Makadirio ya gharama na mapato ya ekari moja ya mkonge

Makadirio ya gharama na mapato ya ekari moja ya mkonge

Kima, Nyani wote wanaharibu mkonge kwa kuvunja kile kiini cha mkonge na kukifyonza. Hawa mara nyingi wanaonea mkonge uliochini ya miaka 2.
Tembo wanafanya hivyo kwa mkonge uliovuka mwaka na kuendelea
Kati ya Korogwe na Muheza ni wilaya gani haina usumbufu mkubwa kwenye kilimo cha mkonge?
 
Si lazima ulimie mkonge mkoa wa Tanga. Labda kama unaishi huko. Ila mkonge unakubali mikoa mingi sana Tanzania. Pwani, Morogoro, Singida, Kilimanjaro na mikoa mingi ya kanda ya ziwa. Angalia wewe upo karibu na wapi, udongo kama unafaa. Then ingia shambani.

Kama unafikiria kulima eka 1 ya mkonge ili ikunyanyue kiuchumi acha. Hiyo hela na muda wako kafanyie mambo mengine. Kwa ambae yupo Morogoro mjini aende pale shamba la CENTRAL maeneo ya Mkambarani, au nenda Mlingano Tanga. Ukaone huduma inayohitaji mkonge na ulinganishe kama kulima ekari moja is worth the hustle.

Kulima eka 1 ya mkonge itakupa hela ya uhakika ya kula tu. Kuna gharama nyingi sana zipo ndani ya kuzalisha mkonge mpaka upate nyuzi zile ili uuze.

Kulipa wakataji
Usafiri wa kutoa mzigo shambani
Gharama za mwenye mashine
Gharama za wafanyakazi
Chakula na maji
Ushuru
Mafuta(diesel)
Gharama za usafiri kumpelekea mnunuzi kama ana stoo mbali na site ya kuzalisha.

Jinsi gharama za maisha zinavyozidi kupanda na ndio gharama za uzalishaji zinapanda pia.

Wanunuzi wa mkonge wengi ni wakandamizaji sana. Hasa hawa wanunuzi wanaonunua kwa wazalishaji wanaotumia mashine za spadle. Pale Morogoro mjini wananua sh 1800 kwa kilo hiyo ni bei ya leo tarehe 03/07/2023. Utalipia usafiri hadi stoo kwa mnunuzi, mzigo ukifika ataukagua. Hata uwe msafi vipi, huwa wengi wao hawakosi sababu ili ashushe bei zaidi.

Lima angalau ekari 20 na kuendelea. Ili uvune mzigo mkubwa na uzalishe kilo nyingi, endapo ikitokea changamoto, wingi wa kilo zako ulizozalisha bado utakutunza usipate hasara. Kilimo cha mkonge ni uwekezaji mkubwa sana ukifanya kwa ukubwa wake.

Ingia kwa pupa kwenye mkonge utapigwa za uso kama vanilla au matikiti afu uanze kulaumu watu. Nipo kwenye mkonge tangu 2014, nimeshapigwa humo, nimeshalaani, kutukana na kufurahi pia.
NB: Fanya utafiti wa kutosha kabla ya kuingia shambani. Ukitaka shamba ninalo pori Maramba nauza laki 3 na nusu kwa eka 1
 
Kati ya Korogwe na Muheza ni wilaya gani haina usumbufu mkubwa kwenye kilimo cha mkonge?
Korogwe ni kuzuri zaidi. Japo factor nyongine km upatikanaji wa Ardhi, umbali kufika maeneo ya uchakataji na wanunuzi. Japo kwanza lazima uchague sehemu itakayokuwezesha kusimamia shamba lako. Mkonge mwanzoni unahitaji kutunzwa vizuri. Hivyo usipoweza kusomamia shamba litaathirika.

Kuna maeneo km Handeni, Pangani, Kilindi na Mkinga bado ardhi ni bei nafuu kiasi. Hivyo km unalenga kumiliki heka kuanzia 50 maeneo hayo.
 
Si lazima ulimie mkonge mkoa wa Tanga. Labda kama unaishi huko. Ila mkonge unakubali mikoa mingi sana Tanzania. Pwani, Morogoro, Singida, Kilimanjaro na mikoa mingi ya kanda ya ziwa. Angalia wewe upo karibu na wapi, udongo kama unafaa. Then ingia shambani.

