Maisha yako ya Ndoa yamekuwaje baada ya kutofanikiwa kuoa/kuolewa na 'your dream man/woman?

Dah mkuuu unajua kukatisha tamaaa.[emoji3]
Wanadamu wanapenda kudanganywa ilhali ukweli mchungu unawasubiri na machozi yako pale pale baada ya majira uongo kuisha. Ni bora umwambie mtu ukweli mchungu...ataumia leo lakini kesho atakushukuru mkuu.

Huwezi kuwa umechakatwa na kijiji kizima halafu kwenye maombi yako unataka mcha Mungu.
Hakika utspewa malaya staafu mwenzio ili mkaishi kwenye danguro lenu wawili mkiwa wastaafu wa uchataji na uchakwataji[emoji28]
 
Ila trust me si maisha wala mapenzi yanaenda kwa kanuni hii..!
Kuna watu very saint wamepata vitu vya ajabu and vice versa..!!
 
Ila trust me si maisha wala mapenzi yanaenda kwa kanuni hii..!
Kuna watu very saint wamepata vitu vya ajabu and vice versa..!!
Kweli usemavyo kumbuka anaweza asiwe malaya kama mkewe lakini akawa na tabia nyingine mbovu iliyojificha na itakuwa maumivu kwa bi dada.
 
Kweli usemavyo kumbuka anaweza asiwe malaya kama mkewe lakini akawa na tabia nyingine mbovu iliyojificha na itakuwa maumivu kwa bi dada.
Usisahau hakuna mtu utampata perfect Mswati..!
 
Ila ipo siku utapata mtu sahihi mtakayekuwa mnapendana, vuta subra mkuu
 
Aiseee how i wish... hongera sana dear, mje mzeeke pamoja🙏
 
Maranyingi tunaoa tunaowahitaji baada ya kutendwa na tuliowapenda.

Nilikuwa na bint niliyempenda sana nilimtoa chini kabisa hadi kufikia kujua kuvaa kisasa, naye alinikuta nikiwa chini kabisa. Hii ilitujenga kupendana kweli.

Lakini mwenzangu alikutana na waliofanikiwa zaidi yangu akanikataa akaolewa huko, baada ya miaka mitatu nikaoa mwingine muda mfupi sana baada ya kufahamiana.

Kuna wakati natamani ningekuwa na yule niliyempenda lakini huyu namheshimu sababu ni mama wa watoto wangu. Yeye pia kuna wakati ananilaumu sipo romantic kwake. Najitahidi huu mwaka wa 7 tunasonga mbele.
 
Usisahau hakuna mtu utampata perfect Mswati..!
Carleen;
Unajua hapo juu nilikuwa ninawaweka sawa lkn bado sijatoa mtazamo wangu katika mapenzi.

Ukweli ni kwamba hautapata mtu sahihi wala mkamilifu.

Mpenzi bora hutengenezwa
Mke bora hutengenezwa na mme wake
Mme bora hutengenezwa na mke wake.

Mimi mwanzo wa maisha yangu kitaa.
Niliwahi kuajiriwa na boss mmoja alikuwa mkubwa flani katika taasisi maarufu ya mke wa namba moja Tz.
Alinifunza kitu.

Walikutana na mme wakiwa kapuku skwea.
Walipanga chumba kibovu na hawakuwa hata na gororo walikuwa wakilalia box yaani makasha ya vifungashio.

Mke ndiye alikuwa mfariji mkuu na mtia moyo mkuu.

Kuna wakati wakati Mungu akawaonekania.
My dear kwasasa ni miongoni mwa wabarikiwa hatari.
Ndoa yao ni bora hatari.

Nini nataka kusema; kutafuta mwenza hasa kwa wasichana wa siku hizi ni changamoto.
Mnasngalia ana future?

Bila kujua future bora mtaitengeneza wawili na hii ndio itakuwa ndoa bora.

Wanaume nao macho juu..wanasska Salha type..mwishowe mkaa na bunduki zinahusika.

Buddy... mme wako ni jamaa flani kitaa hana nyuma wala mbele but anakusubiri wewe mke bora ukamfinyange.

Kadhalika wanaume....mkeo ni kadada flani shape less super flat screen flan, inakusubiri ukailishe iote hips ipendendeze.

Ukaipige sopu sopu ing'ae hakika umepewa na Mungu...itakuheshimu na kukufanya mume boraa aaah
Carleen
financial services
Darlin
 
thank you so so much,
Umenifunza kitu kikubwa sana sana keisangora ubarikiwe..!
Wacha niendelee kujifanyia tathmini na kupambana ili kuzidi kuwa bora..!!
Duu Kama umeusoma una moyo najua Kuna madini sema mpaka tywe like minded Kama Niko against na wewe nadhani utanipinga Mana nitakuwa nimevunja beliefs zako. Jiulize why watu wenye mawazo yanayofanana wanakuwa marafiki Ila mkitofautiana kiimani sio za kidini mnakwepana Mana kila mtu anaona kitu Cha tofauti na mwenzake Mana maisha Ni kioo sio unachokiona namie nikione
 
Dream yako ni lazima mfanane sura pili lazima uwe na maendeleo. Na huwa akifa mmoja mwingine akawi kumfuata. Hii ndo wazazi awajapisha kifo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…