Majibu haya ya serikali ni ya Kihuni!!

Dua.. mahakama yetu haina njia ya kuhakikisha maamuzi yake yanatelekezwa. Period.
 
hakuna atakayekwenda mahakamani, unless wakubaliane kuwa JK, Lowassa, Mkapa, watakuwa tayari kusimama kama mashahidi...

Kwenye hili inaonekana kuwa startegy inawapa taabu what to do, kwanza walinyamaza kimya, meaning walikuwa wanasubiri rais aseme something, he did not, kwa hiyo wakaamua kwenda solo wakitanguliwa na Mkono, then mabalozi wakubwa waliopo bongo wakaanza kuingilia kati, noma!

Sasa wako kwenye panick strategy, kila mmoja anasema lake, serikali inasema yake, hakuna kati yao anayejibu exactly tuhuma za Dr. Slaa, ambazo zinatakiwa kupelekwa mahakamani na sio kujibiwa kwenye majukwaa ya siasa,

Hiii kitu ni lazima iende mahakamani, ama sivyo CCM will never recover na hii sooo, hii ni bonge la soo, kwa sababu ni kwa mara ya kwanza Tanzania a politician is accussing other politicians with "facts" na sio hadithi, sasa ni mahakama tu inyoweza kuwasafisha CCM unless hawana imani na mahakama yao,

Binafsi sioni sababu ya kutokwenda mahakamani, yes kwenda huko itakuwa ni aibu ya mwaka maana yatafumuka tusiyoyataka wananchi kusikia, sasa what to do? Lakini ndio the only way iliyobaki kwa CCM kujisafisha, hawa kina Warioba wangenyamaza tu maana the more they talk wanaonekana wametumwa tu na kuna kitu wanaficha,

CCM na serikali, the minute wakuu wa nje walipoingilia that was it, sasa ni mahakamani tu kwenye sheria, otherwise mtatuulia chama chetu CCM, kuna ambao tuna imani nacho, sasa msiweke ubinafsi wenu mbele na chama nyuma, CCM ni kubwa kuliko nyinyi wote, na tunaweza kuwaweka pembeni wote mlioshutumiwa na kuanza na safu mpya, chini ya mwenyekiti wetu rais Kikwete, kwa hiyo msituletee hizi nyepesi nyepesi, at stake hapa ni taifa letu, sasa nendeni mahamakamani mkajisafishe, na sisi tunawasubiri kwenye uchaguzi wa wabunge tuwape dozier safi, kama mlivyoona kwenye uchaguzi wa NEC,

Tena ingewezekana mjiuzulu kwenye nafasi zenu mpaka mtakapojisafisha mahakamani, kwa nchi yoyote yenye kujali demokrasia hufanya hivyo viongozi watuhumiwa hukaa pembeni kwanza mpaka wajisafishe kwenye sheria, lakini bongo watakufa njaa maana hela nyingi wanazotuibia huishia kujengea nyumba mahawara tu, na kusomesha watoto wao nje, na pia kusubiri kampeni za uchaguzi wanunue pilau za kuwadanganya wananchi,

CCM na serikali acheni maneno mengi, twendeni mahakamani tukaongee legal facts!
 
FMES.. CCM wana njia ya kutokea.. natamani niwasaidie... lakini haya majibu yao ya kihuni ni kujiongezea shimo...
 
FMES.. CCM wana njia ya kutokea.. natamani niwasaidie... lakini haya majibu yao ya kihuni ni kujiongezea shimo...

Wahuni hupewa majibu ya kihuni. Naishangaa serikali kupoteza muda na hawa wahuni. Wengi ni hypocrites, wanasimama kwenye majukwaa kuongea kuhusu ufisadi wakati wao wenyewe wanapocket fedha za vyama vyao.

Ni yale yale.

Hivi unafikiri Nyerere angedeal nao vipi hawa wahuni...eeh wapinzani?
 
mhm, huu moto sasa ! kumbe hapa pana maongezi mengine, subiri nitundike kambi hapa kidogo !
 
...njaa itakuua mnafiki wewe!

acha iniue ! kwani nimekwambia utoe mchango kwenye mazishi yangu ? sasa unakasirika nini kama hujaombwa mchango ? you are lucky nasikia uchovu !
 
there is no truth where there is money.....

yetu macho.
 
