Maisha ya depo

Maisha ya depo

MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 07

Kimya hicho kilichodumu kwa muda mfupi kilivunjwa na maneno ya afande Mvamba ambaye alisema

“Anhaah kumbe mnapenda umbea lakini hamuutaki ukweli, ukweli unauma eeh!”
“Sasa ni hivi ile migomba mnayoiona pale tumeipanda baada ya kuwazika wenzenu ambao nao ni WAZALENDO wa mujibu wa sheria kama nyie wapo wa miaka ya nyuma na wengine ni wa mwaka jana tu hapo”.

“Kwahiyo mjiandae kama mmekuja 200 msijihakikishie mtarudi wote, lazima form six kama 180 hivi wafe alafu wahitimu kama 20 hivi”.

“Na katika hao wazima wanaweza wakawa wanne au watano mana katika mazoezi mtakayokutana nayo kama siyo kifo basi kuna wengine watakuwa vilema”.

"Utakuta huyu kavunjika mguu mwingine hana sikio mara anayefuata shingo imekaa upande mara ukute macho yote anayo ila hayaoni vizuri ama hayaoni kabisa au mwingine akili anazo ila anakuwa hana akili yaani kawehuka ili mradi tu tuwapunguze msimalize wote”.

“Alafu mjue bahati mbaya sana huku hatuna mitihani ya kuwapunguza idadi kama wanavyofanya necta, mitihani yetu huku ni mazoezi na kwenye mazoezi hakunaga chabo wadogo zangu si eti afande Kapanda”

“Ndiyo afande na kama wamefika form six kwa chabo aisee imekula kwao, huku ni bidii tu mazoezini ndo kutakufanya uvuke vikwazo ukiwa legelege mgomba wako utawekwa huku mwanzoni mwa shamba la migomba” alijiubu afande Kapanda.

“Na kitu kingine ambacho hamjui ni kuwa serikali imewaleta huku ili mfe, mbaki wachache ila nyie hamjui tu”.

“Unakuta lijitu linaandaa 50,000 ya nauli linafunga safari mpaka kambini ili lifuate kifo ukiangalia limesoma mpaka form six sasa elimu itakuwa imemsaidia nini”.

“Sasa za ndani ni kuwa baada ya serikali kuona mahitimu yamekuwa mengi mtaani halafu inatupiwa lawama hawayaajiri serikali yetu pendwa vile haitaki kulaumiwa ikaona iwalete jeshini”.

“Mnajua huku jeshini kinatokea kitu gani WAZALENDO?” aliuliza afande Mvamba tukabaki kimya asiwepo hata mmoja wa kumjibu wala kukohoa.

“Anhaah mnakaa kimya ili nisiwaambie ukweli, sasa ukweli ni kuwa huku mnakuja wengi ila mtakufa na kuhitimu wachache kwa maana nyingine wachache sana tena saaaana ndio watakaokwenda chuo”.

“Kule chuo mtapunguzwa kwa mitihani kama kawaida japokuwa watu wa chabo hamtakosekana haswa wale waliostuka wakaacha kuja ila watakuwa wachache mana wengi wao mtakuwa tushawapunguza hukuhuku kwenye shamba letu la migomba”.

“Nina uhakika miaka kumi baadaye wahitimu wasiokuwa na ajira mtaani watakuwa wachache ama hawatakuwepo kabisa na hapo serikali yetu tukufu itakuwa imefanikiwa kuzikwepa lawama nyingi kama ilivyo sasa” aliendelea kututisha afande Mvamba.

Tulibaki kimya kwa muda na hakuna aliyekuwa akinong’ona kwa wakati huo, woga ulituvaa miongoni mwetu kwa kile tulichokuwa tukiambiwa.

Baada ya kumaliza mazungumzo hayo afande Mvamba alituamuru tuhesabu namba.

Tulihesabu kwa usahihi na umakini wa hali ya juu tofauti na awali, afande Kapanda na afande Shadi walihusika kwa kiasi kikubwa kufanikisha hili kwani walituelekeza namna ya kuhesabu na wakasimamia pia zoezi lote mpaka mwisho.

Tulihesabu wote tukiwa tumekaa chini isipokuwa waliohesabu namba 10 wao walisimama na hakukuwa na namba kubwa zaidi ya 10 maana kila ilipofika 10 aliyefuata alianza upya yaani 1.

Tulishangaa namna ilivyokuwa rahisi kuhesabu na hatukujua ni kipi kilichofanya tushindwe hapo mwanzo ila nafikiri ilikuwa ni kitete tu kuwepo eneo lile, eneo ambalo kombati ya jeshi haikuwa tofauti na shamba dress tukiwa mabwenini.

Afande Mvamba aliwaamuru waliosimama wahesabu namba isipokuwa wa mwisho kabisa ambaye aliitika namba 8, walikuwa 23 ambao ni 230 na yule aliyehesabu 8 maana yake tuko 238 namba ambayo haikuwa tofauti na mwanzo.

MADAWILI waliitwa tena mbele wakahesabu namba kwa mara nyingine, walihesabu na walikuwa 47 na kipindi wanaenda bado kidogo na mimi niende ila kuna jamaa alinitonya kuwa mademu ndiyo wanaohitajika.

Akili yangu bado ilikuwa inaniambia kuwa MADAWILI ni wageni na wala sikujua kama tunatofautiana kimaumbo maana sehemu tuliyopo mwanga ulikuwa hafifu na wote tulivaa suruali ya truck na shati kitu ambacho kinafanya tuonekane tunafanana.

Kulibainika kuwepo kwa upungufu wa WAZALENDO watano kama ilivyo mwanzo ila wakati huu aligundua kuwa katika MADAWILI 49 waliosajiliwa wawili hawapo hivyo katika wale watano wasiokuwepo watatu ni wanaume.

Katika kujiuliza wako wapi wengine ndipo afande Shadi alipowaza na kusema huenda wasio kuwepo wakawa ni walinzi wa HANGA, wakateuliwa wanne kati yetu yaani wawili kutoka kila upande wakaangalie idadi ya walinzi waliopo huko.

Nilivuta kumbukumbu ni wapi nilisikia neno hilo nikakumbuka ni kipindi tupo kule ambako tuliacha vitu vyetu tukafuata magodoro afande Shamte aliwaita hivyo wale tuliowakuta nilikumbuka hawakuwa wengi maana wengine walipoulizwa kuwa ni walinzi wa HANGA walikataa.

Niligundua kuwa walinzi wa HANGA ni wale wanaoachwa kutazama usalama wa mali zilizopo mabwenini kwani jeshini bweni hufahamika kwa jina la HANGA.

Tukiwa tunawasubiri waliokwenda kuangalia idadi ya WALINZI WA HANGA masimulizi yaliendelea kama kawaida na kama ilivyo mwanzo afande Mvamba ndiye aliyekuwa msemaji mkuu.

Aliuliza kama kuna swali na ndipo afande Shadi akalirudisha swali la mwanzo lile linalohusu supu kwa atakayevujisha siri za jeshi uraiani.

Afande huyo mzee wa vitisho alisema
“Jeshi linaamini kuwa siri ama habari zinasambaa kwa haraka pale zinapowasilishwa na mwanamke tofauti na mwanamume, kwahiyo kwa sababu wewe kiumbe umetoa siri zetu huko chegani kwenye kusuka ama kwenye kijimeza chenu cha kasusu na sisi tunaamua kuchukua sehemu zako siri ili tuone je, siri iliyotoka ni yetu au ni yako”.

Waliporudi wale jamaa walioagizwa kwenda MAHANGANI walithibitisha uwepo wa walinzi wa HANGA watano kati yao wawili ni MADAWILI na waliobaki ni upande wa pili hivyo idadi ilikaa sawa.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………...
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 08

Baada ya kutimia afande Mvamba aliondoka na kutuacha na afande Kapanda pamoja na afande Shadi ambao walituimbisha mapambio ya jeshi kwa muda mpaka pale aliporudi kwa mara nyingingine.

Awamu hii alikuja na afande mmoja niliyesikia akimuita SAJENTI Pastima ambaye alikuwa na tumbo haswa sidhani kama ningekutana naye mtaani ningeamini kuwa na yeye ni mwanajeshi ama kweli usimdharau usiyemjua mana kwa mwili ule anafanana kabisa na meneja wa bar, cafeteria ama restaurant.

Afande Pastima naye alichukua lokoo na baada ya kujiridhisha kuwa tumetimia alimwambia afande Mvamba aturuhusu ambapo naye alituasa mambo machache kuhusu siku inayofuata na kukasimisha madaraka kwa afande Kapanda.

Afande Kapanda kabla ya kuturuhusu alituambia kuwa ratiba ni ileile watakuja kutuamsha usiku sana, TUTAFOLENI uwanja wa damu na kukimbia MABIO ikifuatiwa na usafi wa mazingira kabla ya kwenda kwenye FATIKI na ratiba nyingine hivyo tunatakiwa kulala macho.

Baada ya maneno hayo tuliruhusiwa kwenda kulala na wakati tunaelekea MAHANGANI kulikuwa na majadiliano mbalimbali haswa juu ya yale yaliyozungumzwa na afande Mvamba na mengineyo mengi.

Nilifika kitandani kwangu na kuweka mazingira sawa na nilipomaliza niliutwaa mwili wangu na kuutupa kitandani kwa ajili ya kuuchapa usingizi.

Mawazo yalikuwa ni mengi kabla sijapatwa na usingizi niliiwaza tangu safari ilipoanza nyumbani hadi kufika kambini pamoja na maswahibu niliyokumbana nayo.

Niliwaza sana kuhusu sehemu iliyoitwa UWANJA WA DAMU, akili ilitengeneza rundo la maswali kwa nini paitwe hivyo? Ama ndiyo sehemu yanapofanyika mazoezi magumu ya kijeshi na hatimaye damu humwagika na kupoteza uhai? maswali yalikuwa ni mengi pasi na majibu.

Sikuwahi kukutana na siku ndefu kuzidi hiyo hali iliyonifanya nitumie muda mrefu kuwaza na hatimaye kuupata usingizi licha ya ukweli kwamba nilichoka sana hivyo nilitegemea kuupata usingizi mapema ila ilikuwa tofauti.

Sikumbuki ni muda gani niliupata usingizi ila nilikuja kustuka majira ya saa 11 alfajiri na vipenga vilivyokuwa vikipulizwa MAHANGANI.

Walikuwa ni maafande waliokuwa wakitusisitiza kuamka haraka iwezekanavyo na kwenda KUFOLENI uwanja wa damu kwani tulikuwa nje ya muda.

Walikuwa pia wakiwakataza wale waliokuwa wakienda kupiga mswaki waliwaambia kuwa watapiga wakirudi kutoka MABIO kwani jambo muhimu kwa wakati huo lilikuwa ni kwenda UWANJA WA DAMU tu basi.

Nilikuwa na shauku kubwa ya kupajua uwanja wa damu hivyo basi ilinibidi nitii maagizo na kuacha kutandika kitanda ilinibidi niongozane na wenzangu kuelekea ilipo Allianz Arena.

Nilitoka nje nikawa naibia uelekeo wa wengi wao uliokuwa ni Kaskazini-Magharibi basi bila ajizi niliungana nao.

Kipindi tunaelekea huko nilikuwa nikiongea na jamaa mmoja ambaye alinifungua baadhi ya vitu na mazungumzo yetu yalikuwa hivi,

“Oya niaje”
“Fresh niambie”
“Poa, hivi huku ndiyo UWANJA WA DAMU”
“Ndiyo mzee si unaliona nyomi lote ndiko linakoelekea KUFOLENI hivyo”
“Anhaa sawa mwanangu mi mgeni nimeripoti jana usiku si unajua tena jeshini huku naogopa kuvamia kundi siyo langu kama yule mshikaji wa jana aliyekuwa anavamia kundi la MADAWILI muda wa lokoo”.

“Daah ila kweli yule mwana alizingua kwahiyo kama afande alikuwa anataka akawapige mashine na yeye angeenda” jamaa aliongea maneno hayo ya kejeli huku akicheka asijue kuwa mtu mwenyewe nilikuwa mimi ingawaje nilijikaza ila moyoni niliumia sikuwa na jinsi zaidi ya kuvunga.

“Ndo hivyo mwanangu na ndiyo maana nikaona nikuulize, hivi na wewe si ni MZALENDO”
“Ndiyo nimemaliza form six na mimi kama wewe”
“Anhaa umekuja jana au juzi”
“Mi nipo hapa tangu day one”
“Anhaah kumbe ushakuwa mzoefu”
“Hamna mwanangu wenyewe wanasema jeshi halizoeleki mambo yanabadilika kile sekunde”.

“Sawa ila siyo kama mimi, hivi MABIO ni kitu gani”
“Ni mbio za kawaida tu wala usiziogope”
“Hamna wala siogopi nataka kujua tu ili niwe na idea ya kile ninachokifanya”
“Sawa ni kama nilivyokwambia ni mbio za kawaida yaani hazina tofauti na mchakamchaka au jogging” alinijibu huku akianzisha mbio kuelekea waliko wenzetu.

Jamaa alinisisitiza tuwahi afande asije akatupa DOSO nilitaka kuendelea kumuuliza ila nikaona kama nitakuwa namkera hivyo nikaona ni muhimu nikafunga bakuli langu.

“Simameni hapo hapo nyie mnaojikuta mnaweza kulala sana” alisikika afande tuliyemkuta sehemu hiyo ambayo ilifahamika kama UWANJA WA DAMU.

Tulimtii na kufanya hivyo na zaidi ya hapo alitutaka tuchuchumae na kuruka kichura chura kuelekea walipo wenzetu waliofika kabla yetu.

Baada ya kusubiri kwa kitambo kidogo afande alituamuru tusimame na kuunda mistari mitatu iliyonyooka na baadaye akatuhesabisha namba.

Kulikuwa na mtiti kwenye kuhesabu namba yaani ni kama tumeanza nursery vile kila muda tulikuwa tukikosea, hesabu zilipokaa sawa tuligawanywa makundi yapatayo matatu.

Kundi la kwanza lililoongozwa na mmoja wetu ambaye nilifahamishwa kuwa alikuwa ndiye mtu wa kwanza kuwasili kambini mapema siku ya kwanza na inasemekana ilikuwa ni asubuhi sana, kwa vile akili yangu haikupenda kujifikirisha sana niliwaza kuwa huenda kwao ni karibu na kambi hiyo.

