Nimeishi mikoani pia nimeishia Dar,kwa kazi ile ile mshahara ule ile nitatoa uzoefu wangu kwenye aspect zifuatazo.
1.Social
A.Ukabila,udini
Dar ni sehemu ambayo haina ubaguzi,ni sehemu unayoweza pata rafiki mpenzi wa kabila,dini,rika na kazi yeyote ile mwenye tabia na shepu unayoitaka.
mikoani unaweza kosa mtu unayemuhitaji,kuna sehemu ukienda hakuna waislamu,zingine hakuna wakristo,zingine hakuna Madaktari,Mainginia wala wanasheria,........yaani unaweza ishi sehemu 80 % ni watu wa kabila moja tu,wanaongea kilugha chao ....Dar huu upuuzi hamna
2.Kibiashara.
Dar kila biashara inafanyika usiku na mchana hakuna kukesha,wateja wakija hawana muda wa kuulizia dini kabila wala umetoka wapi,wanahitaji bidhaa.
Mikoani ni vituko kuna sehemu ukienda kama wewe sio wa kabila lao,hupati wateja hata kama unauza bidhaa bei chini na bora sawa na wao,halafu biashara hazifanyiki muda wote .....hapa kuna sehemu nimefika mjini kabisa eti nimekosa nyama mabucha yamefungwa[emoji1][emoji1787],sasa si uhanithi huu.
Hizi biashara za kudeal na watu mikoani ndio kabisa,yaani daktari uende mkoa flani hujui kilugha chao,wakati kuna kijana kutoka kwao,watu wapo tayari wafe lakini huwagusi.
Tatizo jingine mikoani hamna kila kitu,mfano kanda ya ziwa ni ngumu sana kupata pweza,ngisi na products za baharini wakati Dar kila kitu cha mkoani utakipa kwa bei yeyote ile unayoitaka ......yaani hata sato fresh Dar
watu wanakula tu hawana habari.
3.Usafiri.
Hii sehemu nilipo boda boda ikinyesha mvua hawaendi hata iweje[emoji1787][emoji1787][emoji1][emoji1],wakati Dar hata maradi yapige usiku kucha watu hawana noma kiongozi....halafu mikoani gharama za usafiri ni ghali sana ukilinganisha na Pwani au Dar.....mfano kutoka Dar hadi Kibiti nauli elfu 5,mkoa mwengine kabisa ........kwa umbali huo huo mkoani nauli inaweza fika elfu 15 na usafiri ni wa ovyo mno
Mkoani wafanyakazi wa kawaida wanatumia hadi elfu 5 boda boda,Dar hio ni nauli wa wiki kwa wajanja wengi wanaojulia mji
4.Afya
Dar hospitali ni nyingi sana na maduka ya dawa yanakesha......mkoani kama una emeregency usiku kazi unayo aisee
Hata madaktari ni wachache pia.....yaani hata wazawa wasomi wa mikoani hua hawataki kuishi[emoji1787][emoji16][emoji119]
5.Mzunguko wa pesa
Dar ni mkubwa,viwanda,ofisi etc zipo za kutosha,mkoani ni vya kuhesabu.......kuna mikoa viwanda vya kuajili watu 100,kwa pamoja havifiki hata viwili,yaani kama hujasoma,wewe sio boda boda ulime tu kiongozi[emoji1][emoji1787][emoji1787][emoji119]
6.Giografia.
Mkoani sehemu inayofanana na Dar ni pale makao makuu tu ya mkoa tena kwa asilimia 10% tu..........ambapo utakuta labda baadhi ya watu wa makabila mengine wapo,ukienda wilayani ni vituko vitupu,huko hamna wahindi wala,wachaga,matajiri wao kwa wao tu wanaongea viligha vyao.......[emoji1787][emoji1787][emoji16],ukienda mgeni unaonekana mchawi,makazini/shuleni ndio usiseme watu wanaongea kilugha kazini kawaida tu kumkuta mwalimu anawaelekeza wanafunzi wa lugha za asili[emoji16][emoji16][emoji119]
7.Upatikanaji wa vitu/vyakula.
Mkoani vyakula ni bei rahisi vya kununua ambavyo havijaandaliwa(Raw foods),unaweza pata mkungu hata elfu 3,kuku elfu 5,mayai mia 2........ila changamoto hakuna vyakula vya aina yote.....unajua Dar kila vyakula vipo kutoka mkoa wowote ule Tz.....mikoani vilivyo cheap ni vile tu vinavozalishwa eneo husika.
General Dar ndio penyewe maana utapata unachotaka kutoka mkoa wowote ule.........ukienda mgahawani mikoani ukitaka wali maharage ni kawaida tu kuletewa wali na maharage yaliyochemshwa tu[emoji16][emoji1787][emoji1] ,hamna hata kitunguu, wakati unakuta huo mkoa unaongoza kulima vitunguu,labda na nafaka zinatoa mafuta.....
8.Psychological
Dar huwezi kua mpweke unaweza lazimisha weekend uende beach kula bata,halafu watu wapo social tu mjini mtu hata humjui munapiga tu stori kijiweni fresh tu....unaondoa stress kiaina.
Mkoani kijiweni wanaongea kilugha[emoji1787][emoji16],ukienda mgeni wanamute wanaogopa sana polisi au wanaamini unawachunguza.
9.Ustaarabu
Dar/Pwani ,watu ni wastaarabu tu,....ukienda hospitali watu wanajielewa fresh,mtu kama anajua kitu cha pesa anafight,shuleni walimu wakiagiza wanafunzi mchango wazazi wanatoa fresh tu......mkoani na hivi marehemu shujaaa waliwajaza ujinga,watu wanaweza mpiga hata mwalimu kwa kuchangisha hela ya tuition tu shillingi mia mbili apate chochote[emoji1787][emoji1][emoji1],hospitali Doctor akisema hii dawa haipatikani kanunue,tayari simu kwa DC,.....wakati mtu mtoto wake mwenyewe[emoji1787][emoji1787][emoji16].......yaani watu ni wagumu sana kujiongeza mkoani mtu yupo tayari age aisee........halafu mkoani watu wanapenda
Kuchongeana sana,mwalimu ukiwa u akula wanafunzi msala......ushawahi sikia mwalimu wa Dar kakamatwa na mwanafinzi wa sekondari .......Dar hata mazazi akijua hana noma,anajua huyo mwanafunzi wa kike,dudu kaitaka mwenyewe hajalazimishwa[emoji16].
Kwa Kifupi mkoani sio sehemu ya kuishi kwa mtu anayependa maisha social ya kawaida tu ya kibongo ya kujichanganya popote.......sio sehemu nzuri ya kutafuta maisha na ndio maana vijana wengi wa mkoa wanakuja Dar/Pwani kutafuta maisha.......ushawahi ona kijana wa kizaramo,kindengereko eti ameenda mkoani kutafuta maisha?[emoji1787][emoji1][emoji1]