Elections 2010 Makamba atinga jimboni Bumbuli leo na ufanya vikao vya siri.....

Elections 2010 Makamba atinga jimboni Bumbuli leo na ufanya vikao vya siri.....

Labda niulize swali moja la kizushi: Mnataka Sitta, Shelukindo, Mwakyembe, Kilango, ole Sendeka,..... wapite bila kupingwa?
 
Mablog mengine pia yametumiwa kuwajenga January na dada yake kuwa wabunge watarajiwa; hasa blog la mjomba misupu!!

I support you much hii Blog ya Mjomba masupu inatumika kumpamba January but hata wakipamba hakuna kitu
 
Labda niulize swali moja la kizushi: Mnataka Sitta, Shelukindo, Mwakyembe, Kilango, ole Sendeka,..... wapite bila kupingwa?

Hapa issue siyo wabunge wapambanaji wapite bila kupingwa, la hasha. Issue ni kuwa kuna mkakati maalumu wa kuhakikisha kuwa hawarudi tena Bungeni kwa kutumia kila aina ya foul play, kama vile hila na uhuni mwingine. Kitendo cha mafisadi kumwaga pesa nyingi kwenye majimbo haya na kupandikiza wagombea si jambo la kawaida. Pesa zina nguvu kubwa sana kwenye siasa ya Tanzania, hivyo wapambanaji hawa hawatendewi haki.
Ni kweli pia kama wadau wengine wa JF walivyosema, blog ya Michuzi inatumika sana kumpigia debe January Makamba.
 
Akina SITTA na wenzake wanaojiita wapambanaji wa UFISADI waelezee kwa nn mwenzao MH FREDDY MPENDAZOE ALIJITOA CCM KABLA HATA YA BUNGE KUMALIZA MUDA WAKE?????
 
Kwa hiyo alipofikia kwa mama January, Yusufu alikuwa na ujiko gani wakati huo m
paka January na mamake wakabadili jina la mtoto kuwa Makamba? Hana baba mzazi?[/QUM

Mkuu, Yusuf ndiye anaweza kukujibu vizuri, ila ukumbuke ni msanii mzuri tu
 
Labda niulize swali moja la kizushi: Mnataka Sitta, Shelukindo, Mwakyembe, Kilango, ole Sendeka,..... wapite bila kupingwa?

Wewe inaelekea hujaielewa hoja inayopaswa kujadiliwa kwenye thread ya FAREED. Suala kubwa hapa ni jinsi MAFISADI wanavyotumia pesa waliyotuibia kuweka watu wao Bungeni na kuwaengua mapambanaji wa kweli ambao wao wanawaona ni maadui. Kwa hiyo hapa hatuzungumzii suala la kupita bila kupingwa, bali njama za kuwaengua wapiganaji.
Kwa mtazamo wangu, iwapo mipango ya majasusi hawa itafanikiwa nchi itakuwa imefika pabaya sana. Tutakuwa na Bunge la mafisadi litakalotetea maslahi ya mafisadi na hivyo kulididimiza kabisa taifa letu. Lazima tufungue macho na tukemee kwa bidii ushenzi huu unaofanywa na akina Lowassa na mshirika wake Rostam. Tusaidie pia kuwafumbua macho Watanzania wengine wanaondelea kulala usingizi wa pono huku nchi yao ikifilisiwa.
Ni mategemeo yangu kuwa njama hizi za MAFISADI zitaanikwa kweupe wakati wa kampeni ili wananchi wasije wakadanganyika. Mimi binafsi nimefanya uamuzi rasmi wa kuzunguka nchi nzima kujaribu kuwaelimisha wananchi kuhusu madhara ya ufisadi. Kwa mwaka mzima nilikuwa niki-save pesa kutoka kwenye mshahara wangu na biashara zangu za hapa na pale kwa ajili ya ukombozi wa nchi hii. Wakati huo huo nimekuwa nikisali sala maalum kumuomba Mungu awaamshe Watanzania wenzangu ili waipiganie nchi yao. MUNGU IBARIKI TANZANIA!
 