FMES.. CCM wana njia ya kutokea.. natamani niwasaidie... lakini haya majibu yao ya kihuni ni kujiongezea shimo...

Hapana mkuu, hii iende mahakamani tu either tunaishi kwa the rule of law au we are Banana Republic,

njia ya CCm kutoka inapaswa kuwa mahakama tu, anything less than mkondo wa sheria tunakuwa Banana Republic we are not there yet!,

Dr. Slaa atoe ushahidi wake watuhumiwa wajibu, let the legal dual process proceed, and let the chips fall where they may enough na blah! blah! Mimi sasa nasubiri tu mahakamani! kwenye hili wamechelewa, I mean it is too late kuleta ujanja wowote zaidi ya kwenda mahakamani!
 
Inawezekana kabisa hakuna anayejua hoja ya Dr Slaa ina uzito gani kutokana na kulewa madaraka mno na kuiba sana. Hata wameshindwa kufikiri sawa sawa hawa wenzetu...

Wameshindwa waanzie wapi kutoa ufafanuzi...completely off target... jibu hili linathibitisha competence ya serikali yetu jinsi ilivyo!
 
Kama kweli kuna atayekwenda mahakamani, basi huyo ni capable wa kuonyesha kuwa si mfisadi...otherwise wanazuga kinga sana, ni vigumu kuamini kama hiyo ndiyo level ya competence kweli au wanafanya makusudi hawa
 

Naomba uweke ushahidi hapa mkuuu maana hizi ni tuhuma nzito kuwa wanakula pesa za vyama vyao, hebu fafanua na weka ushahidi .
 
Serikali sasa yaweka wazi faida ya Buzwagi

Mwandishi Wetu
HabariLeo; Tuesday,October 02, 2007


SERIKALI imesema mkataba wa Buzwagi umeboreshwa kwa masilahi ya taifa ikilinganisha na mikataba ya zamani ya madini, na kutaja faida za mradi huo wa uchimbaji dhahabu. Kutokana na hali hiyo, Serikali imesema tuhuma zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa wa upinzani kuwa katika kusaini mkataba wa Buzwagi, sheria na taratibu za nchi zilikiukwa, si za kweli na zina lengo la kuupotosha umma.

Taarifa ya Serikali iliyotolewa Dar es Salaam jana, ilisema mkataba wa Buzwagi uliandaliwa Tanzania na wataalamu wa hapa nchini na ukapitia taratibu zote zinazopaswa kufuatwa, ikiwa ni pamoja na kuidhinishwa na Kamati ya Ushauri ya Madini. Serikali ilieleza kuwa wataalamu waliohusika katika mchakato wa majadiliano ya mkataba huo na Kamati ya Ushauri ya madini iliyoupitisha, wote ni wazalendo na wakati wote walihakikisha masilahi ya nchi yanawekwa mbele.

“Kulinganisha na mikataba mingine iliyotangulia, mkataba huo wa Buzwagi unavyo vipengele vilivyoboreshwa zaidi,” ilisema taarifa hiyo iliyotolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo. Vipengele ambavyo vimetajwa na serikali kuwa vimeboreshwa ni kupungua kwa asilimia 80 kwa mwaka wa kwanza na asilimia 50 miaka inayofuata; Kodi za zuio kwa kazi za kitaalamu kuongezeka kutoka asilimia tatu hadi kufikia asilimia tano.

Eneo jingine ni kodi za zuio kwa gharama za utawala kuongezeka kutoka asilimia tatu hadi asilimia 15; Masharti ya kununua bidhaa na huduma mbalimbali nchini; na kuchangia mfuko wa uwezeshaji dola za Marekani 125,000 kwa mwaka.

Serikali pia imesema ujenzi wa mgodi utakapokamilika na uzalishaji kuanza rasmi inatarajiwa kwamba miaka 10 ya kwanza ya uendeshaji wa mradi huo utakuwa na faida nyingi, ikiwamo mrahaba na kodi nyingine zinatarajiwa kufikia dola za Marekani milioni 198.8. Faida nyingine zilizotajwa na serikali ni ajira kwa Watanzania 696 wa fani mbalimbali; kodi zinazotokana na mishahara ya wafanyakazi (PAYE) dola za Marekani milioni 50.3 na ujenzi wa laini ya umeme utakaogharimu dola za Marekani milioni 30.

