Maisha ya depo

Unachelewesha sana Story we kijana 😜 ila haya mambo yangenipata kule Songea kama ningeenda 🤭
Mchawi muda rafiki yangu tunakimbizana na majukumu hata huu ninaoubahatisha najitahidi sana kuutumia kuandika siyo jambo ila maandalizi ya kuandika ndiyo yananifanya nichelewe kuandika
 
Mchawi muda rafiki yangu tunakimbizana na majukumu hata huu ninaoubahatisha najitahidi sana kuutumia kuandika siyo jambo ila maandalizi ya kuandika ndiyo yananifanya nichelewe kuandika
Usijali. Huenda tungekutana mimi nilipangiwa Bulombora.😊
 


It is approaching to come............................
Maisha ya depo SEASON -|||
 

MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 26

Hali hiyo ilikuwa ikiwashinda watoto wengi wa kishua na siku moja Wini alinipa dili la swahiba yake mmoja waliosoma wote kuwa anataka kutoroka nilivyompelekea dili hilo Shukrani aligoma kulifanya.

Kiukweli nilikuwa na ukata hivyo nikaichukulia kama fursa nililipiga dili hilo nikitumia nondo zilezile za dili lililopita nikalitoboa na kujivutia tembo wawili.

Kifupi hiyo ndiyo ikawa kazi yangu ambayo haikunitupa kwenye maokoto na baada ya kufanikisha dili hilo Shukrani alianza kunielewa na tukawa tunapiga wote na malipo yakawa ni pasu kwa pasu kwa madili yaliyokuwa yanapitia kwangu.

Sifahamu kwa upande wa Shukrani maana kazi alizokuwa akizileta yeye zilikuwa ni za hela ndogo nilikuwa nikihisi ananipiga ila ulikuwa ni kama msimu wa maembe ambao ulikuwa ni adimu kumkuta inzi ama ngedere aliyekonda.

Hela hizo zilikuwa zikinipiga tafu kwenye shida ndogondogo na nilikuwa sikatiki KIWANI kulikokuwa kukiuzwa mihogo, maandazi na vitafunwa vingine.

WAZALENDO wengi tulikuwa tukijazana huko maana ule muda tuliokuwa tukisimuliwa ulikuwa umefika kwani tulikuwa hatushibi chakula cha MZABUNI kutokana na kazi tulizokuwa tukizifanya si kwamba walipunguza kipimo hapana ila ni matumbo yalikwishatanuka na kibaya zaidi hakukuwa na nyongeza.

Kipindi hiki ndicho kilichoikuza misamiati kama vile KUBASTI yaani kula zaidi ya mara moja ila kwa kujificha maana haikuruhusiwa kwani ukila zaidi ya mara moja ina maana wengine watakosa kwa maana hiyo ule msemo wa SIFA WEPESI haukucheza mbali wakati wa KUBASTI.

Msamiati mwingine ulikuwa ni KIJOGOO ambao unamaanisha kiporo ama chakula kinachohifadhiwa usiku kwa ajili ya kuliwa alfajiri kabla ya kwenda kwenye FATIKI ili upate nishati ya kuisogeza siku nyingine.

Ikumbukwe KIJOGOO ambacho nimekipiga sana si chakula kinachotolewa na MZABUNI ila ni wewe mwenyewe unakitunza aidha baada ya KUBASTI, kubakiza ama kununua KIWANI.

Siku zilizidi kukimbia huku idadi ya watu ikiongezeka hali iliyopelekea kuundwa KOMBANIA ya tano na pia majina ya KOMBANIA yalibadilika kutoka majina ya wanyama hatimaye zikawa herufi.

KOMBANIA ya chui chini ya ST Fred wao waliitwa ALPHA COY (A-Coy), nyingine ni ile ya ST Ustadhati Rehema yaani tembo ikaitwa BRAVO COY (B-Coy), simba ya akina Linda iliitwa CHARLIE COY (C-Coy) na ile ya kwetu ikaitwa DANGER COY (D-Coy).

KOMBANIA iliyoongezeka ilifahamika kwa jina la EAGLE COY (E-Coy) na katika kipindi hiki tukatakiwa tuanze kuvaa vipensi vifahamikavyo kama PICKSHORT na kukatishwa kuvaa suruali za track.

Katika moja ya watu walioathirika na mabadiliko haya alikuwa ni Ustadhati Rehema ambaye aliwagomea kabisa kuvaa nguo hizo.

MADAWILI wengine walikuwa wakiona aibu kuvaa nguo hizo ila iliwabidi wavae maana kila pale walipokuja KOMBANIA walikutana na adhabu.

Rehema yeye adhabu hizo zilionekana kutofua dafu ingawaje wakati mwingine alikuwa akitetewa na maafande.

