Makombora ya Kalibr ya Urusi yashambulia mkusanyiko wa siri wa maofisa wa juu wa jeshi la Ukraine na kuua majenerali/maofisa zaidi ya 50

Na wenye hao Bibisii kila habari ya mafanikio ya warusi wananukuu inamaana wao hawana uwezo wa kuzipata moaja kwa moja habari njema kwa jeshi la Urusi.

Au kunukuu wameweka ndo kakipengele ka kujitoa wasije wakakamatika kwa wanaowalazimisha watoe habari za upande mmoja.
 
Unafahamu maana ya neno CLAIMS?
au ndo kipere kinawasha muda wote?
 
Hakuna haja ya mipasho katika habari hii. Hii ni vita. Inawezekana wanachosema Urusi ni kweli au ni propaganda tu. DW wanasema hawajaweza kuthibitisha madai hayo ya Urusi; wao wamemnukuu msemaji wa Urusi tu. Kawaida kuua majenerali sio habari ndogo. Wanafahamika. Mrusi akitaka habari hiyo ionekane kweli, ataje na kusambaza majina na hata kuweka picha za hao majenerali kama Ukraine walivyofanya.

Hata hivyo haya sio mambo ya kushabikia. Ni mjinga tu ndiye anayeweza kuumia moyo au kufurahia vita kishabiki. Watu waliokomaa wanaangalia picha kubwa: maangamizi ya binadamu na rasilimali yasiyo na sababu ya maana (senseless/wanton self destruction of humankind).
 
Taaarifa hizi MK254 siamini kabisa kwamba huwa huwa huzioni 😅 😅 😅 maana sikuonagi kabisa nadhani hadi data huwa unazima

"Russian defence ministry claimed"....

Tukileta zetu huwa mnasema propaganda za magharibi, haya......
Japo sisi huleta na majina ya majenerali kabisa.
 
"Russian defence ministry claimed"....

Tukileta zetu huwa mnasema propaganda za magharibi, haya......
Japo sisi huleta na majina ya majenerali kabisa.
Vyombo vilivyoripo ni vya magharibi ujue? unadhani wataleta uthibitisho, anyway Ukrein amekanusha hii habari?
 
Nenda katembee na jeshi la Urusi, kila wakiua uwe unaenda kuangalia waliouawa na kutuletea taarifa.

Kwa hii dunia tuliyopo hakuna waandishi wala chombo cha habari wanaotembea na majeshi kila siku ili majeshi yakiua waripoti.

Halafu tusipangiane mambo ya kushabikia...kila mtu yupo huru kushabikia atakalo...
 
Russia wenyewe wamesema propaganda imetamalaki sana taarifa za russia kwenye hii vita
 
Vyombo vilivyoripo ni vya magharibi ujue? unadhani wataleta uthibitisho, anyway Ukrein amekanusha hii habari?

Leta source ya chombo cha magharibi kilicho ripoti, na mtaje majina ya majenerali kama ambavyo tunataja wa Urusi moja kwa moja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…