“Laini hii itawezesha upatikanaji wa nishati ya umeme ambayo ni pamoja na maeneo ya mji wa Kahama, vijiji vya Mwine, Chapulwa, Mwendakulima, Sangiwa,” ilisema taarifa hiyo na kutaja faida nyingine kuwa ni ujenzi wa miundombinu ya uchumi na jamii kama vile shule na zahanati katika maeneo yanayozunguka mgodi.

“Hivi karibuni pamejitokeza baadhi ya wanasiasa hususan kutoka vyama vya upinzani kutoa matamshi hadharani, kuwatuhumu viongozi kadhaa wa umma walioko madarakani sasa au awamu zilizopita kuwa walikiuka taratibu au kuvunja sheria kwa kusaini mikataba ya madini,” ilisema taarifa hiyo. Serikali ilisema viongozi hao wamejaribu kupotosha umma juu ya tafsiri sahihi za sheria inayoongoza mikataba hii.

Vile vile kuna jitihada za makusudi za kuuhadaa umma kwamba kusainiwa mkataba wa Buzwagi kulikiuka taratibu na sheria za nchi, ilisema taarifa hiyo. Katika kuwaelimisha wananchi, serikali imeelezea mchakato wa mkataba huo kwa kueleza kuwa mikataba ya uendelezaji wa madini ya mwaka 1998 inampa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya madini kuingia makubaliano na mmiliki au muombaji wa leseni kubwa ya uchimbaji madini.

Taarifa ilisema kwa mujibu wa kifungu hicho, Waziri hutakiwa kupata ushauri wa Kamati ya Ushauri ya Madini kabla ya kusaini mkataba. Kampuni tanzu ya Barrick iitwayo Pangea Minerals ilipatiwa leseni ya utafutaji wa madini katika eneo la Buzwagi wilayani Kahama, Shinyanga kuanzia mwaka 2003.

Baada ya utafiti wa miaka takriban mitatu, kampuni ya Pangea Minerals iliwasilisha maombi yake serikalini ili kuingia mkataba wa uendelezaji wa mradi wa uchimbaji wa madini katika eneo hilo. Maombi hayo yaliambatanishwa na upembuzi yakinifu wa mradi huo. Timu ya wataalamu wa serikali ilianza majadiliano na kampuni ya Pangea Minerals kuanzia Mei mwaka jana kwa nia ya kuingia katika mkataba. Kufikia Februari 16 mwaka huu, taratibu zote za kisheria kwa ajili ya kusaini mkataba huo zilikuwa zimekwisha kukamilika na hatimaye mkataba huo kutiwa saini Februari 17 mwaka huu.

Katika hatua nyingine, malumbano juu ya suala la ufisadi na rushwa yanaweza yakafikia kiwango cha kuleta mafarakano na uhasama katika jamii yakizidi kiasi. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Jaji Mstaafu Mark Bomani alisema kutokana na malumbano ya ufisadi yanayotokea kwa sasa, vitendo vya rushwa na ufisadi ni lazima vipigwe vita kwa nguvu zote, lakini sheria za kutuwezesha kufanya hivyo na sababu za kufanya hivyo vipo, kinachotakiwa ni utashi wa kufanya jambo hilo.
 
Nilikwisha ainisha kwamba uongo haufanani hata siku moja. Ona sasa!

Matamko yote ya serikali ni ya Kiimla hayalengi kujibu hoja bali yanalenga kuwachafua watoa hoja bila kujali uzito wa hoja.

Wasemapo kuna jitihada za makusudi za kuuhadaa umma wanatakiwa waziseme moja moja na kuzipa maelezo ya kutosha.

Serikali haiwezi kutoa matamko ya kubuni na kijumla kwamba kuna njama bila kusisema njama zenyewe.

Hawa wamelewa mvinyo wa madaraka.

Nakubali juu ya kodi za mishahara ya wafanyakazi na kazi zenyewe lakini changio lao ni Secondary.
Primary contributor ni Tax ya Dhahabu yenyewe na shughuli nzima ya kuchimba dhahabu.
Kuhusu kodi ya ardhi?