Jamaa yule aliyefahamika kwa jina la Fred aliteuliwa kuwa kiongozi wetu yaani ST cheo ambacho kilinikumbusha utaratibu uliotumika kupata manahodha wa vilabu vingi vya kihispaniola na timu yao ya taifa.

Wao humteua yule aliyedumu na timu kwa muda mrefu kuliko wote pasi na kujali umri wala kiwango chake ingawaje mpaka inatokea mchezaji anadumu kwa muda wote huo inamaana kiwango kimo na umri unakuwa usogea pia. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………...
 
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 08

Baada ya kutimia afande Mvamba aliondoka na kutuacha na afande Kapanda pamoja na afande Shadi ambao walituimbisha mapambio ya jeshi kwa muda mpaka pale aliporudi kwa mara nyingingine.

Awamu hii alikuja na afande mmoja niliyesikia akimuita SAJENTI Pastima ambaye alikuwa na tumbo haswa sidhani kama ningekutana naye mtaani ningeamini kuwa na yeye ni mwanajeshi ama kweli usimdharau usiyemjua mana kwa mwili ule anafanana kabisa na meneja wa bar, cafeteria ama restaurant.

Afande Pastima naye alichukua lokoo na baada ya kujiridhisha kuwa tumetimia alimwambia afande Mvamba aturuhusu ambapo naye alituasa mambo machache kuhusu siku inayofuata na kukasimisha madaraka kwa afande Kapanda.

Afande Kapanda kabla ya kuturuhusu alituambia kuwa ratiba ni ileile watakuja kutuamsha usiku sana, TUTAFOLENI uwanja wa damu na kukimbia MABIO ikifuatiwa na usafi wa mazingira kabla ya kwenda kwenye FATIKI na ratiba nyingine hivyo tunatakiwa kulala macho.

Baada ya maneno hayo tuliruhusiwa kwenda kulala na wakati tunaelekea MAHANGANI kulikuwa na majadiliano mbalimbali haswa juu ya yale yaliyozungumzwa na afande Mvamba na mengineyo mengi.

Nilifika kitandani kwangu na kuweka mazingira sawa na nilipomaliza niliutwaa mwili wangu na kuutupa kitandani kwa ajili ya kuuchapa usingizi.

Mawazo yalikuwa ni mengi kabla sijapatwa na usingizi niliiwaza tangu safari ilipoanza nyumbani hadi kufika kambini pamoja na maswahibu niliyokumbana nayo.

Niliwaza sana kuhusu sehemu iliyoitwa UWANJA WA DAMU, akili ilitengeneza rundo la maswali kwa nini paitwe hivyo? Ama ndiyo sehemu yanapofanyika mazoezi magumu ya kijeshi na hatimaye damu humwagika na kupoteza uhai? maswali yalikuwa ni mengi pasi na majibu.

Sikuwahi kukutana na siku ndefu kuzidi hiyo hali iliyonifanya nitumie muda mrefu kuwaza na hatimaye kuupata usingizi licha ya ukweli kwamba nilichoka sana hivyo nilitegemea kuupata usingizi mapema ila ilikuwa tofauti.

Sikumbuki ni muda gani niliupata usingizi ila nilikuja kustuka majira ya saa 11 alfajiri na vipenga vilivyokuwa vikipulizwa MAHANGANI.

Walikuwa ni maafande waliokuwa wakitusisitiza kuamka haraka iwezekanavyo na kwenda KUFOLENI uwanja wa damu kwani tulikuwa nje ya muda.

Walikuwa pia wakiwakataza wale waliokuwa wakienda kupiga mswaki waliwaambia kuwa watapiga wakirudi kutoka MABIO kwani jambo muhimu kwa wakati huo lilikuwa ni kwenda UWANJA WA DAMU tu basi.

Nilikuwa na shauku kubwa ya kupajua uwanja wa damu hivyo basi ilinibidi nitii maagizo na kuacha kutandika kitanda ilinibidi niongozane na wenzangu kuelekea ilipo Allianz Arena.

Nilitoka nje nikawa naibia uelekeo wa wengi wao uliokuwa ni Kaskazini-Magharibi basi bila ajizi niliungana nao.

Kipindi tunaelekea huko nilikuwa nikiongea na jamaa mmoja ambaye alinifungua baadhi ya vitu na mazungumzo yetu yalikuwa hivi,

“Oya niaje”
“Fresh niambie”
“Poa, hivi huku ndiyo UWANJA WA DAMU”
“Ndiyo mzee si unaliona nyomi lote ndiko linakoelekea KUFOLENI hivyo”
“Anhaa sawa mwanangu mi mgeni nimeripoti jana usiku si unajua tena jeshini huku naogopa kuvamia kundi siyo langu kama yule mshikaji wa jana aliyekuwa anavamia kundi la MADAWILI muda wa lokoo”.

“Daah ila kweli yule mwana alizingua kwahiyo kama afande alikuwa anataka akawapige mashine na yeye angeenda” jamaa aliongea maneno hayo ya kejeli huku akicheka asijue kuwa mtu mwenyewe nilikuwa mimi ingawaje nilijikaza ila moyoni niliumia sikuwa na jinsi zaidi ya kuvunga.

“Ndo hivyo mwanangu na ndiyo maana nikaona nikuulize, hivi na wewe si ni MZALENDO”
“Ndiyo nimemaliza form six na mimi kama wewe”
“Anhaa umekuja jana au juzi”
“Mi nipo hapa tangu day one”
“Anhaah kumbe ushakuwa mzoefu”
“Hamna mwanangu wenyewe wanasema jeshi halizoeleki mambo yanabadilika kile sekunde”.

“Sawa ila siyo kama mimi, hivi MABIO ni kitu gani”
“Ni mbio za kawaida tu wala usiziogope”
“Hamna wala siogopi nataka kujua tu ili niwe na idea ya kile ninachokifanya”
“Sawa ni kama nilivyokwambia ni mbio za kawaida yaani hazina tofauti na mchakamchaka au jogging” alinijibu huku akianzisha mbio kuelekea waliko wenzetu.

Jamaa alinisisitiza tuwahi afande asije akatupa DOSO nilitaka kuendelea kumuuliza ila nikaona kama nitakuwa namkera hivyo nikaona ni muhimu nikafunga bakuli langu.

“Simameni hapo hapo nyie mnaojikuta mnaweza kulala sana” alisikika afande tuliyemkuta sehemu hiyo ambayo ilifahamika kama UWANJA WA DAMU.

Tulimtii na kufanya hivyo na zaidi ya hapo alitutaka tuchuchumae na kuruka kichura chura kuelekea walipo wenzetu waliofika kabla yetu.

Baada ya kusubiri kwa kitambo kidogo afande alituamuru tusimame na kuunda mistari mitatu iliyonyooka na baadaye akatuhesabisha namba.

Kulikuwa na mtiti kwenye kuhesabu namba yaani ni kama tumeanza nursery vile kila muda tulikuwa tukikosea, hesabu zilipokaa sawa tuligawanywa makundi yapatayo matatu.

Kundi la kwanza lililoongozwa na mmoja wetu ambaye nilifahamishwa kuwa alikuwa ndiye mtu wa kwanza kuwasili kambini mapema siku ya kwanza na inasemekana ilikuwa ni asubuhi sana, kwa vile akili yangu haikupenda kujifikirisha sana niliwaza kuwa huenda kwao ni karibu na kambi hiyo.

Jamaa yule aliyefahamika kwa jina la Fred aliteuliwa kuwa kiongozi wetu yaani ST cheo ambacho kilinikumbusha utaratibu uliotumika kupata manahodha wa vilabu vingi vya kihispaniola na timu yao ya taifa.

Wao humteua yule aliyedumu na timu kwa muda mrefu kuliko wote pasi na kujali umri wala kiwango chake ingawaje mpaka inatokea mchezaji anadumu kwa muda wote huo inamaana kiwango kimo na umri unakuwa usogea pia. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………...

MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 09

ST. Fred aliliongoza kundi la kwanza huku akianzisha wimbo ulionakshiwa na miruzi ambayo ilichangamsha mbio zile hali iliyonifanya nijilaumu kwanini sikuwa miongoni mwao, niliosikia wakiimba.

"Fred: Mdogo mdogo eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Ayeya eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Mdogo mdogo eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Tunayeya eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Hui hai weeh!
Wazalendo: Hai weeh!
Fred: Hai mama weeh!
Wazalendo: Hai weeh!
Fred: Hui hai weeh!
Wazalendo: Hai weeh!
Fred: Hai mama weeh!
Wazalendo: Hai weeh!".

Baada ya muda afande alimtaka mmoja wetu aongoze kundi na kuwafuata waliotutangulia.

Alitokea jamaa mmoja aitwaye Masare ambaye siku za mbeleni tulimuita Shaa Rukh Khan nitakwambia kwanini ila kwa sasa naomba nimuite Masare.

Kupitia yeye hatukuwahi kukimbia kinyonge maana alifanya kila mtu azipende mbio haswa pale alipokimbia naye.

Mwamba hakutufanya tuondoke kinyonge alilianzisha nasi tukamuitikia,

"Masare: Ewiiih!
Sisi: Ewaah!
Masare: Ewiiih!
Sisi: Ewaah!
Masare: Watu walee
Sisi: Watu walee
Masare: Mara woyoo
Sisi: Mara woyoo
Masare: Kwa miruzii
Sisi: Kwa miruziii
Masare: Na mabioo
Sisi: Na mabiooo
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah!
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah!
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah".

Wimbo huu ulikuwa na amsha amsha nyingi pale ulipokuwa ukiimbwa huku ukisindikizwa na miruzi pamoja vigelegele, ulikuwa ni moja ya wimbo pendwa haswa wakati wa mbio ingawaje waanzilishi pia walikuwa na nafasi kubwa kuinua morari wakati wa unaimbwa.

Tulikimbia umbali wa kilometa 2 hivi huku tukibadilisha wimbo huu na ule mpaka tulipofika sehemu iliyopangwa kuwa mwisho wa mbio.

Baada ya makundi yote kukamilisha mbio awamu ya kwenda tulijipanga tena tukaanza mbio za kurejea kambini na moja kwa moja mbio hizo ambazo wao waliziita MABIO ziliishia MAHANGANI ambako tulikwenda kufanya usafi binafsi kwani mbio zile zilituacha na jasho la kutosha mwilini.

Waliopiga mswaki walipiga, walionawa uso na kupiga passport miili yao pia hawakukosekana ila kuna sisi ambao tulikuwa tukijihisi tuko nyumbani tulikuwa kwenye hesabu za kwenda kuoga.

Nilijongea mpaka kitandani kwangu nikalifungua sanduku na kuchukua kila kilichohitajika kwa ajili ya usafi ila nilipoinama uvunguni kuchukua ndoo sikuikuta tayari kuna mtu alikwishaichukua.

Kitu cha kwanza nilifikiri huenda jamaa anayelala sehemu ya juu ya kitanda ndiye aliyeichukua kwa kuwa hakuwepo kwa muda huo.

Nilimuliza jamaa mmoja aliyekuwa kitanda cha pembeni kama alimuona aliyechukua ndoo yangu aliniambia kuwa hakumuona ila kwa jinsi ilivyo mtu huyo hatoweza kuirejesha ila kama nikiiona nitaikumbuka basi nijaribu kuitafuta.

Maneno yale yalinikatisha tamaa kwani hakuna alama yeyote niliyokuwa nikiikumbuka zaidi ya rangi yake hivyo nilibaki kujuta kwa namana ambavyo hela yangu ilipotea kizembe.

Jamaa yule alinipa ndoo yake ambayo kwa wakati ule hakuwa na matumizi nayo ila alinisisitiza nimrejeshee nikishamaliza kwani inahitajika mno kwenye FATIKI.

Vikwazo vilikuwa ni vingi mpaka kufikia hatua ya kuoga kuanzia upatikanaji wa maji mpaka sehemu ya kuoga kote kulihitajika kupanga foleni.

Uchache wa sehemu za kutekea maji na mabafu ndivyo vilikuwa vyanzo vikubwa vya foleni hizo na kwenye mabomba hayo machache yaliyopo maji yalikuwa yakitoka kwa kasi ndogo.

Hali hiyo ilipelekea kuhitajika kwa muda mwingi kujaza ndoo lakini pia walikuwepo wale wa vikombe na makopo kwa ajili kupiga mswaki na kunawa uso wao hawakuhitaji kuwa sehemu ya foleni kwani walikinga muda wowote walipojisikia.

Tukiwa kwenye foleni hiyo ya maji filimbi zilianza kusikika huku baadhi ya maafande wakituamuru tuelekee KOMBANIA.

Tulianza kutawanyika mmoja baada ya mwingine ilinibidi nirudishe mswaki wangu ukiwa na dawa kwani sikufanikiwa kuutumia wala kufanya chochote zaidi ya kupanga foleni ya kusubiria maji na nisiyapate.

Ilinibidi pia niirudishe ndoo ya watu kabla sijaipoteza nilimkuta jamaa akivaa viatu nikamsimulia kilichotokea akaniambia nisijali sana maana tunaenda kufanya usafi kwa muda mfupi kabla ya kurudi tena kujiandaa kwenda kwenye FATIKI.

Hapa sasa nilimuelewa ni kwanini hakujishughulisha wakati ule nikihangaikia maji.

Ilinichukua muda kidogo kujiandaa kwa lengo la kwenda KOMBANIA kwani nilipotoka kwenye MABIO viatu na nguo nilizokimbia nazo nilizivua nikabaki kifua wazi na bukta nikipiga hesabu za kwenda kuoga.

Jirani yangu alikuwa akinisubiri huku akinisisitiza kufanya upesi, ghafla lilitokea kundi la watu ambalo lilikuwa likionekana linakimbizwa.

Nilipomhoji kujua kinachoendelea aliniamuru nishike soksi mkononi na nitumbukize miguu kwenye viatu tusepe nitavaa vizuri mbele kwa mbele ikanibidi nifanye hivyo nasi tukaliunga kwenye lile kundi ambalo hatukujua linakimbizwa na nani.

Tulitoka mkukumkuku hadi KOMBANIA ambako tuliwakuta wengineo ambapo kwangu ndiyo ulikuwa wakati mzuri wa kuangalia kama kuna niliyekuwa nikimfahamu.
Nilimuona jamaa mmoja tuliyesoma naye advance nikamsogelea na kumsalimia alikuwa ni Amos aliyekuwa akisoma CBG.

