Its Pancho
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 15,966
- 26,404
Hatimaye tumefika kileleni
Ila sijajua konda msafi yupo katika hali gani
Ila sijajua konda msafi yupo katika hali gani
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mambo ya mitandaoni bwana yanasikitisha,ninaitwa "mama watoto" na dogo ambae ninaweza kumuoa mama yake na nikawahudumia yeye ,baba yake na wadogo zake nkawapeleka shule
'waasi wote wote ni kitu kimoja ila hugawanyika baadae linapokuja swala la maslahi".
Kwa hio M23 vs FDLR Vs ADF vs Maimai vs RNC wanaweza kua kitu kimoja sio?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Mke wangu naona unalazimisha chai unazonywesha wenzako unataka kila mtu azikubali sio?
We endelea kuelezea kazi zako za ukonda,mambo za 'field' achana nazo unadanganya tu.
Imeisha hio chief.Jiangalie wewe
Hii mitandao.
Kula ulojo na ngisi wa kubanika🙈🙈🙈🙈🙈🙈Kuwa na roho ngumu kama rama unatakiwa ule nini kila siku?
Na mimi..Japo kwa kuchelewa,sijui nilipitwaje hii!!ngija nijiunge
Kuna ile video ya mitandaoni walimpa mashine sokwe kabisa, si akawabadilikia na kuanza kuzipiga walipo? walitoka ndukiWazee, anachosema mtoa Uzi ni kweli kuhusu wajeda wa Congo na hata Burundi. Hawako serious au hawana Ile nidhamu ya jeshi Kama la Tz. Kukuona silaha anakupa kabisa bila shida. Mimi nilienda Burundi Kati ya mwaka 2008, mwenyeji wetu alikuwa mjeshi wa Kule Burundi na alikuwa anaishi kambini. Tulilala kwenye chumba na Cha ajabu kulikuwa na silaha; SMG, G3, na Bastola. Zote zilikuwa na magazine zimejaa na chini risasi zilikuwa zimemwaga Kama rundo la karanga. Nilikuwa na mwenzangu mmoja tuliyeenda nae. Yule mjeda alituambia kuwa, Hali ya usalama kwao ilikuwa tete, yaani jeshi like la watusi lilikuwa haliwaamini wanajeshi waasi wa kihutu waliokuwa wamejumuishwa jeshi. Hivyo, akasema tukiona Hali isiyoeleweka tujilinde. Wote akatupatia bunduki pembeni yetu. Nilishangaa na mm hivyo mnavyoshangaa. Uzuri nilikuwa nimeshapita jkt na nilikuwa nakumbuka kutumia G3 na SMG. Wazee wale hawana nidhamu ya jeshi, amini hivyo.
Ni Serenje sio selenji....Zambia njaa kali, na mademu wao sio wazuri sema wana elimu nzuri na wanachapa kazi hasa...mademu wa bar pale Kapiri Mposhi wanatema yai balaa...Inaendelea sehemu ya Pili.
Kwanza nikili tu kuwa sintojibu comments za watu ntakuwa straight moja kwa moja kwenye story yangu.
Haya basi tuendeleee safari ikawa imeanza alfajiri ya j2 ile wanaume tukaanza kupiga gia kwakweli mwendo wa magari ya IT si wa mchezo kumbuka kesho tumeshaambiwa ifikapo jumanne asubuhi tunatakiwa tumeshavuka boda ya tunduma upande wa pili NAKONDE kuna mizigo pale tunatakiwa tubebe ya wale jamaa imeachwa pale na bus la TaQwa .wazee tukaamsha mashine kama unavyojua gari ikiwa mpya ni kutembea tu mwanzo mwisho...
