Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imesema bangi ni dawa haramu inayoongozwa kwa kupatikana na kutumiwa zaidi nchini ikifuatiwa na heroin, mirungi na cocaine na hivi karibuni methamphetamine ambapo amesema dawa hizo zina madhara ya kiafya ikiwemo Mtu kuona visivyokuwepo na kupelekea kufanya vitu visivvyofaa kwenye Jamii.

Akiongea Jijini Dar es salaam leo, Kamishna Msaidizi wa Kinga na Huduma za Jamii DCEA, Moza Makumbuli amesema bangi ni miongoni mwa vileta njozi ambapo humfanya Mtumiaji kuhisi, kuona au kusikia vitu visivyokuwepo au tofauti na uhalisia.

Makumbuli amewataka Watanzania kujiepusha na matumizi ya bangi na dawa nyingine za kulevya kwakuwa zina madhara huku akishangaa Watumiaji wa mitandao kutofurahia pale madhara ya bangi yanaposemwa au bangi ikikamatwa “Suala la bangi ni mtihani inaonekana wengi wanatumia, hata ukiangalia habari mfano ile ya biskuti za bangi mtandaoni comment za Watu ni kama vile wanaona bangi inachelewa kuhalalishwa, bangi haifai tujiepushe kutumia”
View attachment 2812655
makaveli10 kumbe ndio maana unaniona kivuruge😂😂😂
 
Shirika la Afya duniani (WHO) limeonya kuhusu hali "mbaya na ya hatari" katika kituo kikuu cha matibabu Gaza, Hospitali ya Al-Shifa, ambayo inakabiliwa ukosefu wa umeme na uhaba wa chakula na maji.

Mtendaji Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema "milio ya risasi na milipuko ya mara kwa mara katika eneo karibu na hospitali imezidisha hali ambayo tayari ni mbaya na kwasasa Al-Shifa haifanyi kazi kama hospitali tena," amesema.
Jeshi la Israel limekariri kuwa liko tayari kusaidia kuwahamisha watoto kadhaa wachanga walio katika mazingira magumu wanaohudumiwa hospitalini hapo.

Mkuu wa upasuaji wa Al-Shifa, Dk Marwan Abu Saada, ameiambia BBC kwamba mtoto wa tatu aliyezaliwa kabla ya wakati amefariki kwa sababu ya ukosefu wa nguvu.

Awali akizungumza na BBC hapo, Rais wa Israel, Isaac Herzog alirudia madai kwamba Hamas ina makao yake makuu chini ya Al-Shifa, hata hivyo Hamas inakanusha kutumia hospitali hiyo kwa madhumuni ya kijeshi.

Dk Abu Saada pia alielezea madai ya Israel kuwa ni ya uongo na ametoa mwaliko kwa vikosi vyake vya karibu kuja na kukagua jengo hilo.

Screenshot_20231113_150455_Instagram.jpg
 
[emoji599] JUST IN: MASTAA wa Simba wanaingia kambini leo kujiandaa na mechi ya kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast [emoji1081] itakayopigwa Novemba 25, jijini Dar es Salaam, huku baadhi yao wakikiri wamesikia manung’uniko ya wanachama na mashabiki wa timu hiyo wakiahidi kuwapa raha.
.
Wakati mabosi wa Simba wakitarajia kumalizia vikao vyao vilivyoanza tangu wikiendi iliyopita, leo Jumatatu wanamalizia mikakati ya kumleta kocha mpya, msaidizi na kocha wa viungo baada ya Robertinho, Ounane Sellami na Corneille Hategekimana kufungashiwa virago, ARENA express tunajua Simba inataka kushusha wataalamu hao watatu kabla ya mechi ya Asec Mimosas.
Screenshot_20231113_150854_Instagram.jpg
 
Kocha wa Yanga, Miguel Gamondi amekiangalia kikosi kilicho kwa sasa na nyota waliopo kisha akaandika ripoti na kuikabidhi kwa viongozi akitaka aletewe winga teleza mmoja na straika anayejua kufunga mabao kupitia dirisha dogo litakalofunguliwa mwezi ujao ili amalize kazi mapema.
.
Yanga kwa sasa inajiandaa kwa ajili ya mechi sita za makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikitarajiwa kuanza ugenini dhidi ya CR Belouizdad ya Algeria, Novemba 24 kabla ya kuikaribisha Al Ahly. Lakini pamoja na kuwa kwenye maandalizi kwa ajili ya mechi hizo dhidi ya klabu kutoka Afrika Kaskazini, kocha Gamondi tayari ameshawasilisha ripoti ya benchi la ufundi kwa mabosi wa klabu hiyo, ambayo inaelezwa imeanza kufanyiwa kabla hata kabla dirisha la usajili halijafunguliwa Disemba 16.
.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kuna uwezekano mkubwa straika wa sasa Hafiz Konkoni kupewa mkono wa kwaheri endapo Yanga itapata nyota wanayemfukuzia kwa sasa ambaye hata hivyo jina lake limefanywa siri. Yanga inataka kuachana na Hafiz kutokana na mshambuliaji huyo Mghana kushindwa kukata kiu ya benchi la ufundi la timu hiyo.
.
Gamondi ametaja pia kuhitaji winga mwenye kasi na kujua kupangua ukuta ambaye naye akitakiwa kuwazidi mawinga wote waliopo kikosini akiwamo Mahlatse Makudubela ‘Skudu’, Maxi Nzengeli, Jesus Moloko na Denis Nkane.
Screenshot_20231113_151027_Instagram.jpg
 
MWAMBA SANA
.
04—Ange Postecoglou ni meneja wa nne kwenye Ligi Kuu England, kushinda tuzo ya meneja bora wa mwezi kwa miezi mitatu mfululizo, baada ya Antonio Conte (3 - Octoba-Desemba 2016), Pep Guardiola (4 - Septemba -Desemba 2017) na Jurgen Klopp (3 - Novemba 2019-Januari 2020)

Screenshot_20231113_151130_Instagram.jpg
 
HATARI SANA
.
17—Harry Kane ni mchezaji wa kwanza katika historia ya Ligi Kuu ya Ujerumani, Bundesliga kufunga mabao 17 katika mechi 11 za kwanza za msimu. Juzi Jumamosi alifunga mabao mawili kwenye ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Heidenheim mchezo wa ligi kuu.
Screenshot_20231113_151233_Instagram.jpg
 
Back
Top Bottom