Makapuku Forum

Makapuku Forum

Yanga haitaki mchezo kwani imeendelea kuwekeza ndani na nje ya uwanja na sasa imegeukia kwenye teknolojia ya kisasa ambayo mastaa wa kikosi hicho wanatumia vifaa ghali mazoezini
.
Kambini Avic Town kumeboreshwa kwa kuweka vifaa vipya vya mazoezi sambamba na kuongeza vingine ambayo awali havikuwapo lakini kubwa zaidi ni kifaa aina ya Electrical Muscles Recovery Stimulation (EMS), ambacho ni kwa mara ya kwanza kwa timu ya Tanzania inatumia kifaa hicho ambacho kinatajwa kuwa ni ghali sana.
.
Kifaa hicho kilicholetwa kwa msaada wa tajiri wa klabu hiyo kina kazi zaidi ya moja ikiwamo kusaidia kurejesha utimamu wa mwili, kushitua akili na misuli sambamba na kuonyesha sehemu ambazo mchezaji anaweza kuwa ameumia au kupata jeraha bila yeye kujua, na mastaa wamekuwa wakikifurahia kwa kuwa kinautetemesha mwili.
.
Licha ya kuwapo kimoja lakini kinafanya kazi kubwa ambapo kwa siku kinaweza kutumika kwa wachezaji mmoja hadi watano na kwa kuanzia walianza kutumia Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Aboutwalib Mshery na Kibwana Shomary.
Screenshot_20230912_132519_Instagram.jpg
 
.
[emoji599] Staa wa Simba, Muivory Coast, Kramo Aubin huenda akakosekana kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Power Dynamo kutokana na kujitonesha majeraha katika mechi ya kirafiki dhidi ya Ngome na ARENA imepenyezewa kwamba kama atakuwa na jeraha kubwa basi atapewa mapumziko arudi kwao akajitibu.

…………
Screenshot_20230912_132744_Instagram.jpg
 
WABABE
.
79—NEYMAR amefunga mabao 79 ya timu ya taifa ya Brazil [emoji1054] na kuivunja rekodi ya Pele ya mfungaji bora wa muda wote ya mabao 78. Kwa upande wa Amerika Kusini yote kiujumla kinara ni: Messi (Argentina): Mabao 104 kisha Neymar (Brazil): Mabao 79.

Screenshot_20230912_132932_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom