Mahmoud Abbas kama wenzake amedanganya tu.Hajaenda Gaza

Mahmoud Abbas kama wenzake amedanganya tu.Hajaenda Gaza

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Alipokuwa nchini Uturuki wiki iliyopita kiongozi wa mamlaka ya Palestina alihutubia bunge la nchi hiyo na kujigamba kuwa akirudi nyumbani atakwenda Gaza kwani eneo hilo ni sehemu ya Palestina na hatoruhusu litawaliwe na Israel.Wabunge wa bunge walimshangilia sana.

Tangu arudi ni wiki sasa na hakuna taarifa iwapo tayari ameingia eneo hilo kukagua uharibifu uliofanyika.Ahadi yake hii ni sawa na zile zilizotolewa na zinazoendelea kutolewa na wenzake bila vitendo.

Iran ameahidi mengi kuhusiana na Gaza na bado hawajatenda lolote.Uturuki nayo hivi karibuni ilikuja na kauli nzito iliyotoa matumaini kwa wapalestina.Hata Misri nayo imekuwa ikitoa maneno matupu huku wapalestina wakiuliwa upande wa pili tu wa mpaka.

Hayo yakitokea upande wa waliotarajiwa kuwa watetezi wa wanawake na watoto wa Palestina,viongozi wa Marekani wanaendelea kumiminika Israel na kutoa kauli ambazo ni kama kuilinda Israel kwa kuwatisha Hamas na watawala wa mashariki ya kati ili wakubaliane na matakwa ya Israel.
 
Hicho kizee ndio kinawamaliza wa Palestine, watu wake wanawapa infomation Israel na Yule Mohamed Dahlan. Kizee kina itetea Israel kuliko Palestine
 
Alipokuwa nchini Uturuki wiki iliyopita kiongozi wa mamlaka ya Palestina alihutubia bunge la nchi hiyo na kujigamba kuwa akirudi nyumbani atakwenda Gaza kwani eneo hilo ni sehemu ya Palestina na hatoruhusu litawaliwe na Israel.Wabunge wa bunge walimshangilia sana.
Tangu arudi ni wiki sasa na hakuna taarifa iwapo tayari ameingia eneo hilo kukagua uharibifu uliofanyika.Ahadi yake hii ni sawa na zile zilizotolewa na zinazoendelea kutolewa na wenzake bila vitendo.
Iran ameahidi mengi kuhusiana na Gaza na bado hawajatenda lolote.Uturuki nayo hivi karibuni ilikuja na kauli nzito iliyotoa matumaini kwa wapalestina.Hata Misri nayo imekuwa ikitoa maneno matupu huku wapalestina wakiuliwa upande wa pili tu wa mpaka.
Hayo yakitokea upande wa waliotarajiwa kuwa watetezi wa wanawake na watoto wa Palestina,viongozi wa Marekani wanaendelea kumiminika Israel na kutoa kauli ambazo ni kama kuilinda Israel kwa kuwatisha Hamas na watawala wa mashariki ya kati ili wakubaliane na matakwa ya Israel.
Kwa kiongozi mzuri anayejielewa hawezi kuwatetea magaidi wa Hamas
Huoni walivyokaa kwa amani na Israel bila kushambuliwa
Na yule ni mplastina kabisa achana na wewe mwarabu mweusi wa mchmbawima unatetea magaidi
Stupid
 
Siku wakifika Ramalah ndio ataona umuhimu wa kutetea haki
 
Ukiangalia Al Jazeera dah jamaa no pro hamas hatari kwenye head to head ya Hassan Leo kakutana na prof myahudi Hassani hajafurukuta leo
 
Hicho kizee ndio kinawamaliza wa Palestine, watu wake wanawapa infomation Israel na Yule Mohamed Dahlan. Kizee kina itetea Israel kuliko Palestine
ACha dharua wewe mwarabu mweusi
Yule ni mpalestina mwenye uchungu na nchi yake
Hawezi kuingiza nchi yake kwenye matatizo Kama magaidi wa Hamas
Wewe unajiona mwarabu Sana kwa kuvaa kanzu na kobasi
Una akili kuliko Wamisri , Jordan na nchi zingine za kiarabu asili wanaunga mkono Israel

Jiongeze usiwe mwarabu Koko usiye na akili
 
Mnataka Abas afanye nini? Kwanza atapita wapi ili afike Gaza? Yeye yuko West bank labda apite Misri au Jordani, hawezi kuingia Gaza bila kibali cha Israel na ulinzi wa Israel vinginevyo Hamas watamuua halafu waseme ni Israel, hamas wana hali mbaya sana hawana cha kupoteza, wamepigika vya kutosha, faraja yao imebaki ya kiroho kwa Allah na kupewa bikira 72 endapo watakufa, ili katika ulimwengu wa kimwili wameshapoteza matumaini.
 
