Makanisa yaliyopo Tanzania yakiamua yanaweza kujenga viwanda

Makanisa yaliyopo Tanzania yakiamua yanaweza kujenga viwanda

EllySkyWilly

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2020
Posts
2,204
Reaction score
2,085
Habarini za Leo wapendwa.

Kama kichwa kinavyo someka hapo juu. Ni juu ya makanisa yetu mbalimbali yaliyopo Tanzania.

Sote tunajua jinsi makanisa yetu yanavyo toa mchango katika sekta ya elimu na afya. Kuna shule nyingi sana zinazotoa elimu bora kwa wototo wetu zilizojengwa na makanisa. Lakini pia si hivyo tu kuna vyuo vingine pia vimejengwa na makanisa na hivi navyosema vinaendelea kudahili na kutoa elimu bora kwa watoto wetu.

Katika swala la upande wa afya, nako pia tunaona mchango wa haya makanisa jinsi yalivyo fanya kazi kubwa, fedha zao za michango kanisani zimejenga hospitali ambazo ndugu zetu na Sisi wenyewe tunapata huduma za afya.

Hivyo basi kutokana na mchango muhimu namna hii wa makanisa katika maendeleo ya nchi yetu mimi Nadhani yanaweza pia kuwekeza kwenye kuanzisha baadhi ya viwanda ambavyo havihitaji mitaji mikubwa mfano viwanda vya madawa n.k.

Viongozi wa dini kama mpo humu ndugu zangu tunawategemea sana katika taifa letu maana kazi zenu zinatembea na mkono wa bwana siku zote na ndio maana zinafanikiwa.

Wekezeni pia kwenye viwanda, ili watoto wanaosoma katika vyuo na shule zenu waajiriwe kwenye viwanda hivyo hivyo. Hili swala linawezekana ndugu zangu. Pia watapata nafasi kufanya mazoezi ya vitendo kwenye viwanda vyenu wenyewe.

Tunajua mnaweza, binafsi mimi nimeshiriki sana katika vikao vya wababa kanisani kiukweli huwa tunajiwekea malengo makubwa sana na kwa mkono wa bwana huwa mambo yetu yanafanikiwa.

Tunaona jinsi ambavyo mnaweza kujenga makanisa makubwa ya ghorofa kwa uvumilivu na ustahimilivu wa hali juu bila kuchoka tena kwa muda mrefu kwa moyo mmoja na ushirikiano kwa kutumia nguvu ya kanisa.

Kwakweli Mungu awabariki sana. Amen.
 
Kweli tumeshindwa kupata watu binafsi au wawekezaji mpaka tunataka makanisa ... tunarudi zama zile za wamissionari ....aaahhhhh ...Kanisani Kazi yake ni kuhubiri na kuleta amani.

Tujijemge wenyewe na think tank wetu tutafika mbali
 
Mkuu, hivi unajua hayo makanisa yana ugomvi wa ndani kwa ndani hususan katika masuala ya fedha na uteuzi, sasa ukiyakusanya kwa pamoja itakuwaje unadhani

Kanisa stable hapa Tanzania ni Roman Catholics tu baaas kwa sababu teuzi zooote zinatokea Vatican.
 
Mkuu, hivi unajua hayo makanisa yana ugomvi wa ndani kwa ndani hususan katika masuala ya fedha na uteuzi, sasa ukiyakusanya kwa pamoja itakuwaje unadhani

Kanisa stable hapa Tanzania ni Roman Catholics tu baaas kwa sababu teuzi zooote zinatokea Vatican.
Ugomvi huwa haukosekani katika jumuhia yoyote duniani.
 
Wajenge viwanda kwa uchumi upi?? kila kukicha existed industry vnafunga au kusitisha uzalishaji au we mkuu haupo Tanzania hii ya meko??
 
Hayo wanayofanya ni kwa michango ya waumini au ni msaada kutoka nje?
 
Misikiti ndiyo haswaa inaweza kujenga Heavy Industries ya kumanufacture magari, treni na ndege

Wana hospitali na shule nyingi zenye viwango vya juu
 
Shule za kanisa zinakuwa na bei kubwa sana wakati zimejengwa kwa michango ya waumini,,hii imekaaje kuelekea ujenzi wa kiwanda??
 
Madhehebu m,engi yamekaa katika taswira ya kuabudu tu ila ukikutana na makanisa ya hawa wanajiita SAINT ... MMHH siku hizi watu wanajenga shule.kumbi za starehe ndani yaani mpaka unakutana na shule unashangaa ina vitu vingi sana ndani yake..ni kama majeshi yetu walifika sehemu wakaona wasikae kama namba 1,hao wana kumbi nyingi mjini za burudani kama msasani na briuget mec masaki ni sehemu nzuri sana kutembelea
 
Shule za kanisa zinakuwa na bei kubwa sana wakati zimejengwa kwa michango ya waumini,,hii imekaaje kuelekea ujenzi wa kiwanda??
Na wanaopandisha bei namna hiyo usisahau walisomeshwa pia na waumini wa mnakanisa hayohayo..ukishapata humjui mwenye shida
 
Chukulia mfano sadaka zinazokusanywa pale saint joseph kila jumapili ni shngapi kwa mwaka??
 
Inawafaa zaidi WABUNGE wetu, taasisi za ibada tuziachie mzigo wa elimu na afya kwa sasa!

Ingekua bora zaidi wabunge wote wapewe agizo hili! Kila mbunge jimboni kwake ajenge kiwanda ama alete mwekezaji wa kiwanda na kutengeneza ajira jimboni kwake ili kuisaidia Serikali kuhusu janga la ajira kwa vijana na jamii kwa ujumla!

Na ikiwezekana ifanywe kuwa sheria na mbunge hasiyekua tayari aachie kiti mwenye utayari akae!

Wabunge wa Tanzania wanalipwa pesa nyingi sana lakini mara chache sana hufanya uwekezaji unaorudi kunufaisha jamii ya wale anaowawakilisha bungeni!

Its about time they gave back to the community that has given them too much so far!
 
Wazo zuri sana tena ikibidi itungwe sheria kabisa ya kuwalazimisha kufanya hivyo.
 
Kanisa ni huduma za kiroho na huduma za kimwili kama elimu, Afya, huduma za maji, kutembelea wagonjwa, kutunza mayatima na wasiojiweza nk, kazi ya kanisa sio biashara za viwanda nk. Kwani ukianzisha jambo hilo polepole lengo la kanisa litapotea na kanisa litamuwa ni kichaka cha biashara na hatimaye migogoro ya kimaslahi kati ya waumini itaibuka na hapo kifuatacho ni kifo cha kanisa.

Hata Yesu wakati fulani alipindua meza za wafanyabiashara. Kaisari mpe yake na Mungu mpe yake.
 
Hakuna kanisa la KILOKOLE lenye uwezo wa kujenga shule, hospitali sembuse kiwanda. Kama lipo lililofanya hivyo naomba kufahamishwa tafadhali...
 
Hakuna kanisa la KILOKOLE lenye uwezo wa kujenga shule, hospitali sembuse kiwanda. Kama lipo lililofanya hivyo naomba kufahamishwa tafadhali...


Mlokole na biashara wapi na wapi???---- wao kazi yao ni kutoa mapepo kwa wanawake tu.
 
Back
Top Bottom