Haijawahi kuisha nguvu misemo ya wahenga na pale waliposema “Hakuna marefu yasiyo nan cha” ndicho kilichokuwa kikitokea kwa Rehema ambaye alikuwa akibadilika kidogokidogo maana kuna baadhi ya siku alikuwa akifoleni KOMBANIA bila ya kufunika kichwa.

Kutokana na mabadiliko hayo ya siku baada ya siku SERVICEMEN waliokuwa wakitusimamia kwa kipindi hicho walikuwa wakituambia “Kunyweni maji mengi mioyo ielee maana kozi inakaribia kuanza”.

Hatukuwaelewa walikuwa wakimaanisha nini kwani tulikuwa tukiona kozi imeanza kitambo kilichokuwa kimebadilika ni mavazi pekee.

Ratiba ya shamba haswa kuvuna haikuwahi kukoma kwa siku chache kutokana na ukubwa wa shamba na hata hivyo tulikuwa tukivuna kwa nusu siku hatukuwahi kushindia huko.

Siku moja baada ya kutoka shamba tulipewa jukumu la kuhamisha vitu vyetu kwa ajili ya kuishi kwenye MAHANGA ya KIKOMBANIA.

Yaani awali kipindi tunafika walikuwa wakitupeleka kwenye HANGA lolote lile lililokuwa wazi kwa kipindi hicho kabla ya kutuhesabisha namba na kutugawa KIKOMBANIA hivyo ukawa ni wasaa wa kuishi kwenye MAHANGA ya KOMBANIA.

Hali hiyo ilikuwa ikileta wepesi kwenye usimamizi kama ST nina ushuhuda nalo lakini pia haikucheza mbali na kauli ya kihenga isemayo “Ndege wafananao huruka pamoja”.

Tulikuwa tukipata ugumu pale karani akitaka kujua majina ya walinzi wa HANGA na pale anapokosekana mmoja wetu aidha kwa kudoji ama kuumwa tulikuwa tukishindwa kujua HANGA alilopo kwa ajili ya kujiridhisha kama uongozi wa KOMBANIA😆.


Tukiwa katika zoezi hilo tukufu tulisikia filimbi zikipigwa za kutosha kutokea UWANJA WA DAMU ambako kwetu tulishangaa maana haukuwa muda wa chakula na tuliambiwa TUFOLENI huko baada ya chakula cha jioni yaani tulikuwa na KAUTAWALA fulani hivi ka chinichini.

Kitu cha kushangaza ni kuwa waliokuwa wakipiga filimbi hizo walikuwa ni BAKABAKA ambao walikuwa na Matroni Neema na tulipojipeleka sisi tuliambiwa turudi maana yajayo hayatuhusu.

Basi WALIFOLENI askari wa JKT wakiwa na sare zao za KARANGA full combat juu na chini na walifoleni wakiwa na ndoo kila mmoja.

Walianza kupitishwa lokoo na baada ya muda akasikia Matron Neema akisema “Sikia kutoka kwangu, kwa yeyote asiyekuwepo hapa na anastahili kuwepo basi mfikishieni taarifa mwambieni kuwa awe na maelezo ya kutosha kwanini hayupo mahala hapa”.

Aliendelea kusema “Tukianzia kwenye lokoo ya jana tuliwataarifu kuwa leo asubuhi mnatakiwa kwenda shamba kwa ajili ya kutoa mahindi yetu ila nimesikitishwa sana na kiburi mlichokionesha sijui kama mnaweza kunieleza ni sababu zipi ziliwafanya msiende au hamkunielewa”.

Kilitawala kimya cha sekunde kadhaa na baadaye akaendelea “Kimya maana yake hakuna majibu sasa bila kupotezeana muda ambaye anajijua hajaenda naomba ajisogeze pale mwenyewe haijalishi ana sababu au hana tutaelezana tukiwa pale”.

Zoezi hilo lilifanyika na mchujo mkali ukachukua nafasi ambao ulizalisha makundi mawili ya waliosafi na wasiosafi yaani madoja wa kazi.

Baada ya hapo ilisikika kwa mara nyingine sauti ya Matroni Neema “Jana kipindi tunawaambia mkawa mnatuona kama Mchinga Sound vile tuko stejini tunatumbuizasiyo, sawa sasa leo nasisi tutakuwa tunawatizama ninyi mkitumbuiza naomba makamanda wangu kazi ianze”.

Ebwana eeh ilitokea shoo siyo ya kitoto yalikuwa ni masaa matatu yenye ujazo wa DOSO la machozi, jasho na damu.

Wale jamaa walivurugwa siyo kawaida nashindwa hata nisimulie lipi alafu niache lipi ila tulishaanza kuelewa ni kwanini walituambia tunywe maji mengi mioyo ielee.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

************Itaendelea………………………………...
 
Kwa jinsi Kwa jinsi unavosimulia kupitia location mbalimbali hii ,inaonesha moja kwa moja ni 838KJ
 
Story fupi zisizo na continuation isiyoelewela..

Japo K unaelezea vema. Ila unazingua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…