Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maswali Mengi Majibu Machache

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maswali Mengi Majibu Machache

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Leo nimefuatilia mahojiano aliyoyafanya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman kupitia kipindi cha Clouds360 cha Clouds TV na nimbaki na maswali mengi kuliko majibu

Othman Masoud Othman amewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kabla ya kung’olewa kwa kile kinachosemwa chinichini kuwa ni kusimamia msimamo wake wa kudai Serikali tatu.

Katika mahojiano ya leo, Othman bado ameendelea na msimamo wake wa kudai serikali tatu. Ni jambo jema kuwa bado ana msimamo uleule na leo emesema wazi kuwa mfumo wa Serikali mbili una kasoro lakini swali langu ni:

Je kwanini anaendelea kuhudumu akipata stahiki zote, posho na mishahara katika Serikali ambayo iko na ushirika (muungano) na Serikali Mama ambayo haamini muundo wake?

Kwa kuwa sasa yupo ndani ya Serikali (japo tunaelewa ni ceremonial) je anafanya nini kutetea anachoamini?

Je tukisema kwa maneno anataka Serikali tatu lakini kwa matendoo ya kila siku anaishi na kuitumikia Serikali mbili nitakuwa nimekosea?


Katika mahojiano amegusia masuala mengi zaidi ikiwemo mahusiano yake na Rais Mwinyi, Uhitaji wa Katiba Mpya na mengine kadha wa kadha lakini mimi bado nina maswali mengi kuliko majibu.

Kama una muda bofya hapa utazame sehemu ya aliyoyasema

Masoud.jpeg
 
Leo nimefuatilia mahojiano aliyoyafanya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman kupitia kipindi cha Clouds360 cha Clouds TV na nimbaki na maswali mengi kuliko majibu
Makamo wa kwanza anatoka upinzani Kwa mujibu wa muafaka baada ya mazungumzo ya Rais Hussein Mwinyi na marehemu Maalim Seif.

Hivyo anaweza kuwa na msimamo tofauti na msimamo wa CCM wa serikali mbili.
 
Leo nimefuatilia mahojiano aliyoyafanya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud Othman kupitia kipindi cha Clouds360 cha Clouds TV na nimbaki na maswali mengi kuliko majibu...

Huyu jamaa ni Mznz kindakindaki.

Uelewa wake kuhusu Znz na historia yake ni kiwango cha juu sana.

Hussein Mwinyi amepandikizwa tu kule Znz, lakini uwezo na uelewa wake ni mdogo ukimlinganisha na Othman Masoud.
 
Makamo wa kwanza anatoka upinzani Kwa mujibu wa muafaka baada ya mazungumzo ya Rais Hussein Mwinyi na marehemu Maalim Seif.
Hivyo anaweza kuwa na msimamo tofauti na msimamo wa CCM wa serikali mbili.
Unachokisema ni sahihi na kipo wazi kabisa, sasa kutokana na hayo rejea kwenye hoja sasa tujadili
 
Huyu jamaa ni Mznz kindakindaki.

Uelewa wake kuhusu Znz na historia yake ni kiwango cha juu sana.

Hussein Mwinyi amepandikizwa tu kule Znz, lakini uwezo na uelewa wake ni mdogo ukimlinganisha na Othman Masoud.
Amepandikizwa na nani tena?
 
Huyo kwa sasa ana lamba asali..hakuna cha serikali tatu wala nini.

Muungano tutaulinda daima.

La tuwe na serikali moja tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Othman Masoud huyu ni mwanasheria pia kwa sasa ni kiongozi(makamo wa kwanza wa rais SUK) katiba ya zanzibar inasema serikali ya kitaifa (ushirikiano kati ya chama kiloshinda na wapili kwenye uchaguzi) huyu hajaomba kuwa makamo wa kwanza Bali chama chake kimemteua kuchukuwa hio nafasi. Yupo kwenye nafasi ya kuteuliwa kwa mujibu wa katiba lakini chama na msimamo wake upo palepale juu ya uono wake sio uono wa serikali aliopo. Siasa kama dini unaweza kuwa muislam au mkristo lakini ndani ya hizi dini kuna madhehebu yake na tofauti zake.



Kukuuuu [emoji239][emoji239][emoji239]
 
Ingependeza angetumia nafasi yake kupenyeza hoja za Serikali tatu ili hilo liwe kiini cha mjadala wa Katiba Mpya
 
Huyu jamaa ni Mznz kindakindaki.

Uelewa wake kuhusu Znz na historia yake ni kiwango cha juu sana.

Hussein Mwinyi amepandikizwa tu kule Znz, lakini uwezo na uelewa wake ni mdogo ukimlinganisha na Othman Masoud.
swadakta !
 
Back
Top Bottom