@luambano77 ameuliza swali, kwa uwekezaji uliofanywa kwenye klabu za Simba na Yanga, kuna mchezaji ambaye anapokea mshahara wa Tsh. 1,000,000 [milioni moja]?
Mkongwe @amrikiembatz akasema kwa sasa Simba na Yanga mshahara wa Tsh. 1 milioni labda kwa mchezaji ambaye amepandishwa kutoka timu za vijana lakini anaesajiliwa kutoka sehemu nyingine anachukua zaidi ya hapo.
@jr_farhanjr amesema mchezaji anaechukua mshahara mdogo Simba na Yanga pengine ni kuanzia Tsh. 2,500,000 [milioni mbili na laki tano] hapo bado posho n.k
Luambano akamaliza kwa kusema, kama kuna mchezaji wa Simba au Yanga analipwa Tsh. 1,000,000 [milioni moja] basi anapaswa kujitathmini. Kwa sababu hata timu za kati zinalipa hadi Tsh. 1,500,000 na kuendelea.
Kwa jinsi Simba na Yanga zilivyofanya uwekezaji ni sawa mchezaji kulipwa mshahara Tsh. 1,000,000 kwa mwezi________??
Note ! waliokwenye picha hawana uhusiano na hayo malipo