Maisha halisi nchini Marekani

Wewe nimekielewa vizuri sana mkuu.
 
 

Nimesema inaniruhusu kukaa nje ya marekani miezi 6.

hapo naona hujaelewi ila inawezekana uandishi wangu ndo mbaya
 
Nimesema inaniruhusu kukaa nje ya marekani miezi 6.

hapo naona hujaelewi ila inawezekana uandishi wangu ndo mbaya
You are wrong!

Hakuna kitu kama hicho cha miezi sita!

Nenda kasome barua iliyokuja na green card. Au nenda mitandaoni katafute hiyo stipulation.

Unakujaje kutoa lecture kuhusu ukazi wa USA na mambo ya green card wakati hujui restrictions za green card zikoje ???

Unasema una green card, green card inakuja na barua, barua umepokea husomi! Uzembe mkubwa!
 
Kwani mtu akienda kuishi Marekani lazima atoboe? Change your Stupid and Idiotic Mindset.

Sio lazima atoboe kumbe!!! Huwa wanafuata nini huko sasa🙄🙄🙄 kwa wanavyokuja kutishughulisha heri wangebaki tulime mpunga kyela
Basi kwa hali ya hao wasiotoboa zilivyo wakirudi tukuleteage uwapage msaada
 
Soma hii kutoka serekalini https://help.cbp.gov/s/article/Arti...~:text=If you are a lawful,for 1 year or more.
 
Hii nimeona mara nyingi,Jamaa kaondoka mimi nipo std 1 enzi za maduka ya ushirika kila kitu foleni.

Karejea mwaka juzi katoboa masikio na jeans zilizopauka na kuchakaa.

Sijui shida ni nini lakini nina mifano mingi tu ambayo inakatisha tamaa.


Halafu Wakiambiwa wanang'aka
 
Kwa nini unambishia mdau bila sababu za msingi? Una Green Card ya aina gani ambayo haikuruhusu kukaa nje ya US zaidi ya miezi 6?

Nina Green Card na huwa naondoka US mpaka miezi 9 au 10 na narudi tu bila wasiwasi. Cha muhimu tu usizidishe mwaka. Au mnazungumzia nini?
 
Wapo wabongo wengi hapa hapa Bongo sasa ni wazee wanashinda vijiwe vya kahawa tu , wamerdika na maisha yao ya furaha hapa bongo, tusiwashutumu wa nje


Wa hapa bongo hawatuletea gharama kivileee za kuwasafirisha kurudi nyumbani wakiwa hai au wamefariki

Uafadhali upo buana
 
Sio lazima atoboe kumbe!!! Huwa wanafuata nini huko sasa🙄🙄🙄 kwa wanavyokuja kutishughulisha heri wangebaki tulime mpunga kyela
Basi kwa hali ya hao wasiotoboa zilivyo wakirudi tukuleteage uwapage msaada
Ni kama kutoka Mbeya na kuja Kuishi Dar. Unaweza ukatoboa au usitoboe.
 
Kama Kajinga jinga,ukiangalia logic reason ya kubisha hakuna.
 
Wewe ifakara huku fursa zipo, usiilinganishe ifakara na Kentucky City iakara pesa ipo sana mzunguko wa pesa huko vijijini ni mkubwa sana me na shangaa wanaotaka kwenda State ...

Endelea kulima Mkuu, Dollar zinakuja
Weee kule kwetu mimi siishi huko, nililima yaani kila siku naangalia utabili wa hali ya hewa weee acha presha ilikuwa juuu.
 
Wa hapa bongo hawatuletea gharama kivileee za kuwasafirisha kurudi nyumbani wakiwa hai au wamefariki

Uafadhali upo buana
Mama D, Naogopa sana generalization, niko US siwezi kukueleza nimetuma mara ngapi pesa nyumbani za Matibabu na kusafirisha maiti, si mara moja au mara mbili. Kuchangia misiba ni jadi yetu, daftari la rambi rambi rambi karibu kila msiba utalikuta! Sasa unasemaji kwa mtu aliyeko mbali kama US. Kumbuka si wote Diaspora wanaofariki wanapitishiwa bakuli. Nimeona watu wakichukua Insurance za kukabiliana na mambo hayo, mimi ni mmojawapo, sitaki kumpa burden mtu yoyote wa US hata wabongo wenzangu!
Ndio maana nilisema kama hukuweza ku manage maisha Tanzania hata US inaweza kuwa hivyo! Tuliokuja kuishi Marekani ni sample ya Watanzania wote walioko nyumbani! Wasomi, wabangaizaji, watu wa vijiweni, kila sampuli ya Mtanzania iliyoko bongo iko US pia, tatizo lenu wengi unadhani ukiingia Marekani kuna miracle ina transform your personality! Hapana.

