Mahusiano chuoni huwa kama 'drama'

Mahusiano chuoni huwa kama 'drama'

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Utakuta wanachuo wanatembea kwa kufuatana kama kumbi kumbi; mwanaume hataki kumuacha mwanamke, na mwanamke naye hataki kumuacha mwanaume.

Mmoja akienda maktaba, mwenzake anamfuata, hivyo hivyo hata kwenye magrupu ya 'discussion'. Ulikuwa ukiingia kwenye vyumba vyao, utakuta matunda, juisi, wine n.k zimejaa kwenye friji; sisi wengine tuliishia kutamani tu.

Kulikuwepo na dada mmoja alikuwa na chura hatari sana, ilikuwa kila ukikutana naye lazima uishiwe pumzi; ingawa baadhi ya watu waliowahi kumuona huko nyuma, walikuwa wanasema hiyo chura ameitengeneza. Halafu miaka hiyo, ndio vipedo vimeingia, alikuwa akivipiga vinamtoa hatari. Kwa upande wangu niliishia kutamani tu, kwa sababu sikuwa na meno.

Nilikuwa kila binti nikimtongoza hapo chuoni, wananipiga kalenda, na mwisho wa siku nikawa najiongeza, kuwa hapa nimekataliwa. Baadaye nilikuja kugundua, kwa sababu nilikuwa navaa rafu sana, nilikuwa navaa mashati makubwa huku nyuma yanaachia mkia kama wa mjusi ,halafu sichomekei, pia nywele nilikwa naziacha ziwe ndefu.

Baada ya kuona chuoni sipati, nikaanza harakati za kutafuta wapenzi kwenye vyuo vingine pamoja na wafanyakazi. Ikawa kila wikiendi inabidi nisafiri nikakutane na mwenzangu.

Changamoto zilianza baada ya kuhitimu chuo, hakuna kazi hakuna hela, maisha yamesimama, wote niliokuwa nao tukapotezana kwenye mawasiliano, akabaki mmoja tu alisoma 'pspa' akawa amepata kazi sehemu ya kujishikiza; tukawa tunaendelea naye mpaka kuja kubeba ujauzito.

Kutokana na harakati za maisha, ikanilazimu tuwe mbali mpaka mtoto alipozaliwa; nimekuja kuonana naye amekuwa mama mtu mzima kwa sababu alikuwa amenizidi miaka kama 3 pia ana ule mwili mkubwa; ukichangia na ukuaji wa mwili baada ya kujifungua, akawa anaonekana kama mama kwangu. Kwa hiyo hatukuweza tena kuendelea, ila alikuja kuolewa na mtu mwingine.

Je, katika harakati zako za masomo, zilikupatia mahusiano ya kudumu?
 
Kuna couple moja chuo ilikuwa ya mfano kuanzia walimu mpaka wanafunzi wote walikuwa wanaijua tukajua watakuja kuoana aisee walipomaliza chuo yule demu alipata ujauzito wa mwanaume mwingine huku yule jamaa yake alikuwa mkoa mwingine kikazi ndo nikajua kweli mademu wanajua kuigiza
 
Vyuoni pisi zinaolewa na kutoa mimba kibao halafu zikitoka hapo zinapigwa chini zinaingia mtaani kusaka wanaume upya. Mnaooa wasomi mnaoa wake za watu huku mkijidanganya eti huyu hajawahi kuolewa wala kuzaa utafikiri ndoa ni harusi na cheti. Watu vyuoni wanaolewa kabisa wanaishi kama mke na mume kwa miaka miwili+.

Ila waoeni tu msiogope lakini mjue kuwa mnaoa wake za watu na haina tofauti sana na kuoa singo maza. Nao wakikutana na waume zao hawa wa vyuoni kupasha kiporo ni kama kawa...na wengi wana maumivu makali wanayokuja nayo kwenye ndoa zao mpya. Matokeo yake ni shida tupu yaani...Too much psychological baggages and trauma [emoji706][emoji706][emoji706][emoji706][emoji706]
 
Utakuta wanachuo wanatembea kwa kufuatana kama kumbi kumbi; mwanaume hataki kumuacha mwanamke, na mwanamke naye hataki kumuacha mwanaume.

Mmoja akienda maktaba, mwenzake anamfuata, hivyo hivyo hata kwenye magrupu ya 'discussion'. Ulikuwa ukiingia kwenye vyumba vyao, utakuta matunda, juisi, wine n.k zimejaa kwenye friji; sisi wengine tuliishia kutamani tu.

Kulikuwepo na dada mmoja alikuwa na chura hatari sana, ilikuwa kila ukikutana naye lazima uishiwe pumzi; ingawa baadhi ya watu waliowahi kumuona huko nyuma, walikuwa wanasema hiyo chura ameitengeneza. Halafu miaka hiyo, ndio vipedo vimeingia, alikuwa akivipiga vinamtoa hatari. Kwa upande wangu niliishia kutamani tu, kwa sababu sikuwa na meno.

Nilikuwa kila binti nikimtongoza hapo chuoni, wananipiga kalenda, na mwisho wa siku nikawa najiongeza, kuwa hapa nimekataliwa. Baadaye nilikuja kugundua, kwa sababu nilikuwa navaa rafu sana, nilikuwa navaa mashati makubwa huku nyuma yanaachia mkia kama wa mjusi ,halafu sichomekei, pia nywele nilikwa naziacha ziwe ndefu.

Baada ya kuona chuoni sipati, nikaanza harakati za kutafuta wapenzi kwenye vyuo vingine pamoja na wafanyakazi. Ikawa kila wikiendi inabidi nisafiri nikakutane na mwenzangu.

Changamoto zilianza baada ya kuhitimu chuo, hakuna kazi hakuna hela, maisha yamesimama, wote niliokuwa nao tukapotezana kwenye mawasiliano, akabaki mmoja tu alisoma 'pspa' akawa amepata kazi sehemu ya kujishikiza; tukawa tunaendelea naye mpaka kuja kubeba ujauzito.

Kutokana na harakati za maisha, ikanilazimu tuwe mbali mpaka mtoto alipozaliwa; nimekuja kuonana naye amekuwa mama mtu mzima kwa sababu alikuwa amenizidi miaka kama 3 pia ana ule mwili mkubwa; ukichangia na ukuaji wa mwili baada ya kujifungua, akawa anaonekana kama mama kwangu. Kwa hiyo hatukuweza tena kuendelea, ila alikuja kuolewa na mtu mwingine.

Je, katika harakati zako za masomo, zilikupatia mahusiano ya kudumu?
Mkuu umenichekesha sana.Kwamba shati kubwa nyuma kama mkia wa mjusi na afro imekubali?Hizo ndiyo pigo zetu masela wa hip hop!Warembo walipoteza bahati.Anyway,mimi nilikuwa mpole hadi natoka masomoni.
 
Kuna couple moja chuo ilikuwa ya mfano kuanzia walimu mpaka wanafunzi wote walikuwa wanaijua tukajua watakuja kuoana aisee walipomaliza chuo yule demu alipata ujauzito wa mwanaume mwingine huku yule jamaa yake alikuwa mkoa mwingine kikazi ndo nikajua kweli mademu wanajua kuigiza
Huwa inatokea hivyo
 
Sikuwahi kua na mahusiano chuo..sijui ndiyo nilikua mshamba🤔
 
Back
Top Bottom