Makonda alitoa wapi zaidi ya Sh. Bilioni moja kujenga nyumba binafsi. Je, mshahara wa Mkuu wa Mkoa kwa miaka 3 unatosha?

Hapa tupo pamoja Chief, 60% ya wakurugenzi wa halmashauri kipindi cha Magu walikuwa wasukuma, walianzisha hadi group lao la Whatsapp, nilikuwa pia kwa hilo group, humo ndani ilikuwa kisukuma tu
Ngoma ikilia sana hupasuka. Walijisahau wakajiona wanayo haki ya msingi ya kuwa watawala wa TZ, kina Kigwangallah na wengine wa aina hiyo.
 
Hapo ndipo umuhimu wa Katiba mpya unapokuja. Hatuwezi kuwa na nchi ya kuoneana, kuogopana na kuabudu wenye vyeo ili tuishi kwa uhuru na raha mustarehe wakati wote.
Tufanye pilot test kwanza. Hebu atokee mwanachama mmoja tu amsema Mbowe halafu aone shughuli yake, maana kule kijani tumeona mtu kamsema Rais tu hatujui yuko wapi. Katiba zenu za vyama tu ni za kibabe na kifalme. Katiba mpya wakati ya zamani tu hatuijui wala haitekelezeki
 
Kwani wewe una nyumba ya thamani kiasi gani, na kwa kimshahara chako ulijikusanya miaka mingapi?

Kama wewe unaishi kwa kutegemea mshahara wa mwajiri wako tu, fahamu kuwa huo ni ulimbukeni wako. Na ndo maana unaona maajabu mtu kuwa na jengo la 1b. Wakati jengo la 1b ni la kawaida sana watu kibao nchini wana majengo ya zaidi ya 5b.

Maisha kujipanga ndugu. Usitafute kujua michongo ya mwenzio kisha umpige vita, jipange tafuta yako.
 
Polepole alisema CCM wana wanachama milioni 12, Chadema wanasema wana wanachema milioni 8. Tufanye hizo takwimu zao wote ni za kweli, jumla ni milioni 20.
Sasa wewe achana na hao milioni jikite kwenye raia milioni 40 au 35 wasio na vyama.
Zungumzia Katiba mpya kwa upande huo uache kujificha kuikataa katiba mpya kwa kivuli cha sababu za vyama.
 
Tumia akili wewe kama huna pesa wewe kausha
 
Sijaelewa post yako
RPC wa Dar wakati wa JPM alitolewa sehemu zote hata alipogembea ubunge alishinda kwa kura nyingi za maoni lakini kwa mzee akakatwa jina ikawa kama ndio mwisho wa safari yake ya kisiasa lakini kuja Mama akamtoa shimoni sasa RPC wa Dar
 
Nakubaliana na wewe sio kuwa na katiba mpya tu ila katiba inayoendana na hali ya sasa na miaka ijayo kumlinda kila mtu sio kulinda chama kwa bahati mbaya sana vyama vinataka katiba ambayo inaweza kuwa fursa wao kuja kutawala utakuta kikubwa wanaongelea tume huru, teuzi sababu ndio zenye maslahi yao, ila nakubaliana na wewe katiba iwe inamlinda na kuheshimu kila mtu bila kujali ni nani na kuwe na njia za kupata haki ikiwa mtu anatafuta haki, na hizi haki zipatikane nje ya vyana vya siasa. Hili ni gumu sana sababu tumetawaliwa na uvyama zaidi sio utaifa.
 
Tumuunge mkono Mama sasa anapojitahidi kuliunganisha taifa, na kuhakikisha kila mtu anafurahia nchi yake bila hofu ya kupotezwa
Wanamkwaza kwa kusema anapendelea zaidi Unguja na Pemba, wanasahau namna tulivyotumia nguvu kuitetea Chato alipokuwa ikulu.

Wanaongea ubaguzi usiokuwa na misingi imara wala hoja za uhakika za kueleweka.
 
Huyu mpya wa sasa ana ukaribu na Sabaya, sivyo? UVCCM akili huwa mnaweka wapi?
Sabaya dhambi zake zipo wazi mno, hizi za Makonda nyingi ni tuhuma, huwa hawazianiki wazi.

Sabaya mpaka ushahidi wa CCTV upo, upo ushahidi wa wale jamaa waliopigwa misumari miguuni kama Yesu alivyofanyiwa.

Makonda ni chuki zaidi kulinganisha na Sabaya. Mimi ni mtu mzima nimeshavuka umri wa kuwa UVCCM.
 
Dhambi za makonda ambazo ziliwekwa bayana na Marekani kupitia Secretary Pompeo, zenyewe zimejificha huko CCM? Puumbavo zako kijana.
 
Dhambi za makonda ambazo ziliwekwa bayana na Marekani kupitia Secretary Pompeo, zenyewe zimejificha huko CCM? Puumbavo zako kijana.
Marekani sio malaika mkuu, wanaweza kuwa walipenyezwa umbeya na wanasiasa wa humu humu nchini kina Tundu Lissu. Pumbavu wewe na uko wako wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…