Makomando wa Marekani waingia Somalia na kumuua mkuu wa magaidi wa IS

Baada ya kujibadilisha id unakuja na mtungo eti huna dini ,Kama kweli si ukaoe mama yako mzazi au Dada yako na uanze kula nyama Za maiti za watu 😝😝😝
Nisamehe kwa kuja na ID nyingine.
Mama na dada yangu tayari nishawaoa bwana Gavana.
Hapa nilipo naandika comment huku nikitafuna mishkaki ya nyama za watu mdomoni na glas ya damu zao ikiwa pembeni.

Una jengine mkuu?
 
nahisi ww ni kafir innsui au musilamu dirisha dogo ima umepotelea mbali!
Ingekuwa Muumini Ungeamini qauli hii ya Haqi ya Allah!
[emoji116][emoji116]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا آمِنُوا بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ وَالْكِتَابِ الَّذِي نَزَّلَ عَلَىٰ رَسُولِهِ وَالْكِتَابِ الَّذِي أَنزَلَ مِن قَبْلُ ۚ وَمَن يَكْفُرْ بِاللَّهِ وَمَلَائِكَتِهِ وَكُتُبِهِ وَرُسُلِهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا

[ AN-NISAAI - 136 ]
Enyi mlio amini! Muaminini Mwenyezi Mungu, na Mtume wake, na Kitabu alicho kiteremsha juu ya Mtume wake, na Kitabu alicho kiteremsha kabla yake. Na anaye mkataa Mwenyezi Mungu, na Malaika wake, na Vitabu vyake, na Mitume wake, na Siku ya Akhera, basi huyo amekwisha potelea mbali.
 
Wapi Mungu aliteremsha Biblia?
Afadhali umekuja na id yako halisi
 
Sasa Sema Yesu si Mungu
Yesu si Mungu.

Waulize Magaidi wenzio wanataka niseme Yesu si Mungu mara ngapi itatosha waache kuua watu wasio hatia.

Au wakiwa na hamu ya kuvaa mabomu wavae ya kuwalipua wao wenyewe wengine yasitufikie.

YESU SI MUNGU.
 
Yesu si Mungu.

Wauliza Magaidi wanataka niseme Yesu si Mungu mara ngapi itatosha waache kuua watu bila hatia.

Au wakiwa na hamu ya kuvaa mabomu wavae ya kuwalipua wao wenyewe wengine yasitufikie.

YESU SI MUNGU.
Good, step, sasa unaamini kitu gani?
 
Good, step, sasa unaamini kitu gani?
Kwa sasa Mungu wangu ni Upendo na Amani.
Naamini kila binadamu ana haki ya kupendwa,kuheshimiwa na kuishi maisha yake kwa amani.

Ila pia niko tayari kuamini chochote utakachonichagulia wewe iwapo nikikiamini hicho ulichonichagulia binadamu wataacha kuuana kwa kigezo cha kutetea dini zao.
 
Umepatia!; ilaha nakuuliza hizo ibada na sharia za ummat wa nani??
[emoji116][emoji116]
لِّكُلِّ أُمَّةٍ جَعَلْنَا مَنسَكًا هُمْ نَاسِكُوهُ ۖ فَلَا يُنَازِعُنَّكَ فِي الْأَمْرِ ۚ وَادْعُ إِلَىٰ رَبِّكَ ۖ إِنَّكَ لَعَلَىٰ هُدًى مُّسْتَقِيمٍ

[ AL -HAJJ - 67 ]
Kila umma tumewajaalia na ibada zao wanazo zishika. Basi wasizozane nawe katika jambo hili. Na waite watu kwendea kwa Mola wako Mlezi. Hakika wewe uko kwenye Uwongofu Ulio Nyooka.
 
Tuwekee Yesu Alipo Fundisha Uchafu huo!
Hao wanae mgeza unamjua
 

Unaweza kutuambia kwa nini Yesu si Mungu?
 

Hizo aya zinaongelea Biblia ?
 
Nifundishe wewe!
Unaniuliza hbr za Yesu alokwambia mie mkristo ni nani?

Au ngojea nijaribu kujibu.

Yesu sio Mungu sababu Allah ndie Mungu.
Sijakuuliza wewe ni mkristo au la nilikuuliza jee Yesu ni Mungu ukaniambia Yesu si Mungu , Sasa nimekuuliza sababu zilizokufanya uone Yesu si Mungu unakimbia ki style
 
Kabla sijakuchagulua kitu cha kuamini unaweza kutuambia ni kwa nini huamini kuwa Yesu ni Mungu ?
Sababu naamini kuwa habari za uwepo wa Mungu ni za kutunga kama za Juma na Roza.
Allah,Yesu au Jehova ni uongo wa wazungu na waarabu.

Watu kama wewe mmelewa huu uongo kias cha kusikitisha.
Mmekua vichaa mnaoweza kufungwa mabomu ya kuwaua na kuua wasio na hatia.