Katika kumdodosa aliniambia kuwa yeye ni miongoni mwa waliofika siku ya kwanza nilimtania na kumwambia
“nyie ndo mtakuwa wafia jeshi wenyewe, wazalendo haswa na nchi yao”.

Maafande walifika KOMBANIA na kutugawa katika vikundi kadhaa ambavyo wao waliviita VIBANGALA, vilipatikana VIBANGALA 9 na kila kimoja kilikuwa na angalau afande mmoja ambaye alivaa sare tofauti kidogo na zile za wanajeshi niliokuwa nikiwaona mara kwa mara haswa uraiani ama kwenye runinga.

Nilikuwa kwenye KIBANGALA kimoja na Amos tulijipanga mistari mitatu tukaondoka kuelekea eneo la usafi tulilopangiwa tukiongozwa na afande ambaye ndiye aliyekuwa akianzisha nyimbo na alisikika akiimba,

"Afande: Tutampataje kunguru
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Eeeh na mbawa zake za woga
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Ana ka kei kadogo
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Sema mpaka upulize manyoya
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Kunguru yeye wa Zanzibar
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Anakwiba sidiria!
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize". ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………...
 
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 09

ST. Fred aliliongoza kundi la kwanza huku akianzisha wimbo ulionakshiwa na miruzi ambayo ilichangamsha mbio zile hali iliyonifanya nijilaumu kwanini sikuwa miongoni mwao, niliosikia wakiimba.

"Fred: Mdogo mdogo eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Ayeya eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Mdogo mdogo eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Tunayeya eeh!
Wazalendo: Mwendo!
Fred: Hui hai weeh!
Wazalendo: Hai weeh!
Fred: Hai mama weeh!
Wazalendo: Hai weeh!
Fred: Hui hai weeh!
Wazalendo: Hai weeh!
Fred: Hai mama weeh!
Wazalendo: Hai weeh!".

Baada ya muda afande alimtaka mmoja wetu aongoze kundi na kuwafuata waliotutangulia.

Alitokea jamaa mmoja aitwaye Masare ambaye siku za mbeleni tulimuita Shaa Rukh Khan nitakwambia kwanini ila kwa sasa naomba nimuite Masare.

Kupitia yeye hatukuwahi kukimbia kinyonge maana alifanya kila mtu azipende mbio haswa pale alipokimbia naye.

Mwamba hakutufanya tuondoke kinyonge alilianzisha nasi tukamuitikia,

"Masare: Ewiiih!
Sisi: Ewaah!
Masare: Ewiiih!
Sisi: Ewaah!
Masare: Watu walee
Sisi: Watu walee
Masare: Mara woyoo
Sisi: Mara woyoo
Masare: Kwa miruzii
Sisi: Kwa miruziii
Masare: Na mabioo
Sisi: Na mabiooo
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah!
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah!
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah
Masare: Kama hatuondoki vile
Sisi: Anhaah".

Wimbo huu ulikuwa na amsha amsha nyingi pale ulipokuwa ukiimbwa huku ukisindikizwa na miruzi pamoja vigelegele, ulikuwa ni moja ya wimbo pendwa haswa wakati wa mbio ingawaje waanzilishi pia walikuwa na nafasi kubwa kuinua morari wakati wa unaimbwa.

Tulikimbia umbali wa kilometa 2 hivi huku tukibadilisha wimbo huu na ule mpaka tulipofika sehemu iliyopangwa kuwa mwisho wa mbio.

Baada ya makundi yote kukamilisha mbio awamu ya kwenda tulijipanga tena tukaanza mbio za kurejea kambini na moja kwa moja mbio hizo ambazo wao waliziita MABIO ziliishia MAHANGANI ambako tulikwenda kufanya usafi binafsi kwani mbio zile zilituacha na jasho la kutosha mwilini.

Waliopiga mswaki walipiga, walionawa uso na kupiga passport miili yao pia hawakukosekana ila kuna sisi ambao tulikuwa tukijihisi tuko nyumbani tulikuwa kwenye hesabu za kwenda kuoga.

Nilijongea mpaka kitandani kwangu nikalifungua sanduku na kuchukua kila kilichohitajika kwa ajili ya usafi ila nilipoinama uvunguni kuchukua ndoo sikuikuta tayari kuna mtu alikwishaichukua.

Kitu cha kwanza nilifikiri huenda jamaa anayelala sehemu ya juu ya kitanda ndiye aliyeichukua kwa kuwa hakuwepo kwa muda huo.

Nilimuliza jamaa mmoja aliyekuwa kitanda cha pembeni kama alimuona aliyechukua ndoo yangu aliniambia kuwa hakumuona ila kwa jinsi ilivyo mtu huyo hatoweza kuirejesha ila kama nikiiona nitaikumbuka basi nijaribu kuitafuta.

Maneno yale yalinikatisha tamaa kwani hakuna alama yeyote niliyokuwa nikiikumbuka zaidi ya rangi yake hivyo nilibaki kujuta kwa namana ambavyo hela yangu ilipotea kizembe.

Jamaa yule alinipa ndoo yake ambayo kwa wakati ule hakuwa na matumizi nayo ila alinisisitiza nimrejeshee nikishamaliza kwani inahitajika mno kwenye FATIKI.

Vikwazo vilikuwa ni vingi mpaka kufikia hatua ya kuoga kuanzia upatikanaji wa maji mpaka sehemu ya kuoga kote kulihitajika kupanga foleni.

Uchache wa sehemu za kutekea maji na mabafu ndivyo vilikuwa vyanzo vikubwa vya foleni hizo na kwenye mabomba hayo machache yaliyopo maji yalikuwa yakitoka kwa kasi ndogo.

Hali hiyo ilipelekea kuhitajika kwa muda mwingi kujaza ndoo lakini pia walikuwepo wale wa vikombe na makopo kwa ajili kupiga mswaki na kunawa uso wao hawakuhitaji kuwa sehemu ya foleni kwani walikinga muda wowote walipojisikia.

Tukiwa kwenye foleni hiyo ya maji filimbi zilianza kusikika huku baadhi ya maafande wakituamuru tuelekee KOMBANIA.

Tulianza kutawanyika mmoja baada ya mwingine ilinibidi nirudishe mswaki wangu ukiwa na dawa kwani sikufanikiwa kuutumia wala kufanya chochote zaidi ya kupanga foleni ya kusubiria maji na nisiyapate.

Ilinibidi pia niirudishe ndoo ya watu kabla sijaipoteza nilimkuta jamaa akivaa viatu nikamsimulia kilichotokea akaniambia nisijali sana maana tunaenda kufanya usafi kwa muda mfupi kabla ya kurudi tena kujiandaa kwenda kwenye FATIKI.

Hapa sasa nilimuelewa ni kwanini hakujishughulisha wakati ule nikihangaikia maji.

Ilinichukua muda kidogo kujiandaa kwa lengo la kwenda KOMBANIA kwani nilipotoka kwenye MABIO viatu na nguo nilizokimbia nazo nilizivua nikabaki kifua wazi na bukta nikipiga hesabu za kwenda kuoga.

Jirani yangu alikuwa akinisubiri huku akinisisitiza kufanya upesi, ghafla lilitokea kundi la watu ambalo lilikuwa likionekana linakimbizwa.

Nilipomhoji kujua kinachoendelea aliniamuru nishike soksi mkononi na nitumbukize miguu kwenye viatu tusepe nitavaa vizuri mbele kwa mbele ikanibidi nifanye hivyo nasi tukaliunga kwenye lile kundi ambalo hatukujua linakimbizwa na nani.

Tulitoka mkukumkuku hadi KOMBANIA ambako tuliwakuta wengineo ambapo kwangu ndiyo ulikuwa wakati mzuri wa kuangalia kama kuna niliyekuwa nikimfahamu.
Nilimuona jamaa mmoja tuliyesoma naye advance nikamsogelea na kumsalimia alikuwa ni Amos aliyekuwa akisoma CBG.

Katika kumdodosa aliniambia kuwa yeye ni miongoni mwa waliofika siku ya kwanza nilimtania na kumwambia
“nyie ndo mtakuwa wafia jeshi wenyewe, wazalendo haswa na nchi yao”.

Maafande walifika KOMBANIA na kutugawa katika vikundi kadhaa ambavyo wao waliviita VIBANGALA, vilipatikana VIBANGALA 9 na kila kimoja kilikuwa na angalau afande mmoja ambaye alivaa sare tofauti kidogo na zile za wanajeshi niliokuwa nikiwaona mara kwa mara haswa uraiani ama kwenye runinga.

Nilikuwa kwenye KIBANGALA kimoja na Amos tulijipanga mistari mitatu tukaondoka kuelekea eneo la usafi tulilopangiwa tukiongozwa na afande ambaye ndiye aliyekuwa akianzisha nyimbo na alisikika akiimba,

"Afande: Tutampataje kunguru
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Eeeh na mbawa zake za woga
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Ana ka kei kadogo
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Sema mpaka upulize manyoya
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Kunguru yeye wa Zanzibar
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize
Afande: Anakwiba sidiria!
Sisi: Aaaaai! aai!
Afande: Agaaah!
Sisi: Sote tukae chini tujiulize". ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………...

MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 10

Tulielekea lilipo eneo husika ambapo tulifanya usafi huku tukibadilishana mawazo.

Kwa kuwa nilikuwa nina shauku ya kujua baadhi ya vitu nilimsogelea Amos ambaye yeye aliifanya shauku yangu iwe ya juu zaidi kwani alikuwa na uwenyeji wa kutosha ambao ungefanya nipate majibu ya maswali yangu.

Amos alianza kunitatulia utata wa sare zinazovaliwa kambini aliniambia kuwa sare ninazozionaga kwa wanajeshi wakizivaa uraiani zile wanaziita BAKABAKA na hizi ambazo nimeziona kwa mara ya kwanza pale kambini wanaziita KARANGA.

Tofauti yao kubwa ni kuwa BAKABAKA ni sare zinazovaliwa na wanajeshi ambao wapo kwenye ajira ya kudumu jeshini na KARANGA ni sare za wanajeshi wanaosubiri ajira za kudumu jeshini.

Wale wanaovaa BAKABAKA wao ndio wanaotambulika kama askari wa Jeshi la Wananchi yaani JWTZ na wale wanaovaa KARANGA wao ni askari wa Jeshi la Kujenga Taifa yaani JKT.

Kwa maelezo hayo niliweza kubaini ni kwanini sehemu kubwa ya mapokezi yetu yalifanywa na vijana wa JKT na hata pale walipopewa amri na BAKABAKA walitii kwa uharaka na unyenyekevu wa hali juu.

Nilivuta kumbukumbu siku moja nyuma kule dukani jinsi ambavyo muuzaji aliyevaa gwanda ya JWTZ aliwapelekesha wale waliovaa gwanda za JKT.

Baada ya kukamilisha usafi tulijipanga mistari mitatu tukapiga jaramba kurudi KOMBANIA tukakinukisha tukiwa na afande aliyeanzisha songi.

“Afande: Wii
Sisi: Waah
Afande: Ewii
Sisi: Ewaah
Afande: Elewii
Sisi: Elewaah
Afande: Si uliutaka mwenyewe mchezo wa bolingoo, tuliza boli mwanangu mpira umejaa
Sisi: Si uliutaka mwenyewe mchezo wa bolingoo, tuliza boli mwanangu mpira umejaa
Afande: Selina eeh Selina
Sisi: Haya twende
Afande: Tunaondoka
Sisi: Haya twende
Afande: Alee tunaondoka
Sisi: Haya twende”.

Tulifika KOMBANIA na kuwakuta baadhi ya wenzetu wakitusubiri japo hatukuwa wa mwisho hivyo ilitupasa kuwasubiri wengineo.

Tukiwa tunawasubiri maafande walikuwa wakituelekeza mambo mbalimbali ambayo tulistahili kuyajua.

Moja ya maafande alituambia kuwa kila tusikiapo filimbi ni wajibu wetu KUFOLENI sehemu husika tukifanya hivyo tutamaliza kozi yetu salama na hatutauona ugumu wowote wa kozi.

Alituambia kuwa kozi yetu ni ya muda mfupi hivyo basi ni muhimu kuzingatia ratiba na kufuata taratibu ikiwepo kuheshimu na kutii amri kutoka kwa walio juu yetu.

Walitusisitiza kuzingatia filimbi zote tutakazozisikia na kujua zina maana ipi na wakatoa mfano kuwa zile zinazopigwa baada ya chakula huwa zinatutaka kwenda KOMBANIA.

Vilevile baada ya FATIKI tutazisikia zile zitakazotutaka kwenda MESI kwa mzabuni na pia zipo zile za asubuhi kabisa ni kwa ajili ya MABIO hivyo yatupasa kuelekea UWANJA WA DAMU.

Walipomaliza kutuhubiria askari hao wa JKT walituruhusu kurudi MAHANGANI na kutuagiza ndoo tutakaporejea KOMBANIA.

Tuliporuhusiwa kuondoka niliambatana na jirani yangu ambaye wakati huu alinitajia jina lake kuwa anaitwa Baraka.

Nilimuuliza maana ya FATIKI akaniambia kuwa haina tofauti na mission ama jukumu kama vile kuchimba vifusi ambayo ndiyo FATIKI kubwa waliokuwa wakiifanya tangu wafike.

Aliponiambia hivyo ndipo nikagundua kwanini tuliagizwa ndoo nikamuuliza jamaa kama nitapewa adhabu nisipoenda nayo.

Jamaa yule mwenye asili ya kiarabu aliniambia kuwa atanipa yakwake maana kwenye FATIKI siyo wote wanabeba vifusi wapo wanaochimba hivyo watapewa majembe na machepe.

Tukiwa tunarudi HANGANI tulikuta ndoo karibu na mabafu ikiwa na maji Baraka akaniambia,

“Tushapata ndoo kaka ngoja tusome mazingira TUITEKE”.

Nilimsihi tuiache maana mwenyewe akitukuta utakuwa msala lakini pia siyo uungwana ila jamaa hakunielewa akaniambia,

“SIFA WEPESI ukiwa na huruma hutoboi kaka”.

Baada ya kusoma mazingira Baraka aliichukua ndoo na maji yake akabadili uelekeo kulizunguka moja ya HANGA ambalo si tulilofikia akaenda kutokea upande wa pili ambako sikujua yaliyoendelea.

Nikiwa nashangaa shangaa nisijue ni kipi kinaendelea mwenye maji yake alikuja akiwa na kopo la sabuni, mswaki na taulo begani akionesha dhahiri ni mtu mwenye mipango ya kwenda kuoga.

