Maisha ya mwana JamiiForums nje na ndani ya JamiiForums

Acheni kufuatilia maisha ya watu hayawahusu. Pambaneni na hali zenu. Si kila mtu humu ni muongo wa kujikweza. Niliobahatika kuwafahamu humu ni watu bomba sana na wengine wana maisha mazuri sana kwa kuchakarika kwao kwenye elimu na biashara.

Mbona kuna wengi humu wanakuja kuomba misaada ya aina mbali mbali na wanasaidiwa!? Mbona hao hamuwasemi!?

Mambo ya Ngoswe mwachieni Ngoswe. Si kila mtu humu ni muongo au mtu wa kujikweza wengi wako kimya mpaka mpate bahati ya kufahamiana kwa karibu.
 
Hahaaaaaaa haaaaa haaaaa... Daaah!! Hapo kwa wanawake wa JF kiboko
 
Hahaaa mjomba mie sio hater ni jamaa simple sana mwenye kupenda furaha, tuko pamoja sana
 
Anaongelea aliokutana nao lazima.
 
Kweli kabisa mzigua
 
Hiyo nambari 5 (v) inaonekana umgeni humu.kuna waalimu kibao na wala hawajifichi kuna mpaka nyuzi ya waalimu kubadilishana vituo vya kazi.

Cha msingi nakushauri usipoteze muda kuwatafakari na kutaka kuwajua watu.haitakusaidia lolote.we ingia jadili hoja/mada zilizopo ukimaliza kafanye mambo mengine
 
Alichoshindwa kuelewa mtoa mada ni kwamba. Kwenye jamii yoyote hao aliowataja wapo. Wapo watu wana sifa zote humu alizozitaja na kweli ndo maisha yao halisi hawaigizi. Na wapo watu sio maisha yao wanaigiza. Kwenye mitandao yote tunao hao watu. Sio humu tu.
 

Cape Town Fish Market mimi naendaga kweli.
 
Asipokuelewa kwa ulichoandika basi ana lake jambo.

Ila BAK inabidi na Emmy umfundishe kuandika gazeti sababu sio kwa gazeti hili. Lol [emoji85]
 
Hahaaa mjomba mie sio hater ni jamaa simple sana mwenye kupenda furaha, tuko pamoja sana

Sijasema ni hater mkuu..namaanisha mambo ya huku ni ya hukuhuku na mtaani ni ya mtaani. BAK ametoa maelezo mujarab, inategemea na mtu anataka nini JF, kwangu cha kwanza ni kupata burudani, napunguza nyongo za stress zangu, pili elimu na updates za mambo mbalimbali.

Pia kuna watu wenye uzoefu wa kada mbalimbali huku, huwezi kupata hiyo fursa kwingine kwa wakati mmoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…