Makapuku Forum

Rais wa Rwanda, Paul Kagame amemteua aliyekuwa Ofisa Mkuu wa Jeshi, Jenerali James Kabarebe nchini humo kuwa Waziri wa Nchi kwa Ushirikiano wa Kikanda licha ya kwamba anashutumiwa kufanya kazi kwa karibu na kundi la waasi la DR Congo.

Jenerali Kabarebe ambaye kwa miongo kadhaa amekuwa mshirika wa karibu wa Rais Kagame, alistaafu jeshi mwezi uliopita.

Wataalamu wa Umoja wa Mataifa walichapisha ripoti mwezi Juni wakimtuhumu Jenerali Kabarebe kuwa na jukumu kubwa katika kuratibu operesheni za kundi la waasi la M23 mashariki mwa DR Congo huku Rwanda ikikanusha uvumi huo.
 
Ripoti ya utafiti wa ujumuishi wa kifedha ya Finscope ya mwaka 2023 inaonyesha kuwa asilimia 22.2 ya Watanzania wenye miaka zaidi ya 16 wanatumia huduma za kibenki, idadi hiyo ikiongezeka kutoka asilimia 17 mwaka 2017.

Kutokana na ongezeko la idadi ya watu ambao kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 ilionyesha kuwa Watanzania wapo zaidi ya milioni 61, maana yake ni kuwa idadi ya watumiaji wa huduma za kibenki inaongezeka.

Mwamko wa matumizi ya huduma rasmi za kifedha kwa ujumla ni mkubwa, kwani Finscope 2023 inaonyesha kuwa Watanzania watatu kati ya wanne wenye umri wa kuanzia miaka 16 wana uwezo wa kuzifikia huduma za kifedha na kuzitumia.

Hata hivyo, kadiri huduma zinavyozidi kuboreshwa hitaji la elimu ya fedha na mifumo yake linazidi kuongezeka ili kuhakikisha mali na amana za watu zinakuwa salama.

Je, ukiwa miongoni mwa wateja wa benki wa sasa au watarajiwa umewahi kujiuliza nini kitatokea endapo benki hiyo itafilisika?

“Kwa kweli sifahamu, ninachojua ikifilisika inakuwa haina kitu kabisa, lakini nikizipata taarifa hizo mapema nitawahi kwenda benki kuchukua kabla hazijaisha kabisa,” anasema Noel Desdelius, mkazi wa Dar es Salaam.

Taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa Tangu mwaka 2000 hadi Juni mwaka huu jumla ya benki 9 ziliwekwa kwenye mufilisi kwa sababu mbalimbali, kwa asilimia kubwa sababu ikiwa ni kutokuwa na uwezo wa kujiendesha.

Benki hizo 9 ni Greenland Bank Tanzania Limited (2000), Delphis Bank Tanzania Limited (2003), FBME Bank Limited (2017), Mbinga Community Bank Plc (2017), Njombe Community Bank Limited (2018), Meru Community Bank Limited (2018), Covenant Bank for Women (T) Limited (2018), Kagera Farmers' Cooperative Bank Limited (2018) na Efatha Bank Limited (2018).
 
Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga @judith__kapinga amelipa Shirika la Umeme (TANESCO) saa mbili kurudisha uzalishaji wa umeme kwenye kituo cha kuzalisha umeme cha Ubungo I ambacho kimezimika umeme kuanzia usiku mpaka sasa hivi na mitambo sita inayotakiwa kuzalisha umeme kwa sasa hivi haizalishi na hivyo kupelekea baadhi ya Wananchi kukosa umeme.

Kapinga amesema hayo leo September 29,2023 alipotembelea Makao Makuu ya TANESCO, Ubungo Jijini Dar es salaam “Tumefika hapa na leo kwa bahati mbaya pia kituo cha Ubungo I kimezimika umeme kuanzia usiku mpaka sasa hivi na mitambo sita inayotakiwa kuzalisha umeme kwa sasa hivi haizalishi lakini Wataalamu wako saiti wanahakikisha inawaka”

"Nimewaelekeza TANESCO kuhakikisha ndani ya masaa mawili kituo kile kinarudi katika uzalishaji na kama hakitorudi kwenye uzalishaji watafute njia mbadala ya kuhakikisha ndani ya masaa sita yajayo kituo hiki kinarudi kwenye uzalishaji ili hali ya upatikanaji umeme iweze kuimarika”