Alipigwa na butwaa kwa kutoikuta ndoo yake akawauliza watu kama kuna aliyemuona akiichukua lakini hakuna aliyempa jibu.

Katika kutupatupa macho akanifuata nadhani aliniona nina uoga fulani hivyo akahisi kama kuna kitu ninakijua hivyo nina shauku ya kuulizwa ili nitoe majibu.

“Oya mshikaji maji yangu yaliyokuwa pale umepeleka wapi?” aliniuliza huku akinikazia macho.

“Maji gani tena mwanangu”
“Maji yalikuwa kwenye ndoo nyekundu mi nina uhakika kuna sehemu umeyapeleka”
“Kwahiyo mwanangu umeniona mimi ni mwizi siyo haya kachukue basi ulipoona nimepeleka” nilijaribu kumkazia na kumpandishia sauti maana niliona ameanza kunipanda kichwani.

“Daah kwahiyo mwanangu maji nimekuchotea umeniona mi bwege na bado unanikoromea, poa hamna noma”.

“Hamna sina maana hiyo nakushangaa tu from nowhere unakuja unanimbia nimekuibia maji yako, mi ningechukua ningekuwa hapa kweli!”.

“Poa mwanangu mjanja wewe” awamu hii aliongea akionesha dalili za kushindwa.

Kwa upande wangu sikuweza kushikilia bomba ilinijia roho ya huruma nikatamani nimsaidie ila nikahisi Baraka atanimaindi.

Roho ya huruma na ile ya ukatili zikawa zinashindana nguvu ikanibidi nimpe jamaa last chance nikamfungulia code.

“Kuna watu wawili nimewaona wakipita na ndoo za maji ila sikumbuki zilikuwa na rangi gani mmoja ameelekea chooni na mwingine ameelekea HANGANI ila hakupita mlangoni amepita pembeni ya HANGA kama hajafika mbali unaweza kukutana naye”.

Jamaa hakutaka kuhangaika na aliyeko chooni maana hata kwa akili ya kawaida hakutakiwa kuamini hivyo kwani bado kulikuwa na foleni ya watu wanaosubiri kuingia.

Niliondoka zangu na kuelekea lilipo HANGA nililofikia nikamkuta Baraka amekwishafika na ndoo ile ya mchongo na maji yake aliiweka uvunguni mwa kitanda.

Nilimueleza yaliyotokea baada ya yeye kuondoka ila aliishia kusisitiza kauli yake ya awali akisema,
“Jeshini SIFA WEPESI, ukiwa mzembe hutoboi”.

Baraka alichukua ndoo yake na kuhamisha maji yaliyokuwemo kwenye ile ndoo ya wizi na kunipa mimi ambapo nilichukua na kwenda kuoga, Baraka yeye hakuhitaji kwenda kuoga isipokuwa alibakiza maji kidogo ya kunawa uso.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea…………………………………
 
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 10

Tulielekea lilipo eneo husika ambapo tulifanya usafi huku tukibadilishana mawazo.

Kwa kuwa nilikuwa nina shauku ya kujua baadhi ya vitu nilimsogelea Amos ambaye yeye aliifanya shauku yangu iwe ya juu zaidi kwani alikuwa na uwenyeji wa kutosha ambao ungefanya nipate majibu ya maswali yangu.

Amos alianza kunitatulia utata wa sare zinazovaliwa kambini aliniambia kuwa sare ninazozionaga kwa wanajeshi wakizivaa uraiani zile wanaziita BAKABAKA na hizi ambazo nimeziona kwa mara ya kwanza pale kambini wanaziita KARANGA.

Tofauti yao kubwa ni kuwa BAKABAKA ni sare zinazovaliwa na wanajeshi ambao wapo kwenye ajira ya kudumu jeshini na KARANGA ni sare za wanajeshi wanaosubiri ajira za kudumu jeshini.

Wale wanaovaa BAKABAKA wao ndio wanaotambulika kama askari wa Jeshi la Wananchi yaani JWTZ na wale wanaovaa KARANGA wao ni askari wa Jeshi la Kujenga Taifa yaani JKT.

Kwa maelezo hayo niliweza kubaini ni kwanini sehemu kubwa ya mapokezi yetu yalifanywa na vijana wa JKT na hata pale walipopewa amri na BAKABAKA walitii kwa uharaka na unyenyekevu wa hali juu.

Nilivuta kumbukumbu siku moja nyuma kule dukani jinsi ambavyo muuzaji aliyevaa gwanda ya JWTZ aliwapelekesha wale waliovaa gwanda za JKT.

Baada ya kukamilisha usafi tulijipanga mistari mitatu tukapiga jaramba kurudi KOMBANIA tukakinukisha tukiwa na afande aliyeanzisha songi.

“Afande: Wii
Sisi: Waah
Afande: Ewii
Sisi: Ewaah
Afande: Elewii
Sisi: Elewaah
Afande: Si uliutaka mwenyewe mchezo wa bolingoo, tuliza boli mwanangu mpira umejaa
Sisi: Si uliutaka mwenyewe mchezo wa bolingoo, tuliza boli mwanangu mpira umejaa
Afande: Selina eeh Selina
Sisi: Haya twende
Afande: Tunaondoka
Sisi: Haya twende
Afande: Alee tunaondoka
Sisi: Haya twende”.

Tulifika KOMBANIA na kuwakuta baadhi ya wenzetu wakitusubiri japo hatukuwa wa mwisho hivyo ilitupasa kuwasubiri wengineo.

Tukiwa tunawasubiri maafande walikuwa wakituelekeza mambo mbalimbali ambayo tulistahili kuyajua.

Moja ya maafande alituambia kuwa kila tusikiapo filimbi ni wajibu wetu KUFOLENI sehemu husika tukifanya hivyo tutamaliza kozi yetu salama na hatutauona ugumu wowote wa kozi.

Alituambia kuwa kozi yetu ni ya muda mfupi hivyo basi ni muhimu kuzingatia ratiba na kufuata taratibu ikiwepo kuheshimu na kutii amri kutoka kwa walio juu yetu.

Walitusisitiza kuzingatia filimbi zote tutakazozisikia na kujua zina maana ipi na wakatoa mfano kuwa zile zinazopigwa baada ya chakula huwa zinatutaka kwenda KOMBANIA.

Vilevile baada ya FATIKI tutazisikia zile zitakazotutaka kwenda MESI kwa mzabuni na pia zipo zile za asubuhi kabisa ni kwa ajili ya MABIO hivyo yatupasa kuelekea UWANJA WA DAMU.

Walipomaliza kutuhubiria askari hao wa JKT walituruhusu kurudi MAHANGANI na kutuagiza ndoo tutakaporejea KOMBANIA.

Tuliporuhusiwa kuondoka niliambatana na jirani yangu ambaye wakati huu alinitajia jina lake kuwa anaitwa Baraka.

Nilimuuliza maana ya FATIKI akaniambia kuwa haina tofauti na mission ama jukumu kama vile kuchimba vifusi ambayo ndiyo FATIKI kubwa waliokuwa wakiifanya tangu wafike.

Aliponiambia hivyo ndipo nikagundua kwanini tuliagizwa ndoo nikamuuliza jamaa kama nitapewa adhabu nisipoenda nayo.

Jamaa yule mwenye asili ya kiarabu aliniambia kuwa atanipa yakwake maana kwenye FATIKI siyo wote wanabeba vifusi wapo wanaochimba hivyo watapewa majembe na machepe.

Tukiwa tunarudi HANGANI tulikuta ndoo karibu na mabafu ikiwa na maji Baraka akaniambia,

“Tushapata ndoo kaka ngoja tusome mazingira TUITEKE”.

Nilimsihi tuiache maana mwenyewe akitukuta utakuwa msala lakini pia siyo uungwana ila jamaa hakunielewa akaniambia,

“SIFA WEPESI ukiwa na huruma hutoboi kaka”.

Baada ya kusoma mazingira Baraka aliichukua ndoo na maji yake akabadili uelekeo kulizunguka moja ya HANGA ambalo si tulilofikia akaenda kutokea upande wa pili ambako sikujua yaliyoendelea.

Nikiwa nashangaa shangaa nisijue ni kipi kinaendelea mwenye maji yake alikuja akiwa na kopo la sabuni, mswaki na taulo begani akionesha dhahiri ni mtu mwenye mipango ya kwenda kuoga.

Alipigwa na butwaa kwa kutoikuta ndoo yake akawauliza watu kama kuna aliyemuona akiichukua lakini hakuna aliyempa jibu.

Katika kutupatupa macho akanifuata nadhani aliniona nina uoga fulani hivyo akahisi kama kuna kitu ninakijua hivyo nina shauku ya kuulizwa ili nitoe majibu.

“Oya mshikaji maji yangu yaliyokuwa pale umepeleka wapi?” aliniuliza huku akinikazia macho.

“Maji gani tena mwanangu”
“Maji yalikuwa kwenye ndoo nyekundu mi nina uhakika kuna sehemu umeyapeleka”
“Kwahiyo mwanangu umeniona mimi ni mwizi siyo haya kachukue basi ulipoona nimepeleka” nilijaribu kumkazia na kumpandishia sauti maana niliona ameanza kunipanda kichwani.

“Daah kwahiyo mwanangu maji nimekuchotea umeniona mi bwege na bado unanikoromea, poa hamna noma”.

“Hamna sina maana hiyo nakushangaa tu from nowhere unakuja unanimbia nimekuibia maji yako, mi ningechukua ningekuwa hapa kweli!”.

“Poa mwanangu mjanja wewe” awamu hii aliongea akionesha dalili za kushindwa.

Kwa upande wangu sikuweza kushikilia bomba ilinijia roho ya huruma nikatamani nimsaidie ila nikahisi Baraka atanimaindi.

Roho ya huruma na ile ya ukatili zikawa zinashindana nguvu ikanibidi nimpe jamaa last chance nikamfungulia code.

“Kuna watu wawili nimewaona wakipita na ndoo za maji ila sikumbuki zilikuwa na rangi gani mmoja ameelekea chooni na mwingine ameelekea HANGANI ila hakupita mlangoni amepita pembeni ya HANGA kama hajafika mbali unaweza kukutana naye”.

Jamaa hakutaka kuhangaika na aliyeko chooni maana hata kwa akili ya kawaida hakutakiwa kuamini hivyo kwani bado kulikuwa na foleni ya watu wanaosubiri kuingia.

Niliondoka zangu na kuelekea lilipo HANGA nililofikia nikamkuta Baraka amekwishafika na ndoo ile ya mchongo na maji yake aliiweka uvunguni mwa kitanda.

Nilimueleza yaliyotokea baada ya yeye kuondoka ila aliishia kusisitiza kauli yake ya awali akisema,
“Jeshini SIFA WEPESI, ukiwa mzembe hutoboi”.

Baraka alichukua ndoo yake na kuhamisha maji yaliyokuwemo kwenye ile ndoo ya wizi na kunipa mimi ambapo nilichukua na kwenda kuoga, Baraka yeye hakuhitaji kwenda kuoga isipokuwa alibakiza maji kidogo ya kunawa uso.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea…………………………………
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 11

Baada ya muda kupita zilisikika filimbi ambazo zilitufanya tukakusanyike KOMBANIA ambako nilienda na ndoo ya Baraka.

Nilibahatika kumuona yule jamaa aliyeibiwa maji na Baraka akinitazama kwa mazingatio sana ni kana kwamba kuna kitu alikuwa akikivizia kwangu.

Nilikuwa karibu na Baraka kwa wakati huo ambaye yeye alikuwa mikono mitupu kwani ile ndoo ya wizi aliiacha HANGANI jambo ambalo lilikuwa ni la kushukuru sana kwani kwa ukaribu ule ungempa mwanya wa kuhisi kuwa ndoo yake baada ya kumuibia nimebadilishana na Baraka.

Tulihesabu namba na kutenganishwa kati ya waliokuwa na ndoo na wasio nazo.

Wale wasiokuwa na ndoo akiwepo Baraka waaliagizwa na afande stoo kufuata majembe, sururu na bereshi.

Waliporudi TULIFOLENI mistari mitatu kama ilivyo ada na kuushika uelekeo vilipo vifusi kwa mbio za kistaarabu zisizo za kukera wala kuumiza.

Jukumu lililopo mbele yetu lilikuwa ni kuchimba vifusi na kubeba kwenye ndoo na hatimaye kuupeleka umbali wa kilomita zaidi ya moja kwa ajili ya kufukia mashimo yaliyopo kwenye barabara mbalimbali za kikosi.

Tuliendelea na jukumu hilo mpaka ulipokaribia muda wa chai TUKAFOLENISHWA na kupiga jaramba tukiwa tumechoka ila aina ya nyimbo tulizokuwa tukiimba zilichangia mno kurudisha MORALI mara zote tukaonekana watamu kama Mchalo.

Kwa wakati huu mwanzilishi wetu alituimbisha songi lenye amsha yake kama ifuatavyo,

Mwanzilishi: Ale mama kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
"Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Umekyona kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Aaah kisambu kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Umekyona kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
Sisi: Aiiih!"

Tulipofika kambini moja kwa moja tulielekea MAHANGANI kuchukua vikombe na kuelekea MESI ambako chai ilikuwa ikigawiwa na WAZABUNI ambao walichukua tenda ya kuandaa vyakula kikosini.

Hili lilinifanya nikumbuke yanayosemwa mtaani ambako wanatuaminisha kuwa wapo wanajeshi wanaoajiriwa jeshini kwa aajili ya kupika kumbe haiko hivyo.

Tulikunywa chai yenye asili ya maziwa na pande la mkate ilikuwa ni chai iliyokuwa ikisemekana kuwa ni ya maziwa ila ukweli yalikuwa ni maziwa yaliyochanganywa na maji katika uwiano wa 1 kwa 16 yaani kikombe kimoja cha maziwa kinachanganywa na vikombe kumi na sita vya maji.

Punde si punde tulirudi KOMBANIA na kwenda kwenye vifusi wenye kuchimba walichimba na sisi wengine wenye nyota ya tipa tulibeba zetu vifusi na kuwapelekea wakandarasi wa kufukia mashimo.

Muda huu watu walionekana kuwa na shibe ya boflo la MZABUNI hivyo kazi ikaanza kwa kulegalega tofauti na mwanzo.

Wengine walikuwa bize na simu zao hali iliyowafanya maafande waliokuwa wakitusimamia kutumia nguvu nyingi kutusimamia.

