Kamwagiwa maji sababu jamaa(Makonda) ni wa moto kwa sasa, yuko kwenye chat, ana trend kwenye media, kafanya ya maana hata kama ni ya kukurupuka, kawafunguwa watu macho jinsi TZ ilivyokuwa inaangamia kwa matumizi ya madawa ya kulevya na utajiri usiokifani wa watu wanaouza unga, huku mtaani hao hao wakisifika, kwa kutoa sadaka misikitini na makanisani, wakipaisha juu bei za viwanja, nguo hata vyakula, bila kusahau vitu vya anasa kama wine, bia, magari n.k. Kwa sasa ni nidhamu, hakuna ile "waletee walee wote"! n.k. Msifuni kwa hayo, na sio kumbeza kwa yale walio wengi walikuwa wakiogopa hata kuyasema..