“Mashine zile sita zinazalisha kati ya megawati 42 hadi 43 lakini kwasababu zimepata hitilafu hizo megawati ziko nje, nimewaagiza warudishe kituo kwenye uzalishaji na umeme upatikane kwa Wananchi”
 
[emoji599] Yanga inahitaji sare, ushindi wowote au isifungwe zaidi ya bao moja kubaki salama kubadilisha historia yao kwa kurejea tena Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi.
.
Nahodha Bakar Mwamnyeto aliyekuwa anamuuguza Baba yake amerejea, sambamba na Mahlatse Makudubela ‘Skudu’ ambaye Gamondi anajipanga kumtumia kesho. Staa huyo hajaonekana uwanjani kipindi kirefu.

 
Daktari wa Simba, Edwin Kagabo amesema nyota wa kikosi hicho, Aubin Kramo anaendelea vizuri na matibabu ya goti na kinachoendelea kwa sasa kwake ni taratibu mbalimbali ili kugundua ni lini atarejea uwanjani tena.
.
Dk Kagabo alisema Kramo amesharudi baada ya kwenda, Ivory Coast kwa uchunguzi zaidi ila bado hajaruhusiwa kuanza mazoezi na wachezaji wenzake kikosini.
.
“Siwezi kuweka wazi ni lini atarudi kwa sababu kuna awamu ambazo sisi kama madaktari tumempa na tunaendelea kumfanyia uchunguzi hatua kwa hatua ingawa mashabiki wa simba watambue jeraha lake sio kubwa sana,” alisema na kuongeza madaktari wanaendelea kupambana ili kuhakikisha anarudi haraka iwezekanavyo kwani mashabiki wengi wa timu hiyo wanashauku kubwa ya kumuona akikitumikia kikosi hicho kutokana na ubora aliokuwa nao.

……….
 
Klabu ya Chelsea imeendelea kukumbwa na janga la majeraha kwa wachezaji wake sambamba na mwenendo mbovu kwenye Ligi Kuu England ambako imeshinda mara moja katika mechi sita.
.
Sasa Chelsea imepata pigo jingine baada ya beki wake tegemeo Ben Chilwell kuumia wakati wa mechi ya raundi tatu ya Kombe la Carabao dhidi ya Brighton. Chilwell ameumia siku chache tu baada ya nahodha wa timu hiyo Reece James kuondolewa kikosini baada ya kuumia, ikimpa wakati mgumu kocha Mauricio Pochettino ambaye bado anajenga kikosi chake.
.
Mpaka sasa Chelsea ina wachezaji majeruhi saba akiwamo Christopher Nkunku na Romeo Lavia ambao walisajiliwa hivi karibuni kwenye dirisha la kiangazi.

 
Kocha wa Yanga, Miguel Gamondi katika kuhakikisha anapata ushindi kwenye mchezo wao dhidi ya Al Merrikh Jumamosi hii ameonekana kuwaongezea dozi ya mazoezi wachezaji wake ambapo leo alionekana akiwakimbiza wachezaji wake kwa kasi mazoezini, wakizunguka uwanja.
.
Aidha, Gamondi alionekana kuwafanyisha mazoezi ya nguvu akilenga kuwaongezea stamina na kasi kuelekea kwenye mchezo huo utakaochezwa Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
.
Akizungumza Gamondi alisema anataka kona wanacheza kwa kasi muda wote na kutowapa nafasi wapinzani wao.

“Tulikuwa na mfumo mwingine kwenye mchezo wetu wa kwanza wa ugenini, na mchezo wa marudiano pia tutakuwa na mfumo mwingine kabisa, mazoezi ninayowafanyisha wachezaji wangu ni katika kuhakikisha kikosi kinakuwa imara na tunafikia malengo yetu, nataka kucheza soka la kasi zaidi,” alisema Gamondi.
 
