Uchaguzi 2020 Majaliwa: Uongozi wa nchi hauendi kwa upepo na ushabiki

Uchaguzi 2020 Majaliwa: Uongozi wa nchi hauendi kwa upepo na ushabiki

Mjumbe wa kamati kuu ya halmashauri kuu ya taifa ya Chama cha mapinduzi (CCM), na waziri mkuu Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa Singida kutafakari aina ya kiongozi wanayemtaka aiongoze Tanzania...
Atutoleee ujinga huyo viti maalumu jitu limeshindwa kumshawishi mwanamke kubadili dini litawezaje kuwashawishi watu wachague kijani?
 
uongozi haujaribiwi kwani majaliwa wapi kuna chuo cha uraisi kura ndo zinaweka watu madarakani
 
Mjumbe wa kamati kuu ya halmashauri kuu ya taifa ya Chama cha mapinduzi (CCM), na waziri mkuu Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa Singida kutafakari aina ya kiongozi wanayemtaka aiongoze Tanzania...
Hana hoja za maana apishe demokrasia tena anapaswa kurudi jimboni kwake akafanye kampeni kama alivyoagizwa na bashiru.
 
Tulishawajaribu wao sasa watuachie tumjaribu Mwingine. Na kama walitaka wawe peke yao wasingekubali uchaguzi huu uwe chini ya vyama vingi.

Nilikuwa namheshimu sana Majaliwa lkn kuanzia leo nae namchukulia....kama yule mama wa risasi tatu tu chali.
 
Majaribio ni sehemu ya demokrasia pia,ndio maana ya uchaguzi kila baada ya miaka mitano.
 
Huyu mpaka piko kichwani asionekane mzee ..nimemdharau unaanzaje kuwateka wapinzani wako kisiasa..ndio maana Magu analifanya atakavyo
 
Mtanzania yoyote mwenye akili timamu anaweza kuwa rais wa nchi hii. Kama JK na Magufuli wameweza kuwa marais, nani atashindwa kazi hiyo?
Ndiomaana nasema yeyote yule aliyepitishwa na tume anafaa kuwa rais wa nchi hii kama hafai basi na tume haifai na aliyeiteua tume naye hafai.
 
Mjumbe wa kamati kuu ya halmashauri kuu ya taifa ya Chama cha mapinduzi (CCM), na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa Singida kutafakari aina ya kiongozi wanayemtaka aiongoze Tanzania.

Waziri mkuu ametoa wito huo leo Septemba 15, 2020 wakati akizungumza na wananchi waliohuhudhuria mkutano wa kuwanadi wagombea wa CCM uliofanyika kwenye viwanja vya CCM kata ya Ilongero wilayani Singida.

“Uongozi wa nchi siyo jambo la mchezo, siyo jambo la kujaribiwa, wala haliendi kwa upepo na ushabiki. Ni lazima mkae na kutafakari ni nani anafaa kuongoza nchi hii,” amesema Majaliwa.

Wakati huohuo, Waziri mkuu amempokea aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wilaya ya Singida, Frank Petro Akunay ambaye ameamua kuhamia CCM.

Akunay amehamia CCM akiambatana na mkewe Betina Petro pamoja na mdogo wake Daniel petro akisema kuwa amerejea nyumbani kwani alikuwa CCM kabla ya kujiunga CHADEMA ambako ametoka sasa.

Chanzo: Dar Mpya
Wananchi walishatafakari siku nyingi! Yeye anaona ni sawa kwake kupita bila kupingwa? Watu wa namna hii sijui hata mnawezaje kuwasikiliza
 
Back
Top Bottom