Mahojiano ya Rais Samia na BBC yataongeza maswali na sio majibu

Mahojiano ya Rais Samia na BBC yataongeza maswali na sio majibu

Rais anaingilia kesi iliyoko mahakamani. Kwa kauli yake hiyo aliyotoa tayari keshamuweka hakimu katika wakati mgumu

Kwa jinsi ilivyo mahakama zetu zinafanya kazi kwa tone ya rais. Kwa maneno marahisi hakimu/ Jaji tayari ameshaandikiwa hukumu iweje. Hatuna mahakama ya kutoa haki kinyume na mtazamo wa rais.
 
Leo kwenye interview kaupigwa mwingi sana..kikeke kalabiwa juu mpaka anakosa cha kuuliza. Kila swali anapata jibu sahihi mpaka na yeye anatungisha kichwa cha kukubali jibu murua...

Yale yalikuwa ni majibu na sio majawabu. Imeisha hiyo.
 
Leo kwenye interview kaupigwa mwingi sana..kikeke kalabiwa juu mpaka anakosa cha kuuliza. Kila swali anapata jibu sahihi mpaka na yeye anatungisha kichwa cha kukubali jibu murua...
Itabd waje na Agenda nyingine
 
Kwenye hili la Mbowe mama kajiharibia sana ,sijui kama anashauriwa na wanao mpenda!
Kile kinachodaiwa ni makosa ya awamu ya sita mnasema mama hashauriwi vizuri.lawama zinaelekezwa kwa washauri wake.kana kwamba yeye ni too immature.

Ila 'Makosa' yanayotajwa kutokea wakati wa awamu ya tano ni ya magufuli peke yake.kana kwamba hakuwa na washauri wake.
 
Kama umemsikiliza akihojiwa na salim kikeke hajashindwa swali hata moja, kikete kaishia kutingisha tu kichwa cha kukubali kwa kila swali...
Hapa ni kwamba yale mafisi yatakosa pa kushikia, kama yalipanga angefeli basi imekula kwao...
Salimu kikeke alijua wazi anaenda kuleta mjadala sio kuwapa watu majibu.
 
Kama umemsikiliza akihojiwa na salim kikeke hajashindwa swali hata moja, kikete kaishia kutingisha tu kichwa cha kukubali kwa kila swali...
Hapa ni kwamba yale mafisi yatakosa pa kushikia, kama yalipanga angefeli basi imekula kwao...
Ukiwa mjinga, unaweza kuamini kuwa mtu akiropoka chochote baada ya kuulizwa, basi ameweza kujibu.
 
Umeonaje mama yako asiye dhalimu?

Sio dhalimu kama lile dubwasha lako lililoko motoni, yeye anaiga tembo kunya, na uzuri mama wa kambo yuko mwenyewe humu humu jukwaani tunampa ukweli wake.
 
Sio dhalimu kama lile dubwasha lako lililoko motoni, yeye anaiga tembo kunya, na uzuri mama wa kambo yuko mwenyewe humu humu jukwaani tunampa ukweli wake.
Siyo dhalimu kama lile dubwasha lako!

Na anaupiga mwingi! Magaidi ndani! Alafu kumbe yalijificha Nairobi!

Mi 10 kwa mama
 
Salimu kikeke alijua wazi anaenda kuleta mjadala sio kuwapa watu majibu.

Hapana sio majibu bali majawabu. Majibu yanaweza kuwa yoyote kama mama wa kambo alivyofanya hata kama sio sahihi, lakini majawabu ni yale yaliyo sahihi, kitu ambacho mama wa kambo hakufanikiwa.
 
Ukweli natamani kuwa mshauri wa Rais. Rais wetu ni muungwana sana. Ana mtazamo chanya kuhusu taifa. Ila kupitia mahojiano ya leo watu wanaofikiri sana atakuwa kama washauri walitakiwa wabuni maswali na majibu yote baada ya mahojiano.
Kama mama anaongea kwa kumaanisha NI lazima ajue.

1. Tofauti ya chaguzi na tume zetu za uchaguzi ndio zinazopelekea minyukano ya kisiasa baada ya uchaguzi. Hatuwezi kujilinganisha na nchi za Magharibi kwani uchaguzi wetu uacha makovu makali na yasiyovumilika.

2. Hata Ulaya mabadiliko kufikia Demokrasia ya kweli yalipitia kwenye misuguano na mijadala mikali. Democrasia haikutua tu tokea mbinguni. Kuna French Revolution, Chartisim na Ludism Uingereza na zilikuwa mbaya sana. Kama wapinzani wakihisi hawatendewi haki lazma watashinikiza mabadiliko.

