Makapuku Forum

Siku chache baada ya @AyoTV kuripoti taarifa ya Mvuvi kuuawa na mamba na Watu wengine zaidi ya wanne kujeruhiwa katika Bwawa la Mtera lililopo katika Kata ya Migoli Halmashauri ya Wilaya ya Iringa , Mkuu wa Mkoa wa Iringa Halima Dendego ameagiza mamba hao watafutwe na kuvuliwa kwakuwa ni tishio, ili shughuli nyingine ziweze kuendelea.

Kauli hiyo imetolewa mara baada ya RC Dendego kufika katika Kata ya Migoli ili kuonana na Wananchi wanaopata kadhia ya kujeruhiwa pamoja na kuuawa na mamba na ametaka Mamlaka husika (TAWA) kuhakikisha inashirikiana na Wananchi na kwa kutumia vifaa vya asili kama vile ndoano na vifaa vingine ili wawavue mamba hao na kadhia hiyo iweze kuisha.

Dendego amesema katika mwaka wa fedha ujao Serikali itatenga fedha kwa Wananchi wa Kata hiyo na wanaozunguka Bwawa hilo kwa ajili ya ununuzi wa boti za kisasa ambazo zitawasaidia Wavuvi hao katika shughuli zao, tayari Watu zaidi ya wanne wamejeruhiwa na mamba pamoja na kiboko katika Bwawa hilo na mmoja amefariki kwa kuuawa na mamba.
 
[emoji187] “Phiri kinachomuondoa ni kiburi ana misimamo na sio mtu wa kusikiliza kile anachoambiwa hilo chini ya Benchika sio rahisi kuvumilika.” Chanzo changu makini ndani ya Simba.
 
[emoji599] Baada ya panga la kocha Benchika kuwapitia wazawa, panga hilo kwa sasa limehamia kwa nyota wa kigeni na fasta limeanza na kiungo mshambuliaji Said Ntibazonkiza “Saido”
.
Chanzo changu makini ndani ya Simba komeniambia, Licha ya Kocha Benchika kuvutiwa na nidhamu ya Saido, amekiri mwenyewe hawezi kuwa na msaada kikosini hasa kipindi hiki ambacho timu inataka kufikia malengo ya kutinga Nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa.
.
Ikumbukwe Saido mkataba wa mwaka mmoja alioingia na Simba umemalizika kwani alisajiliwa dirisha dogo la Disemba 24 mwaka juzi akitokea Geita.
 
Kazi ipo. Kuna mastaa ambao wana saa 72 za kuamua hatma yao katika timu ya Simba. Clatous Chama, Moses Phiri na Aubin Kramo ni miongoni mwao. Mastaa walio kwenye wakati mgumu kwa sasa wakiomba dua ili watoboe salama katika dirisha hili wengi ni wa kigeni, kwani lazima panga lipite kwa baadhi yao ili kuruhusu wapya waliosajiliwa au walio mbioni kusajiliwa kuingia kwani klabu hiyo imeshazidisha idadi inayotakiwa ya nyota 12.
.
Simba inataka kumalizia usajili kwa kushusha watu wawili kiungo mchezeshaji, lakini Benchikha amewaambia mabosi wa klabu hiyo, kuna mtu muhimu anamhitaji haraka basi ni straika mbali ya kiungo huyo.
.
Hii imetokana na dakika 90 za mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi, wakati Simba ikiing’oa kwa matuta Singida Fountain Gate, kuamsha balaa jipya, baada ya kocha huyo kuwakomalia mabosi hao akiwaambia suala la usajili wa mshambuliaji haliepukiki. Kocha Benchikha amewaambia, Simba bado inahitaji mshambuliaji mwenye msuli wa kuwapanguza mabeki na kufunga ili kikosi chake kipate nguvu kubwa.
.
Simba tayari imeshafikisha idadi ya wachezaji 12 wa kigeni hadi sasa, huku ikiwa imeshamshusha kiungo mkabaji Babacar Sarr kutoka senegal na kulazimisha mmoja kati ya waliopo sasa kupigwa panga na upepo unatajwa kuwaelekeza hao watatu Chama, Kramo na Phiri.
.
Arena tunafahamu kuwa kocha Benchikha amewaambia mabosi wake kazi ya nani ataondoka aachiwe yeye muhimu watafute watu ambao anaowataka kwenye kikosi chake.
 
[emoji2788] “Kuna vitu rahisi nilikuwa naviona wakati nikiwa mdogo, lakini kuvipata kwa sasa nalipa pesa nyingi sana. Nimepoteza uhuru wangu kama binadamu.

Siwezi kufanya mitoko kama navyotaka. Kila kitu lazima kiwe kwenye mpangilio, kipangwe.

Ningependa kwenda kula kwenye migahawa, kufanya mitoko, kukutaka na marafiki zangu, kwenda kwenye sherehe na vitu vya aina hiyo...” — straika wa PSG, Kylian Mbappe akizungumzia umaarufu.

 
INATAKA REKODI
.
25 —IVORY Coast inashiriki Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON kwa mara 25 (mabingwa mara mbili 1992 na 2015). Misri imecheza AFCON mara 26. The Elephants inatazamia kuwa mwenyeji wa kwanza kubeba kombe hilo tangu Misri ilipofanya hivyo mwaka 2006.
 
[emoji2788] “Mimi na wenzangu wakati tunakubali kuifundisha Chelsea tulifahamu itaenda kuwa na changamoto lakini sio kwa kiasi hiki, mambo yamekuwa mengi mara majeraha, wachezaji kusimamishwa kumesababisha hali kuwa mbaya zaidi,” Kocha wa Chelsea Mauricio Pochettino.
 
KOCHA wa mpira wa miguu, Sven-Goran Eriksson amefichua taarifa mbaya, akisema ameambiwa kwamba ana mwaka mmoja tu wa kuwa hai baada ya kupimwa na kugundulika kuwa na saratani isiyokuwa na tiba wala kinga.
.
Kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England mwenye umri wa miaka 75, amefichua ishu ya afya yake kupitia kituo kimoja cha redio cha P1 cha huko kwao Sweden. “Kila mtu atambua kwamba nina ugonjwa ambao si mzuri, ni kansa. Lakini, nitapambana kwa kadiri ninavyoweza. Nafahamu nikijariwa mema basi ni kuishi mwaka mmoja, ikiwa tofauti basi inaweza isifike mwaka, lakini nataka niishi muda mrefu zaidi.
.
“Sidhani kama madaktari wana uhakika wa asilimia zote, hawawezi kusema ni siku gani itakuwa ya mwisho. Ni heri usifikirie hilo ili kutoupa mashaka ubongo wako.”
.
Eriksson aliwahi kuzinoa timu nyingi ikiwamo Manchester City, Leicester City, Fiorentina, AS Roma, Benfica, Lazio, Sampdoria, England, Mexico, Philippines na Ivory Coast kwa kuzitaja kwa uchache.

 
Akapimwe akili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…