Unajua ishu si kuwachalenge wabunge waliokuwepo..issue ni motive unayoenda nayo...kwa Januari ni obvious kwamba ameandaliwa na watu fulani kwa interest zao ili akachukue nafasi ile, hata kwenye harambee yake watu waliomchangia ni walewale...RA, YM....
 
Mablog mengine pia yametumiwa kuwajenga January na dada yake kuwa wabunge watarajiwa; hasa blog la mjomba misupu!!

BULESI ..this is true huyu jamaa mwenye hiyo blogo ya mifupa pia anafanya kazi undercover!
 
Wana JF tuwe makini hasa wale tunaotaka kupambana na ufisadi:
Rai ni la Rostam Aziz
Makamba Yusuf ndiye mtendaji mkuu wa CCM inayolinda mafisadi;
Sasa mnategemea anambeba mtoto wale ili iweje? Si ni kwenda kulinda ufisadi alioufanya baba yake?
Shelukindo sifahamu historia yake, lakini namna alivyoongoza kamati ya nishati na madini ambayo ndiyo iliomba bunge kuunda kamati ya mwakyembe, hadi kufikia kuumbuka kwa EL na mawaziri wengine , nilimkubali kwa hoja zake. Kwa maana hiyo Januari Makamba atawekwa pale ili kulinda mafisadi.
Uzee na ujana inaweza kuwa hoja endapo tunaona mzee ameishiwa hoja za msingi na tunaona kijana ana mtizamo mpya wa kimapinduzi/kimaendeleo. Lakini kwa muelekeo wa Januari - sidhani kama ni kijana sahihi tunayemuhitaji katika mapambano ya sasa!
 
Blah bla blah blah blah blah blah blah blah..

The same old shyt different day.

Naona maandalizi ya mediocre JK kumpa uwaziri huyu Makamba.

Twafwa!
was goin to say this soon,why huyu february anafight sana kuhusu hiyo chance??he gpromised to be a minister after,hivi ndio mmeona kuna dalili za kuisha ufisadi hapo kweli??mi ndio nabadili uraia kabisa hivyo potelea karibu.kila viongozi wakuu wanavyonitia maudhi na mimi ndio nazidi kutokomea,wabaki na bumbuli yao kesho aje mtoto wa nani mwingine keshokutwa mtoto wa nani sijui,bora tukae utumwani lakini democracy 50-50 baba yako mzazi humueshimu itakua mtoto wa makamba,mi naendelea kupiga box nyie bakini na politiki zenu.
 
was goin to say this soon,why huyu february anafight sana kuhusu hiyo chance??he gpromised to be a minister after,hivi ndio mmeona kuna dalili za kuisha ufisadi hapo kweli??mi ndio nabadili uraia kabisa hivyo potelea karibu.kila viongozi wakuu wanavyonitia maudhi na mimi ndio nazidi kutokomea,wabaki na bumbuli yao kesho aje mtoto wa nani mwingine keshokutwa mtoto wa nani sijui,bora tukae utumwani lakini democracy 50-50 baba yako mzazi humueshimu itakua mtoto wa makamba,mi naendelea kupiga box nyie bakini na politiki zenu.

Mdau naona una ghadhabu kama umeumwa na nyigu mdomoni..
Jipe moyo, haya yote yana mwisho..
 
Babukijana,
Punguza munkari. Tanzania ni yetu sote, walio ndani na wale wanaobeba mabox nje ya nchi. Bado naamini kuwa Tanzania ya haki kwa wote bado inawezekana. Hawa wanaopandilia migongo ya majina na baba zao kuna mwisho wake. Believe me.
 
Swali la kizushi---Do you guys believe everything you read on the internet?
 
TAKUKURU wana taarifa na vikao hivi? Je, sheria ya uchaguzi inaruhusu?
 
Swali la kizushi---Do you guys believe everything you read on the internet?

No we don't, we don't even believe those who say "Don't believe everything you read on the internet" when it is to their advantage to say so.
 
No we don't, we don't even believe those who say "Don't believe everything you read on the internet" when it is to their advantage to say so.
Poa sana. The idea of not believing everything you read on internet is rather a common sense. Whether one is advantageious to it or not. I guess, that is the beauty of commonsense and cold facts.
 
Back
Top Bottom