Kama unafikiria kulima eka 1 ya mkonge ili ikunyanyue kiuchumi acha. Hiyo hela na muda wako kafanyie mambo mengine. Kwa ambae yupo Morogoro mjini aende pale shamba la CENTRAL maeneo ya Mkambarani, au nenda Mlingano Tanga. Ukaone huduma inayohitaji mkonge na ulinganishe kama kulima ekari moja is worth the hustle.

Kulima eka 1 ya mkonge itakupa hela ya uhakika ya kula tu. Kuna gharama nyingi sana zipo ndani ya kuzalisha mkonge mpaka upate nyuzi zile ili uuze.

Kulipa wakataji
Usafiri wa kutoa mzigo shambani
Gharama za mwenye mashine
Gharama za wafanyakazi
Chakula na maji
Ushuru
Mafuta(diesel)
Gharama za usafiri kumpelekea mnunuzi kama ana stoo mbali na site ya kuzalisha.

Jinsi gharama za maisha zinavyozidi kupanda na ndio gharama za uzalishaji zinapanda pia.

Wanunuzi wa mkonge wengi ni wakandamizaji sana. Hasa hawa wanunuzi wanaonunua kwa wazalishaji wanaotumia mashine za spadle. Pale Morogoro mjini wananua sh 1800 kwa kilo hiyo ni bei ya leo tarehe 03/07/2023. Utalipia usafiri hadi stoo kwa mnunuzi, mzigo ukifika ataukagua. Hata uwe msafi vipi, huwa wengi wao hawakosi sababu ili ashushe bei zaidi.

Lima angalau ekari 20 na kuendelea. Ili uvune mzigo mkubwa na uzalishe kilo nyingi, endapo ikitokea changamoto, wingi wa kilo zako ulizozalisha bado utakutunza usipate hasara. Kilimo cha mkonge ni uwekezaji mkubwa sana ukifanya kwa ukubwa wake.

Ingia kwa pupa kwenye mkonge utapigwa za uso kama vanilla au matikiti afu uanze kulaumu watu. Nipo kwenye mkonge tangu 2014, nimeshapigwa humo, nimeshalaani, kutukana na kufurahi pia.
NB: Fanya utafiti wa kutosha kabla ya kuingia shambani. Ukitaka shamba ninalo pori Maramba nauza laki 3 na nusu kwa eka 1
Asante kwa guidance,
Nakubaliana na wewe, mkonge wengi tunaangalia mapato ghafi bila kujua kuwa kuna gharama mpk kufikia hilo pato.
Kwa maeneo mengi Tanga kuzalisha tani 1 inaweza kugharimu 1.2-1.8M kutegemea ukubwa wa mkonge (meta ngap zinazalisha tani), usafiri mpk kwenye korona, gharama za korona, na kupiga kayamba. Kwa wastani kg 1 ni 3500.

Pia kuhusu ukubwa wa shamba ni sahihi kabisa, shamba dogo linakuwa na administration cost kubwa unless uwe ulima mwenyewe. Kuanzia heka 10, upande mbegu bora na ukautunza vizuri, binafsi naona ni hatua nzuri kuanza. Nashauri km ni mgeni na hauna kipato cha uhakika usikimbilie kuanza na heka 50.
Kuhusu maeneo mengine, kwa mwekezaji anayemudu kuzalisha na kuprocess na kuexport/kuzalisha mazao ya mkonge ni sahihi kutafuta eneo maeneo mapya. Ila kwa mkulima mdogo ni vizuri kulima maeneo yenye wakulima wengine. Kuna maeneo yenye AMCOS imara wanamiliki korona zao na wana access ya mikopo kupanua na kundeleza mashamba. Pia ukiwa mfano Singida itakusumbua kupata soko la uhakika. Access ya baadhi ya huduma km vituo vya utafiti, board ya mkonge, viuatilifu, itakuwa changamoto ukilinganisha na maeneo yenye wakulima wengine.

Asante
 
Asanteni kwa guidance, sasa nimepata picha halisi. Kwa haraka haraka nimegundua mkonge ni "dhahabu" nyeupe, pesa ipo. Nitaanza na ekari 50 kwanza, then nitaendelea kuongeza mdogo mdogo baada ya mavuno ya kwanza (3 to 4 years later)
 
Back
Top Bottom