Timu ya Simba ukitaka kuibana, basi hakikisha unamalizana nayo ndani ya dakika ya dakika 45 za kwanza za mchezo husika kwani bila hivyo sahau kupata ushindi dhidi yao. Simba imecheza mechi sita za mashindano, lakini katika mechi hizo michezo miwili ya Ngao ya Jamii haijafunga bao lolote.
.
Timu hiyo katika michezo minne imecheza mitatu Ligi Kuu na mmoja wa hatua ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Katika mechi hizo imeonyesha kutoruhusu mabao mengi kipindi cha pili ikiruhusu bao moja tu katika mchezo dhidi ya Power Dynamos uliomalizika kwa sare 2-2. Simba irihusu bao hilo dakika ya 74 huku lile la kwanza likifungwa kipindi cha kwanza dakika ya 28. Bao hilo la kipindi cha pili ndilo pekee ambalo Simba imeruhusu hadi sasa na ikionyesha ni wazi haina cha kupoteza muda huo ukifika.
.
Katika kipindi cha kwanza timu hiyo iliruhusu mabao matatu mawili katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mtibwa Sugar na lingine ni la mchezo dhidi ya Dynamos dakika ya 28.
.
Wakati Simba ikiwa ni ngumu kufungwa kipindi cha pili, yenyewe imeonyesha ubora wa kufunga muda wowote. Simba katika kipindi cha kwanza imefunga mabao saba, matatu yakiwa katika mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar dakika za 5, 9 na 45, mchezo dhidi ya Dodoma Jiji dakika ya 44 na mechi dhidi ya Coastal Union dakika za 7, 11 na 40. Wakati huohuo katika kipindi cha pili Simba imefunga mabao manne moja dhidi ya Mtibwa Sugar dakika ya 81, mchezo dhidi ya Power Dynamos.
 
Badae tukaja kwa mpinzani wa kuchezanae, nafikiri yule mkenya alitiwa maneno na watu kuwa anacheza na bondia mkubwa Tanzania halafu analipwa pesa ndogo, yule bondia akaongeza dau...ile promotion ikashindwa kufikia makubaliano kwenye dau ambalo amependekeza mkenya, mwisho wa siku akaahirisha pambano kwa sababu ambazo hazijulikani lakini sababu ilikuwa ni pesa.

Muda mchache uliobaki hatukuweza kupata bondia ambaye angekuwa mbadala wa yule mkenya, ikabidi watafute mpinzani mwingine ambaye atakuwa anatoka Afrika kwa haraka ambaye anaweza kuziba hiyo nafasi kwa sababu zilikuwa zimebaki siku tatu tu!

Tukapata mpinzani ambaye mahitaji yake yalikuwa juu ya ofa waliyokuwanayo. Nikasema kwakuwa dhamira ni kulifanya jambo hili litokee na mimi mashabiki wanataka kuniona lakini mimi pia nataka kujipima nimefikia wapi katika maandalizi yangu.

Tukafanya mazungumzo na huyo bondia akataja kiasi anachotaka, nikamwambia promoter atoe nusu na sisi tutaongezea nusu nyingine ili jambo hili lifanyike katika makubaliano kwamba tunafanya kazi promotions mbili hakuna mtu mwingine nyuma yetu.

Hadi siku ya kupima uzito inakaribia ambayo ni jana tukaona wale watu ambao hatutaki kuhusiananao wamefika pale sehemu ya kupimia uzito! Tukahoji uwepo wao pale, yule promoter tunaefanyanae kazi akasema hawahusiki kwa lolote.

- Hassan Mwakinyo
 
Badae tukaja kwa mpinzani wa kuchezanae, nafikiri yule mkenya alitiwa maneno na watu kuwa anacheza na bondia mkubwa Tanzania halafu analipwa pesa ndogo, yule bondia akaongeza dau...ile promotion ikashindwa kufikia makubaliano kwenye dau ambalo amependekeza mkenya, mwisho wa siku akaahirisha pambano kwa sababu ambazo hazijulikani lakini sababu ilikuwa ni pesa.

Muda mchache uliobaki hatukuweza kupata bondia ambaye angekuwa mbadala wa yule mkenya, ikabidi watafute mpinzani mwingine ambaye atakuwa anatoka Afrika kwa haraka ambaye anaweza kuziba hiyo nafasi kwa sababu zilikuwa zimebaki siku tatu tu!

Tukapata mpinzani ambaye mahitaji yake yalikuwa juu ya ofa waliyokuwanayo. Nikasema kwakuwa dhamira ni kulifanya jambo hili litokee na mimi mashabiki wanataka kuniona lakini mimi pia nataka kujipima nimefikia wapi katika maandalizi yangu.

