Majirani wamemripoti jamaa kituo cha polisi kisa kazi yake haijulikani! Sasa anadai Milioni 500 kwa kuletewa usumbufu

Kuishi uswahili ni kazi kama kazi nyingine.yan kabisa jamaa wameungana na kwenda kureport kisa hawa muelewi mshkaji.?

Hao jamaa wanatakiwa kuhangaishwa hivyo hivyo mahakamani mpaka akili ziwakae sawa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Amna kesi hapo ata angeenda na tundu lissu kwanza mnajua maana ya kuzalilisha? Na iyo fidia yeye ndo anajipangia?
Hujui kama mtu ukimdhalilisha anajipangia yeye mwenyewe fidia sababu yeye ndio umemdhaliisha ba hiyo ndio hasara aliyoingia kutokana na kumdhalilisha
 
Madhara ya kukaa mitaa ya masikini wa kunuka na kutupwa ndiyo haya sasa.unapeleka taarifa Kwa watekaji au na yeye anataka atekwe kama sativa?Mtu umpeleke polisi pasipo kuwa na uhakika kama ni mharifu huo ni ujinga na uzwazwa na inaonekana huo mtaa ni masikini na wa mbeya
 
Huyo anataka pesa zake na mawakili nao wale pesa zake pamoja na mahakimu,polisi ndio mahali pakupeleka tuhuma na kazi ya polisi ni kuchunguza tuhuma zilizopelekwa kwao,wakibaini kuwa tuhuma unazotuhumiwa nazo siyo za kweli huo unakuwa ndio mwisho wa tuhuma zako na huwezi ukamshitaki aliyekutuhumu.
 
Majirani wako sahihi, tunaambiwa Kila mara Kama Kuna mtu unamtilia shaka karipoti kwa mamlaka. Wengine wanakuwaga majambazi.
Halafu watu wa kubet achen kuleta stori za kujifariji 😂😂 betting sio ajira kafanyeni kazi
 
Majirani wako sahihi, tunaambiwa Kila mara Kama Kuna mtu unamtilia shaka karipoti kwa mamlaka. Wengine wanakuwaga majambazi.
Halafu watu wa kubet achen kuleta stori za kujifariji 😂😂 betting sio ajira kafanyeni kazi
Lakini wanahitajika mahakamani wakajitetee usahihi wao sababu mahakamani pia ni sehemu sahihi ya haki
 
Hapo Sasa anajua yeye kwanini kafanya hivyo
 
Majirani hawana kosa, aseme anafanya kazi gani na ithibitike.
Niliwahi kuwa na mpangaji, anashinda ndani. Akirudi toka nje anaingia ndani chap na kufunga geti. Yupo karibu na geti, akiwa anatoka ni kama mke wa mtu anachomoka gest.
Nikamwambia dada toka umehamia hapa sikuelewi. Tafuta nyumba nyingine
 
Hatoboi hiyo case
Hakuna element za malicious prosecution
 
Mi nazani wewe wangekuzushia la kukwepa kodi na kuhujumu uchumu au kutakatisha pesa, yaani wewe ndio ungeenda kutoa hela ndeeeeefu ili kutoka lupango.
Mkuu,

Labda kwa huko.

Huku nilipo kila mwaka nina file kodi. Yani nalipa kodi zaidi ya ninavyotakiwa halafu mwisho wa mwaka TRA yao (IRS) wananirudishia hela nyingine kwa sababu nimewazidishia kodi ninazotakiwa kulipa.

Na rekodi zote zipo.

Kwa hiyo labda huko, kwa huku ni vigumu kuzusha mambo hayo kwa sababu kila kitu kinafanywa kwa kitabu na rekodi zote zipo.

Yani hata nikipoteza makaratasi yangu na electronic recirds ni kitendo cha siku tatu tu napiga simu natumiwa kutoka taasisi ya kodi ya Marekani, hata nikiwa Tanzania.
 
Lazima wamlipe fidia. Hiyo ni False imprisonment.
 
Hawezi kushinda hiyo kesi, ni jukumu la mwananchi kutoa taarifa polisi kwa mtu asiyemuelewa, raia hawajamfungulia mashitaka bali wametoa taarifa polisi, wafanye kazi yao.

kwahiyo sasa tunatakiwa turipoti source zetu za vipata kwa majirani?
 
Mbona nimeshaelezea kazi yake ni kubeti na kaonyesha mikeka anayokula mamilioni akiwa polisi kazi inabaki Kwa majirani kuthibitisha hizo kazi haramu mahakamani walizomuhisi
 
Washaambiwa kuna Wanaijeria wanaishi kwa kufanya biashara ya kuteka watu na kuwatoa figo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…