Makamu wa Rais Dkt. Mpango: Wabunge wa upande wa pili (CHADEMA, ACT na CUF) ni vema mkajiunga CCM ili kwa pamoja tujenge nchi

Makamu wa Rais Dkt. Mpango: Wabunge wa upande wa pili (CHADEMA, ACT na CUF) ni vema mkajiunga CCM ili kwa pamoja tujenge nchi

Kwa hiyo wewe ni mwelewa? Umemsikiliza msaliti Lissu anavyoumbuliwa leo na Lumumba?
Umemsikia rais Samia alivyo muumbua Mwendazake kwa uporaji wa wafanya biashara? Au CAG kwenye hasara ya ATCL tuliyoaminishwa na Mwendazake kuwa imetengeneza faida mpaka na gawio kutoa serikalini?? Mbona humwiti Rais Samia msaliti??
Anueni MATANGA, Tanzania ni ya watanzania wote
 
Nimeona Lissu leo amejipanga kuchafua nchi.

Yani Mkenya PLO Lumumba amejipanga kuitetea Tanzania lakini mzaliwa wa Singida Tundu Lisu anajipanga kuchafua.

Ni aibu kubwa kwa taifa letu

Lisu ni makamu mwenyekiti hewa wa Chadema mnalipa mshahara wa bure.
Kuna watu walifunga internet kuzuia jumuiya ya kimataifa isijue kinachoendelea,na wao waibe uchaguzi.
Kuna watu wasiojurikana wanaojurikana ambao waliendesha genge la utekaji na Mauaji.
Kuna watu walijaza kabila lao kwenye nafasi nyeti Ili waibe pesa za umma.
Kuna watu hawakupenda Watz waongee ya moyoni.
Kuna watu kwa miaka 5,deni la Taifa limefikia Tilioni 71!
Kuna watu wamejenga uwanja wa Ndege Chato,ambao mpaka leo tangu march 17,hakuna Ndege iliyotua.
Kuna watu wanajenga bwawa la umeme kwa upembuzi yakinifu wa mwaka 1970!
Watu wenye sifa hizi ndio wanaoichafua nchi.
 
Sasa si bora wapeleke bungeni mswaada wa kufuta vyama vya siasa kama anataka wapinzani wote waende CCM...

Maana kwa tafsiri ya lugha aliyoiongea ni kwamba Tanzania ni CCM
 
Sasa si bora wapeleke bungeni mswaada wa kufuta vyama vya siasa kama anataka wapinzani wote waende CCM...

Maana kwa tafsiri ya lugha aliyoiongea ni kwamba Tanzania ni CCM
Mpango nae ana acquired Stupidity kama kina Kabudi na wengineo.
 
Dr mpango unazidi kujishushia hadhi yako!
Chadema wana wabunge bungeni?
Hao ni wabunge wenu na ndugai na sii vinginevyo.
Dr, credibility yako ni kubwa sana usiingie ktk siasa za watu wagonjwa.
 
Makamu wa Rais Dkt. Mpango amesema wabunge wa upande wa pili akimaanisha Chadema ACT wazalendo na CUF ni vema wakajiunga na CCM ili kwa pamoja tuijenge mama Tanzania.

Dkt. Mpango amewashauri wabunge hao kwamba kama kuna ugumu wa wao kuhamia CCM basi wawe hata wanajenga hoja zenye kuleta maslahi ya kimaendeleo kwa mama Tanzania na siyo vinginevyo.

Chanzo: TBC.

Maendeleo hayana vyama!
Kwa hiyo anataka tuwe na wabunge kama huyu wa CCM? Kweli ccm imetuona mazoba hasa

 
Back
Top Bottom