Mtumia ardhi yeyote ni lazima ailipie kodi serikalini hilo si ombi ni sheria.
Kodi ya Mapato ya dhahabu yenyewe?
Ukitengeneza Marimba Chair unatozwa kodi ya bidhaa yaani marimba chair, iweje dhahabu haitozwi kodi?
Kodi ya ushuru wa Barabara? Hii ni lazima walipe
Kodi uchafuzi wa Mazingira????
Siku wakiondoka mashimo yao atafukia nani?
Je kama ni open mining wapo tayari kupanda mimea ya kuzuia mmonyoko wa ardhi?

Huu ndo mkataba Mswano kuliko ile ya mwanzo?
Haya maneno kama ni ya kweli kuna haja ya kuipata mikataba yote na kuiweka hadharani watu wote tuisome.
Inaelekea watendaji wa serikali yetu pengine wanashindwa
tofautisha Maslahi ya taifa na Maslahi yao Binfsi.

Kwa sababu wamefanya kazi serikali muda mrefu hawajui serikali inaanzia wapi na kuishia wapi vile vile hawajitofautishi wao na serikali.

Tamko la serikali linadhihirisha kitu kimoja kwamba ili mradi Rushwa imetolewa na kupokelewa na Watanzania kadhaa, taifa limenufaika kwani watumishi wa serikali na serikali ni kitu kimoja!!!!!

Kuwabughudhi watumishi wa vyeo vya juu wa serikali waliopokea rushwa ni Kuhatarisha Usalama wa Taifa kwani wakiamua Kutumia Polisi, USalama wa Taifa, FFU, na JWTZ kuwanyamazisha watoa tuhuma kuna hatari ya;

Watu kuwekwa Selo kwa muda mrefu na Polisi bila kufunguliwa mashtaka.

Kupigwa virungu na FFU na kuumuzwa vibaya kunakoweza sababisha ulemavu wa maisha au hata kifo.

Kufunguliwa Kesi za uongo mahakamani na mahakimu na majaji kusimama upande wa serikali na hivyo haki kushindwa kutetendeka .

Kufuatwa na maofisa wa Usalama wa Taifa kila siku na kuulizwa maswali ya Kunya( Kama anavyoulizwa yule kijana aliyemlamba Swali zito MH sana Edward lowassa.)

Vile vile Usalama wa nchi na Amani unaweza hatarishwa na hasira kuu ya mmoja wa watuhumiwa,Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuamua kuwaweka ndani Dr Slaa na Zitto kwa kutumia mamlaka anayopewa na katiba.

Kwa misingi yao Serikali ya SISIEMU Hoja nzima ya Buswazi ni kuhatarisha AMANI NA UTULIVU Kama si Usalama wa nchi.


Tunaijua serikali ya SISIEMU ni hodari wa kuandika na kujieleza iweje Suala la Buzwagi linakuwa gumu kulijibu hoja kwa hoja?

Wana JF na wananchi kwa ujumla, subirini kidogoo SIRIKALI wataleta tamko jingine la serikali.
 
Haya ndio majibu ya serikali , yanatia aibu sana ,



COMMENT YA DR. SLAA: Nadhani ili serikali nayo isiwapotoshe wananchi inatakiwa kutoa majibu ya kina na kuridhisha. Taarifa niliyoitoa kupitia “Maelezo ya Hoja yangu iliyokuwa iwasilishwe Bungeni yalikuwa na maswali ya msingi ambayo hayawezi kujibika tu kwa kutamka kuwa ‘ni ya uzushi’. Kila mtu anaweza kutamka hivyo. Serikali inatakiwa kujibu maswali ya msingi yaliyokuwepo kwenye maelezo niliyotaja mathalan:
a) Mkataba wa ujenzi wa Twin Towers utolewe hadharani ili wananchi wajue kuwa tuhuma ni uzushi au la.
b) Tenderers walikuwa nani, Tender ilitolewa lini na mchakato wake ulikuwaje,
c) Mshindi wa Tender ni nani na wakurugenzi wa Kampuni hiyo na sifa zao.
d) Gharama ilivyokuwa kwenye Mkataba na variations zote, na jinsi zilivyoidhinishwa( miniti za vikao vilivyoidhinisha)
Vinginevyo: Majibu ya Serikali hayakidhi haja, na hayajawasaida watanzania ambao ndio wenye mali na ndio wanaotaka kujua ukweli. Ukweli haupatikani kwa Tamko uchi bila vielelezo vyovyote.Dr.Slaa


