Maisha yamekuwa magumu sana huku uswahilini kwetu. Ninatamani hata kuuza hii Taxi bubu yangu (Chase Avante GX-100) nifungue walau pub ndogo

Maisha yanatisha lakini ukikubaliana na hali halisi ukabuni biashara ambayo unaweza kumudu mambo yataenda- Kama Bajaj ukiweza kununua hata kama siyo mpya inaweza kukusaidia cha muhimu jali matengenezo yake tu
Sawa mkuu
 
Faida haipigwi mahesabu hivyo. Faida ni kinachobaki baada ya kutoa uendeshaji
Hii inategemea na aina ya uwekezaji kwa mantiki ya bajaji ya mkataba jamaa yupo sahihi ngoja nimalize kula maana kula tena mpaka kesho muda kama huu
 
Si dili kwanini?
Bodaboda wanaoingiza hela nzuri hapa town ni wale wanaopiga kazi katikati ya jiji.

Sasa wateja ukiwabeba na fekon au sanlg hawatakuomba namba ili wakupigie simu ya kazi.

Wadada poa pia hawapandi fekon na pikipiki zingine zisizowapa mneso mzuri.

Wadada poa wanataka boxer ambazo huwapa raha wakipakiwa.
 
Hongera sana mkuu
 
Bajaj kwa 3M mkuu? Hiyo si itakuwa ni chakavu sana.
Ooh,,sasa fanya hivi,,uza hiyo gari nenda bk pakia mikungu ya ndizi kwenye mv victory,, njoo ushushe mwanza,,saa sita tu ushauza mzigo unahesabu faida,piga trip nne tu kwa mwezi,baada ya miezi sita,utakua ushatoboa
 
Mimi mwaka huu nimefungua biashara mbili..moja ya taaluma yangu na moja ndo huo mgahawa.

Mgahawa frem,ukarabati,vifaa kama viti na meza,masufuria,sahani nk nimetumia 984k nimeajiri wafanyakazi wawili ila mmoja nina ukaribu nae sana...
Upo vizuri sana mkuu
 
Mawazo yako hayaendani iyo Gari ukiuza ni 2.-2.4Million labda ununue pikipiki sio Bajaji wala kufungua Pub. Huu ndio Ukweli au ninasema uongo ndugu zangu. Tupambane hata uku kwangu maisha ni magumu Sijawahi kuona toka nibalehe
Pole sana na Mungu azidi kukupigani mkuu
 
mimi na mke wangu kupitia hiyo biashara tumeweza kununua kiwanja na kuhusu mimi kutoa pesa ya matumizi nyumbani sitoi kabisa.. mke anamaliza mambo yote
Bro! Nikwambie kitu[emoji848] mkeo nahisi kuna mwamba anakusaidia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…