airtime, msg na miamala.
 
Leo tarehe 23.02.2022 mkurugenzi wa TANESCO, MAHARAGE CHANDE ameongea na vyombo vya habari kwa kueleza umma kuwa hakuna umeme wa tsh 27, 000/= tuache kupeana maneno matamu matamu katika kuendesha shirika hilo. Amesema ni vigumu sana kutofautisha mjini na vijijini kwani wote wanahitaji huduma hiyo kitu ambacho inasababisha shirika hilo kujiendesha kwa hasara kubwa!

Aidha kwa maoni yangu waziri wa nishati na Naibu wake je wakati wakiwasilisha taarifa mbalimbali za utendaji wa shirika hilo hawakai na wataalamu wakaambiwa kuhusu bei hizo za kuunganishiwa umeme?

Kutokana na kauli hizo kati ya waziri na mkurugenzi wa Tanesco ni kauli zipi ambazo umma utakuja kuziamini kutokana na mkanga'nyiko huo ambao hauleweki wa umeme wa tsh 27,000/=?

Ni hatari sana kwa mkurugenzi wa Tanesco kuambia umma kuwa unawezaje kununua tv ya sh 1,000,000/= halafu uhitaji umeme wa tsh 27000/= akumbuke kuwa hii nchi ni ya kwetu sote hata hivyo kutokana na nyakati tulizopo tulihitaji umeme wa gharama ya chini na siyo kukatisha tamaa umma kuwa hakuna umeme wa tsh 27,000/=.


Kwa hali hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana kila sababu kufatilia kwa karibu utendaji wa shiraka hilo na Wizara ya Nishati kwa ujumla kwani tayari wananchi wameshaanza kutokuwa na imani na watendaji wa Tanesco na wizara husika.
Sawa ni hasara kwa 27,000 walitoe kwenye monopoly waanzishe mashirika 3 au 4 yashindane kama mashirika ya simu tuone
 
Leo tarehe 23.02.2022 mkurugenzi wa TANESCO, MAHARAGE CHANDE ameongea na vyombo vya habari kwa kueleza umma kuwa hakuna umeme wa tsh 27, 000/= tuache kupeana maneno matamu matamu katika kuendesha shirika hilo. Amesema ni vigumu sana kutofautisha mjini na vijijini kwani wote wanahitaji huduma hiyo kitu ambacho inasababisha shirika hilo kujiendesha kwa hasara kubwa!

Aidha kwa maoni yangu waziri wa nishati na Naibu wake je wakati wakiwasilisha taarifa mbalimbali za utendaji wa shirika hilo hawakai na wataalamu wakaambiwa kuhusu bei hizo za kuunganishiwa umeme?

Kutokana na kauli hizo kati ya waziri na mkurugenzi wa Tanesco ni kauli zipi ambazo umma utakuja kuziamini kutokana na mkanga'nyiko huo ambao hauleweki wa umeme wa tsh 27,000/=?

Ni hatari sana kwa mkurugenzi wa Tanesco kuambia umma kuwa unawezaje kununua tv ya sh 1,000,000/= halafu uhitaji umeme wa tsh 27000/= akumbuke kuwa hii nchi ni ya kwetu sote hata hivyo kutokana na nyakati tulizopo tulihitaji umeme wa gharama ya chini na siyo kukatisha tamaa umma kuwa hakuna umeme wa tsh 27,000/=.


Kwa hali hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana kila sababu kufatilia kwa karibu utendaji wa shiraka hilo na Wizara ya Nishati kwa ujumla kwani tayari wananchi wameshaanza kutokuwa na imani na watendaji wa Tanesco na wizara husika.
Kwaninimtu analipia ili kuunganishiwa umeme lakini vifaa vinakuwa Mali ya TANESCO?
 
Wanachokosea Tanesco ni kutaka pesa ya papo papo kwa huduma ambayo mtu lazima atumie baada ya kuunganishwa.

