Makala: Mfahamu Simba Karatasi wa Umakondeni

Makala: Mfahamu Simba Karatasi wa Umakondeni

Kuna simlizi nilizisikia, zikidai huenda hiyo nadharia ina ukweli kiasi ndani yake.

Wanasema, inasadikika kuna baadhi ya maeneo miaka ya huko nyuma, ulikuwa unaenda kununua nyama ukijua ni nyama ya Ng'ombe au Mbuzi ila siyo.

Wale wanaoona yasiyoonwa na wengi walikuwa wanathibitisha kuwa baadhi ya siku inakuwa nyama ya binadamu inayouzwa na si nyama ya mnyama husika uliyemtarajia.

Wanaenda mbali zaidi kwa kusema ukiona nyama umeichemsha ikawa na( .... )tambua hiyo siyo nyama ya ng'ombe au mbuzi bali ya mtu.

Ila yote kwa yote inabaki ni nidharia tu ambazo sidhani ilikuwa ni za kweli bali huenda ni mwendelezo wa simlizi za simba wa karatasi.

Ninasema hivyo maana sikuwahi ona au thibitisha hilo pamoja na umri wangu.
Mkuu tuondolee hayo mabano tafadhali!

Ikawa na nini?
Povu?
Chumvi?
Maji?
...?
 
Mkuu tuondolee hayo mabano tafadhali!

Ikawa na nini?
Povu?
Chumvi?
Maji?
...?
Acha niishie hapo, kumbuka tunaangazia biashara za watu, hivyo isijetokea mtu akakutana na hicho ambacho nimeacha kukiandika ikaleta taswira hasi.

Kuna mengine si busara kuongea kwenye hadhara, ikibidi sana labda PM.
 
Acha niishie hapo, kumbuka tunaangazia biashara za watu, hivyo isijetokea mtu akakutana na hicho ambacho nimeacha kukiandika ikaleta taswira hasi.

Kuna mengine si busara kuongea kwenye hadhara, ikibidi sana labda PM.
Kweli mkuu Mimi ninatamani kufahamu.

Nipm ikibidi🙏
 
  • Thanks
Reactions: K11
Acha niishie hapo, kumbuka tunaangazia biashara za watu, hivyo isijetokea mtu akakutana na hicho ambacho nimeacha kukiandika ikaleta taswira hasi.

Kuna mengine si busara kuongea kwenye hadhara, ikibidi sana labda PM.
Mkuu, lakini utasaidia wengi ukiandika hapa.

Wanasema, "akili za kuambiwa changanya na zako".

Waliomo humu wana akili zao, watachanganya na kupata jibu walihitajilo.
 
  • Thanks
Reactions: K11
Na

Niliendaga Lindi kutembea baada ya kumaliza shule, pale mjini Mpilipili kuna kichuguu huwa kinawakaga moto usiku, hakuna anayewasha.
Wakazi wa pale siku wanakibomoa wakakutana na damu iliyoganda.
Nahisi kilikuwa kinatumika kwa kafara.
Ila wazee wa pale wanasema pale kazikwa mtu asiyeineonekana....nilistaajabu sana, japo niliushuhudia moto, ila hakuna sarakasi ya 'sayansi' iliyotumika kweli pale🤔
Moto huu huu unaoangaza au Moto wa kiini macho tu? Unaposema alizikwa mtu asiyeonekana unamaanisha nini haswa?
 
Mtu anakuwaje simba na nyie acheni kutupanga
Baki na elimu hiyo hiyo ya mzungu😆😆
Kuna ukoo tuna undugu nao huko Mlimba Morogoro kwa upande wa mama, ma babu zao huwa hawafi bali hugeuka simba. Nilibisha na kukataa katakata mpaka nilipokuja kuthibitishiwa na babu nilipotembelea eneo husika na kanisimulia vizuri kilichofanyika mpaka hali ikawa hivyo.
Ila kwasasa hawabadiriki baada ya mambo flani flani kufanyika na kurekebisha hiyo hali.
 
Hiki kisa ni maarufu sana huko mikoa ya kusini
kama ni miaka ya themanini ni yule simba mla watu ambae alitengenezewa documentary kwenye national geographic nadhani title yake imefanana na 'man-eating lion of Rufiji'

nadhani ipo kwenye youtube
 
Baki na elimu hiyo hiyo ya mzungu😆😆
Kuna ukoo tuna undugu nao huko Mlimba Morogoro kwa upande wa mama, ma babu zao huwa hawafi bali hugeuka simba. Nilibisha na kukataa katakata mpaka nilipokuja kuthibitishiwa na babu nilipotembelea eneo husika na kanisimulia vizuri kilichofanyika mpaka hali ikawa hivyo.
Ila kwasasa hawabadiriki baada ya mambo flani flani kufanyika na kurekebisha hiyo hali.
Wewe uliwaona wakibadilika?? Au kisa babu yako kakusimulia basi ukaamini.
 
Hao waganga huko msumbiji bado wapo mkuu? Kuna likamjamaa limeniingilia kwa Valentina Linajifanya linajua kuimbisha mi nachuniwa tu sasa hivi.

Nifanyie mpango wa kontakti bloo nigeuke simba mie nifanye mambo yangu adabu irudi
Tafuta mwigine,achana naye
 
Wewe uliwaona wakibadilika?? Au kisa babu yako kakusimulia basi ukaamini.
Hahaha kwakweli nipo nusunusu katika kuamini maana tukio alilonihadithia bibi na mjomba angu nao walithibitisha katika kushiriki baadhi ya matukio la ubadirikaji kuwa simba. Yaani iko hivi huyo mzee alikuwa umri umeenda sana na alikuwa analala tu akimaliza haja zote huko huko katika kijumba walichomjengea kwa pembeni. Huu ndio utamaduni wao pale muda unapofika wa wazee wao kubadirika, huwajengea kibanda then wanamuweka humo ndani. Nje wanaandaa ngoma za kitamaduni na matambiko. So siku ikifika wakati wanaendelea kuomba na kucheza kwenye kile kibanda atatoka simba na kuunguruma na kuelekea porini tena kwa madaha na mkienda kwenye kile kibanda hamkuti mtu yoyote so imani yao inajengeka kuwa huyo mtu amegeuka simba
 
Back
Top Bottom