Majina ya watoto (Vikembe) wa wanyama/viumbe

Ndugu yangu ndege anakuwa kifaranga mara tu baada ya kuanguliwa kutoka yai, baada ya muda anaitwa kinda yaani si kifaranga tena na pia hajapea.kama unavyoona binadamu watoto, kichanga, mwana, kigori/mwari/baleghe/barobaro then binti/kijana.
 
Ndugu yangu ndege anakuwa kifaranga mara tu baada ya kuanguliwa kutoka yai ,baada ya muda anaitwa kinda yaani si kifaranga tena na pia hajapea.kama unavyoona binadamu watoto,kichanga ,mwana,kigori/mwari/baleghe/barobaro then binti/kijana

Kichanga kiswahili kipya hicho,barobaro ndio kwanza nisikie leo,nafikiri umeenda nje ya hoja,hayo uliyoyaeleza hapa ni mfumo wa ukuuaji wa mtoto wa binadamu na majina yake

lakini,kiswahili ni lugha kubwa inategemea hicho kiswahili ni cha sehemu gani,maelezo yako siwezi kuyapinga

mfano neno panda na manati,kibatari na koroboi, hayo maneno maana yake moja lakini yanatamkwa tafauti inategemea anaezungumza anatoka sehemu gani
 
Hehehehe samaki mbilikimo:yo:, uko sawa madameX dagaa hakuwi umbo lake ndio hilo hilo,baba wa dagaa umbo lake liko hivyo mama wa dagaa umbo lake liko hivyo

Hahaaa ndio hivyo mkuu. Watu wanadhani dagaa ni samaki mtoto sa kueleweshana tuseme tu "Samaki mbilikimo". Kiswahili kigumu aiseeee
 
Ng'ombe......Ndama
Nzige...kimatu/maige/tunutu/matumatu/funutu
Ndege....Kinda
Kipepeo/nondo....kiwavi
Nzi......Buu
Farasi....Kitekli
Mamba...... Kigwena
Nyangumi..... Kinyangunya
Fisi.... Kikuto/bakaya
Ngamia..... Nirigi/nirihi
Paka.......kinyaunyau/kipusi
Ndovu.... Kidanga
Mbweha.... Nyamawa
Nyani...... Kigunge
Kondoo..... Kibebe/katama
Mbuzi.....Kibui/kibuli/kimeme
Farasi na punda.... Nyumbu
Punda.... Kiongwe/kihongwe
Mbu....kiluwiluwi
Chura.... kiluwiluwi
Kuku..... Kifaranga
Papa.... Kinengwe
Nyuki.... Jana
Simba..... Shibli
Sungura.....Kitungule
Kwanga/wibari.... " "
Samaki.... Chengo/kichengo
Chui.... Chongole/kisui
Mbwa..... Kilebu/kidue/kibwa
Nyoka...... Kinyemere
Njiwa..... Kipura
Wazazi wenye rangi tofauti.... Chotara/suriama
 
List yako ni batili kwa kuwa mnyama pendwa amesahaulika kwenye list...unamsahauje mdudu kwamfano..
 

Elimu nzuri, Hayo majina ni lugha ya kiswahili au kilugha?
 
Mmmmh! Mkuu hapo kwenye vichanga vya farasi na punda..iweje Nyumbu..Nyumbu si Wildebeest!
 
Chura.....Ndubwi
 
1. Ng'ombe.... Ndama

2.Mbuzi.... kibui/ kibuli/ kimeme

3.Kondoo... kibebe/ katama

4. Ngamia... Nirigi/ nirihi

5. Kuku... Kifaranga

6. Sungura... Kitungule/ kwanga/ wibari

7. Ndege... Kinda

8.Njiwa... kipura

9. Simba.... Shibli

10. Chui... Chongole/ kichengo

11. Fisi... Kikuto/ bakaya

12.ndovu... kidunga

13. Papa..... Kinengwe

14. Nyangumi.... Kinyangunya

15. Punda.... Kiongwe/ kihongwe

16. Farasi.... Kitekli

17.Nzi... buu

18. Nzige... Kimatu/ maige/ tumatu/ matumatu

19.Nyuki... jana

20. Mbweha... Nyamawa

21.Nyani...kigunge

22. Mamba... Kigwema

23. Chura... Kiluwiluwi

24. Mbu.... Kiluwiluwi

25.Paka... kinyaunyau/ kipusi

26. Kipepeo.... Nondo/ kiwavi

27.Mbwa... kilebu/ kidue/ kibwa

28.Samaki... chengo/ kichengo

29.Nyoka...kinyemere
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…