Hali hiyo iliendelea mpaka pale ulipofika muda wa chakula uliofahamika kama wasaa wa MZABUNI.

Tulirudi kikosini na kuelekea MAHANGANI kufuata vyombo vya msosi na hatimaye kituo cha mwisho kikawa pale MESI kwa MZABUNI.

Tuliunyuka zetu ugali maharagwe na kurudi zetu KOMBANIA ambako stori za hapa na pale hazikukauka tukiwa na Afande Amina ambaye alikuwa akituimbisha nyimbo mbalimbali walizokuwa wakiziita CHENJA.

Katika BOGI hilo la karibia watu 400 lilisikika likirapu,

"Afande Amina: Kiiila baada ya kula
Sisi: Soda bia
Afande Amina: Kila baada ya kula
Sisi: Soda bia
Afande Amina: Kiiila baada ya kula
Sisi: Kombania
Afande Amina: Kila baada ya kula
Sisi: Kombania".

Wimbo huu ulikuwa ni kama Summary ya ratiba kikosini kwa kila MZALENDO ambaye alitakiwa kwenda KOMBANIA baada ya kukamilisha ratiba kwa MZABUNI.

Tulipofika idadi iliyomshawishi Afande tulipelekwa eneo la kazi ambayo kwa wakati huu haikuwa kubeba vifusi tena ila tulikwenda kusafisha baadhi ya maeneo yaliyopo kikosini tulibeba majembe makwanja na mafagio.

Usafi uliendelea mpaka pale jua lilipokaribia kuzama tuliruhusiwa kwenda kuoga na kung’ata alichokiandaa MZABUNI.

Nilipofika HANGANI niliinamisha kichwa uvunguni mwa kitanda niliyakuta yale maji niliyopewa asubuhi na Baraka tuliyomuibia yule jamaa ikumbukwe nilikosa muda wa kuyaoga kutokana na uchache wa mabafu na wingi wa watu.

Kwakuwa sikuwa na kipengele cha kupanga foleni ya kuteka maji moja kwa moja nilielekea zangu kuoga ambako nilikutana na foleni pia ila si sawa na ile ya asubuhi hali iliyonifanya nisikae kwa muda mrefu.

Baada ya kumaliza kuoga nilikuwa nikipaga stori za hapa na pale huku tukiusubiri wasaa wa MZABUNI.

Baada ya muda tulizisikia filimbi TUKAFOLENI tulikohitajika nakumbuka nilikuwa wa mwanzoni kupewa chakula.

Kilikuwa ni wali ndondo na chai moja transparency yaani imeandaliwa kwa pakti moja ya majani na kuchanganywa na ndoo kumi za maji.

Baada ya msosi nilirudi zangu HANGANI na kuzama zangu kwenye sanduku kutoa simu ambayo niliikuta na missed calls na mesji za kutosha.

Nyingi zilikuwa za Linda, Ambrose na nyingine ni kutoka nyumbani ilibidi niwatafute ila Linda nilimuweka kiporo mana nilijua mazungumzo yangekuwa marefu mno.

Ambrose aliniambia kuwa amesharipoti kikosini hivyo alikuwa akinitafuta akiwa safarini ila kwa muda huo nilipomtafuta alikuwa hapokei wala kujibu meseji hali iliyonifanya niende na simu KOMBANIA ili tuweze kuonana.

Kunako KOMBANIA kilikuwepo chuma kimoja kilichoitwa Selemani maarufu kama afande Sele kilikuwa kikituimbisha.

“Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba manyekunyeku
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba Selule
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba mama eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Wewe hapo weeh!
Sisi: Amba
Afande Sele: Waitwa nani weeh?
Sisi: Amba
Afande Sele: Watokea eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Mkoa gani weeh?”

Huu ni wimbo uliokuwa ukisikika KOMBANIA huku tukipiga kofi moja moja (Paah! Paah! Paah!) kama biti la wimbo huo.

Afande alimshika mkono DAWILI mmoja na kumnyanyua ambaye nae alinyanyuka na kuendeleza wimbo.

“Dawili: Mimi hapa eeh
Sisi: Amba
Dawili: Naitwa Aisha
Sisi: Amba
Dawili: Natokea
Sisi: Amba
Dawili: Mkoa wa Mtwara eeh
Sisi: Nilimakonde eeh limakonde eeh limakondee eeh tushalijua ee”.

Aisha alirudi kukaa na wakati huu kipaza kikarudi kwa Afande Sele

“Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba manyekunyeku
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba Selule
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba mama eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Sina mwingine
Sisi: Mwinginee eeeeh mwingiii
Afande Sele: Sina mwingine maa
Sisi: Mwinginee eeeeh mwingii
Afande Sele: Wewe hapo weeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Waitwa nani eeh?
Sisi: Amba
Afande Sele: Watokea eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Mkoa gani weeh?”.

Wakati huu Afande Sele alienda kumuinua mwamba mmoja hivi naye akapokea kipaza,

“Mwamba: Mimi hapa eeh
Sisi: Amba
Mwamba: Ni Ambrose eeh
Sisi: Amba
Mwamba: Natokea eeh
Sisi: Amba
Mwamba: Tabora eeh
Sisi: Nilinyamwezi eeh Linyamwezi eeh Linyamwezi ee tushalijua eeh”. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………
 
SEASON-1

EPISODE 01

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa kila mmoja wetu kwa kufika hatua hiyo ya kumaliza elimu ya upili baada ya kumaliza mitihani ya kidato cha sita.

Kilichobaki kwa wakati huo ilikuwa ni kuagana👋 kwa kila mmoja wetu kwani tulijua ya kuwa hakuna kitu kingine cha kutukutanisha kwa namba kubwa kama ile tena, ilikuwa ni huzuni😥 miongoni mwetu kwani ule undugu tuliokuwa nao ndani ya miaka miwili ndiyo ulikuwa unakoma wakati huo.

Kwa kulitambua hilo lilitolewa wazo la kukutana pamoja katika shule hiyo wakati wa kufuata vyeti vya kidato cha sita pale vitakapotolewa na wazo hilo liliungwa mkono na kila mmoja wetu.

Kipindi zikiendelea ratiba za kuagana kwa kupeana namba za simu na namna nyingine nilitizama saa🕖 na kugundua kuwa nina wastani wa masaa mawili na dakika zipatazo tano kabla tiketi iliyopo mikononi mwangu haijaisha muda wake.

Nilishugulisha kichwa changu kwa dakika moja nikagundua kuwa nikilaza damu hela💰 yangu nitakuwa nimemchangia mwarabu kijinga hivyo nikaona mambo yasiwe mengi mana kwetu ni pazuri na nilikwishapakumbuka.

Niliwatizama wahitimu wenzangu nikawaona bado wanaagana huku wengi wao wakiwa hawana tiketi kama mimi kwani mabasi ya kwenda kwao hayakuwepo mchana huo kutokana na umbali wa route yao uliokuwa ukiwahitaji masaa zaidi ya kumi hadi kufika makwao tofauti na kwetu ambako yalinitosha masaa sita pekee.

Kitu ambacho nilikuwa nikikisikia kwao walikuwa wakipanga kwenda kituo cha mabasi majira ya jioni kwa ajili ya kukata tiketi kwani hakukuwa na utaratibu wa shule kuandaa usafiri wa pamoja kwa wahitimu maana kulikuwa na mchanganyiko michepuo ya sayansi, sanaa na uchumi hali iliyopelekea kutomaliza kwa wakati sawa tofauti na wakati wa likizo za mihula ambapo wanafunzi wote humaliza mitihani kwa pamoja siku ya Ijumaa na kusafiri pamoja alfajiri ya Jumamosi.

Nikagundua hapo sina wa kuondoka naye hivyo niliiba muda wangu kidogo kwakuchukua namba za simu kama tatu ikiwemo ya dada mmoja mwenye urembo wake aliyefahamika kwa jina la Zainabu Khamis binafsi nilikuwa nikimwita Zaimisi.

Kulikuwepo na utaratibu wa kuchafuliana shati za shule kwa kuwa zilikwishakumaliza muda wa matumizi hivyo kila aliyeona shati la mwenzake likiwa safi ama likiwa na sehemu ya kuandika pasi nakuombwa alimsogelea na kuchukua kalamu ya kawaida ama makapeni🖍 na kuchora alichojisikia.

Lengo kubwa la kufanya hivyo ilikuwa ni kupeana namba za simu📱 kwani hakukuwa na mwenye simu ya kuhifadhi namba maana hatukuruhusiwa kuzimiliki kipindi cha masomo,📚📖 lakini mbali na hapo tulifanya hivyo kama sehemu ya kutunza kumbukumbu kwa wanadarasa kwani tuliandika namba za simu na majina yetu pamoja na kuweka saini zetu.

Kwa upande wangu sikuona umuhimu wa kuchafua shati la yeyote kwani sikuwa nikimiliki simu wala namba yake lakini pia muda ulikuwa ukiniendea matiti, hivyo basi pasi na kuaga mdogomdogo nilianza kujongea kuelekea lilipo bweni lililofahamika kwa jina la Mikumi.
Nikiwa nimepiga hatua kadhaa nilisikia sauti nyororo ikitamka “Hallow K baby”.

Waooh alikuwa ni mwanangu wa nguvu mwanadada Linda, msichana mwenye PCM yake ingawaje michepuo yetu ilikuwa ni kulia na kushoto lakini mara nyingi tulikuwa tukijisomea pamoja.
“Nambie mamdogo”,
nilimjibu huku nikimsubiri kwwani tayari alikuwa akipiga hatua kuupunguza umbali uliopo baina yetu.

“Mbona kama unajitenga mwanangu wapi unaelekea”,
aliendelea kuniuliza nami nikamjibu

“Oooh mummy so sorry, I do have a ticket to home on my hand and it is going to expire soon so nawahi kujiandaa mana I think kuna lisaa limoja na dakika chache kabla bus halijang’oa nanga”.

Maneno yale yalionekana kumhuzunisha Linda niligundua hilo kupitia uso wake naye akasema

“Mkaka una roho mbaya wewe yaani umekata tiketi hujaniambia haitoshi unaamua kuondoka kimyakimya bila kunijuza”.

Linda alinitupia shutuma hizo ambazo zilinifanya nijione mkatili mbele yake japo sikutaka kuonesha unyonge nikajitetea kwa kusema
“Jamani Linda ndo unapoteza kumbukumbu hivyo mbona nilikwambia tangu juzi kuwa nikimaliza mtihani wa mwisho sitoweza kulaza mbavu zangu hapa nikawanufaisha kunguni”.

Aliendelea kuniambia “Sawa ulisema na hiyo tiketi ulikata saa ngapi nisijue?”

Nikamjibu “Ni kweli sikukwambia ila tiketi yenyewe nimeipata leo asubuhi nilimuagiza jana jamaa wa dukani alipokwenda mjini kufungasha ndo leo kabla sijaingia kwenye mtihani nikaipitia kwahiyo jana ilikuwa vigumu kukwambia maana bado sikuwa na uhakika kama amepata au vinginevyo, samahani lakini mhandisi mama yangu mdogo kama nimekukwaza”.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

Itaendelea...........................View attachment 3202479
Nzuri kiasi
 
Nakimbiza mwizi kimya kimya hapa tuendelee mkuu
Basi ngoja nikudondoshee hiki kipande ukipunguze mdogomdogo kabla hawajaamka.

MAISHA YA DEPO
SEASON-2
EPISODE 12

Nilipokuwa naisikiliza ile sauti ni kama nilikuwa nikiifahamu ila sikukumbuka ni ya nani lakini alipotaja jina tu nikajua ni yeye japo aliwadanganya kwani yeye ni mzigua wa Tanga ila O level alisomea Tabora.

Aliporudi kukaa ilibidi nimsogelee alipo na kweli alikuwa ni yeye, tulisalimiana na tukawa wote mpaka tuliporuhusiwa kwenda kulala mishale ya saa tano.

Nilipofika HANGANI nilimtafuta Linda ambaye alikuwa bado hajalala nilishangazwa kwanini alikuwa macho mpaka wakati huo ingawaje alinipa majibu ambayo hata wewe ungeyatarajia.

Linda alinambia kuwa isingekuwa rahisi kwake kulala bila ya kuongea na mimi ilihali nilimuahidi kuwa ningemtafuta usiku huo.

Nilijaribu kumtania kama angeiweza mikikimikiki ya jeshi mana huku tunachelewa kulala akasema ni kawaida mana yeye mwenyewe hulala saa 7 au 8 kifupi alijipakulia minyama.

Sikumbuki tuliongea mpaka muda gani lakini nilikuja kustushwa na filimbi zilizokuwa zikipulizwa MAHANGANI.

Kelele hizo ziliambatana na mineno kutoka kwa maafande Jeshi la Kujenga Taifa yaani SERVICE MEN ambao walifanya eneo hilo lionekane kana kwamba tuko gulioni.

Maafande hao walisikika wakiropoka,
Afande wa 1: “Amkeni nyie mazombi msikumbatie hizo shuka kana kwamba mko serena Hotel”.

Afande wa 2: “Huku hamkuja Semina WAZALENDO mpo kozi ya kikamanda na ndio mana hamkuagizwa mje na madaftari”.

Afande wa 3: “Hii sauti siyo mlinzi wa k4s ni kamanda wa jeshi la kujenga taifa, popote uisikiapo huna budi kutoa mikono yako kwenye makende na uende kufoleni KOMBANIA”.

Afande wa 2: “Kama unajihisi umekuja kushiriki Big Brother endelea kulala nikukute kitandani utanieleza ni kwanini SAJENTI Pastima ana kitambi tumboni badala ya mgongoni”.

Afande wa 3: “Sasa kama sauti hii unaifananisha na ya Bibi kidude inakubembeleza kitandani we endelea kulala tu si umekuja JKT kulala lala baba”.

Afande wa 1: “Kamanda ndo naenda zangu UWANJA WA DAMU hivyo sasa mambo ni mawili ufike kabla yangu au nifike baada yako vinginevyo utanikumbusha jina langu utoto niliacha kuitwa lini”.