COMMENT YA DR.SLAA: a) Uchunguzi unaofanywa na anayeitwa ‘International Auditing Firm” ni tone la Mchanga katika Bahari. Ukaguzi huo hauhusishi maeneo niliyoyaeleza ambako fedha za Walipa kodi zimetumika katika Meremeta, Tanagold, Mwananchi Gold Company Ltd, na kadhalika. Inahusu tu eneo la EPA, Isipokuwa kama “Terms of Reference” zimeongezeka tofauti na zilizotolewa Bungeni. Iwapo hivyo ndivyo, Audit inayofanyika ni sehemu ndogo sana na Hoja yangu haiwezi kupata majibu kutokana na Ukaguzi huo.Dr.Slaa.

COMMENT ZA DR.SLAA: Maelezo ya Serikali inayoonyesha aliyeyatoa hajui msingi wa hoja au hajafanya utafiti wa kina:-
a) Taarifa ya ukaguzi ya BOT inayosemekana ilipelekwa kwa Kamati ya Fedha hazijafika Bungeni. Hadi leo hii, karibu ya mwaka mzima kinyume na Sheria ya BOT Taarifa hiyo haijawasilishwa Bungeni. Naomba Mhusika atazame sheria inayohusika. Huu ni uvunjaji wa Sheria usioweza kuvumilika kwa Taasisi kubwa kama BOT.
b) Inawezekana mhusika hajachunguza Maelezo ya Hoja yangu na Taarifa ya Ukaguzi ya CAG iliyowasilishwa kwa Kamati ya Fedha. Hoja zote nilizozieleza hazijajibiwa. Nadhani ni vema akachukua muda wake kufanya utafiti wa kina, asome maelezo ya hoja yangu ya msingi, na yapatiwe majibu. Lugha inawezekana imerekebishwa kidogo lakini hoja za msingi ziko pale pale. Watanzania tunataka kufahamu kilichojiri, na maelezo ya kina.
c) Mhusika anasema hoja za Dokta Slaa hazina ushahidi. Ni wazi, Ushahidi wa kamili ni sillaha yangu.Serikali ingelikubali Kuunda Kamati Teule, ushahidi wote ungelitolewa katika Kamati hiyo. Hivyo ushahidi wangu nitautoa siku itakapokuwa lazima kuutoa yaani Mahakamani. Iwapo Serikali inania ya kuuputa siyo kwa kutoa Matamko uchi bali kwa taratibu za kawaida za kisheria.


COMMENT YA DR. SLAA: Inawezekana Mhusika anafanya kazi na Documents zisizo sahihi. Nadhani ni vema asome hoja yangu ilieleza nini kuhusu thamani ya Tshs 522,459,255,000. Hoja hiyo inahitaji majibu, na yatapatikana kimsingi wakati Serikali itakapoweka hadharani mkataba wa ujenzi, na Hati mbalimbali zilizopitisha Variations husika.Dr.Slaa.

COMMENT YA DR.SLAA:
a) Nashukuru kwa serikali kuthibitisha tena kuwa TANGOLD ni kampuni ya Serikali na inamilikiwa na Serikali asilimia mia 100%. Iwapo hii ni kweli:-
b) Serikali haijaeleza kwanini Kampuni hii ya Serikali ya Tanzania ilisajiliwa Mauritius na kupata tu Tanzania Certificate of Compliance? Ilifanya Biashara gani kule Mauritius wakati Sheria ya Mauritius na hati ya usajili ilifakataza isifanye Biashara Marititus?
c) Serikali iwatangaze wahusika wote, ili jamii ya Watanzania iweze kupekua vitabu vya Sheria kama kuna “conflict of interest” popote?
d) Serikali inaitaja tu na kueleza ni ya Hoja yangu inataka kujua “Tanzania tumenufaika nini na Kampuni hiyo” na kwanini taarifa ya Tangold haiko kwenye Taarif ya Ukaguzi, angalau kutaja tu kuwa Benki kuu inahisa katika Kampuni hiyo? Haya Maswali yasipopata majibu ya kuridhisha Serikali bado itakuwa imetoa majibu ya kubabaisha.

