Bin Laden alikuwa na tatizo la figo na alikuwa akihitaji mashine ya kusafishia damu , hili limeelezwa mara kadhaa na viongozi wa kiserikali wananchi mbalimbali, hivyo alishakufa muda mrefu hata kabla Obama hajakitangaza kifo hicho na yeye kuwa ni mtu wa tisa kufanya hivyo. Ni kama Osama amekufa mara tisa na kufufuka kila mara.
Wakati shambulizi la 9/11 likitokea, Osama alikuwa amelezwa kwenye hospitali ya kijeshi Pakistan akitibiwa tatizo lake hilo la figo. October 2001, Bin Laden alitokea kwenye video akiwa kavalia kijeshi na kajifunga kilemba, mwili umedhoofu na anaonekana kukonda.
BIN LADEN ALIVYOONEKANA MWAKA 2001, OKTOBA
Disemba 2001 akatokea kwenye video nyingine, akiwa kavalia kijeshi na kilemba, lakini hapa alionekana amechoka zaidi na afya yake imedhoofu maradufu kiasi kwamba hakuweza hata kunyanyua mkono wake wa kushoto.
BIN LADEN ALIVYOONEKANA MWAKA 2001, DISEMBA
Ilipofika Disemba 26, 2001, Fox News ilirusha habari iliyoichukua kutoka katika gazeti la Pakistan Observer ikisema kuwa viongozi wa Taliban walitangaza rasmi kifo cha Osama mapema mwezi Disemba 2001, na kwamba alizikwa ndani ya masaa 24 kama zilivyo taratibu za Kiislam.
TAARIFA YA TALIBAN JUU YA KIFO CHA OSAMA MWAKA 2001.
Januari 18, 2001, Rais wa Pakistan Pervez Musharraf alinukuliwa akisema kuwa, Osama Bin Laden alishakufa. Musharaf akaendelea kusema kuwa alifahamu Osama amechukua mashine mbili za kumuwezesha kuishi kama njia ya kusafishia damu yake kwa vile figo yake imekufa na mazingira ya kuhama hama anayoishi, pamoja na wataalam ambao wanahitajika kuziendesha mashine hizo, na umeme pia, ni vigumu kusema kuwa Osama yuko hai, na picha zake za hivi karibuni zinamuonesha amezidi kudhoofu.
Julai 17, 2001, kiongozi wa FBI kwenye kitengo cha kupambana na ugaidi, bwana Dale Watson alisema haya:
‘Mimi binafsi nafikiri Osama hayuko pamoja nasi tena’
October 2001, rais wa Afighanstan na kibaraka wa Illuminati, Hamid Karzai kupitia kwenye mahojiano na CNN alisema hivi,
‘ Naamini Bin Laden ameshakufa.’
Novemba 2001, Senator Harry Reid alisema kuwa ameambiwa kwamba Osama alikufa kwenye tetemeko la aridhi lilitokea Pakistan October, 2005.
September 2006, kitengo cha ujasusi cha Ufaransa kilivujisha habari kuwa Osama bin Laden amefia Pakistan.
Novemba 2, 2007, aliyekuwa waziri mkuu wa Pakistan Benazir Bhutto alisema kwenye mahusiano na kituo cha Al-Jazeera kuwa Osama bin Laden ameshauwawa na akamtaja muuaji wa Osama kuwa ni Omar Sheikh. Bhutto aliishi wiki moja tu baada ya mahojiano hayo, aliuwawa na mtu wa kujitoa muhanga.
Machi 2009, mtu aliyeshikilia wadhifa kwenye kitengo cha ulinzi cha Marekani na ambaye ni profesa katika chuo cha Buston bwana Angelo Codevilla alisema kuwa Elvis Presley anaweza kuwa hai lakini si Osama.
Mei 2009, kiongozi wa Pakistan, Asif Ali Zardari alisema kuwa, mashirika ya kijasusi ya Marekani hayajasikia chochote kutoka kwa Osama kwa miaka saba na sidhani kama bado yupo hai.
Leo hii Obama kaongezeka kwenye orodha ya watu hao mchanganyiko waliotangaza kifo cha Osama. Wengine wanaweza kusema taarifa za viongozi hao walio tangulia kabla ya Obama hazina ushahidi wa kutosha bali ni maneno matupu.
Lakini Pia taarifa ya Obama haina ushahidi wowote zaidi ya picha za mtu ambaye anaonekana nusu ni Osama, nusu mtu mwingine. Hata hivyo picha hizo tumeshazigundua kuwa ni za kughushi.
Sent using
Jamii Forums mobile app