Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 33,679
- 49,841
Utakuta wanachuo wanatembea kwa kufuatana kama kumbi kumbi; mwanaume hataki kumuacha mwanamke, na mwanamke naye hataki kumuacha mwanaume.
Mmoja akienda maktaba, mwenzake anamfuata, hivyo hivyo hata kwenye magrupu ya 'discussion'. Ulikuwa ukiingia kwenye vyumba vyao, utakuta matunda, juisi, wine n.k zimejaa kwenye friji; sisi wengine tuliishia kutamani tu.
Kulikuwepo na dada mmoja alikuwa na chura hatari sana, ilikuwa kila ukikutana naye lazima uishiwe pumzi; ingawa baadhi ya watu waliowahi kumuona huko nyuma, walikuwa wanasema hiyo chura ameitengeneza. Halafu miaka hiyo, ndio vipedo vimeingia, alikuwa akivipiga vinamtoa hatari. Kwa upande wangu niliishia kutamani tu, kwa sababu sikuwa na meno.
Nilikuwa kila binti nikimtongoza hapo chuoni, wananipiga kalenda, na mwisho wa siku nikawa najiongeza, kuwa hapa nimekataliwa. Baadaye nilikuja kugundua, kwa sababu nilikuwa navaa rafu sana, nilikuwa navaa mashati makubwa huku nyuma yanaachia mkia kama wa mjusi ,halafu sichomekei, pia nywele nilikwa naziacha ziwe ndefu.
Baada ya kuona chuoni sipati, nikaanza harakati za kutafuta wapenzi kwenye vyuo vingine pamoja na wafanyakazi. Ikawa kila wikiendi inabidi nisafiri nikakutane na mwenzangu.
Changamoto zilianza baada ya kuhitimu chuo, hakuna kazi hakuna hela, maisha yamesimama, wote niliokuwa nao tukapotezana kwenye mawasiliano, akabaki mmoja tu alisoma 'pspa' akawa amepata kazi sehemu ya kujishikiza; tukawa tunaendelea naye mpaka kuja kubeba ujauzito.
Kutokana na harakati za maisha, ikanilazimu tuwe mbali mpaka mtoto alipozaliwa; nimekuja kuonana naye amekuwa mama mtu mzima kwa sababu alikuwa amenizidi miaka kama 3 pia ana ule mwili mkubwa; ukichangia na ukuaji wa mwili baada ya kujifungua, akawa anaonekana kama mama kwangu. Kwa hiyo hatukuweza tena kuendelea, ila alikuja kuolewa na mtu mwingine.
Je, katika harakati zako za masomo, zilikupatia mahusiano ya kudumu?
Mmoja akienda maktaba, mwenzake anamfuata, hivyo hivyo hata kwenye magrupu ya 'discussion'. Ulikuwa ukiingia kwenye vyumba vyao, utakuta matunda, juisi, wine n.k zimejaa kwenye friji; sisi wengine tuliishia kutamani tu.
Kulikuwepo na dada mmoja alikuwa na chura hatari sana, ilikuwa kila ukikutana naye lazima uishiwe pumzi; ingawa baadhi ya watu waliowahi kumuona huko nyuma, walikuwa wanasema hiyo chura ameitengeneza. Halafu miaka hiyo, ndio vipedo vimeingia, alikuwa akivipiga vinamtoa hatari. Kwa upande wangu niliishia kutamani tu, kwa sababu sikuwa na meno.
Nilikuwa kila binti nikimtongoza hapo chuoni, wananipiga kalenda, na mwisho wa siku nikawa najiongeza, kuwa hapa nimekataliwa. Baadaye nilikuja kugundua, kwa sababu nilikuwa navaa rafu sana, nilikuwa navaa mashati makubwa huku nyuma yanaachia mkia kama wa mjusi ,halafu sichomekei, pia nywele nilikwa naziacha ziwe ndefu.
Baada ya kuona chuoni sipati, nikaanza harakati za kutafuta wapenzi kwenye vyuo vingine pamoja na wafanyakazi. Ikawa kila wikiendi inabidi nisafiri nikakutane na mwenzangu.
Changamoto zilianza baada ya kuhitimu chuo, hakuna kazi hakuna hela, maisha yamesimama, wote niliokuwa nao tukapotezana kwenye mawasiliano, akabaki mmoja tu alisoma 'pspa' akawa amepata kazi sehemu ya kujishikiza; tukawa tunaendelea naye mpaka kuja kubeba ujauzito.
Kutokana na harakati za maisha, ikanilazimu tuwe mbali mpaka mtoto alipozaliwa; nimekuja kuonana naye amekuwa mama mtu mzima kwa sababu alikuwa amenizidi miaka kama 3 pia ana ule mwili mkubwa; ukichangia na ukuaji wa mwili baada ya kujifungua, akawa anaonekana kama mama kwangu. Kwa hiyo hatukuweza tena kuendelea, ila alikuja kuolewa na mtu mwingine.
Je, katika harakati zako za masomo, zilikupatia mahusiano ya kudumu?