Tukafanya mazungumzo na huyo bondia akataja kiasi anachotaka, nikamwambia promoter atoe nusu na sisi tutaongezea nusu nyingine ili jambo hili lifanyike katika makubaliano kwamba tunafanya kazi promotions mbili hakuna mtu mwingine nyuma yetu.

Hadi siku ya kupima uzito inakaribia ambayo ni jana tukaona wale watu ambao hatutaki kuhusiananao wamefika pale sehemu ya kupimia uzito! Tukahoji uwepo wao pale, yule promoter tunaefanyanae kazi akasema hawahusiki kwa lolote.

- Hassan Mwakinyo | LeoTena @cloudsfmtz
 
Badae kulizuka utata baada ya promotion kukwama kwenye fedha kwa hiyo wakawa wanahitaji kampuni/promotion nyingine kushirikiana nayo ili kuweza kulifanya hili jambo liwe.

Hiyo ilikuwa ni kinyume na utaratibu kwa sababu ilibidi kila kitu wanachokusudia kukifanya na mimi niwe nashirikishwa hata kama sina mchongo wowote lakini karatasi ya makubaliano yetu ilikuwa inaelekeza hivyo.

Wakaingia mkataba na promoter mmoja ambaye sisi hatuna uhusiano naye katika kazi kutokana na changamoto zetu binafsi ambazo zipo nje na hiyo promotion ambayo tunafanya nayo kazi.

Kwa hiyo nilivyosikia hivyo nikawauliza promotion ambayo nafanya nayo kazi kuhusu wao kuingia mkataba na promoter huyo, wakaniambia hakuna ukweli. Muda unavyozidi kwenda nikawa nahisi vitu tofauti nikiwauliza wanasema mambo yapo sawa niwaamini.

Badae nikawaambia kama kuna ukweli kwamba wanashirikiana na huyo promoter nikijua sitakuwa tayari kuendelea na event. Wakasema event yako tunataka iwe ya mkanda kama tulivyokubaliana, huyo mtu ambaye humtaki akiingia ataweza kulipia mkanda lakini kwakuwa humtaki itabidi tutafute mtu mwingine wa kulipia mkanda.

Nikawauliza thamani ya mkanda ni kiasi gani? Wakaniambia ni USD 4,750 ambayo tulijitolea kujilipia sisi wenyewe ili ile kampuni ya promotion iachane na watu wengine.

- Hassan Mwakinyo | LeoTena @cloudsfmtz
 
Kuna changamoto kati yangu na promotion ambayo nafanyanayo kazi, kwanza niliwafatilia baada ya kuwa wametaka kufanya kazi na mimi na nikakuta kuna baadhi ya tuhuma kwa mabondia waliowahi kufanyanao kazi kuwa hawakulipwa na wanawazungusha.

Nikaona labda ni hila tu za mabondia wa nyumbani kwamba wakati mwingine wanataka event ikiisha basi mtu alipwe chake palepale, kwa hiyo sikuchukulia kwa uzito mkubwa.

Aliyenikutanisha na Mkurugenzi wa hiyo promotion ni mtu ambaye ninamuheshimu sana kwa hiyo niliwaheshimu kwa heshima ambayo ninayo kwa huyo mtu.

Moja ya makubaliano yetu ni kufanya kazi kama promotion mbili na sio kama bondia, kila mmoja alikuwa na haki kuleta mdhamini au kuleta jambo mezani kujadili na sio kwakuwa wao ni promotion basi wataamua kila jambo na watakalosema ndio liwe.

Maana ya kuwa na promotions mbili ilikuwa pia mimi niwe na haki ya kuleta mabondia wangu ambao nawaandaa ili nao wapate nafasi ya kupigana kwenye hilo pambano ambalo na mimi nashiriki.

- Hassan Mwakinyo | LeoTena @cloudsfmtz
 
Farhan Jr

CHAMPEZ MWAKINYO anapambania standard kwenye game ya boxing kwa mujibu wa chanzo ni kuwa Promoter wa hii fight kuna vitu havipo sawa kwa mujibu wa makubaliano yao.

- Kubadilishiwa Bondia, yes alipaswa kupigana na Okwiri, Hassan akatrain vyema lakini wiki moja kabla akaambiwa kuwa Bondia huyo ameumia kwahiyo atabadilishiwa Bondia, Hassan alikubaliana na hilo na akaanza kutrain kwa Bondia mpya waliyompangia, shida sio Bondia kubadilishwa.

