Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20240125_073604_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20240125_073619_Opera%20Mini.jpg
 
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Dunia, Papa Francisco ameridhia ombi la askofu msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Mkoa wa Kagera, Methodius Kilaini la kustaafu kwake.

Taaarifa za kustaafu kwake zimetolewa na Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (TEC), Askofu Gervas Nyaisonga katika sherehe ya kuwekwa wakfu kwa Jovitus Mwijage kuwa askofu wa Jimbo la Bukoba, inayofanyikia Uwanja wa Kaitaba, mkoani humo, leo Jumamosi, Januari 27, 2024

“Tumepata taarifa kutoka Roma muda huu saa nane, ombi la Baba Askofu Kilaini la kutaka kustaafu limekubaliwa rasmi,” amesema Askofu Nyaisonga.

Baada ya taarifa hiyo, Askofu Kilaini ameitwa sehemu ya kuzungumzia na kuimba, “nimeumaliza mwendo, nimeumaliza mwendo, nimevipiga vita vilivyo vizuri…” huku wakiitikia wimbo huo.

Kisha Askofu Kilaini amesema, alimualika Rais mstaafu Jakaya Kikwete katika shughuli hiyo lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake ameshindwa kufika.

Screenshot_20240128_065236_InstaPro%20.jpg
 
Mkoa wa Katavi umeripotiwa kuwa na mtu mmoja aliyegundulika kuwa na ugonjwa wa kipindupindu. Mtu huyo amebainika katika Halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele.

Kutokana na hali hiyo, wananchi wameiomba Serikali kusisitiza suala la usafi kwenye makazi na maeneo ya biashara ikiwemo kuzoa taka kwa wakati.

Wakizungumza na Mwananchi leo Jumamosi Januari 27, 2024 baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Mpanda, wamesema Serikali isipochukua hatua, ugonjwa huo utaiathiri jamii kwa kiasi kikubwa.

Ofisa afya wa Manispaa ya Mpanda, Erick Kisaka amesema wanaendelea kuielimisha jamii kufanya usafi na kunawa mikono mara kwa mara.

"Tunapita kaya kwa kaya kukagua na uchafu uliopo kwenye masoko umeanza kuzolewa, magari yameongezeka badala ya kutumia moja,"amesema Kisaka.

Mkuu wa mkoa huo, Mwanamvua Mrindoko ametoa onyo kali kwa wakuu wa wilaya, wakurugenzi watendaji na maofisa afya kuhakikisha wanasimamia usafi.
Screenshot_20240128_065336_InstaPro%20.jpg
 
Back
Top Bottom