Kwakweli kilichokuwa kinaendelea hakikuwa rahisi kukielezea maana zogo si zogo, kejeli si kejeli, vitisho si vitisho yalikuwa ni makelele ambayo hata kama una usingizi haikuwepo namna yoyote ya kuendela kulala.Basi nilijiinua pale nilipo ambapo niligundua kuwa sikujifunika wala kuvua chochote kati ya viatu ama nguo yaani nilivyotoka KOMBANIA nikajitupa kitandani nikiongea na Linda kwenye simu basi nililala hivyo hivyo pasi na kujifunika shuka licha ya kuwa kambi hiyo ilikuwa maeneo yenye baridi la kwenda.Siku hii ya pili nilianza kuzizoea ratiba za kikosi hicho maana sikuwa na mambo mengi wakati wa kuamka kama vile kukimbilia kwenye sanduku kwa ajili ya kutoa mswaki ama kutandika kitanda.Nilifika KOMBANIA nikakuta watu wachache WAMEFOLENI na afande mmoja, niliungana nao yule afande akanipa namba 34 na baada ya muda idadi ilisoma watu 73 kati ya wale 491 waliosajiliwa kufikia jana usiku.
 
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 11

Baada ya muda kupita zilisikika filimbi ambazo zilitufanya tukakusanyike KOMBANIA ambako nilienda na ndoo ya Baraka.

Nilibahatika kumuona yule jamaa aliyeibiwa maji na Baraka akinitazama kwa mazingatio sana ni kana kwamba kuna kitu alikuwa akikivizia kwangu.

Nilikuwa karibu na Baraka kwa wakati huo ambaye yeye alikuwa mikono mitupu kwani ile ndoo ya wizi aliiacha HANGANI jambo ambalo lilikuwa ni la kushukuru sana kwani kwa ukaribu ule ungempa mwanya wa kuhisi kuwa ndoo yake baada ya kumuibia nimebadilishana na Baraka.

Tulihesabu namba na kutenganishwa kati ya waliokuwa na ndoo na wasio nazo.

Wale wasiokuwa na ndoo akiwepo Baraka waaliagizwa na afande stoo kufuata majembe, sururu na bereshi.

Waliporudi TULIFOLENI mistari mitatu kama ilivyo ada na kuushika uelekeo vilipo vifusi kwa mbio za kistaarabu zisizo za kukera wala kuumiza.

Jukumu lililopo mbele yetu lilikuwa ni kuchimba vifusi na kubeba kwenye ndoo na hatimaye kuupeleka umbali wa kilomita zaidi ya moja kwa ajili ya kufukia mashimo yaliyopo kwenye barabara mbalimbali za kikosi.

Tuliendelea na jukumu hilo mpaka ulipokaribia muda wa chai TUKAFOLENISHWA na kupiga jaramba tukiwa tumechoka ila aina ya nyimbo tulizokuwa tukiimba zilichangia mno kurudisha MORALI mara zote tukaonekana watamu kama Mchalo.

Kwa wakati huu mwanzilishi wetu alituimbisha songi lenye amsha yake kama ifuatavyo,

Mwanzilishi: Ale mama kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
"Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Umekyona kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Aaah kisambu kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Umekyona kisambukile
Sisi: Aiiih!
Mwanzilishi: Kisambukile
Sisi: Aiiih!"

Tulipofika kambini moja kwa moja tulielekea MAHANGANI kuchukua vikombe na kuelekea MESI ambako chai ilikuwa ikigawiwa na WAZABUNI ambao walichukua tenda ya kuandaa vyakula kikosini.

Hili lilinifanya nikumbuke yanayosemwa mtaani ambako wanatuaminisha kuwa wapo wanajeshi wanaoajiriwa jeshini kwa aajili ya kupika kumbe haiko hivyo.

Tulikunywa chai yenye asili ya maziwa na pande la mkate ilikuwa ni chai iliyokuwa ikisemekana kuwa ni ya maziwa ila ukweli yalikuwa ni maziwa yaliyochanganywa na maji katika uwiano wa 1 kwa 16 yaani kikombe kimoja cha maziwa kinachanganywa na vikombe kumi na sita vya maji.

Punde si punde tulirudi KOMBANIA na kwenda kwenye vifusi wenye kuchimba walichimba na sisi wengine wenye nyota ya tipa tulibeba zetu vifusi na kuwapelekea wakandarasi wa kufukia mashimo.

Muda huu watu walionekana kuwa na shibe ya boflo la MZABUNI hivyo kazi ikaanza kwa kulegalega tofauti na mwanzo.

Wengine walikuwa bize na simu zao hali iliyowafanya maafande waliokuwa wakitusimamia kutumia nguvu nyingi kutusimamia.

Hali hiyo iliendelea mpaka pale ulipofika muda wa chakula uliofahamika kama wasaa wa MZABUNI.

Tulirudi kikosini na kuelekea MAHANGANI kufuata vyombo vya msosi na hatimaye kituo cha mwisho kikawa pale MESI kwa MZABUNI.

Tuliunyuka zetu ugali maharagwe na kurudi zetu KOMBANIA ambako stori za hapa na pale hazikukauka tukiwa na Afande Amina ambaye alikuwa akituimbisha nyimbo mbalimbali walizokuwa wakiziita CHENJA.

Katika BOGI hilo la karibia watu 400 lilisikika likirapu,

"Afande Amina: Kiiila baada ya kula
Sisi: Soda bia
Afande Amina: Kila baada ya kula
Sisi: Soda bia
Afande Amina: Kiiila baada ya kula
Sisi: Kombania
Afande Amina: Kila baada ya kula
Sisi: Kombania".

Wimbo huu ulikuwa ni kama Summary ya ratiba kikosini kwa kila MZALENDO ambaye alitakiwa kwenda KOMBANIA baada ya kukamilisha ratiba kwa MZABUNI.

Tulipofika idadi iliyomshawishi Afande tulipelekwa eneo la kazi ambayo kwa wakati huu haikuwa kubeba vifusi tena ila tulikwenda kusafisha baadhi ya maeneo yaliyopo kikosini tulibeba majembe makwanja na mafagio.

Usafi uliendelea mpaka pale jua lilipokaribia kuzama tuliruhusiwa kwenda kuoga na kung’ata alichokiandaa MZABUNI.

Nilipofika HANGANI niliinamisha kichwa uvunguni mwa kitanda niliyakuta yale maji niliyopewa asubuhi na Baraka tuliyomuibia yule jamaa ikumbukwe nilikosa muda wa kuyaoga kutokana na uchache wa mabafu na wingi wa watu.

Kwakuwa sikuwa na kipengele cha kupanga foleni ya kuteka maji moja kwa moja nilielekea zangu kuoga ambako nilikutana na foleni pia ila si sawa na ile ya asubuhi hali iliyonifanya nisikae kwa muda mrefu.

Baada ya kumaliza kuoga nilikuwa nikipaga stori za hapa na pale huku tukiusubiri wasaa wa MZABUNI.

Baada ya muda tulizisikia filimbi TUKAFOLENI tulikohitajika nakumbuka nilikuwa wa mwanzoni kupewa chakula.

Kilikuwa ni wali ndondo na chai moja transparency yaani imeandaliwa kwa pakti moja ya majani na kuchanganywa na ndoo kumi za maji.

Baada ya msosi nilirudi zangu HANGANI na kuzama zangu kwenye sanduku kutoa simu ambayo niliikuta na missed calls na mesji za kutosha.

Nyingi zilikuwa za Linda, Ambrose na nyingine ni kutoka nyumbani ilibidi niwatafute ila Linda nilimuweka kiporo mana nilijua mazungumzo yangekuwa marefu mno.

Ambrose aliniambia kuwa amesharipoti kikosini hivyo alikuwa akinitafuta akiwa safarini ila kwa muda huo nilipomtafuta alikuwa hapokei wala kujibu meseji hali iliyonifanya niende na simu KOMBANIA ili tuweze kuonana.

Kunako KOMBANIA kilikuwepo chuma kimoja kilichoitwa Selemani maarufu kama afande Sele kilikuwa kikituimbisha.

“Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba manyekunyeku
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba Selule
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba mama eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Wewe hapo weeh!
Sisi: Amba
Afande Sele: Waitwa nani weeh?
Sisi: Amba
Afande Sele: Watokea eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Mkoa gani weeh?”

Huu ni wimbo uliokuwa ukisikika KOMBANIA huku tukipiga kofi moja moja (Paah! Paah! Paah!) kama biti la wimbo huo.

Afande alimshika mkono DAWILI mmoja na kumnyanyua ambaye nae alinyanyuka na kuendeleza wimbo.

“Dawili: Mimi hapa eeh
Sisi: Amba
Dawili: Naitwa Aisha
Sisi: Amba
Dawili: Natokea
Sisi: Amba
Dawili: Mkoa wa Mtwara eeh
Sisi: Nilimakonde eeh limakonde eeh limakondee eeh tushalijua ee”.

Aisha alirudi kukaa na wakati huu kipaza kikarudi kwa Afande Sele

“Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba manyekunyeku
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba Selule
Sisi: Amba
Afande Sele: Amba mama eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Siera eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Sina mwingine
Sisi: Mwinginee eeeeh mwingiii
Afande Sele: Sina mwingine maa
Sisi: Mwinginee eeeeh mwingii
Afande Sele: Wewe hapo weeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Waitwa nani eeh?
Sisi: Amba
Afande Sele: Watokea eeh
Sisi: Amba
Afande Sele: Mkoa gani weeh?”.

Wakati huu Afande Sele alienda kumuinua mwamba mmoja hivi naye akapokea kipaza,

“Mwamba: Mimi hapa eeh
Sisi: Amba
Mwamba: Ni Ambrose eeh
Sisi: Amba
Mwamba: Natokea eeh
Sisi: Amba
Mwamba: Tabora eeh
Sisi: Nilinyamwezi eeh Linyamwezi eeh Linyamwezi ee tushalijua eeh”. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………

MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 12

Nilipokuwa naisikiliza ile sauti ni kama nilikuwa nikiifahamu ila sikukumbuka ni ya nani lakini alipotaja jina tu nikajua ni yeye japo aliwadanganya kwani yeye ni mzigua wa Tanga ila O level alisomea Tabora.

Aliporudi kukaa ilibidi nimsogelee alipo na kweli alikuwa ni yeye, tulisalimiana na tukawa wote mpaka tuliporuhusiwa kwenda kulala mishale ya saa tano.

Nilipofika HANGANI nilimtafuta Linda ambaye alikuwa bado hajalala nilishangazwa kwanini alikuwa macho mpaka wakati huo ingawaje alinipa majibu ambayo hata wewe ungeyatarajia.

Linda alinambia kuwa isingekuwa rahisi kwake kulala bila ya kuongea na mimi ilihali nilimuahidi kuwa ningemtafuta usiku huo.

Nilijaribu kumtania kama angeiweza mikikimikiki ya jeshi mana huku tunachelewa kulala akasema ni kawaida mana yeye mwenyewe hulala saa 7 au 8 kifupi alijipakulia minyama.

Sikumbuki tuliongea mpaka muda gani lakini nilikuja kustushwa na filimbi zilizokuwa zikipulizwa MAHANGANI.

Kelele hizo ziliambatana na mineno kutoka kwa maafande Jeshi la Kujenga Taifa yaani SERVICE MEN ambao walifanya eneo hilo lionekane kana kwamba tuko gulioni.

Maafande hao walisikika wakiropoka,
Afande wa 1: “Amkeni nyie mazombi msikumbatie hizo shuka kana kwamba mko serena Hotel”.

Afande wa 2: “Huku hamkuja Semina WAZALENDO mpo kozi ya kikamanda na ndio mana hamkuagizwa mje na madaftari”.

Afande wa 3: “Hii sauti siyo mlinzi wa k4s ni kamanda wa jeshi la kujenga taifa, popote uisikiapo huna budi kutoa mikono yako kwenye makende na uende kufoleni KOMBANIA”.

Afande wa 2: “Kama unajihisi umekuja kushiriki Big Brother endelea kulala nikukute kitandani utanieleza ni kwanini SAJENTI Pastima ana kitambi tumboni badala ya mgongoni”.

Afande wa 3: “Sasa kama sauti hii unaifananisha na ya Bibi kidude inakubembeleza kitandani we endelea kulala tu si umekuja JKT kulala lala baba”.

Afande wa 1: “Kamanda ndo naenda zangu UWANJA WA DAMU hivyo sasa mambo ni mawili ufike kabla yangu au nifike baada yako vinginevyo utanikumbusha jina langu utoto niliacha kuitwa lini”.

Kwakweli kilichokuwa kinaendelea hakikuwa rahisi kukielezea maana zogo si zogo, kejeli si kejeli, vitisho si vitisho yalikuwa ni makelele ambayo hata kama una usingizi haikuwepo namna yoyote ya kuendela kulala.

Basi nilijiinua pale nilipo ambapo niligundua kuwa sikujifunika wala kuvua chochote kati ya viatu ama nguo yaani nilivyotoka KOMBANIA nikajitupa kitandani nikiongea na Linda kwenye simu basi nililala hivyo hivyo pasi na kujifunika shuka licha ya kuwa kambi hiyo ilikuwa maeneo yenye baridi la kwenda.

Siku hii ya pili nilianza kuzizoea ratiba za kikosi hicho maana sikuwa na mambo mengi wakati wa kuamka kama vile kukimbilia kwenye sanduku kwa ajili ya kutoa mswaki ama kutandika kitanda.

Nilifika KOMBANIA nikakuta watu wachache WAMEFOLENI na afande mmoja, niliungana nao yule afande akanipa namba 34 na baada ya muda idadi ilisoma watu 73 kati ya wale 491 waliosajiliwa kufikia jana usiku.

Ilibidi waliokuwa wakija kwa muda huo watenganishwe na sisi tuliowahi huku wakiamriwa kupiga pushapu na wale wengine waliokuwa wakikaribia walitakiwa waruke kichurachura mpaka kwa wenzao.

Kundi hilo baadae liliruhusiwa na kuungana nasi tukahesabu namba, tukafika idadi ya WAZALENDO 245 idadi ambayo bado haikuridhisha na kikubwa zaidi hakukuwepo na DAWILI hata mmoja.

Walikuwepo maafande wawili ambao walikuwa wakitusisitiza kufuata ratiba na kutii maagizo yanayotoka kwao kipindi chote cha kozi maana kutofanya hivyo ni sawa na kuwadharau maafande na hivyo basi ingetugharimu.

Punde si punde lilionekana kundi la viumbe lililokuwa likitembea kwa mashakamashaka kana kwamba wako Darfur ama ukanda wa Gaza yaani walikuwa wakitembea kwa kuvizia ama kwa kunyata.

Moja ya wale maafande alisikika akisema, “Fanyeni haraka nyie mnaotembea kama mko kwenye onyesho la Umisi tunawasubiri nyie muda wote mjue”.