Jamaa yangu Rama alikuwa mzoefu wa njia check point za maaskali na tochi zinapokaa hivyo ilibidi mimi nikae nyuma yake akiaamsha nami naamsha akipunguza mwendo nami napunguza na kweli bwana mbele unakuta wazee na vitochi vyao wanaomba document na hela ya soda sisi tunachapa mwendo saa nne asubuhi tukanywa supu msamvu-morogoro tukafungasha nyama choma pale duma mwendo hapo sasa speed ikawa ni noma yanii jamaa yangu Rama anakimbia hadi naogopa aise .
Basi mwendo ukawa mwendo kweli kweli pia usisahau abiria tulikuwa tunabeba wa hapa na pale ili kupata kusave angalau kale ka hela ketu kasiishie njiani saa mbili usiku tunaingia Mbeya aise kama sijasahau tukapata hotel pale mwanjelwa sehemu safi tukapaki magari yetu lodge tukala tukalala mapema ili asubuhi tuwahi Tunduma ili tusubiri bus la Taqwa tuchukue mizigo yetu.
Tukalala pale kila mtu nachumba chake kama kawaida Rama akawa na mchuchu wake pale chumbani sijui alikomtoa ila mimi nilivyochoka hakika sikuwa hata na hamu ya demu mzee nikaangusha mapema saa kumi na mbili asubuhi tupo kwenye chuma zetu tunaitafuta Tunduma taratibu kama kawaida tuna vichwa vyetu viwili vitatu .
Saa tatu tupo Tunduma tunakunywa supu tukaonana clearing wa jamaa akafuta bond na kuclear baadhi ya document sisi tukawa tunasubiri mizigo japo jamaa alitutaka tuvuke siku hiyo hiyo upande wa pili lakini tulikata tukamwambia tutasubiri hapa hapa mizigo. Saa nne taqwa ikaingia tukaenda chukua mizigo tukapakia kwa gari mizigo yenyewe ni makapeti ya nyumbani tukafunga vizuri kabisà tulala .
Mapema asubuhi tukaamka tukaka kwenye foleni ya kuvuka boda baada ya kugonga passport zetu kufikia saa nne tukawa tumevuka boda ya tunduma tupo Nakonde jamaa yangu akanishauri tupumzike ili tutembee usiku lli tusipisha na maroli pia kuna kuwa na atuluvi hivyo akashauri tukapumzike mahala jioni ndo tuamshe .ikabidi nimsikilize tukaenda eneo pale pale boda ukiwa pale nakonde unaweza dhai upo tanzania kumbe ni upande wa zambia yani kunamchanganyiko wa wabongo na wazambia kibao.
Saa kumi na mbili tukaamsha aise sikujua.kumbe Zambia kubwa aise tulitembea giza likaingia aise unatembea kilomita hata mia hupishani na gari lolote halafu pori tupu.
Nyie tukafika kwenye kimji fulani kinaitwa SELENJI tukapaki hapo ili tule na tupumzike ebwanae kulala huo mji ni bora kulala kwenye gari kuna baridi seleenji njombe ikasome tukala pale kwenye hotel ya wasomali tukapaki na magari yetu pale tukalala pale asubuhi mapema bila hata kuoga tukaamsha mapema hapo ndipo nilipo anza kuona usumbufu wa askali wa zambia aise mnasemaga askali wetu wetu wanapenda rushwa nenda zambia yani gari mpya anakwaMbia kosa lako gari ni chafu gari hiyo ipo transit aise yote umwachie hata kwacha elfutano tu aise jamaa wana njaa sijapa ona.
Tukawa tunaitafuta mji wa KAPIRI MPOSHI hapo unajionea watu wana uolima aise kule jamaa wanalima serious sijui kwanini kuna njaa namna ile ...zambia kupata wali maharage ni ishu.
Kama sijasahau kutoka selenji kuna mji unaofuata pale unaitwa MPIKA ( mtanikumbusha kama ntakuwanimesahau) aise kile kipande ni hatari kutembea asubuhi sanaa au usiku kumbe wanapiga mawe hatariii wazambia ni washenzii.
Itaendelea.....soon.