3. Mbowe hakukamatwa peke yake Mwanza, Je wenzake wote ni magaidi.

4. Kwanini mashtaka ya Ugaidi yatokee Mara baada ya ishu ya Katiba?

5. Pia onyo la chokochoko lilitolewa kabla na Rais na Kama alimaanisha wale wanaodai Katiba. Mbowe alipinga vikali Sana kupitia Twitter. hivyo tayari kulikuwa na mabishano juu ya suala la Katiba Kati ya Raisi na Mbowe juu ya Katiba na hili la Ugaidi likaja gafla.

6. Ulipuaji visima vya mafuta ungemsaidiaje Mbowe kisiasa?

7. Magaidi wengi huwa na uhusiano, mfano Alqaida, Alshababu, ISS na Boko Haramu na mengine karibu yote hushirikiana na kusaidia kwa namna moja. Je Mbowe Yuko na uhusiano na kundi lipi la Ugaidi?

8. Kundi la kigaidi linaloongozwa na Mbowe ni lipi? Au ndio CHADEMA.

9. Ni Silaha zipi na mafunzo yapi ya kigaidi CHADEMA humiliki?

10. Viongozi wapi Mbowe aliwalenga kuwaua na kwa namna gani na silaha zipi.

Hayo ndio majibu ambayo dunia inategemea kujua. Na ndio maana dunia inaomba ushahidi.

Nje ya misukosuko na Polisi ukweli CHADEMA kimeepuka kwa 100 asilimia kuanzisha vurugu kwa namna yoyote ile, kuvamia , kupiga watu au kumiliki silaha ata mawe tu.

Nje ya CCM CHADEMA Sasa ndio taasisi iliyojijenga zaidi kila kona Tanzania.

Tujipe nafasi ili kilakitu kikiwa wazi mahakamani Tumjue vizuri gaidi Mbowe Kama ni Osama wa Tanzania. Ila Kama itakuwa kesi ya danadana itatuchafua Sana.

Lazma Raisi afikirie Mara mbili mbili na asimame na ukweli na atafute washauri wapya. Hili swala likiwa la kufungwa litamchafua Sana.

Kuna hatua mama alipiga Sana kwenye utawala Bora. asiruhusu mawazo na Iman za kinaz zikamrudisha nyuma.



Tatizo la Tanzania vyombo vya usalama vimeingizwa sana kwenye siasa. Tatizo lingine ukisha ingiza vyombo vya usalama kwenye kazi na siasa utakuwa na matatizo makubwa sana mfano angalieni uchaguzi na wizi wa kura 2020 yaani mgombea anapata kura zero hata kwenye kituo ambacho yeye kapiga kura! Sasa kama nchi ni kwanini tulitumia mabilioni kwenye uchaguzi kama pesa zinapotezwa hivi kwa shughuli ambazo ni za kudanganya wananchi. Hatuwezi kuacha kumlaumu Hayati Magufuli kwa hili kafanya makosa makubwa sana kwa kuingiza usalama na polisi kwa kiasi hiki serikalini. Sasa wanajiona wenyewe ndiyo wanajua wafanye nini kuanzia ulinzi mpaka siasa
 
LEO MAMA KATUANGUSHA SANA WATETEZI WAKE SIAMINI KAMA ANGEWEZA KUJIINGIZA KWENYE MAHIJIANO AMBAYO YAMELETA MASWALI KULIKO MAJIBU

SUALA ZIMA LA KUKAMATWA NA KUPEWA UHAINI MBOWE TULIAMINI ATALIMALIZA KATIKA HALI AMBAYO ISINGEMUUMIZA KISIASA LAKINI LEO KATUMBUKIA MAZIMA KWENYE MTEGO WA MAADUI zake HASA NDANI YA CCM AMBAO WANATAKA KUMUWEKA KWENYE HALI YA TAHARUKI NA KUKOSA UTULIVU ILI UTAWALA WAKE UKOMEEE 2025

SANA SANA HAKUA HATA NA HAJA YA KUJIBU HILO SWALI ANGESEMA TU KESI IKO MAHAKAMANI

MAMA LEO KAANGUSHA WANAOMTAKIA MEMA NDANI YA CCM NA HATA NJE YA CCM

WAKATI HAYA YAKITOKEA ULINZANI NDANI YA CCM UNAENDELEA KUWA IIMARA

MAMAA ANATAKIWA MAOMBI ILI ATULIZE AKILI
 
Tunamshukuru Mungu kwa kutuondolea lile jitu liovu bila damu kumwagika. kwa sasa tuko na mama wa kambo, na inaeleweka mama wa kambo si mama.
Kabisa lile jitu lenu ovu mungu wenu aliliondoa bila damu kumwagika.
Na sasa tuko vizuri hadi magaidi sasa yanakamatwa, kumbe lilie jitu ovu lilikuwa linalea magaidi!

Nashauri huyu mama kwa kuwa siyo dhalimu aipige miaka elfu kabisa, tunakuwaje na magaidi nchini?
 
Back
Top Bottom