Mnataka Abas afanye nini? Kwanza atapita wapi ili afike Gaza? Yeye yuko West bank labda apite Misri au Jordani, hawezi kuingia Gaza bila kibali cha Israel na ulinzi wa Israel vinginevyo Hamas watamuua halafu waseme ni Israel, hamas wana hali mbaya sana hawana cha kupoteza, wamepigika vya kutosha, faraja yao imebaki ya kiroho kwa Allah na kupewa bikira 72 endapo watakufa, ili katika ulimwengu wa kimwili wameshapoteza matumaini.
Nani anakuambia Gaza hata wanataka kumuona.
 
Strategy.
Ametengeneza relevance,moral bargain na leverage.
Hapo watu wamekaa wanasubiri itakuwaje Abbas akifika Gaza!
HAMAS NA FATAH wakiungana Ushindi ni DHAHIRI kwa Palestine.
 
Mahamoud Abbas ni Mkristo,Vita havimchomi sawasawa moyoni.
Hii ni Vita ya Imani,Fatah wanaangalia kama observers tu,🥲.
Lakini wakifika muafaka Fatah na HAMAS,vita vitaisha Haraka.
Huyo Abbas hafai kabisa ni kibaraka wa USA.

 
Abbas ameshatuma ombi Kwa Netanyahu.. anachosubiri ni majibu tu... na Mo. Abbas amesema anataka kuingia Gaza kwa kupitia border la Israel na sio Egypt.. Mtihani ni anao Netanyahu kwani Abbas anatafuta ujiko tu kwani Hamas walishasema hawataki PA after wao na kwa ujio wa Abbas watajua mipango ishasukwa na vile vile kama mpango wa Israel utakuwa umeharibika Abbas ni political Gain tu nae aonekane yupo na Hamas...

Kibaya Hamas wanaweza mburuza hadi kifo akumbuke Fatah walivyouliwa na Hamas kwa kurushwa chini from maghorofani na wengine walifungwa kamba na kuburuzwa barabarani hadi wakabakia mifupa
 
Mo. Abbas ni kiongozi mkubwa na kwa umri wake ni vigumu kumchukilia kama akili zake zipo sawa.. ndio maana watu wa usalama huwa wanachukua maamuzi magumu kumzuia.. yule kwa umri wake anaweza sema anataka kwenda Disco n.k au aendeshe gari mwenyewe bila ulinzi kisa yeye ni raisi watu wa uslama wanachukua maamuzi magumu ya kumzuia hata kama akiwafukuza kazi
Mara ya kwanza umeongea kwa akili.
 
Watu pekee wenye uwezo wa kutekeleza ahadi pale Middle East ni wayahudi.
Baada ya ugaidi wa 0ct 7 waliapa kuwasaka na kuwaua magaidi pamoja na viongozi wao popote pale walipo na matokeo yake tumeyaona.
 
Watu pekee wenye uwezo wa kutekeleza ahadi pale Middle East ni wayahudi.
Baada ya ugaidi wa 0ct 7 waliapa kuwasaka na kuwaua magaidi pamoja na viongozi wao popote pale walipo na matokeo yake tumeyaona.
Wewe ahadi gani walizo tekeleza, ngojea nikukumbushe kama unapoteza akili hukumbuki walicho kiongea.

1 Tutaifuta Hamas, je wameifuta.

2 Hatutaongea na Hamas je vipi hapo.

3 Tutawauwa viongizi wao, sa walio wauwa wangapi? Yahya Sinwar yupo. Mohamad Al Dhaifu yupo na wengi tu bado wapo. Yule Ismail Haniya hawakumuwa wao, inasemekana ni US ndio kamuwa na pili yule ni mtu wa siasa sio askari 😄

4 Tutaiteka Gaza kwa week tatu, mpaa leo hawakuweza kupata ushindi wa military strategy na kusema wataka ile area kiusalama.

We sijui ahadi gani unayo iongelea, ile ya kulilia silaha kaishiwa na kulazimisha wananchi wake waingie jeshini kwa nguvu.
 
Hicho kizee ndio kinawamaliza wa Palestine, watu wake wanawapa infomation Israel na Yule Mohamed Dahlan. Kizee kina itetea Israel kuliko Palestine
Mohammed Dahlan anatafutwa kwa ukibaraka wake
 
Back
Top Bottom