Makamu wa Rais Afghanistan awagomea Taliban, asema yeye ndiye Rais halali

Criterion

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2008
Posts
11,797
Reaction score
11,891
Eee bwana wee!

Vita vya ndani havina mshindi. Bila kukaa mezani na kutengeneza muuundo usio na ubaguzi wala ugandamizaji wa haki za watu katika jamii, historia inaendelea kuonyesha kwamba "Utulivy wowote unaoweza kuonekana huwa ni unafiki, unaovundika machafuko".

Baada ya watalibani kutangaza ubabe, Makamu wa rais aitwaye, ameapa kutokukubali kukaa chini ya magaidi wa kundi la Taliban na ameomba msaada wa kimataifa.


Ni nini hatima ya amani katika nchi hiyo iliyojaa watu wasiokuwa na tumaini na ambao kwao kuishi ni ukurasa tu katika kitabu?
 
Nchi hiyo haikaliki tena, hapo USA Eu na washirika wa NATO watamtumia huyo makamu kama fimbo dhidi ya Taliban na watampa support yote then kifuatacho ni ITV.

Yaani hapo bora waliopelekwa Uganda.
 
Huyu jamaa Amurullah Saleh wa kabila la Tajik, alikua makamu wa Rais Ashraf Ghani wa Afghanistan alieikimbia nchi, katokea Afghanistan kaskazini kwenye jimbo la Panjshir na ndiko kuliko kuwepo muungano wa NORTH ALLIANCE ulioshirikiana na USA kuwafurusha Taliban 2001 na ndiko alikokimbilia baada Taliban kuuteka kabul. Amurullah kaondoka na makamanda wa kijeshi kwenda kuanzisha vuguvugu la kupinga utawala mpya wa Taliban.

PANJSHIR ni jimbo pekee mpaka sasa hivi halijaangukiya mikononi mwa Taliban.

 
Jumuiya ya kimataifa tena wakati wababe wasiyoshinda vita aka wamarekani wameomba poo? Huyo makamu wa raisi bora angesoma alama za nyakati atulize wenge jamaa wamuingize kwenye serikali.

Hao wakuda hawachelewi kumkata kichwa akizingua. Kama Marekani imeshindwa sembuse yeye?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…