Mwenzake alimjibu akimwambie,
“Usiwapelekeshe putaputa afande wasije wakaangusha vyungu vyao kumbuka ni binadamu pekee wanaotembea na shida zao”.

Yule wa kwanza naye akamjibu,
“Hata kama bob ndo watuweke muda wote huo watu tumeacha usingizi alafu wao wanakuja kama wamekeketwa vikojoleo bwana”.

Ndiyo hujakosea walikuwa ni MADAWILI, WACHIMBA CHINI, NGUO NYINGI, VIFUA VIKUU, SERENGETI na majina mengine mengi yasiyo na idadi.

WAZALENDO hao walikuwa wakitoka MAHANGANI mwao wakiwa na afande ambaye hakuwa mgeni kwangu siyo kwa sura, umbo wala sauti ingawaje kulikuwa na kigiza fulani kilichopelekea kutomuona vizuri usoni ila kupitia umbo na sauti yake niliweza kumtambua.

Alikuwa ni Afande Anna aliyekuwa akiandikisha PARTICULARS siku niliyowasili kikosini.

Wakati huu nilianza kuziona rangi zake kwani alikuwa akitoa majibu makali kwa afande aliyekuwa akimkaripia kutokana na kuchelewa kwao.

Wakati hayo yakiendelea kulikuwa na maafande wawili ambao walikuwa wakikimbizana na WAZALENDO waliochelewa kutoka MAHANGANI.

Ilichukuliwa idadi ya MADAWILI ikajumuishwa na yetu ambapo maafande hawakuridhishwa na usahihi wa idadi iliyopo ikabidi tuhesabu kwa mara nyingine na wakati huu tulihesabiwa wote MADAWILI na NGORONGORO bila kutenganishwa.

Ilionekana ni kama jeshini walikuwa wanapenda mno kuhesabu namba maana hazikuisha dakika tatu tulisimama na kuhesabu tena.

Walituhesabisha mara kadhaa ikabidi wakubaliane na idadi iliyopo maana kila tulipohesabu walioongezeka hawakuzidi watatu hivyo walitusisitiza kukariri namba hizo maana kuna watakaoumia baadaye.

Baada ya maneno hayo tuligawanywa na kuunda MABOGI matatu yenye mistari mitatu iliyonyooka kwa kila BOGI nikamsikia afande,

“Haya wekeni CHENJA shoo ianze” basi nikaanza kumsikia Masare.

“Masare: Ewii
Sisi: Ewaaa
Masarei: Ewii
Sisi: Ewaaa
Masarei: Elewii
Sisi: Elewaaa
Masarei: Nani kasema kwa mguu mbali
Sisi: Adoado tunaondoka
Masarei: Awee tunaondoka
Sisi: Haya twende
Masarei: Tunaondoka
Sisi: Haya twende
Masarei: Awee tunaondoka
Sisi: Haya twende
Masarei: Haya tunaondoka
Sisi: Haya twende”.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea…………………………………
 
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 12

Nilipokuwa naisikiliza ile sauti ni kama nilikuwa nikiifahamu ila sikukumbuka ni ya nani lakini alipotaja jina tu nikajua ni yeye japo aliwadanganya kwani yeye ni mzigua wa Tanga ila O level alisomea Tabora.

Aliporudi kukaa ilibidi nimsogelee alipo na kweli alikuwa ni yeye, tulisalimiana na tukawa wote mpaka tuliporuhusiwa kwenda kulala mishale ya saa tano.

Nilipofika HANGANI nilimtafuta Linda ambaye alikuwa bado hajalala nilishangazwa kwanini alikuwa macho mpaka wakati huo ingawaje alinipa majibu ambayo hata wewe ungeyatarajia.

Linda alinambia kuwa isingekuwa rahisi kwake kulala bila ya kuongea na mimi ilihali nilimuahidi kuwa ningemtafuta usiku huo.

Nilijaribu kumtania kama angeiweza mikikimikiki ya jeshi mana huku tunachelewa kulala akasema ni kawaida mana yeye mwenyewe hulala saa 7 au 8 kifupi alijipakulia minyama.

Sikumbuki tuliongea mpaka muda gani lakini nilikuja kustushwa na filimbi zilizokuwa zikipulizwa MAHANGANI.

Kelele hizo ziliambatana na mineno kutoka kwa maafande Jeshi la Kujenga Taifa yaani SERVICE MEN ambao walifanya eneo hilo lionekane kana kwamba tuko gulioni.

Maafande hao walisikika wakiropoka,
Afande wa 1: “Amkeni nyie mazombi msikumbatie hizo shuka kana kwamba mko serena Hotel”.

Afande wa 2: “Huku hamkuja Semina WAZALENDO mpo kozi ya kikamanda na ndio mana hamkuagizwa mje na madaftari”.

Afande wa 3: “Hii sauti siyo mlinzi wa k4s ni kamanda wa jeshi la kujenga taifa, popote uisikiapo huna budi kutoa mikono yako kwenye makende na uende kufoleni KOMBANIA”.

Afande wa 2: “Kama unajihisi umekuja kushiriki Big Brother endelea kulala nikukute kitandani utanieleza ni kwanini SAJENTI Pastima ana kitambi tumboni badala ya mgongoni”.

Afande wa 3: “Sasa kama sauti hii unaifananisha na ya Bibi kidude inakubembeleza kitandani we endelea kulala tu si umekuja JKT kulala lala baba”.

Afande wa 1: “Kamanda ndo naenda zangu UWANJA WA DAMU hivyo sasa mambo ni mawili ufike kabla yangu au nifike baada yako vinginevyo utanikumbusha jina langu utoto niliacha kuitwa lini”.

Kwakweli kilichokuwa kinaendelea hakikuwa rahisi kukielezea maana zogo si zogo, kejeli si kejeli, vitisho si vitisho yalikuwa ni makelele ambayo hata kama una usingizi haikuwepo namna yoyote ya kuendela kulala.

Basi nilijiinua pale nilipo ambapo niligundua kuwa sikujifunika wala kuvua chochote kati ya viatu ama nguo yaani nilivyotoka KOMBANIA nikajitupa kitandani nikiongea na Linda kwenye simu basi nililala hivyo hivyo pasi na kujifunika shuka licha ya kuwa kambi hiyo ilikuwa maeneo yenye baridi la kwenda.

Siku hii ya pili nilianza kuzizoea ratiba za kikosi hicho maana sikuwa na mambo mengi wakati wa kuamka kama vile kukimbilia kwenye sanduku kwa ajili ya kutoa mswaki ama kutandika kitanda.

Nilifika KOMBANIA nikakuta watu wachache WAMEFOLENI na afande mmoja, niliungana nao yule afande akanipa namba 34 na baada ya muda idadi ilisoma watu 73 kati ya wale 491 waliosajiliwa kufikia jana usiku.

Ilibidi waliokuwa wakija kwa muda huo watenganishwe na sisi tuliowahi huku wakiamriwa kupiga pushapu na wale wengine waliokuwa wakikaribia walitakiwa waruke kichurachura mpaka kwa wenzao.

Kundi hilo baadae liliruhusiwa na kuungana nasi tukahesabu namba, tukafika idadi ya WAZALENDO 245 idadi ambayo bado haikuridhisha na kikubwa zaidi hakukuwepo na DAWILI hata mmoja.

Walikuwepo maafande wawili ambao walikuwa wakitusisitiza kufuata ratiba na kutii maagizo yanayotoka kwao kipindi chote cha kozi maana kutofanya hivyo ni sawa na kuwadharau maafande na hivyo basi ingetugharimu.

Punde si punde lilionekana kundi la viumbe lililokuwa likitembea kwa mashakamashaka kana kwamba wako Darfur ama ukanda wa Gaza yaani walikuwa wakitembea kwa kuvizia ama kwa kunyata.

Moja ya wale maafande alisikika akisema, “Fanyeni haraka nyie mnaotembea kama mko kwenye onyesho la Umisi tunawasubiri nyie muda wote mjue”.

Mwenzake alimjibu akimwambie,
“Usiwapelekeshe putaputa afande wasije wakaangusha vyungu vyao kumbuka ni binadamu pekee wanaotembea na shida zao”.

Yule wa kwanza naye akamjibu,
“Hata kama bob ndo watuweke muda wote huo watu tumeacha usingizi alafu wao wanakuja kama wamekeketwa vikojoleo bwana”.

Ndiyo hujakosea walikuwa ni MADAWILI, WACHIMBA CHINI, NGUO NYINGI, VIFUA VIKUU, SERENGETI na majina mengine mengi yasiyo na idadi.

WAZALENDO hao walikuwa wakitoka MAHANGANI mwao wakiwa na afande ambaye hakuwa mgeni kwangu siyo kwa sura, umbo wala sauti ingawaje kulikuwa na kigiza fulani kilichopelekea kutomuona vizuri usoni ila kupitia umbo na sauti yake niliweza kumtambua.

Alikuwa ni Afande Anna aliyekuwa akiandikisha PARTICULARS siku niliyowasili kikosini.

Wakati huu nilianza kuziona rangi zake kwani alikuwa akitoa majibu makali kwa afande aliyekuwa akimkaripia kutokana na kuchelewa kwao.

Wakati hayo yakiendelea kulikuwa na maafande wawili ambao walikuwa wakikimbizana na WAZALENDO waliochelewa kutoka MAHANGANI.

Ilichukuliwa idadi ya MADAWILI ikajumuishwa na yetu ambapo maafande hawakuridhishwa na usahihi wa idadi iliyopo ikabidi tuhesabu kwa mara nyingine na wakati huu tulihesabiwa wote MADAWILI na NGORONGORO bila kutenganishwa.

Ilionekana ni kama jeshini walikuwa wanapenda mno kuhesabu namba maana hazikuisha dakika tatu tulisimama na kuhesabu tena.

Walituhesabisha mara kadhaa ikabidi wakubaliane na idadi iliyopo maana kila tulipohesabu walioongezeka hawakuzidi watatu hivyo walitusisitiza kukariri namba hizo maana kuna watakaoumia baadaye.

Baada ya maneno hayo tuligawanywa na kuunda MABOGI matatu yenye mistari mitatu iliyonyooka kwa kila BOGI nikamsikia afande,

“Haya wekeni CHENJA shoo ianze” basi nikaanza kumsikia Masare.

“Masare: Ewii
Sisi: Ewaaa
Masarei: Ewii
Sisi: Ewaaa
Masarei: Elewii
Sisi: Elewaaa
Masarei: Nani kasema kwa mguu mbali
Sisi: Adoado tunaondoka
Masarei: Awee tunaondoka
Sisi: Haya twende
Masarei: Tunaondoka
Sisi: Haya twende
Masarei: Awee tunaondoka
Sisi: Haya twende
Masarei: Haya tunaondoka
Sisi: Haya twende”.,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea…………………………………
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 13

Tuliondoka zetu mdogomdogo kama songi lisemavyo mpaka tukazikata kilomita zipatazo mbili tukapoza injini kwa tuliotangulia huku tukiwasubiri wenzetu.

Wakati tunajiandaa kurudi tulihesabu tena namba kwa kurudiarudia na tulisisitizwa kwa mara nyingine kuzikariri namba hizo ambazo idadi ilionekana kupungua ikilinganishwa na ile ya mwanzo UWANJA WA DAMU.

Tulihoji uhalali wa namba tulizohesabu awali tukiwa kikosini tukaambiwa tuachane nazo na tukariri hizi za wakati huu.

Hakukuwa na namna nyingine zaidi ya kukubaliana nao ila mpaka muda huo tulishahesabu namba zaidi ya mara kumi hivyo haikuwa rahisi kuzisahau na kukariri nyingine kila wakati.

Tuliianza safari ya kurejea kikosini na nyimbo mbalimbali na wakati tunakalibia MAHANGANI wimbo ulibadilika ukawa unasikika uliotoholewa kwenye ule maaruufu wa “Jua lile literemke mama” ikawa kama hivi,

“Mwanzilishi: Ewii
Wote: Ewaaa

Mwanzilishi: Ewii
Wote: Ewaaa

Mwanzilishi: HANGA lile literemke mama
Wote: HANGA lile literemke mama

Mwanzilishi: Ayaya iya iya mama
Wote: Ayaya iya iya mama

Mwanzilishi: Ndo lile HANGA ndo lile, ndo lile HANGA ndolilema
Wote: Ndo lile HANGA ndo lile, ndo lile HANGA ndo lile mama

Mwanzilishi: Ndo lile HANGA ndo lile, ndo lile HANGA ndolilema
Wote: Ndo lile HANGA ndo lile, ndo lile HANGA ndo lile mama”.

Tulifika MAHANGANI tukiwa tumechoka vya kutosha, tuna majasho, mavumbi na matongotongo machoni hivyo basi ratiba iliyopo mbeleni ilikuwa ni usafi ingawaje siyo wote tulioizingatia.

Kwa kuwa nilishaanza kujiona nimekuwa mwenyeji sikujisumbua kwenda kupanga foleni nilijituliza kitandani kupunguza uchovu uliotokana na MABIO kama ilivyokuwa Baraka.

Nikiwa nakaribia kupata usingizi ghafla nikastuliwa na filimbi zilizokuwa zikipulizwa mfululizo MAHANGANI walikuwa ni waheshimiwa wa jeshi la akiba waliokuwa wakitusisitiza kuelekea KOMBANIA.

TULIFOLENI tukiwa na mafagio pamoja na ndoo tukagawanywa kwenye maeneo mbalimbali kwenda kufanya usafi na tulipomaliza tulirudi MAHANGANI kwa ajili ya usafi binafsi.

Nilifika moja kwa moja sandukuni na kutoa mswaki na dawa ya meno nikaenda KUFOLENI kwenye mabomba kwa ajili ya kuteka maji kwa ajili ya kusafisha uso.

Bombani hali haikuwa nzuri kwani mabomba yalikuwa ni machache na maji yalikuwa yakitoka kwa kasi ndogo hali iliyopelekea kuwepo kwa msururu wa watu mabombani.

Kwa sisi ambao hatukuwa na uhitaji wa maji mengi yaani tulikuwa na vikombe tu kwa aajili ya kunawa uso tuliruhusiwa kukinga pasi na kupanga foleni japo tulipokuwa wengi ikawa kero kwa wale wenye ndoo kwani ndoo zao zilikuwa hazipati muda wa kukingwa badala yake ilikuwa ni toa kikombe weka kikombe.