Wapige hesabu gharama halisi, Kisha mwananchi alipie 30% ya gharama halisi siku ya kwanza baada ya hapo 70% alipie kidogo kidogo kila anponunua umeme.

Unaweza kukata 40% ya kila pesa inayowekwa kwenye meter husika mpk kumaliza deni.

Dawasa wameweza kutoa maji ya mkopo mpaka raia wa chini kabisa mwenye kibanda ana Bomba la maji wao Tanesco kwa nini hawafikirii nje ya box?
 
Telecom and electronics engineer.......tujipange 27000 itaua Kampuni sio halisi acha kijijini walipe 27k
Mkuu utaiuaje TANESCO wakati bei hiyo ya 27, 000/- ni kwa ajili ya
vijijini chini ya miradi wa REA. Tatizo la Tanesco ni kuwa na bajeti kubwa ya Matumizi ya Kawaida wakati bajeti ya Miradi ni ndogo. Mradi wa REA ni msaada toka Ugaibuni na ilitakiwa tufungiwe bure. Leo TANESCO inataka kuuteka mradi ambao ulikuwa unafanya kazi zake kwa ufanisi. Waacheni watu wa vijijini waendelee na REA yao, mbona ninyi wa town mnafaidi sana: lami, maji, mwendokasi, viwanja vikubwa vya michezo n.k
 
Leo tarehe 23.02.2022 mkurugenzi wa TANESCO, MAHARAGE CHANDE ameongea na vyombo vya habari kwa kueleza umma kuwa hakuna umeme wa tsh 27, 000/= tuache kupeana maneno matamu matamu katika kuendesha shirika hilo. Amesema ni vigumu sana kutofautisha mjini na vijijini kwani wote wanahitaji huduma hiyo kitu ambacho inasababisha shirika hilo kujiendesha kwa hasara kubwa!

Aidha kwa maoni yangu waziri wa nishati na Naibu wake je wakati wakiwasilisha taarifa mbalimbali za utendaji wa shirika hilo hawakai na wataalamu wakaambiwa kuhusu bei hizo za kuunganishiwa umeme?

Kutokana na kauli hizo kati ya waziri na mkurugenzi wa Tanesco ni kauli zipi ambazo umma utakuja kuziamini kutokana na mkanga'nyiko huo ambao hauleweki wa umeme wa tsh 27,000/=?

Ni hatari sana kwa mkurugenzi wa Tanesco kuambia umma kuwa unawezaje kununua tv ya sh 1,000,000/= halafu uhitaji umeme wa tsh 27000/= akumbuke kuwa hii nchi ni ya kwetu sote hata hivyo kutokana na nyakati tulizopo tulihitaji umeme wa gharama ya chini na siyo kukatisha tamaa umma kuwa hakuna umeme wa tsh 27,000/=.


Kwa hali hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana kila sababu kufatilia kwa karibu utendaji wa shiraka hilo na Wizara ya Nishati kwa ujumla kwani tayari wananchi wameshaanza kutokuwa na imani na watendaji wa Tanesco na wizara husika.
Huyu ni Mkurugenzi bwege! Ni makosa ya rais kuendelea kuamini kwamba 'vijana' wanaweza kuendesha mashirika makubwa kama haya bila uzoefu. Siyo yeye tu, ilikuwa hivyo kwa NHC ya mchechu, PPF ya Erio, nk. Mashirika makubwa ya uzalishaji hutakiwi kumpa mtu asiye na rekodi ya mafanikio ktk nchi yeyote ile! Hilo ni jaribio la kishenzi tu!

Tanesco haipati faida kwa kuunganisha umeme. Tanesco wangeweza hata kuunganisha bure maana vyote vinavyolipiwa na mteja ni mali yao. Nguzo, nyaya, mita na upuuzi wote ni mali ya Tanesco sasa kwa nini anataka mteja alipie? Yeye auze umeme kwa faida, basi!
 
Back
Top Bottom