Mahusiano kwa sasa yamekuwa kama ajira ya kudumu kwa wanawake wa kizazi hiki

Mahusiano kwa sasa yamekuwa kama ajira ya kudumu kwa wanawake wa kizazi hiki

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
Kuna muda mwanamke yupo na wewe kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa sababu ni masikini hana chaguo lingine la ziada.

Ukweli ni kwamba wanawake wengi tunaotembea nao na wale mliowaoa wanashikilia mahusiano ya mapenzi na wanaume zao kwa sababu wanataka msaada wa kiuchumi.

Ni masikini ,hawana kazi kwa sasa na wewe mwanaume ndio jibu la matatizo yao .Ila kuwa makini na vitu vichache ,wakishaanza kutengeneza pesa na kuipambania wenyewe utaona tu mabadiliko kwenye mahusiano yenu .

Wataanza kuuliza maswali wakiamini tayari wameanza kuwa juu yako.Utasikia wanakwambia wanataka waanze kujitafuta bila uwepo wako. Hayo ni mahesabu makali ambayo wanawake wanakuwa wamepiga kwa bahati mbaya wanaume wengi wanakuwa wahanga kwenye udhalimu wao.

Huo ndio ukweli wanawake wengi matajiri duniani hawajaanzia chini ,Wengi wao wamefaidika na utajiri huo kutoka kwenye talaka za ndoa ,au kupata baadhi ya hisa za makampuni kutoka kwa waume zao au wazazi wa😵prah ni mmoja wa wanawake wachache wanaoweza kusimama na kujitamba kuwa utajiri wake kaanza kuutafuta mwenyewe akiwa chini.

Uchunguzi uliofanywa na Forbes Billionaires unaonesha asilimia kubwa ya wanawake matajiri duniani wameupata kutokana na urithi na talaka.Majina kama Mackenzie Scott na Melinda French Gates hapo kichwani mwangu .Hawa ni baadhi ya wanawake mashuhuri ambao utajiri wao umetokana na mali walizopata baada ya kudai talaka kutoka kwa waume zao.

Angalia Marekani ,wanawake kwa asilimia 70% ndio waanzilishi wakubwa wa talaka. Wanawake wanasukumwa na kuvunja mahusiano ya mapenzi hili wapate nusu za mali kutoka kwa wanaume. Wanaume wanapokonywa mali zao walizozichuma kwa muda mrefu huku wake zao wakifaidika nazo bila hata kuzitolea jasho.

Mawazo ya wanawake wa sasa kwenye mchezo wa mapenzi yanatisha.Unaweza ukadhania yupo na wewe kihisia ,kumbe yupo kihisia za kiuchumi .Siku akipata nafasi nzuri ya kiuchumi lazima atatafuta mlango mwingine wa kutokea nje ya mahusiano aliyokuwa nayo sasa.

Mfumo umetengeneza hizi tabia ,Sheria za mahakama ya Talaka siyo rafiki kwa upande wa wanaume duniani .Kila kitu kinaenda kumfaidisha mwanamke kuanzia urithi wa baadhi ya mali,matunzo ya watoto na vitu vingine vingi .

Mahusiano kwa sasa yamekuwa kama ajira ya kudumu kwa wanawake wa kizazi hiki cha sasa ,kama mwanaume una jukumu binafsi la kulinda mali zako na uchumi wako binafsi .Dunia ya sasa imejaa wanawake ambao wanawatumia wanaume kama ngazi ya kutafuta mafanikio na kutoboa kimaisha .
 
Mahusiano kwa sasa yamekuwa kama ajira ya kudumu kwa wanawake wa kizazi hiki cha sasa ,kama mwanaume una jukumu binafsi la kulinda mali zako na uchumi wako binafsi .Dunia ya sasa imejaa wanawake ambao wanawatumia wanaume kama ngazi ya kutafuta mafanikio na kutoboa kimaisha .🥺🤔🙇🏿‍♂
 
Kuna muda mwanamke yupo na wewe kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa sababu ni masikini hana chaguo lingine la ziada...
Suluhisho la tatizo Kama hilo kwa maoni yangu ni kusainiana Mikataba ya Pre-nuptial Contract kwa Wanandoa tarajali.

Hii itakomesha utapeli katika Ndoa kwa sababu Kama kutatokea talaka baada ya ndoa Basi kila Mwanandoa atavuna kilicho chake ambacho alipanda.
 
Mahusiano kwa sasa yamekuwa kama ajira ya kudumu kwa wanawake wa kizazi hiki cha sasa ,kama mwanaume una jukumu binafsi la kulinda mali zako na uchumi wako binafsi .Dunia ya sasa imejaa wanawake ambao wanawatumia wanaume kama ngazi ya kutafuta mafanikio na kutoboa kimaisha .🥺🤔🙇🏿‍♂
Mackenzie Scott alikuwa mke wa Jeff Bezos aisee aliidai talaka na akapewa umiliki binafsi wa hisa kwenye kampuni ya Amazon. Dunia ya sasa imekuwa na mambo ya ajabu sana.

Melinda French Gates naye kadai talaka mpaka kampromosha Bill Gates na hela zinaliwa tu na Kijamaa na Kijamaa hata hakimpendi Bibie Melinda, na anataka kurudisha majeshi kwa Bill 😄😄😄
 
Jukumu binafsi la kulinda mali zako na uchumi wako binafsi kwa dunia ya sasa iliyojaa wanawake ambao wanawatumia wanaume kama ngazi ya kutafuta mafanikio na kutoboa kimaisha ni KUTOKUOA BASI.

KATAA NDOA KWA NGUVU ZAKO NA KWA AKILI ZAKO ZOTE 😎🤝
 
Suluhisho la tatizo Kama hilo kwa maoni yangu ni kusainiana Mikataba ya Pre-nuptial Contract kwa Wanandoa tarajali.
Hii itakomesha utapeli katika Ndoa kwa sababu Kama kutatokea talaka baada ya ndoa Basi kila Mwanandoa atavuna kilicho chake ambacho alipanda.
Pre naptal contracts zinakubalika katika sheria za Tanzania mkuu?
 
Wewe unaonaje mkuu? Yaani unapambana familia ikae kiuchumi vizuri yeye anawaza magari, nyumba, mashamba na biashara zitakuwa lini ili nimpunyue zote..huyo ni nyoka tena koboko, ukigundua ni kumuwahi tu mmalizane mapema.
Sema weee mwamba sijawahi kukupinga yaani una misimamo ya hali ya juu....🙌🙌🙌🙌

Na unajua kwanini nàkuona mtu wa misimamo 🙌🙌🙌🙌🙌🙌😂😂😂
 
Back
Top Bottom