Baada ya kuumaliza mchakato huo nilirudi zangu sandukuni na kurudisha nilivyovitoa na kuitwaa simu niliyoikuta na missed calls 12 zote zikitoka kwa Linda na meseji karibia 7 huku zikitoka kwa Linda, 1 ya wasafibet, 1 kutoka sportpesa, 1 kutoka ofa kabambe, 1 ya 15572 na nyingine kutoka 15570 kifupi simu yangu ilipendeza.

Nilifungua meseji za Linda ya kwanza ilisomeka, “Hello K mbona hupokei simu mpenzi wangu?” na nyingine ilikuwa ikisema,

“Najua simu zangu unaziona ila hutaki kupokea vibaya ivyo hata kama hunipendi ndo usipokee simu zangu, sawa bana mimi nimeshaanza safari nakuja huko nikuletee nini”.

Huwezi amini mwanaume bila kujifikiria nikajikuta namjibu “Eat some more na Pepsi ya take away kubwa” yaani nilikuwa kama kichaa mwenye rungu mkononi niliagizia kana kwamba nimempa hela mdogo wangu Uledi akaninunulie dukani.

Hali ilikuwa ni mbaya maana chakula cha MZABUNI nilianza kukikinai hivyo basi nilipokutana na fursa kama hiyo ya kubadili radha kidogo kutoka mtaani sikutaka inipite.

Mara baada ya kutoa majibu hayo akili ikakaa sawa nikapata nafasi ya kuangalia muda niliyotumiwa ujumbe nikagundua kuwa ile ya kwanza ni zaidi ya nusu saa limepita ila hii ya pili ndo kwanza ina dakika mbili.

Nikiwa natizamia hilo ghafla simu iliita namba niliyosevu “Linda Babe” nikapata kigugumizi kuipokea mpaka pale ilipo kata ila hakukata tamaa baada ya kukatika simu ile alipiga tena.

Nilipokea nikakutana na maneno yaliyoniacha kinywa wazi kwani ni kama alikuwa akinisuta mana aliniambia,
“kwahiyo kisa nimekwambia nikuletee nini ndo umeamua kujibu ila simu zangu na text nyingine wala hukuziona”.

Nilijikaza na kamuelezea hali ilivyokuwa kwamba simu ilikuwa sandukuni na mimi nilikuwa kwenye FATIKI hivyo sikuwa nayo ndiyo maana sikupokea.

Alinitaka niwe nayo muda wote mpaka pale atakapofika kikosini nilipomwambia tunakatazwa kutumia tukiwa kwenye FATIKI aliniambia nijiibe aliamini kuwa kama iliwezekana kufanya hivyo tukiwa shule basi huku nako inawezekana kabisa.

Kifupi alikuwa ni king’ang’anizi balaa ilinibidi nimkubalie kwa lengo la kumzuga akate simu mambo ili mengine yaendelee, aliikata simu nikaizima na kuitupa sandukuni na kulifunga.

Muda ulipowadia zilipigwa filimbi za kutosha tukamiminika KOMBANIA ambako afande wa zamu alikumbushia namba zake wakati wa kurudi kwenye MABIO akadaka watu wake aliowarusha kichurachura na adhabu nyingine ndogondogo mpaka pale tuliporuhusiwa kwenda saiti kubeba vifusi.

Safari hii tulikuwa na Afande mmoja aliyekula chumvi ya kutosha jeshini aliyefahamika kwa Jina la Mtalibani kama a.k.a yake kikosini hapo.

Mtalibani yeye alitutaka tupeleke vifusi ndoo zipatazo tano na akateua WAZALENDO ambao walikuwa kama makarani yaani waliandika majina na kutuhesabia idadi ya ndoo tunazomwaga.

Afande huyo ambaye cheo chake ni Mteule wa jeshi kule saiti kunakochimbwa vifusi aliwaachia SERVICE MEN na huku kunakomwagwa vifusi alisimamia shoo yeye mwenywewe.

Katika moja ya tukio ambalo sijalisahau moja ya MZALENDO aliyekuwa karani alimjazia jamaa yake kuwa keshamaliza ndoo zote tano ilihali wengine ndo kwanza tumejaziwa ndoo mbili mbili.

Mtalibani pale tu alipoishika ile karatasi na kuligundua hilo aliichana akamkamata yule karani akaanza kumpa mibanzi na ngwala mfululizo na kwa vile palikuwa na vifusi visivyoshindiliwa eneo hilo itoshe kusema vumbi lilitimka.

Hakukuwa na wakugombelezea kutokana na gap la cheo cha Afande huyo na sisi japo tulimhurumia MZALENDO huyo ambaye muda wote alikuwa akishambuliwa bila kujibu mashambulizi.

Ilikuwa ni mfano wa litakavyokuwa pambano baina ya Karimu Mandonga-Mtu kazi dhidi ya Selemani Kidunda-Jini Makata.

Kwa bahati eneo tulilokuwa tukimwaga vifusi lilikuwa karibu na ofisi za mapokezi zilizokuwa karibu na zahanati ya kikosi hivyo afande mmoja alisogea na kugombelezea ugomvi ule na kumwambia MZALENDO yule akimbie waliko wenzie yaani kule vinakochimbwa vifusi.

Afande yule ambaye alimtuliza Mtalibani na kutuambia kuwa tukamwambie jamaa abaki kulekule na asipandishe mpaka FATIKI ile itakapoisha. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

******Itaendelea……………………………………………...
 
MAISHA YA DEPO

SEASON-2

EPISODE 15

TULIFOLENI tukiwa na Afande Rashidi aliyekuwa akisaidiana na Afande Devi, tukiwa tunasubiri maelekezo ni kipi kifanyike Afande Devi alianza kuwatoa mbele waliokuwa na nywele ndefu.

Afande Rashidi alituambia,
“Yaani mmepewa UTAWALA badala ya kwenda kufanya usafi wa mwili mkaenda kukuna AMALA zenu” walicheka wachache miongoni mwetu ila wengine tulikaa kimya maana tulisikia msamiati uliokuwa mpya kwetu.

“Mkipewa UTAWALA nyie WAZALENDO kitu cha kwanza ni kwenda kufanya usafi wa mwili wako na mavazi kulala na hayo mengine ni baada ya kumaliza usafi” aliongeza afande Rashidi.

“Hembu fikiria siku zote hizo zilizopita kuna siku afande yeyote aliwaambia nendeni mkaoge au mkafue WAZALENDO, eti nyie si nawauliza”.

“Hapana Afande” tulimjibu akaendelea kusema,
“Haya waoneni wenzenu kule na rasta zao kichwani kama wajamaika” tuliangua vicheko aliposema hivyo maana hao wanaoambiwa wana rasta kichwani walikuwa na mipara ya kwenda.

“Mnacheka WAZALENDO zile nywele huku jeshini ni rasta yaani kama umenyoa leo baada ya siku tatu unatakiwa unyoe tena zishakuwa rasta hizo”.

“Niwaulize swali WAZALENDO”
“Uliza afande”
“Kipara kimoja hunyolewa kwa dakika mbili, je vipara vitatu vitanyolewa kwa muda gani?” alituuliza swali hilo la kizushi afande Rashidi huku akiwa anatabasamu.

“Atakayetoa jibu sahihi badala ya majawabu namtandika UTAWALA BINAFSI aende akajitawale HANGANI” aliendelea kukazia afande huyo.

Kwakuwa tulishaonja radha ya UTAWALA na kuufaidi utamu wake kila mtu alinyoosha mkono kutaka kujibu ili akale zake bata kwenye deka za jeshi.

Afande Rashidi kuona wingi wa mikono iliyonyooshwa akasema,
“Ina maana swali langu limekuwa jepesi kiasi hicho sawa ila nataka jibu siyo mnipe majawabu”.

Afande Rashidi alianza kuyapokea majibu ambapo watu wote watano waliochaguliwa walijibu sawa kuwa “Kipara hakinyolewi”.

Afande akatuambia “Ina maana nyie wote jibu ni hilohilo moja hakuna lingine, oya na nyie wajamaika huko mnakubaliana na hawa jamaa zenu huku”.

Marastafari wale kwa pamoja wakajibu “Ndiyo afande”.

Afande akasema “nyie kweli MANANGA na form six yenu basi mnajikuta mnajua kuchemsha bongo haya bana, hakuna mwenye jibu la tofauti na hilo lililokuwa sahihi nimtandike UTAWALA?”.

Kaukimya kalitawala sijui nikapatwa na nini nikajikuta nanyoosha mkono juu afande akaniuliza kama nina jibu jipya ama ni lilelile nikamjibu ni jipya akaniruhusu kujibu.

Nikamwambia “Vipara vitatu vitanyolewa kwa dakika sita afande” umati wote wa WAZALENDO uliangua kicheko ndipo akili zikanirudi eeh kumbe nimetoa boko tena.

Afande aliniuliza kama nina uhakika ikabidi nikaze na kumjibu kwa herufi kubwa “NDIO”.

Aliendelea kuulizia kama kuna jibu lingine ndipo akanyoosha dada mmoja na kujibu kama nilivyo jibu mimi nafsi ikapata Faraja kwa kuanza kupata wafuasi.

Kukawa na pande mbili sasa hivyo afande aliuliza wanaounga mkono jibu la mwanzo ama langu.

Tulikuwa wanne pekee katika umati ule ambao tulisimama na jibu nililolitoa na kati yetu mwanaume nilikuwa peke yangu na MADAWILI watatu ilibidi afande atutenge.

Afande alichokoza mjadala na kusema,
“Kwahiyo nyie mnafikiri kama mtakuwa mmepata tutawapa UTAWALA wote na kwenda kwenye FATIKI na hawa wanne”.

“Why not” ilisikika sauti ya kwanza kutoka kwenye kundi lililokuwa likiliunga mkono jibu la kwanza.

“Eeh UTAWALA kidogo tu mshaanza kuongea na kizungu” nilijikuta nimeropoka na kuwafanya wacheke kana kwamba wameiona nanihii yangu.

Afande akaniuliza “hivi jibu lako umelipataje hembu tuambie”.

“Anhaa of course yes nimechukua vipara vitatu nikazidisha na dakika mbili nikapata dakika sita ndiyo nikanyoosha mkono na kukupatia jibu” nilianza kugain momentum kwa wakati huu nikawa mchekeshaji pale KOMBANIA mana niliendelea kuwavunja mbavu.

“Kwahiyo umetumia table ipi ya pili au ya tatu?” aliniuliza afande Rashidi.

“Ah hapo ni table ya tatu si tatu mara mbili ni table ya tatu afande”.

Walizidi kucheka wanazengo afande Devi nayeye akauliza “We mwanangu ni kombi gani kwanza?”.

Nilisita kidogo nikamjibu “EGM mwanauchumi kabisa”.

Nikasikia mngurumo wa sauti ya nne ukisema “tangu lini tena” alikuwa ni Ambrose niliyekuwa nikisoma naye HGK tulipokuwa advance.

Nilimsikia afande Rashidi akisema,
“Apo sawa kumbe umesoma hesabu ndiyo mana umetoa jibu la kimahesabu hesabu mana hawa HGK na HKL wametoa majawabu na wanaungana pamaja”.

Hakugundua tu ila moyoni nilimmaindi kwa kusema vile maana hata mimi mwenyewe nimesoma HGK nilimdanganya tu pale kuwa nimesoma EGM hivyo niliona kama katusema ma HGK kuwa hatuna akili.

Afande alituchanganya kwa wenzetu akatuamuru tuketi chini kwenye zulia la jeshi akatupangilia kwa kusema “WAZALENDO chukueni hii kipara kinanyolewa, asikudanganyeni mtu kuwa kipara hakinyolewi jeshini ni sehemu pekee ambayo vipara vinanyolewa”.

Tayari nilishakumbwa na furaha mpwite mpwite maana kwa mbaali nilishaanza kuinusa harufu ya UTAWALA.

Afande aliendelea kunena kwamba, “Ndiyo maana tukawaambia wale,wajamaica kule waende wakanyoe mana vile ni vipara kweli ila nywele zimeshakuwa kubwa mno hakuna namna ukakaa na nywele zaidi ya siku tatu jeshini haswa kwenye kozi bila kunyoa hilo ni kosa kubwa”.

Afande aliendelea kukazia,
“narudia tena jeshini ni sehemu pekee ambayo vipara vinanyolewa na ndiyo maana namtangaza swahiba yangu pale mwana uchumi na mahesabu kuwa mshindi wa challange yetu nyie wengine endeleeni kukalili hadithi za Kinjektile Ngwale na Chifu Mkwawavinyika wa vita ya majimaji”.

Baada ya Afande kusema hivyo nilisimama na kunyoosha mikono juu mfano wa mchizi wangu Mrusi bingwa wa mapambano asiyepigika Boyka anavyofanyaga ulingoni baada ya kushinda pambano.

Nilizunguka pande zote za dunia mikono ikiwa juu mithili ya sanamu wa konyagi nikajikuta nawaambia “pigeni makofi basi” nafikiri ni wale tu watatu waliokuwa wakiniunga mkono ndiyo waliofanya hivyo maana niliyasikia kwa uchache mno.

Nilimsikia Afande Rashidi akisema “Kumbe mchumi wetu naye mwehu haya mpigieni makofi mwenzenu achene wivu” hapo niliyasikia ya kutosha namimi nikawa nayasindikiza kwa kutingisha kichwa yaani kama ni upele ulimpata mwenye kucha kazi ikawa ni kujikuna tuu.

Mwisho wa pongezi hizo nilikaa chini afande Rashidi akasema “Ila mwanangu unafaa sana twende kwenye FATIKI ukatuchangamshe mana kazi ikiwa ngumu tukafurahi kama hivi inakuwa nyepesi kabisa”.

Aliendelea kusema “Leo waache hawa wadada wakalale we twende tu kwenye FATIKI”.

Nilimjibu kwa sauti ya huruma “Aaah afande nipe UTAWALA wangu kumbuka nimeutolea jasho” watu waliangua vicheko lakini mwisho wa picha tukaruhusiwa na wale wadada na kwenda kuubonda zetu UTAWALA tukiwaacha wenzetu KOMBANIA wakijiandaa na mauzauza ya vifusi. ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

*****************Itaendelea………………………………..
Nimependa hii maana nimejikuta natabasamu
 
Operesheni Makao Makuu Dodoma!

Afande mgeni rasmi.........

Mbele yako ni vijana ........ Op Makao Makuu Dodoma...

Nipo tayari kwa ukaguzi wako..... Afande mgeni rasmi!
 
Back
Top Bottom