Majasusi wa dunia wametuma Meseji ngumu kwa Putin na washirika wake

Hii ngoma bado mbichi maana hao jamaa wana mfumo.......sio show ya mtu mmoja hapo labda aangushwe ayatollah na mfumo wake na ndo maana anamuweka rais
Wanafikiri iran ni kama nchi za africa kila rais akiingia anaanza na mambo yke ukitaka kujua misimamo ya iran angalia alivyokuwa ahmednejad na Ebrahim rais misimamo ileile hakuna kuyumba hata akija mwengne mtasema ya aliyekuwepo
 
Na kama Iran yenyewe imeamua kumtakeke out.

Yeye kawaza kiushindani zaidi ili kubalance mzani wa battle na Israel πŸ˜‚πŸ˜‚

pu
Amefanya haraka sana kuja na conclusion ya hivi.Nilikuwa na angalia reporting za Aljazeera hata wao mpaka sasa hawajui nini kimetokea na wana reporter wao kwenye eneo la tukio. Sasa leo mtu yupo Tanzania anakupa hitimisho la hivi aya si matumizi mabaya ya akili

Ukiangalia eneo la tukio unaona kabisa hali ya hewa haikuwa nzuri,ukungu umetanda, and this could be a possible reason ya helikopta yao kuanguka japo mpaka sasa haijaonekana na hakuna ripoti kamili inayoeleza ni kitu gani kimetokea mpaka helikopta ikaanguka
 
Yupo hai, tusubiri muda uongee.. majasusi wa humu ni majasusi wa kishabiki... Mfuatilie mtoa mada wala hutosumbuka kujua kwann kaandika haya
 
Yupo hai, tusubiri muda uongee.. majasusi wa humu ni majasusi wa kishabiki... Mfuatilie mtoa mada wala hutosumbuka kujua kwann kaandika haya
Humu hatuna jasusi tuna watu wanatumia akili zao vibaya.Yani upo bongo tukio limetokea halina ata 24 hrs tayari umeshatoa hitimisho kwamba ni tukio la kijasusi.How? Kwamba alikuwa kwenye scene,au ana classified information yoyote juu ya kilichotokea(Mtanzania? Hapana hawezi kuwa nazo)

Ningeweza kusema kafanya analysis kulingana alivyoona tukio but guess what s/he was not on the scene.Then what? Kasoma tu taarifa sehemu ndio anakuja kufanya hitimisho hapa(kwamba huu ni ujasusi?Hapana)
 
Iran ni Taifa kubwa. Haitikiswi na kifo cha Rais. Rais wa Iran atembee na siri za nchi kila pahala ya nini? Hata mataifa madogo tu hayatikiswi na vifo vya marais, let alone Iran.
 
Iran ni Taifa kubwa. Haitikiswi na kifo cha Rais. Rais wa Iran atembee na siri za nchi kila pahala ya nini? Hata mataifa madogo tu hayatikiswi na vifo vya marais, let alone Iran.
Mnajidanganya nakujifurahisha huku mmebana marinda mkiwa na uchungu na maumivu makali.
 
Rais anachaguliwa kwenye uchaguzi mkuu na hawekwi na Ayattoullah.
Maigizo tu hayo Ayatollah ana nguvu kuliko rais,, na huwezi kua rais kama unapingana nae,,,,hadi uwe rais hapo ni lazima huyo jamaa pia akukubali,,, hao wapiga kura hawawezi mpigia kura mtu ambae haendani na falsafa za Ayatollah
 
Cha kwanza kuwauliza majasusi wa Iran hivi hawakujua usalama wa ndege inayobeba Rais na Waziri wa Mambo ya Nje??? Hivi hawakulinda Na kufuatilia mienendo ya Helcopter hiyo ilipoondoka na njia inazopita kwa kutumia vyombo maalumu kwa usalama?? Ni kwanini Rais na Waziri wake wakasafiri pamoja katika hali ngumu kama hii wanayokabiliana na mayahudi...

Kwanini imekua kawaida kwa Iran kushindwa kulinda na hatimae kudhibiti matukio ya hujuma kwa Viongozi wake wa Kuu kila mara Wanauwawa kama kuku hivi karibuni...Gen. Qasseem Soleyman
Wale waliouwawa majuzi kule Syria
Na Sasa inaoenekana Rais na Waziri wa Mambo ya Nje wameuwawa..

Idara ya Kijasusi ya Iran ina Shida
 
Hamna lolote iyo ajali ya kawaida hali ya hewa haikua nzuri kulikua na ukungu mzito kiasi cha kusababisha Giza
 
Waliendaje Kwenye Ukungu?
 
Waliendaje Kwenye Ukungu?
Sina taarifa kama helikopta ilianza safari kwenye hali kamaa hii(na hata kama sina taarifa hii haiwezekani kufanyika).Ukungu umeonekana kwenye taarifa ya Aljazeera wakati wakijaribu kutafuta wapi helikopta ilianguka(labda hali ya hewa haikuwa hivyo kabla yalitokea mabadiliko baada ya kuwa safari imeanza,who knows)
 
Helicopter zilikuwa 3 ujue! 🐼
 
Helicopter zilikuwa 3 ujue! 🐼
Ndio lakini jambo langu linabaki kwamba bado mapema kusema hii ni kazi ya muisrael.Niamini hakuna mbongo ambaye ana classified information juu ya hili tukio kabla ya kutokea na ata taarifa zinazoletwa hapa ni baada ya kuwa aired out kwenye media huko duniani.

Lolote linawezekana lakini bado ni mapema.Kama mtu anasema Israel kahusika basi anipe mtiririko mzuri wa mawazo yake mpaka anafikia hitimisho hilo.Kwamfano,wewe unasema helikopta zilikuwa tatu na moja ndio ikapata shida .Je,hii hoja moja inafanya utoe hitimisho kwamba ni kazi ya Israel
 
Hapo Iran utawalani kuna Wayahudi kibao kama ilivyo Russia

Unamsokomeza Rais kwenye Chopa yenye abiria 9?

Wairan wenyewe tangu jana wanajiuliza maswali mengi Sana na hilo la hali ya hewa hawalitilii maanani
 
sasa hivi ikitokea Ayatollah Alli Khomein akabanwa na gogo halafu likashindwa kutoka ujue kuna watu watasema Waisrael wamelidukua hilo gogo ukiuliza kwanini mwasema hivyo watakuwambia ni taifa teule lenye miujiza! Wengine watasema kuna ndege F35 rapter ilipita juu ya choo wakati mzee anakata n'nya sasa ikafanya Jamming of toilet
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…