Iman zenu za Yesu na Allah hazinisumbui na ninaziheshimu na huwa sidharau iman ya mtu hata akisema Wowowo la mkewe ndo Mungu wake nitaheshimu.

Kinachonipa shida ni uharibifu wa amani pale mnapotetea hao Miungu yenu.
Its time sasa Muache Yesu au Allah wajipiganie wenyewe.

Its time mtu akimtukana Yesu aachwe Yesu apambane na adui yake.

Its time mtu asiyemuamin Allah adharauliwe tu na Allah ndo awe muamuz wa kumpa mabikira au kumpa malaya au kumnyima kabisa mbususu.

Nyie wakristo na waislam achen viherehere vya kupigana vita isiyowahusu.
 

Ni nini maana na lengo la maisha?

' Hili labda ni swali muhimu zaidi ambalo limewahi kuulizwa.

Katika miaka yote, wanafalsafa wameona kuwa ni swali la msingi zaidi.

Wanasayansi, wanahistoria, wanafalsafa, waandishi, wanasaikolojia na watu wa kawaida wote hupambana na swali hilo wakati fulani katika maisha yao.


Je, Mantiki ni Mwongozo wa Kutosha?​

“Kwa nini tunakula?” “Kwa nini tunalala?” 'Kwa nini tunafanya kazi? '

Majibu tunayopata ya maswali haya yatakuwa yale yale. “Nala ili niishi.” “Nalala ili nipumzike.” 'Nafanya kazi ili nijisaidie na nisaidie familia yangu.

' Lakini linapokuja kwa suala la maana ya maisha, watu wanachanganyikiwa.

Tunaona tahayuri wao katika aina ya majibu tunayopokea.

Vijana wanaweza kusema, “Ninaishi kwa ajili ya pombe na usherati.”

Mtaalamu mwenye umri wa kati anaweza kusema, “Ninaishi kuchanga vya kutosha ili nistaafu vizuri.”

Mtu mzee anaweza kusema, “Maisha yangu yote, nimekuwa nikijiuliza kwa nini niko hapa.

Ikiwa kuna lengo, sijali tena.” Na labda jibu la watu wengi litakuwa, “Kwa hakika Sijui!”

Je, basi, utagunduaje lengo la maisha?

Tuna hiari mbili.

Ya kwanza ni kuwacha 'mantiki ya mwanadamu'- mafanikio yaliyoadhimishwa ya enzi ya Elimu ya Kisayansi- kutuongoza.

Baada ya yote, enzi hiyo ilitupatia sayansi ya kisasa kulingana na uchunguzi wa makini wa ulimwengu wa kiasili.

Lakini wanafalsafa waliokuja baada ya enzi hiyo walielewa lengo hilo?

Camus alielezea maisha kama “upuuzi”;

Sartre alizungumzia “uchungu, kutelekezwa na kukata tamaa.” Kulingana na hao, maisha hayana maana

Wadarwini walidhani maana ya maisha ni kuzaana.

Will Durant, kupambana na msiba wa mtu wa kisasa, aliandika, “Imani na matumaini yametoweka; shaka na kukata tamaa yamekuwa ada ya kila siku... si nyumba zetu na hazina zetu ndizo tupu, ni 'mioyo yetu.”

Linapokuja kwa lengo la maisha, hata wanafalsafa wenye hekima wanakisia tu.

Will Durant, mwanafalsafa aliyejulikana zaidi karne iliyopita, na Dk. Hugh Moorhead, profesa wa falsafa katika Chuo Kikuu cha Illinois Kaskazini, wote waliandika vitabu tofauti vilivyoitwa 'Maana ya Maisha.'

Waliandika kwa wanafalsafa maarufu, wanasayansi, waandishi, wanasiasa, na wasomi wa wakati wao duniani, wakiwauliza “Ni nini maana ya maisha?”

Kisha walichapisha majibu yao.

Wengine walitoa dhana zao , wengine walikiri kwamba walijitungia wenyewe lengo la maisha, na wengine walikuwa waaminifu kwa kusema kuwa hawakuwa na mwelekeo.

Isitoshe, idadi kadhaa kati ya wasomi maarufu waliwauliza waandishi wawaandikie na kuwaambia kama lengo la maisha limegunduliwa!
 


Hebu Tuache mbingu “Ziseme”​

Ikiwa mwanafalsafa hana jibu la uhakika, labda jibu linaweza kupatikana ndani ya moyo na akili ambayo sisi wenyewe tunamiliki.

Je! Umewahi kutazama angani usiku ukiwa wazi?

Utaona idadi isiyo hesabika ya nyota.

Tazama darubini na utaona thurea ya nyota, nebula nzuri ambapo nyota mpya zinaundwa, mabaki ya mlipuko ya kale wa supanova yaliyoundwa katika mlipuko wa mwisho wa nyota, miviringo maridadi ya Zohali na miezi ya Mshtarii.

Je, inawezekana mtu akose kuathirika na kuona nyota hizi nyingi katika anga ya usiku ikiangaza kama vumbi la almasi kwenye tandiko la mahameli nyeusi?

