Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 154,929
- 459,607
Mtoto wa mwaka mmoja na miezi nane amefariki dunia kwa kuungua na moto baada ya mama yake mzazi kumuacha ndani kukiwa na jiko la mkaa lenyewe moto.
Tukio hilo limetokea Machi 25, 2024 katika mtaa wa Igangidung'u uliopo Kata ya Kivavi halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe.
Akizungumza na Mwananchi leo Machi 26, 2024 mama wa mtoto huyo Anna Mabiki (28) amesema alimuacha ndani akiwa amelala kwenye kochi na kwenda kupokea mafuta ya kupikia barabarani kwa dereva bodaboda ambaye hakupafahamu nyumbani kwake.
Amesema baada ya kuchukua hayo mafuta na kurudi nyumbani, ndipo alikutana na janga hilo la moto ambao uliondoa maisha ya mtoto wake huyo.
"Niliagiza mtu aniletee mafuta kule chini hapa kwangu hapafahamu akataka tukutane barabarani, lakini wakati ananikabidhi mafuta nageuka nyuma nyumbani kuna moto tukaanza kukimbia na yule kaka kuja kumuokoa mwanangu" amesema Anna.
Tukio hilo limetokea Machi 25, 2024 katika mtaa wa Igangidung'u uliopo Kata ya Kivavi halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe.
Akizungumza na Mwananchi leo Machi 26, 2024 mama wa mtoto huyo Anna Mabiki (28) amesema alimuacha ndani akiwa amelala kwenye kochi na kwenda kupokea mafuta ya kupikia barabarani kwa dereva bodaboda ambaye hakupafahamu nyumbani kwake.
Amesema baada ya kuchukua hayo mafuta na kurudi nyumbani, ndipo alikutana na janga hilo la moto ambao uliondoa maisha ya mtoto wake huyo.
"Niliagiza mtu aniletee mafuta kule chini hapa kwangu hapafahamu akataka tukutane barabarani, lakini wakati ananikabidhi mafuta nageuka nyuma nyumbani kuna moto tukaanza kukimbia na yule kaka kuja kumuokoa mwanangu" amesema Anna.