Majina haya yanatoweka kwa kasi katika Jamii

Hata wazee wameacha majina ya asili, siku hizi kuna wakina Mzee Sadam Husein, Mzee Bush, Mzee Osama na kuna mwingine kwetu kwa Azizi Ali anaitwa Mzee Van Damme mi ndio nimechoka kabisa
 
1.Sengiyumva Bugaigai
2.Balengagabo Bale
3.Lindalisebe Mpemba
4.Ngayalina (Nameless) Mayala
5.Mwakifulefule Atufigwege
6.Mbamba Uswege
7.Taji Liundi

Inakera sana siku hizi unakuta mtu ana majina ya kigeni tupu bila la asili,kama:

1.James Alain Philipo John
2.Suleiman Rashid Juma (Tena Zanzibar ndo wamezidi).

Yaani mtu hata huwezi jua huyu mtu ni kabila gani au ukoo gani. Hovyo sana!
 
Kuna huyu mzee Anato mwanae akampa jina la Mbwaga.


Shida ilikuja pale alipompeleka mwanae shule aisee muunganiko wake walimu wakamwambia mzee wa watu hana akili.


Sijui walipata jina gani walipounganisha.
Chai....
Mwalimu anamuuliza Mwanafunzi: "unaitwa nani"
Mwanafunzi: "naitwa Nato"
Mwalimu akauliza Tena: "baba yako anaitwa nani?"
Mwanafunzi: "baba anaitwa Mbwaga"
Mwalimu alipounganisha jina la Mwanafunzi na la baba yake, alibaki ameduwaaa na kushindwa jinsi ya kulitamka mbele ya hadhara.
 
Nilisoma na mtu anaitwa Nsengiyumva Magogwa
 
Haya majina yote ya Kizaramo! kati ya hayo namba 2,4,6,12 yapo kwa dada zangu na binamu zangu!

Sijui hizi Wazaramo kuna Nasma (Naa),Asrat, Narjat, Nusrat, Balqis,Nargis Asma,..na mengine kama kina Happy,Janet yamekuwa mengi kutokana na migration kubwa ya watu toka vijijini ingawa pia ni ya zamani.
 
Mohammed kwa kuwa mashoga wengi uitwa jina hilo as Aunty Muddy
 


Mkuu hio sio chai.


Hilo ni moja ya majina yalotolewa ktk ukoo wa mzee Bwaga.
 
Naona mengi ni ya wazaramo tu
 
Mateso,mawazo,majaliwa,Sabuni,mbeleko,gunzi,asumwisye,mwandendeko,ngufwa,nchemba,shilingi,sumuni,semeni,kijiko,atupele.chujio,ndiko,mange etc.
 
Uzaramuni huku kuna
Chuki
Havijawa
Havintishi
Mnayenu
Mtakae
Semeni
Shida
Mama mmoja enzi hizo tandika, wanae wanaitwa Semeni, chuki, shida, mnayenu
akianza kuwaita ni burudani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…