Maisha yatakosa maana baada ya miaka 20 tu ijayo

Maisha yatakosa maana baada ya miaka 20 tu ijayo

2024 yetu ni 1990 ya Wazungu.

2045 yetu ni 2020 ya Wazungu.

Tunakoenda ujue kuna wenzetu wameshapita na Maisha kwao bado yana maana na kila mtu aliyekohuku anatamani kuishi huko ulaya.

Maisha yajayo ni mazuri na yenye maana zaidi kuliko haya ya Leo.
 
Sasa hivi watu wanajimilikisha mali hata viongoizi hawajali wengine ...Maisha tu ya leo mtu hana thamani mpaka awe na kitu , huko mbele ndio balaa kabisa .
Dunia ina system ya kuji reset, binadamu atafanya ufedhuli wee ufisadi, kukata miti, kuchoma ozone, oil spillage, pandemic za kuundwa, A.I, kuharibu maadili na mambo yote ila itafikia ku ji reset ianze upya tena!

Nafikiri huko kuji reset ndo tunachukulia kama kiama na tushakisogelea mno.
 
Kwa kuanzia nafikiri ifikiriwe namna ya kupunguza idadi ya watu kwa 70%!
Dunia haipanuki lakin teknolojia inapunguza kwa kasi ushiriki wa watu kwa idadi ila inahitaji watu kwa ulaji wa bidhaa.
Ardhi ndo mali itakayotutesa sana.
Mwenye akili na uwezo leo ni amiliki ardhi nyingi kadri awezavyo.
Ila sisi binafsi tukiamua kuishi katika kutokomeza umaskini kwa idadi ya watu waliopo inawezekana , kupunguza ubinafsi , kusaidiana kwa sana .

Dunia chini ya ubepari ni hatari sana .
 
Dunia ina system ya kuji reset, binadamu atafanya ufedhuli wee ufisadi, kukata miti, kuchoma ozone, oil spillage, pandemic za kuundwa, A.I, kuharibu maadili na mambo yote ila itafikia ku ji reset ianze upya tena!

Nafikiri huko kuji reset ndo tunachukulia kama kiama na tushakisogelea mno.
Kwa bahati nzuri sana Leo taarifa ni nyingi..wababe pekee ndiyo wanaamua nini kuwepo
 
Labda kwa huko ulaya,Kwa Africa labda baada ya miaka500.
Kama sasa TU tunaishi Karne ya 17.je miaka20 baadae huoni kama ni karbu sana.
Sisi hata kupanda ndege ni hanasa na ni sherehe kwa familia
Umetazama kwa picha ndogo....hakuna kinachofanyika huko duniani ambacho hakiji kwetu. Tatizo lipo hapa.

Kama hatushiriki kwenye kuunda na kuweka sera basi sisi ndiye tutakuwa na mkwamo wa Kila kitu. Kwa sababu tunapokea Kila kitu.
 
Nikusalimu Ndugu!!

Kwa kuwa tumepewa UHAI basi wajibu wetu ni kuhakiki wajibu unatimizwa wa Kila mmoja wetu akiwa na huu Mwili, usijipe woga Wala USIOGOPE Kuwa na wazo mbadala.

Maisha ya hapa ulimwenguni yameanza KUKOSA maana Lakini ifikapo 2045 takriban miaka 20 ijayo maisha ya mwanadamu YATAKOSA maana kabisa.

1-Ngono kwa lengo lile kuu la uzazi na kuleta uzao, litakuwa limepoteza maana au halina maana kabisa. Why?

Leo Kuna technology ya IVF na nyingine nyingi ambazo zimeleta mbadala wa kupata uzao, mwanamke anaweza kupata mtoto maabara wa jinsi na RANGI anayotaka yeye, hapa kwetu tumefanya na uzinduzi wake kabisa, ni jambo jema. Lakini kwa future ya utu wa MTU kwa Asili yake inaenda kupotea .

Tumeruhusu wanaume wawili nao wawe na watoto wa maabara as if ni jambo jema, huu ni mwelekeo wa kuangamiza kizazi chenye Asili ya uumbaji, as nature laws speak.

