Maisha magumu mpaka nataka kuwa mshirikina

Maisha magumu mpaka nataka kuwa mshirikina

.. Mkuu, kama hutajali tunaomba ufafanuzi zaidi hapa. Utakuwa umesaidia vijana wetu wengi.
Issue inakuwaje ili kuipata hiyo deiwaka??

Nenda asubuhi na mapema mikocheni industrial area kuulizia deiwaka,kazi haziji kirahisi lazima ufight ,ukifika tafuta vijana wanaosubiri kuingia viwandani mueleze hitaji lako atakupa info jinsi ya kupata mzigo....kazi nyingi za viwandani huwa zinapatikana sana kwasababu mapato yake ni kinyonge!!
 
Maisha magumu sana mpaka nataka kujaribu ushirikina watu wananishauri huenda nyota yangu imefifishwa maana kila jambo linaishia njiani na kuharibika kabla halijafanyika.

Nimeshaahidiwa kazi hata humu JF na baadhi ya members lakini ghafla ukungu unaingia mtu anaingia uzito hatimaye ananipotezea.

Sielewi hatma ya maisha yangu nimepitia maduka ya dawa za kisuna nimeanza na kukoga dawa inaitwa mzizima nimeambiwa pia dawa nyingine inaitwa Msaka Uchawi ukiinywa kama ulilishwa Uchawi basi utatapika sana , nyingine nimeambiwa inaitwa Nyota inasaidia sana kupandisha Nyota , nyingine inaitwa Ufunguo na Mkumbi.

Kuna mtu anataka kunipeleka kwa mganga nikaoshwe Dawa maana si kawaida .
naimbie unapo kaa nikupitie twenzetu ukatibiwe malawi hakuna haja ya passport! Tutashuka hapo kwako sita kamili.lkn uwe uchi wa mnyama.njia panda mtu akikuongeresha piga kimya!!! Hakuoni ila anajaribu
 
Huenda kila aliyefanikiwa ni "mshirikina " ujue Mungu hagawi pesa ila unajitafutia kwa maujanja yako. Endelea kijana ila usiue mtu ujitese mwenyewe. Usiniulize kuhusu kujitesa muulize kalumanzila

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kama unafanya zinaa acha hiyo kitu..kama unaenda kwa mpalange ndio balaa...hivi vitu vijana wengi tunachukulia kawaida ila vinaharibu sana "nyota" za watu..kama huna habari hizo well and good..rudi kwa Mungu sali/omba kwa imani sio lazima uende kanisani au msikitini..Mungu yuko mahala popote..then utaona mabadiliko.
 
Kwakweli sikukusudia kucheka ila kiukweli nilivyoona Heading ya huu uzi nimecheka sana aisee ila ukweli ni kwamba ajira ni janga la dunia kwa sasa ingawa halisemwi kama COVID nk, , , ,
Pamoja na hayo ukosefu wa ajira pia wakati mwingine inahusiswa na imani za kishirikina (Ingawa sina uhakika) lkn kikubwa nadhani ni kuamini kwamba kila jambo na wakati wake!
Hata mimi hapa nilipo nimetafuta ajira sana karibu 3 yrs, kama barua nimetuma sana, nimebadili taaluma karibu mara mbili lkn wapi, nimekwenda hadi kigoma mahali fulani kwa ajili ya mambo hayo ya dawa sijaambulia chochote, mwaka huu January nilitaka kumeza dawa kujiua nilifumaniwa na kupelekwa kwenye maombi, nasikia mapepo yakasema yamenifungia mng'ao wa nyota, , , saiv nimeamua kukaa tu hadi wakati wa Mungu utapofika!
 
Maisha magumu sana mpaka nataka kujaribu ushirikina watu wananishauri huenda nyota yangu imefifishwa maana kila jambo linaishia njiani na kuharibika kabla halijafanyika.

Nimeshaahidiwa kazi hata humu JF na baadhi ya members lakini ghafla ukungu unaingia mtu anaingia uzito hatimaye ananipotezea.

Sielewi hatma ya maisha yangu nimepitia maduka ya dawa za kisuna nimeanza na kukoga dawa inaitwa mzizima nimeambiwa pia dawa nyingine inaitwa Msaka Uchawi ukiinywa kama ulilishwa Uchawi basi utatapika sana , nyingine nimeambiwa inaitwa Nyota inasaidia sana kupandisha Nyota , nyingine inaitwa Ufunguo na Mkumbi.