COMMENT YA DR. SLAA:
a)Serikali haijaeleza Kesi iliyofunguliwa mahakamani inahusu nini yaani ‘Grounds za kesi” . Ni vema Mhusika akasoma hoja yangu akaomba na file ya mahakamani ili aweze kuona grounds zilizoko mahakamani na uhusiano ukoje.
b) Hoja yangu iko wazi, kuna taarifa kuwa “Waziri anatuhumiwa kuwa anamiliki asilimia 12.5 ya Hisa ya Kampuni ya Alex Stewart. Serikali ingelituambia kuwa ilifanya utatifi ningelielewa.
d) Serikali itoe hadharani mkataba kati ya Benki Kuu (kwa niaba ya serikali) ili kubaini kuna hujuma/ufisadi au la. Kujitetea peke yake hakutoshi. Kinachotakiwa ni majibu ya Serikali siyo “TAMKO”, hii mtu yeyote anaweza kuitoa na akajifichamo.

COMMENT YA DR.SLAA:
a) Tunasubiri Ufafanuzi wa kina wa serikali kuhusu tuhuma hizi baada ya Mkataba kupatikana hadharana. Watanzania wanaendelea kuuchambua kwa nafsi zao. Hivyo tunasubiri kwa hamu kubwa ufafanuzi wa Serikali.Dr.Slaa.


COMMENT YA DR.SLAA:
a) Tuhuma tulizotoa katika eneo hili ni mahususi. Tulitaja majina na sababu ya kuwataja. Serikali imejibu utumbo na kuwapotosha watanzania. Kipindi cha majibu ya mafumbo kimesha, nadhani Serikali hii bado haijagundua hili. Tunahitaji majibu moja moja kwa kila tuhuma kama tulivyoyatoa. Vinginevyo Watanzania tunahaki bado ya kusema kuwa ufisadi mkubwa umejaa katika eneo hilo.
b) Tumeeleza kwa mfano ni kweli kuwa Plot no 15 Luthuli Street ilitumika kama Ofisi ya Biashara badala ya kuwa Ofisi ya Ikulu, inayolipiwa Kodi na watanzania wote?
c) Kama ni kweli Ofisi yetu ya Plot na 15 Luthuli Street kwa kipindi hicho chote Serikali imekusanya kodi ya pango kiasi gani?
d) Na masuali yote yaliyohusiana na tuhuma hizo zinahitaji kujibiwa kikamilifu. Serikali haijajibu, na imepoteza fedha za watanzania bure kuchapa Barua, kuzitawanya na kadhalika jambo ambalo linaongezea matumizi mabaya ya fedha za umma.


COMMENT YA DR.SLAA:
a) Nashukuru kuwa Serikali imetumia Ilani ya Uchaguzi wa CCM kuwa kigezo chake. Nadhani hoja hii haihitaji kuelezwa kwa Watanzania kwani sote tumeshuhudia kwenye vyombo vya Habari Matendo ya rushwa yalivyojaa ndani ya CCM yenyewe. Cha ajabu nini kama wanafanyiana hiyana wenyewe? Majibu yatapatikana tutakapotakiwa kutoa ushahidi mahali panapostahili kisheria.
b) Kujenga chuki. Ni nani kati yetu tunaotumia haki zetu za kikatiba kujua rasilimali na mali zetu au yeye anayezificha. Serikali ni lini ikawa mmiliki wa rasilimali za Taifa? Immesahau kuwa wana ‘hold in Trust” kwa niaba ya Wananchi, na hivyo, inapotakiwa ni lazima waje na majibu. Nadhani Watanzanania watatambua sasa nani anajenga chuki, nani anatafuta umaarufu wa kisiasa kati ya CCM na vyama vya Upinzani. Serikali ifahamu kuwa umaarufu hautafutwi. Utakuja tu mtu akitimiza wajibu wake. Kambi ya Upinzani tunatekeleza tu wajibu wetu, wananchi wakituamini watatuona maarufu. Hatuhitaji Serikali kututangazia hilo. Hata hivyo, tunashukuru kwa serikali kuendelea kutujengea umaarufu, kwani “Matendo ya Serikali ndiyo yametufikisha hapa tulipofika”.