Tuendako MTU akichoka kubembelezana na MTU mwenye HISIA ataenda kujipatia MTU mwenye akili bandia ambaye kwa maana ya uwezo wa akili atakuwa amemzidi mwanadamu huko ndiko tuendako. ...hapafurahishi hata kidogo.

2: ELIMU (education system) "Ukiwa mjinga hutapona ujinga wako kwa kuonewa huruma Bali kuelewa na kutambua vitu vinafanyikaje"

20yrs to come kwa Elimu hii inayotolewa na mifumo yetu itakuwa useless kwa zaidi ya 50%. Speed ya KUKUA kwa technology kunawatisha hata nchi tajiri Duniani. Je sisi tumeianza safari ya 2045?

Nafahamu ni ngumu kubadilisha mifumo kwa haraka,Lakini ni rahisi sana kubadilisha mifumo hasa unaoumiliki ambao ni familia yako. Change from there our future scare. Ruhuusu mtoto akili yake ifanye kazi, taaluma imeletwa Bali akili amekuja Nayo mwenyewe as gift.

Yapo mengi..tuanzie hapa
Asilimia kubwa umeongelea hofu mfano mimi niko tayari kutengeneza familia kupitia IVF sio kosa sababu kupata mwanamke wa ndoa imekua ni ngumu sana
 
Asilimia kubwa umeongelea hofu mfano mimi niko tayari kutengeneza familia kupitia IVF sio kosa sababu kupata mwanamke wa ndoa imekua ni ngumu sana
Siyo kosa kwa Mujibu wa Sheria za wanadamu Lakini kwa Mujibu wa Sheria za Asili si sahihi
 
Dunia ina system ya kuji reset, binadamu atafanya ufedhuli wee ufisadi, kukata miti, kuchoma ozone, oil spillage, pandemic za kuundwa, A.I, kuharibu maadili na mambo yote ila itafikia ku ji reset ianze upya tena!

Nafikiri huko kuji reset ndo tunachukulia kama kiama na tushakisogelea mno.
Extinction imeshaanza. Sixth extinction
 
labda ulaya uko lakini sio hapa Africa

au movie ya black panther imekudanganya mkuu

hizo sci-fi movies na mambo ya AI yata athiri uko magaharibi na sio Hapa kwetu sisi

ni primitive na tutastay hapo kizazi na kizazi
 
2024 yetu ni 1990 ya Wazungu.

2045 yetu ni 2020 ya Wazungu.

Tunakoenda ujue kuna wenzetu wameshapita na Maisha kwao bado yana maana na kila mtu aliyekohuku anatamani kuishi huko ulaya.

Maisha yajayo ni mazuri na yenye maana zaidi kuliko haya ya Leo.
Tukipata muda vizuri tunaweza kujenga hoja kumi kumi Mimi na wewe then turuhusu wenzetu wachague....future ni mbaya narudia future ni mbaya
 
Kuna kipindi watu kama wewe walihofia kompyuta na hata smartphones
Hiyo siyo hofu ni prediction tu....haiondoi ukweli kwamba Madhara ya Tech ni makubwa kuliko faida when it comes kwenye maadili ya kijamii
 
Kumsomesha mtoto shule ya ada million 10 halafu akimaliza anauza matunda ni majanga.
 
Umetazama kwa picha ndogo....hakuna kinachofanyika huko duniani ambacho hakiji kwetu. Tatizo lipo hapa.

Kama hatushiriki kwenye kuunda na kuweka sera basi sisi ndiye tutakuwa na mkwamo wa Kila kitu. Kwa sababu tunapokea Kila kitu.
Hizo ni project za mabilioni,Dunia itajibalance,ipo hvyo Karne na karne.Hilo robot TU la akili mgando ni 60million above.We mshahara tu laki na nusu uezee wapi.DNA TU hapa ni tabu kupima,tunaishia kukubali kishingo upande watoto ambao ushahidi wa kimazingira si wetu.So still ni long journey mazee.
 
Back
Top Bottom