- Promoter kuvunja makubaliano, Kuna taarifa kuwa Promoter wa hii fight alipungukiwa pesa hivyo akashirikiana na Promoter mwingine ili pambano lipigwe, Hassan baada ya kusikia hivyo aliwasiliana na Promoter na kumwambia kama changamoto ni pesa basi yeye atatoa zake kuongezea ili pambano lipigwe pasi na kulihamishia kwa mwingine, inasemekana alipokea mzigo huo Promota.

Nikajaribu kufuatilia kwanini Hassan alikataa Promota asimpe Promota mwingine? Ni kuwa Hassan alishawahi kupishana kibiashara na huyo Mtu hivyo kiamani hakutaka ahusike kwenye biashara yake, hakutaka hata Mabondia wake waje kwenye pambano lake.

Kwakuwa Hassan alishatoa mzigo kwa Promota ili pambano lipigwe bila kutafuta mwingine wa kumsaidia, leo hii anashangaa kwenye kupima uzito anakutana na sura ambazo alizikataa ikizingatia kuwa alishatoa hela zake kuongezea, ndipo hapo shida ilipoanzia.

Yaani Promota alipungukiwa pesa akataka kuuza Pambano kwa mwenzake ambaye hawaivi na Hassan, Champez akagoma akaongezea hela yake halafu ghafla anakutana na sura alizozikataa leo kwenye kupima uzito.

Kwa mujibu wa chanzo changu, Hassan amekutana na Azam Media usiku huu maeneo ya Don Bosco ambao wao ndio Broadcasters, wanataka kuliweka sawa kati ya Hassan na Promoter, kama vitu vitaenda sawa basi fight kesho itakuwepo kwa mujibu wa chanzo changu.

Hassan hana shida na Bondia kubadilishwa bali masuala ya kibiashara.
 
Farhan Kihamu

Baada ya jana kuripoti kuhusu kwanini Champez Hassan Mwakinyo hataki kupanda ulingoni leo hii na sababu kuwa ni Promota kutoka kwa chanzo changu, nikapokea taarifa kutoka chanzo cha upande wa pili juu ya kwanini Hassan hataki kupanda, hivyo nakamilisha stori kutoka vyanzo vyote (pande mbili)

- Sababu inadai Hassan ana mgogoro na Mafia Promotions hilo kweli chanzo changu kimekiri na sababu ni kuwa kulikuwa na Watoto kama wawili wa Tanga walikuwa wanatrain kwenye dojo la Hassan akiwemo Salim Mtango ‘Messi wa Boxing’ ambapo wameondoka na kujiunga na Mafia Promotions.

“Kilichopo ni kuwa Hassan anawabania Ndugu zake wawili kutoka Tanga wasipande ulingoni akiwemo Salim Mtango kutokana na kuwa waliondoka kwake na anawamind Mafia Promotions kutokana na kuwapa thamani kubwa hawa watoto kuliko yeye, hiyo ndio sababu yake kuwabania watoto” kilisema chanzo hicho cha pili.

Wakati nazidi kuzungumza na chanzo cha pili akaendelea kuniambia “Hassan alishasaini mkataba ambao hauna kona kona na ashalipwa pesa yake yote kwa dola za Kimarekani (anataja) hivyo kilichosalia ni yeye kupigana na sio kuangalia wakina nani watapigana kabla yake kwakuwa sio mkataba wake unavyosema” kilitanabaisha chanzo hicho.

Katika kuendelea kuhojiana na chanzo hicho cha pili nikamuuliza kuhusu Bondia kubadilishwa hilo lipoje? Akasema namnukuu “Mengine tuyaache tu lakini huyu Bondia wa pili baada ya wa kwanza kuumia (anacheka) tulishirikiana kwenye kumtafuta na tulikubaliana sote wala hapakuwa na kona kona yoyote” kilihitimisha chanzo changu.

Kwa mujibu wa chanzo cha pili inaonekana Hassan hawezi kupanda ulingoni bila hao Vijana kuondolewa kwakuwa hawapikiki chungu kimoja na Mafia Promotions, hivyo ni kazi kwa Promoter wa pambano kuona namna gani anaokoa jahazi hilo kwakuwa msimamo wa Hassan haubadiliki, amenyooka.

Hii ni kwa mujibu wa chanzo cha pili ambacho ni kinzani na chanzo cha kwanza! So utata upo hapo.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…