Makundi ya nyota, yanayoendelea mpaka nyuma; yanayokuwa nzito sana kiasi kwamba yanaonekana yakiungana katika visima maridadi.

Uadhama huu hutunyenyekeza, hutufurahisha, huhamasisha tamaa ya uchunguzi, na hutufanya tutafakuri. Ni jinsi gani ilikuja kuwa?

Tunahusianaje na hilo, na tuna nafasi gani ndani yake? Je, tunaweza kusikia mbingu “zikizungumza” nasi?

”Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili. Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa mbingu na ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika!” (Qur'an 3:190 -191)

Tunaposoma kitabu, tunakubali kwamba kuna mwandishi.

Tunapoona nyumba, tunakubali kuwa wajenzi wapo.

Mambo hayo yote yalifanywa kwa kusudi na wale walioyafanya. Ubunifu, utaratibu, na utata wa ulimwengu pamoja na ulimwengu unaotuzunguka ni ushahidi wa kuwepo kwa akili kuu, mtengenezaji kamili.

Sehemu zote za mbinguni zinadhibitiwa na sheria thabiti za fizikia.

Je, kuna sheria bila mwanasheria?

Mwanasayansi wa roketi Dr. von Braun alisema: “Sheria za kiasili za ulimwengu ni sahihi na thabiti sana kiasi kwamba hatuna shida ya kutengeneza roketi ya kupaa hadi kwa mwezi na tunaweza kuirusha na kuhesabu mwendo wake kwa kila sekunde. Lazima sheria hizi zimewekwa na mtu.

” Paul Davies, profesa wa fizikia, anahitimisha kwamba kuwepo kwa mwanadamu sio tu jambo la kibahati lisilotarajiwa. Anasema: “Hakika tuliwekwa hapa.”

Na anasema kuhusu ulimwengu:

“Kupitia kazi zangu ya kisayansi, nimekuja kuamini zaidi na zaidi kwamba ulimwengu wa dhahiri umewekwa pamoja na ujuzi wa kushangaza sana kiasi kwamba siwezi kukubali tu kama ukweli usiopingika. Lazima, inaonekana kwangu, kuwa kuna kiwango cha kina cha maelezo.”

Ulimwengu, ardhi, na vitu vilivyo hai duniani vyote vinatoa ushuhuda kwa ukimya kwa Muumba mwenye hekima, mwenye nguvu.




Kielelezo 2 Kanda ya Kati ya Nebula iliyochukuliwa na darubini ya Gemini kwenye Mauna Kea kwenye Kisiwa Kikubwa cha Hawaii, Juni 5, 2002. Iko katika kundi la Mshale, na ni nebula nzuri yenye wingu kubwa, yenye nguvu ya gesi na vumbi ambako nyota zinazaliwa. Moja ya nyota kubwa kwenye katikati ya nebula ilizaliwa takriban miaka 100,000 iliyopita. Umbali wa nebula kutoka mfumo wa Jua kwa ujumla umekubaliwa kuwa takriban kati ya miaka ya nuru 2,200 hadi 9,000.




Picha kwa hisani ya picha wa Uchunguzi Wa Gemini /Tume ya GMOS

Ikiwa tuliumbwa na Muumba, basi hakika Muumba lazima awe na sababu, kusudi, katika kutuumba.

Hivyo, ni muhimu kwamba tutafute kujua kusudi la Mungu kwa kuwepo kwetu.

Baada ya kufikia lengo hili, tunaweza kuchagua kama tunataka kuishi kulingana na hilo.

Lakini inawezekana tujue nini kingetokea iwapo tungeachwa pekee yetu bila mawasiliano yoyote kutoka kwa Muumba?
 


Mbadala Wa Uvumi: Muulize Mungu​

Hii inatuleta kwenye chaguo la pili: mbadala wa uvumi kuhusu maana na madhumuni ya maisha ni ufunuo.

Njia rahisi zaidi ya kugundua madhumuni ya uvumbuzi ni kuuliza mvumbuzi.

Ili kugundua lengo la maisha yako, muulize Mungu.

Je, Ukristo Unaweza Kujibu Swali?​

Katika Ukristo, maana na lengo la maisha linategemea imani katika injili ya Yesu Kristo, katika kumkubali Yesu kama Mwokozi.

Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”

Hata hivyo, pendekezo hili halikosi matatizo makubwa. Kwanza, kama hii ndiyo kusudi la uumbaji na sharti la uzima wa milele, kwa nini haikufundishwa na manabii kwa mataifa yote ya ulimwengu?

Pili, Mungu angegeuka kuwa mwanadamu wakati wa Adamu wanadamu wote wangekuwa na nafasi sawa ya uzima wa milele, ila wale waliokuja kabla ya wakati wa Yesu walikuwa na lengo lingine la kuwepo kwao!

Tatu, jinsi gani watu wa leo ambao hawajasikia habari za Yesu watatimiza kusudi la Kikristo la uumbaji?

Kwa kawaida, kusudi na lengo hilo ni jembamba sana na linakwenda kinyume na haki ya Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…