Niliacha kutumia nguvu 2015 palee biafra
Wenye nchi walikuja kukwala matokeo vimbele mbele sie tukajifanya wafata mkumbo et! Wazee wasiondoke na matokeo , ilikuwa mshike mshike hatari palee biafra
Zilipigwa njugu live na sio kupigwa juu unalengwa yaani live live bila chenga, wapo waliokamatwa palee wakaenda nyea debe, kuna jamaa alikanyangwa mguu na baada ya matibabu kushindikana jamaa alienda kukatwa mguu- kama kuna mtu ana kumbuka ataikumbuka hii
Mimi kuna asikari mmoja alinikimbiza yaani aliniungia mpaka kwenye kona ya chuo kikuu huria kutoka shule ya biafra , aliniacha kwenye ilee kona ya chuo kikuu huria yaani sikurudi tena wallah nilipofika magheton nikachota maji bombani nikaoga nikaenda kulala moja Kwa moja yaani
Matokeo ya misuko suko ya wengine nilisikia kesho yake
Na nna huhakika kuna watu wanalamba asali kwenye hizi inshu sisi vimbele mbele tutaenda jiuguza baada ya kujitia kimbele mbele- sitaki kabsa mambo ya kutumia nguvu na vyombo vya dola other ways kuna kitu napata.’
Jamaa aliyokatwa mguu yupo tu aangaliwi na yeyote yaani imemgharimu kizembe tu, maisha hayaa daaah nachukia siasa kinoma noma sitaki kusikia chama chochote kilee