Makapuku Forum

Makapuku Forum

Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na matukio ya mbwa wa kufungwa majumbani kuwashambulia wamiliki wake huku sababu mbalimbali zikitajwa ikiwemo kichaa.

Akizungumza na Mwananchi Digital, mtaalamu wa mifugo, Joseph Ndalu amesema sababu za mbwa kuwashambulia wamiliki wake zinatofautiana kulingana na mazingira.

Amesema utamaduni wa kufuga wanyama hao kiholela na kwa mazoea ni sababu kuu.

Ndalu ametaja sababu nyingine kuwa ni ugonjwa wa kichaa cha mbwa, kutopewa chanjo na dawa za kuua vimelea wa nje na ndani ikiwamo minyoo, kutopewa chakula kwa wakati na kwa ujazo unaohitajika, kufanyishwa michezo wasiyoipenda na kuanzisha mazingira hatarishi kwa kiumbe huyo.

View attachment 2869714
Siwapendi hawa viumbe🙆
 
Nchi ya Rwanda imesema imesikitishwa na uamuzi wa Burumdi kuufunga mpaka wake na Rwanda ikiwa zimepita wiki mbili baada ya kuituhumu Nchi hiyo jirani yake kuunga mkono Waasi waliofanya mashambulizi kwenye ardhi yake.

Rwanda imesema uamuzi huo utawakwamisha ufanyaji wa biashara na muingiliano mwingine wa Watu na bidhaa kati ya Nchi hizo mbili na kukiuka makubaliano ya ushirikiano wa kikanda na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Itakumbukwa jana Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi Matin Nitereste, alitangaza kwamba wameamua kufunga mpaka na Rwanda na kwamba yeyote anayejaribu kupitia mpaka huo hatofanikiwa.

Waziri Nitereste amesema Rwanda inawahifadhi Wahalifu wanaowadhuru Raia wa Burundi na kuongeza kuwa wao pia hawawataki Raia wa Rwanda.

Burundi inasema kundi la Waasi wa RED-Tabara ambao linadai linahifadhiwa na Rwanda, lilifanya shambulizi December 22 karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na kuuwa Watu 20, wakiwemo Wanawake na Watoto.

Tangu kutokea kwa shambulio hilo, Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye amekuwa akiituhumu Rwanda kuwaunga mkono Waasi hao, madai ambayo Serikali ya Rwanda imeyakanusha mara kwa mara.
Screenshot_20240112_151116_InstaPro%20.jpg
 
Ukishamaliza matibabu, dawa unazopewa na wataalamu wa afya umewahi kuhoji au kujiuliza ni za aina gani, zitasaidia nini na zinaweza kukupa athari gani baada ya kuzitumia?

Watafiti wamechambua hilo na kubaini wataalamu wa afya wamekuwa wakitoa dawa nyingi za antibaotiki kwa wagonjwa tofauti na kiwango kinachotakiwa kimataifa, huku zile za mstari wa tatu na nne ambazo hazishauriwi zikitumika.

Hali hiyo imetajwa kusababisha ongezeko la usugu wa vimelea dhidi ya dawa za antibaotiki mwilini ‘Antimicrobial resistance AMR’.

Hiyo ni kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zilizofanywa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (Muhas) zilizoonyesha Tanzania imefikia matumizi ya asilimia 88.0 kwa dawa za antibaotiki kinyume na mwongozo uliowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) unaoelekeza nchi zitumie asilimia 20.0 hadi 26.8.

View attachment 2869717
Madaktari wetu hawa hawa uhoji😳😳😳
 
Rais wa Marekani Joe Biden amesema vikosi vya kijeshi vya Nchi yake na Uingereza vimefanya mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo kadhaa nchini Yemen yanayotumiwa na Waasi wa Kihouthi wanaoungwa mkono na Iran.

Mtandao wa @DW_Kiswahili umeripoti kuwa hatua hiyo imekuja baada ya mashambulizi ya Waasi hao ambayo wameyafanya dhidi ya meli za kibiashara katika Bahari ya Shamu ambapo mashambulizi hayo ya angani ya Marekani na Uingereza yamepiga Miju kadhaa ya Yemen, ambako Waasi wa Kihouthi wanadhibiti maeneo mengi na kuhusisha ndege za kivita na makombora ya Tomohawk.

Katika taarifa yake, Biden ameyataja mashambulizi hayo kuwa ni jibu la moja kwa moja kwa mashambulizi yasiyokuwa ya kawaida ya Wahouthi, ikiwa ni pamoja na matumizi ya makombora ya Balistiki ya kuzuia meli kwa mara ya kwanza katika historia “Leo, kwa maelekezo yangu, vikosi vya kijeshi vya Marekani pamoja na Uingereza na kwa usaidizi kutoka Australia, Bahrain, Canada na Uholanzi, vilifanikiwa kufanya mashambulizi dhidi ya maeneo kadhaa nchini Yemen yanayotumiwa na Waasi wa Kihouthi kuhatarisha uhuru na usafirishaji katika mojawapo ya njia muhimu zaidi za baharini duniani”

Waziri Mkuu wa Uingereza Rishi Sunak pia aliitisha kikao cha dharura cha Baraza la Mawaziri Mjini London siku ya jana Alhamisi kujadili mashambulizi dhidi ya Wahouthi.

Kiongozi wa kundi hilo la Waasi Abdul-Malik al-Houthi ameapa kulipiza kisasi dhidi ya mashambulizi hayo ya anga ya kimataifa na ameonga kwamba uchokozi wowote wa Marekani hautopita bila kushughulikiwa, Waasi wa Kihouthi wamefanya mashambulizi kadhaa katika njia muhimu ya kimataifa ya baharini tangu kuzuka kwa vita vya Gaza na shambulizi la kushutukiza la Hamas dhidi ya Israel Oktoba 7.
Screenshot_20240112_151316_InstaPro%20.jpg
 
Back
Top Bottom