Nilisema mahali pengine kwenye article fulani, kuna wabongo hapa US nikiangalia maisha natamani niwarudishe Tanzania, lakini nikija Tanzania pia kuna jamaa ni wahangaikaji ila wamekosa opportunities natamani ningeweza kuwaingiza Marekani, na kna watu Tanzania wanalilia kuja Marekani nikiwaangalia tu najua Marekani hawatafika popote.

Sijui utasemaje Mama D.
 
Kazi hizo za kada ya chini zipo nyingi sana haswa baada ya corona watu wengi wameacha kazi na hawataki kazi, lakini pia kazi hizo ni ngumu sana kuendesha maisha kwakuwa maisha ni ghali sana kuliko kipato, mfumuko wa bei ni hatari. Wamarekani wengi wanakimbilia Asia kama philipines, Thailand, Vietnam ambako maisha ni rahisi huku wakijaribu kazi za kufundisha kiingereza.

Kazi zipo ila ni hand-to-mouth na ni lazima ujitume ufanye kazi zaidi ya moja kwa siku, sio.mambo ya bongo saa 10 jioni kazi imeisha mpaka kesho.

Lazima uwe unafanya kazi 2 au 3 kwa siku yaani kulala labada masaa manne tu.

Pia kuishi kwa $600 marekani? Naona kama haiwezekani ,hayo yatakuwa ni maisha magumu sana.
Yote kwa yote kama huna la maana bongo bora kujaribu marekani fursa zipo za kukufanya uishi na ulipe bills. Yote kwa yote africa ndio kila kitu, wamarekani weusi wanahamia afrika haswa ghana na gambia kwa kasi sana hawataki kabisa kurudi kwao.
 
😀Ahsante Kaka nitajaribu hii
 
Nakubaliana na wewe kwa sehemu not 100% Rate ya Africa Americans wanaohama sio kubwa hivyo, nimefika Accra ni kweli, lakini kwa Mtazamo wangu African Americans wana picha mbaya ya Africa kuliko hata wazungu! Wachace niliokutana nao wana picha mbaya sana ya Africa! Hata wasomi AfricanAmericans hawapendi kutafuta kazi kama wenzao wazungu! Rate ya Americans wao ondoka Marekani ni baadhi ya Matajiri ili kukwepesha pesa zao zisipwe kodi., lakini mguu mmoja unabakia Marekani, sio kuondoka kimoja.

Nimekaa Bangkok, Thailand wengi wazungu wa wanokwenda huko nikutafuta cheap life, women na mwisho wa siku hawaiishi hata kurudi pesa nyumbani, I mean US.Nenda Bars, Casino za huko, vijana na mabinti wengi toa US, UK au europe kwa ujumla utakuta dizaini hizo! In short most of them they are still searching what to do in life.
Na unaposema Africa kila kitu sijui una maana gani? Na Mmarekani Mweusi juzi alikuwa Mwanza, Shinyanga na Mtwara, amerudi US katika mji amesema hawezi kuishi ni Dar! Amekuwa na sababu nyingi siwezi kuaninisha. Na mfano halisi ya Marekani weusi waliokwama Bongo, ni shida sana kwanza kupata vibali vya kazi, huwa wanahangaika sana, na maisha ni ghali mno Dar, kuitengeneza pesa ya kitanzania kutoa maisha wanayoyataka ni ngumu sana.

Wamrekani wengi hasa weupe wanapenda Africa kuja kufanya kazi kama expartiate! Wanalipwa mno, na hii inafanyika makusudi (hiyo ni topi nyingine) mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…