Makarani wa Sensa si mmepewa hela ya kula? Kwanini mida ya saa 7 hadi Saa 9 mnapenda kung'ang'ania katika nyumba moja tu?

Makarani wa Sensa si mmepewa hela ya kula? Kwanini mida ya saa 7 hadi Saa 9 mnapenda kung'ang'ania katika nyumba moja tu?

Na gia yenu Kubwa hiyo Mida huwa mnajifanya Vishkwambi vyenu vimeisha Chaji hivyo mnaomba mvichaji kumbe Timing yenu Kuu huwa ni Kuwepo katika Ratiba zetu za Kula mkijua kuwa Watanzania ni Wakarimu hivyo mtakaribishwa na mtakula tu.

Kuna Mwenzenu leo kajua kwanini Nyoka hana Ugoko au kwanini Wimbo wa Taifa hauna Kolabo baada ya kuja na hii Mbinu ambapo muda wa Kula ulipofika nikaomba Mjuba wa Kipemba Nungwi Nitengewe Chakula changu Mwenyewe na akawa ananiangalia kwa Huruma ila Nikala hadi mwisho na Yeye akaishia tu Kunikodolea.

Baadae nikaona kaja Mwenzake Mmoja na nikamsikia akiniteta kuwa Nimekaza sana hata sijamkaribisha Chakula na Mwenzake nae akanitizama kwa Kuibia ibia na kumsikia akisema kwa Sura yangu ilivyo ya Kikauzu ( Ngumu ) hata kama ningemkaribisha hicho Chakula kingegoma kupita Kooni Kwake na angekitapika hivyo ashukuru tu Mwenyezi Mungu.

Yaani kila Siku nasikia Makarani wa Sensa mnapewa Shilingi Elfu Arobaini na Tano ( Tsh 45,000/= ) Hela ya Chakula ikiwemo halafu bado mnataka Kudoea Vyakula vyetu Sisi Hustlers ili mteleze tu katika Ganda la Ndizi kisha mkajisifu.
We kama unaweza kuwapa msosi wape kama mchoyo tulia 😂😂
 
Basi madam leo natoka job saa 10 namkuta karani. Alikuja mara ya kwanza akakuta sipo akawa anamuhoji mpangaji mwenzangu aliekua amemsimamia mlangoni kwake. Nikamwambia ukimaliza na mimi bro sijahesabiwa. Nikaingia ghetto kwangu.

Jamaa alivomalizana na yule akaja kwangu. Sema sikua na msosi ila nikamtoa juice takeaways mbili ainjoy.

Masagiswali clean ushirikiano nimempa A+

Hii hali ninayoisikia leo ni kama ile niliyoisikia October 25 nilivyopiga kura. Najiona Mtanzania aisee.

Na mimi nilimuuliza maswali mawili matatu, jamaa ni mwanachuo 2nd year kwahiyo ukipima unajua anamaisha ya kawaida tu kma asilimia kubwa yetu.
Safi Sana mkuu
 
Daaah ushamba mzigo, sasa wewe kama ulikosa kazi ya sensa usitumie kigezo cha kusema wenzako wana njaa.

Kwani walikuomba chakula??? Ebu wape data waondoke.
 
Na gia yenu Kubwa hiyo Mida huwa mnajifanya Vishkwambi vyenu vimeisha Chaji hivyo mnaomba mvichaji kumbe Timing yenu Kuu huwa ni Kuwepo katika Ratiba zetu za Kula mkijua kuwa Watanzania ni Wakarimu hivyo mtakaribishwa na mtakula tu.

Kuna Mwenzenu leo kajua kwanini Nyoka hana Ugoko au kwanini Wimbo wa Taifa hauna Kolabo baada ya kuja na hii Mbinu ambapo muda wa Kula ulipofika nikaomba Mjuba wa Kipemba Nungwi Nitengewe Chakula changu Mwenyewe na akawa ananiangalia kwa Huruma ila Nikala hadi mwisho na Yeye akaishia tu Kunikodolea.

Baadae nikaona kaja Mwenzake Mmoja na nikamsikia akiniteta kuwa Nimekaza sana hata sijamkaribisha Chakula na Mwenzake nae akanitizama kwa Kuibia ibia na kumsikia akisema kwa Sura yangu ilivyo ya Kikauzu ( Ngumu ) hata kama ningemkaribisha hicho Chakula kingegoma kupita Kooni Kwake na angekitapika hivyo ashukuru tu Mwenyezi Mungu.

Yaani kila Siku nasikia Makarani wa Sensa mnapewa Shilingi Elfu Arobaini na Tano ( Tsh 45,000/= ) Hela ya Chakula ikiwemo halafu bado mnataka Kudoea Vyakula vyetu Sisi Hustlers ili mteleze tu katika Ganda la Ndizi kisha mkajisifu.
Gentamycine una ID nyingi sana hapa JF

Hata hii ni yako

Mkuu uandishi wako ni wa aina moja ndio maana tunakutambua

Tumia ID ya Gentamycine inakufaa tu

Hizi ID unajiabisha
 
Kwangu karani alikuja jana saa moja na nusu usiku...

Pisi moja ya makamo tu... amenihesabu huku tukipata dinner...
 
Gentamycine una ID nyingi sana hapa JF

Hata hii ni yako

Mkuu uandishi wako ni wa aina moja ndio maana tunakutambua

Tumia ID ya Gentamycine inakufaa tu

Hizi ID unajiabisha
Pumbavu MImi ni MINOCYCLINE na si huyo Mume Wenu mnaempenda na Kumshobokea Kutwa.

Nimewachoka sasa kila mara Kunihusisha nae wakati ukweli wa 100% Mimi siyo Yeye na Yeye siyo Mimi.

Mnakera!!!!
 
Tanzania ni Nchi yenye chakula cha kutosha sana ila kila kukicha wahuni mnamindi sana lishe kama vile tupo Nchi zenye ukame ni ngumu kupata maendeleo kama kwako ishu ya chakula ni kipengele hata kama kipo muda wote unawaza chakula tuu..tuondokane na hii dhana ya chakula chakula
 
Tanzania inasifika kwa ukarimu ila sasa makarani nao wasitake kutengeneza mazingira ya kukushawishi ili wapate msosi wa bure, ya nini ujibaraguze kwa watu ili upate msosi wa bure ilhal Kuna wali hata wa buku na jero tu mtaani, usitarajie kupata Chochote pindi uwatembeleapo strangers...huyo kafundishwa kuwa hakuna chakula cha bure kwa mwanaume mwenye nguvu na akili
 
Acha uchoyo na wivu mkuu. Wape msosi waupige😂😂😂😂😂😂😂
 
A59BCA2F-0FB8-49BC-AE71-CFB4F3FF6BB4.jpeg
 
Back
Top Bottom