Kuna mtu anataka kunipeleka kwa mganga nikaoshwe Dawa maana si kawaida .

Kuhusu suala la mipango kuaribika inaweza kuwa mipango yako hukuiweka vizuri hivyo lazima ifeli, kingine May be tu ni changamoto tu katika maisha , endelea tu kupambana, usikate tamaa, omba Mungu .

Cha mwisho kabisa, kama ukiona umefikia mwisho kabisa, sio mbaya ukajaribu upande wa nguvu za Giza . Kabla hujaenda kwa waganga inabid unitafute nikupe mbinu ( Free of charge) msije kusema nafanya biashara. Cha Muhimu tu ukubali kumtumikia shetani kwa nguvu zako zote na usiwe muoga ukiwa unatafuta mafanikio.

As long as huko hai , pambana tu , jaribu kanisani , misikitini kwa waganga, ma sheikh kila sehem tu , ipo sehem utafanikiwa, ukiwa closed minded katika haya maisha hakuna utakachofanya
 
Nenda asubuhi na mapema mikocheni industrial area kuulizia deiwaka,kazi haziji kirahisi lazima ufight ,ukifika tafuta vijana wanaosubiri kuingia viwandani mueleze hitaji lako atakupa info jinsi ya kupata mzigo....kazi nyingi za viwandani huwa zinapatikana sana kwasababu mapato yake ni kinyonge!!

Unaongelea mjin daslaam Lkn watu tupo mikoan uku hali ni balaa
 
Maisha magumu sana mpaka nataka kujaribu ushirikina watu wananishauri huenda nyota yangu imefifishwa maana kila jambo linaishia njiani na kuharibika kabla halijafanyika.

Nimeshaahidiwa kazi hata humu JF na baadhi ya members lakini ghafla ukungu unaingia mtu anaingia uzito hatimaye ananipotezea.

Sielewi hatma ya maisha yangu nimepitia maduka ya dawa za kisuna nimeanza na kukoga dawa inaitwa mzizima nimeambiwa pia dawa nyingine inaitwa Msaka Uchawi ukiinywa kama ulilishwa Uchawi basi utatapika sana , nyingine nimeambiwa inaitwa Nyota inasaidia sana kupandisha Nyota , nyingine inaitwa Ufunguo na Mkumbi.

Kuna mtu anataka kunipeleka kwa mganga nikaoshwe Dawa maana si kawaida .
"Amelaaniwa yule amtegemeaye mwanadamu...."
 
Maisha magumu sana mpaka nataka kujaribu ushirikina watu wananishauri huenda nyota yangu imefifishwa maana kila jambo linaishia njiani na kuharibika kabla halijafanyika.

Nimeshaahidiwa kazi hata humu JF na baadhi ya members lakini ghafla ukungu unaingia mtu anaingia uzito hatimaye ananipotezea.

Sielewi hatma ya maisha yangu nimepitia maduka ya dawa za kisuna nimeanza na kukoga dawa inaitwa mzizima nimeambiwa pia dawa nyingine inaitwa Msaka Uchawi ukiinywa kama ulilishwa Uchawi basi utatapika sana , nyingine nimeambiwa inaitwa Nyota inasaidia sana kupandisha Nyota , nyingine inaitwa Ufunguo na Mkumbi.

Kuna mtu anataka kunipeleka kwa mganga nikaoshwe Dawa maana si kawaida .
Pole brother ila usikate tamaa and the good thing upo dar sehemu ambapo fursa zipo kibao jaribu hata vibarua viwandani coz kwa hapo dar viwanda ni vingi also makampuni ya ulinzi unaweza kupita huko ukaulizia and vigezo sio vigumu na mshahara sio mkubwa sana kivile ila maisha yanasonga na ukijibana unaweza kufanya saving ukapata mtaji ukafanya michakato mingine usisubili sana kaz za ofisin kila la kheri!!!!!!!!!
 
Kama unasali sana na haufanikiwi ujue ushirikina ni njia pekee ya kufanikiwa. Kumbuka maneno aliyoambiwa nabii Issa pale mlimani na shetani
 
Mkuu hali unayo pitia wewe ndio tunapitia vijana wengi sana asikuambie mtu.
nimemshangaa sana[emoji26]
nadhani vijana tuliotoka chuo tunaongoza kupata depression, tunapitia nyakati ngumu mno
 
Back
Top Bottom