Comment ya dr. Slaa:
a) Sitegemei kuwasilisha Taarifa yeyote kwa vyombo vinavyohusika. Vyombo hivyo vinawataalam, wanalipwa kwa kazi hiyo, walitakiwa kuwa wamefanya upelelezi huo muda mrefu si leo. Taarifa nyingine zimesambaa zaidi ya mwaka sasa. Hakuna hatua iliyochukuliwa wala na Serikali wala na vyombo hivyo.
b) Ilishatangazwa hadharani kuwa Taarifa na vielelezo vya Dr.Slaa vimefikishwa kwa Polisi na ikasemekana kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Nadhani hiyo inatosha. Serikali ziko ngapi haiwasiliani na vyombo vyake/
c) Iwapo hoja ilifanyiwa mizengwe izuiwe isiingie Bungeni kwa vile ikiingia Bungeni ina athari mbaya kwa Serikali, na kwamba inachunguzwa ‘Leakage hiyo ilifikaje kwa wapinzani” kama Serikali inatumia fedha za Walipa kodi kuchunguza “leakage” badala ya kuchunguza ubadhirifu kuna sababu gani ya kupeleka taarifa kwa vyombo hivyo?


COMMENT YA DR. SLAA:
a) Hoja hii ni ya watu walioshiwa na wamebaki na fikra mgando. Nani kati yetu kipindi chote hiki amezungumzia masuala ya uchaguzi. Ni kazi yetu ya kikatiba kuelezea watanzania pale ambapo Serikali imefanya makosa. Si kazi ya Upinzani kuipigia makofi Serikali. Kazi ya Kambi ya Upinzani duniani kote inajulikana. Na Ndiyo maana tuko kikatiba.
b) Serikali ijieleze kwa wananchi ieleweke isitafute mchawi. Leo wananchi wanalalamika kila kona ya nchi maisha Bora hayajaonekana inatuhusuje sisi? Chuki haitokani na Vyama vya Upinzani kutaka kujua rasilimali zao bali wananchi kuonja joto la jiwe baada ya ahadi isiyotekelezeka ya CCM mwaka 2005, na maneno matamu yanayoendeleo kutolewa na Serikali. Kama ni shule wananchi ndiyo wanaojua adha ya michango. Kama ni zahanati vivyo hivyo. Maisha bora yako wapo? Ajira ziko wapi? Mbona Bungeni waziri husika alipata kigugumizi kujibu ajira ngapi hadi leo zimepatikana miaka karibu miwili tangu uchaguzi. CCM ichunguze sababu ya chuki ya Wananchi isitafute mchawi mbali na korridor zake. Dr.Slaa

 
Ukisoma kwa makini utajua ni jinsi gani slaa amewabana kwani wamemtaja zaidi ya mara mia....,

Haya kazi kwenu kwenye kujibu nimeliweka tamko lote ili muweze kuijibu serikali kipengele kwa kipengele
 
Kaazi kweli kweli,kama utafiti uliofanyika wa kina ndo umeleta hayo majibu,wadanganyika tuna kazi!Kule mkoani Kagera mkimkamata mtu anaiba ndizi,mkamtwisha mkungu wake huo wa ndizi aliouiba mumpeleke polisi,watu hata polisi wakimuuliza njiani nini kimetokea hasemi nimekamatwa naiba ndizi bali husema,"ETI NIMEIBA NDIZI''

Hata tuwakabe vipi hawatasema kama ni mafisadi,wataendelea tu kusema,''ETI SISI NI MAFISADI''

Tuna sehemu moja tu ya kusemea kama ni mafisadi,''UCHAGUZI 2010''
 
Nilijua tu kuna siku ita-backfire!
Katika tamko lake hilo, serikali, inaziita tuhuma zote za Slaa, kuhusu Benki Kuu (BoT), Kampuni ya Tangold na nyinginezo kuwa ni za kizushi na ambazo zimetolewa pasipo kufanyika kwa utafiti wa kutosha.
Nazikumbuka sana kauli hizi za serikali... Kila anachoongea raia YEYOTE ambaye hayumo kwenye 'list yao' basi huitwa 'Mzushi'!

Na wao wenye 'nia njema' wakamshikilia Liyumba na mpaka sasa anahenya Keko!

Kuna upuuzi mwingine watanzania hamtakiwi kunyweshwa mkanywa kama unavyokuja...

Hebu pata nakala ya mkataba wa Buzwagi hapa JF na uone ambacho serikali yetu 'tukufu' ambayo 'haijaishiwa' tena 'yenye nia njema' inachokitetea:

 
duh! hii ndiyo Serikali ya Mhe. Kikwete! nchi hii bwana, tunashinda sana, integrity ya Serikali zero.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…