Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 154,929
- 459,607
Waafrika hawavumilii vitendo vya ushoga - Papa Francis
Papa Francis amekaririwa na gazeti moja la nchini Italia akisema kwamba kwa Waafrika ushoga ni kitu kibaya sana na hawavumilii jambo hilo. Papa Francis ameyasema hayo kufuatia waraka ulitolewa na idara ya elimu ya waamini huko Vatican kuruhusu watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja kupewa baraka.
Waraka huo umezua gumzo miongoni mwa waumini wa Kanisa Katoliki na hata maaskofu wa kanisa katoliki Afrika wamekataa kwamba hawawezi kuwabariki watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Katika mahubiri yake, Askofu Kasala wa Jimbo Katoliki la Geita alisema, "kubariki mashoga bora nibariki jiwe ujengee nyumba."
Katika mahojiano yake na gazeti hilo Papa Francis amesema anaamini kwamba ipo siku watu wataelewa msimamo wake na kuacha kuwatenga watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja hata hivyo Papa amekiri kwamba kwa Waafrika ni kinyume na wanapinga jambo hilo, Papa amesema, "Kwa Waafrika, kwao ushoga ni jambo mbaya na hawavumilii".
Licha ya waraka huo uliozua gumzo bado msimamo wa Kanisa Katoliki kuhusu ndoa ni ule ule kwamba ndoa ni kati ya mwanaume na mwanamke na si vinginevyo..!
Papa Francis amekaririwa na gazeti moja la nchini Italia akisema kwamba kwa Waafrika ushoga ni kitu kibaya sana na hawavumilii jambo hilo. Papa Francis ameyasema hayo kufuatia waraka ulitolewa na idara ya elimu ya waamini huko Vatican kuruhusu watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja kupewa baraka.
Waraka huo umezua gumzo miongoni mwa waumini wa Kanisa Katoliki na hata maaskofu wa kanisa katoliki Afrika wamekataa kwamba hawawezi kuwabariki watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.
Katika mahubiri yake, Askofu Kasala wa Jimbo Katoliki la Geita alisema, "kubariki mashoga bora nibariki jiwe ujengee nyumba."
Katika mahojiano yake na gazeti hilo Papa Francis amesema anaamini kwamba ipo siku watu wataelewa msimamo wake na kuacha kuwatenga watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja hata hivyo Papa amekiri kwamba kwa Waafrika ni kinyume na wanapinga jambo hilo, Papa amesema, "Kwa Waafrika, kwao ushoga ni jambo mbaya na hawavumilii".
Licha ya waraka huo uliozua gumzo bado msimamo wa Kanisa Katoliki kuhusu ndoa ni ule ule kwamba ndoa ni kati ya mwanaume na mwanamke na si vinginevyo..!